Tundu Lissu ameongea na Radio Citizen Kenya asubuhi ya leo, ameleezea hali ya usalama nchini pamoja na suala la Corona

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,693
218,211
Jambo Kenya ( 620 X 640 ).jpg

Hii ndio taarifa mpya inayozagaa mitandaoni kwa sasa.

wote mnakaribishwa

===



Mgombea wa Urais, kupitia Chama cha Upinzania CHADEMA Tundu Lissu, alivyohojiwa na Citizen Online Radio Station, kutoka Nairobi Kenyan Tundu Lissu aongea mengi kuhusu mustakabali wa Tanzania, ambae anagombania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 28 Oktoba, 2020

Katika mahojiano hayo Waandishi wa habari Vicent Ateya na Meody Sinzore wa kipindi cha Jambo Kenya wamemuuliza masuala mbalimbali ya Kinchi na uchaguzi kwa ujumla.

Wakiuliza kuhusu suala la usalama kwa wagombea wa Upinzani Tundu Lissu amesema "Kama ambavyo nimesema mara nyingi hali ya nchi ya Tanzania sio suala lenye afya hata kidogo. Ukizungumzia sisi wa Chadema, viongozi wetu, wanachama wetu wameuawa katika mazingira ambayo hakuna uchunguzi wa Polisi hakuna chochote kilichofanyika."

"Kuna watu wetu wametekwa nyara miaka zaidi ya miwili mwandishi wa habari Azory Gwanda alichukuliwa nyumbani kwake na hajilikani alipo". Ben Saanane hajulikani alipo tangu Novemba 2016. Watu wameumizwa sana. Mimi nimeponea chupuchupu nimepigwa risasi 16. Mwenyekiti wangu amevunjwa mguu kama mwezi mmoja na ushehe uliopita, hali imekuwa mbaya kwelikweli.

Kwahiyo tunapozungumza kuwa Tanzania ina hali mbaya tuna maana hiyo. Hali ya haki z binadamu imeporomoka sana. Sio sisi tu tunaolalamika bali hata mashirika ya haki za binadamu ya nchini na kimataifa yanasema hivyo hivyo.

Sasa tunakwenda katika uchaguzi Mkuu ambao utakuwa ni wa kihistoria. Rais Magufuli na Chama chake wamesemahadharani bungeni kwamba wakishinda watabadilisha katiba kuondoa ukomo wa madaraka. Maana yake ni kwamba tutakuwa na Rais wa Maisha. Sasa sisi ambao Mwalim Nyerere alisema hatuwezi kuwa na Rais wa Maisha kama ilivyokuwa kwa kiongozi wa Malawi Kamuzu Banda, atuwezi tukakubali kurudi kwenye utawala wa aina hiyo.

Rais Magufuli mwenyewe alitangaza tarehe Febuali 6,2016 kwamba anataka kuangamiza vyama vya upinzani ifikiapo mwaka 2020. Sisi hatutokubali kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja. Uchaguzi huu utaamua mambo mengi sana katika nchi yetu na tunaamini kwamba watanzania hawatamkubalia Magufuli na ajenda yake na Chama chake ya kuturudisha katika miaka ya giza ya utawala wa chama kimoja.

Aidha, wakimhoji jitihada za Tanzania katika kukabili Covid 19 Lissu ameeleza kuwa Majirani zetu wote wana Corona, Tanzania ukitangaza kuwa kuna Corona ni kosa la jinai. Katika hili Lissu amesema "Sasa serikali inayoamini kwamba hakuna Corona na inawatangazia watu hakuna Corona haijatoa taarifa yoyote ya maambukizi, ya waliofariki, ya waliopona tangu tarehe 29 mwezi wa nne mwaka huu, wanaamini kwamba tukinyamaza basi Corona itapotea. Tusiposema chochote kuhusu Corona maana yake Corona hamna. Huo ndio msimamo wa serikali yetu.

Mwisho, Tundu Lissu amewashukuru Redio hiyo ya Kenya kwa kumhoji na kuweka bayana kuwa tangu amefika nchini mpaka leo hakuna kituo chochote cha habari kilichomwita na kumhoji kwa sababu viombo hivyo vinaogopa kuzuiliwa.
 
