Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
@El Maestro naomba nikuulize tuswali tuchache, je unajua tunatumia lugha rasmi ngapi ndani ya taifa hili? Hivi sheria zote zilizotungwa kwa lugha ya Kiingereza hapa nchini zinamlenga nani?I fail to understand... post za Lissu ambazo zipo kwenye lugha ya kiingereza zinakua zinamlenga mtanzania ama?? Ukiitwa wakala wa mabeberu utalalamika?
Katika katiba yetu, ziko lugha mbili zimetumika ambazo ni Kiingereza na Kiswahili, je unajua kunapotokea mkanganyiko katika kutafsiri Katiba, tafsiri ipi inatumika kuondoa huo mkanganyiko?
Na je unajua kuwa hiyo lugha ya Kiingereza inayotumika inawalenga Watanzania na si viumbe kutoka sayari ya Mars? Someni vijana, msikumbatie ujinga mkaamini mnajua kumbe hamjui chochote.