Fursa zote kama kiongozi mtarajiwa wa nchi lazima ziwe explored.

Hii ina maana nchi majirani, nchi za kanda kama SADC, COMESA, AU - UMOJA WA AFRIKA na wadau wengine wa maendeleo lazima kuwa karibu nao kupunguza tofauti na pia kutengeneza fursa kwa Tanzania na waTanzania.

Hatuwezi kujifungia, Tanzania inaihitaji dunia kuliko dunia inavyoihitaji Tanzania hivyo lazima kuwa na mikakati ya ki-geopolitics kujenga ushawishi na kutafuta blocks za nchi zinazofanana nasi ili kuweza ku negotiate treaties, multilateral negotiaions n.k kwa kifupi kuwa na diplomasia-ya-kiuchumi imara kwa manufaa ya raia wa Tanzania na nchi kwa ujumla.

Heko kwa kamanda Tundu Lissu na CHADEMA kwa kuifungulia milango Tanzania iliyokuwa imejitenga na kukosa fursa kibao katika ulimwengu huu ambao umekuwa kijiji yaani mfumo wa Globalization.

Huwezi kujua ushindani au mapungufu ya nchi fulani kama hatutakuwa na diplomasi- ya-kiuchumi itakayo inyanyua Tanzania irudi katika nafasi yake husika kimataifa.
The quotation is from Otto von Bismarck, first Chancellor of Germany : There are no permanent enemies, and no permanent friends , only permanent interests Otto von Bismarck
https://www.forbes.com › quotes
This is quite a game, politics. There... William Clay - Forbes ...

This is quite a game, politics. There are no permanent enemies, and no permanent friends , only permanent interests
 
Awe makini kuhusu maswali ya mtego kuhusu Korona.

Wakenya wanataka kumtumia Lissu kipropaganda kuhusu ishu ya Korona ili ionekane sisi Watanzania tumefanya ujinga tulivyopambana na Korona halafu wao Wakenya eti wamefanya vyema na malockdown yao.

Lissu akumbuke tu wapiga kura wake watarajiwa yaani Watanzania wanamuunga mkono sana Magufuli kwenye ishu ya kutoweka lockdown, kwa hiyo asiwape Wakenya wanachotaka yaani "endorsement" kutoka ndani ya Tanzania kwa jinsi wao walivyodeal na Korona. Maana sasa hivi ndani ya Kenya kuna public pressure ya kutaka Kenya ifanye kama Tanzania!

Swali la Korona inabidi Lissu alijibu kisiasa, ila akijaribu kuiponda approach ya Magufuli alivyohandle hilo suala atapoteza uungwaji mkono nchini. Magufuli alifanikiwa kuvurugavuruga vyanzo vya taarifa rasmi kuhusu Korona, kisha akapiga propaganda kubwa sana kuwa tumeidhibiti Korona kiasi kwamba sehemu kubwa ya umma inakubaliana naye. Kwa hiyo inahitaji akili ya ziada kucrash sehemu kubwa ya approach ya Magufuli katika mapambano dhidi ya Korona.
 
Yaani mie huyu simuelewi kabisa, hivi wapiga kula wake wako kenya?, Watanzania wangapi wana access na hizo radio za kenya!
Kwamba hujui sababu au ni kujitoa ufahamu? Kama dola imevipiga mkwara vyombo vya habari vya hapa nyumbani afanyeje?

Vyombo vya habari vya nyumbani, kwa sasa hata mahojiano ya DW, BBC AL Jazeera na VOA yanayomhusu Lissu wanakata na kuweka kwaya au matangazo ya biashara.

Yana mwisho lakini
 
Awe makini kuhusu maswali ya mtego kuhusu Korona.

Wakenya wanataka kumtumia Lissu kipropaganda kuhusu ishu ya Korona ili ionekane sisi watanzania tumefanya ujinga tulivyopambana na Korona halafu wao Wakenya eti wamefanya vyema na malockdown yao.
Ataingia tu mtego wa nyang'au; manaake jamaa alivyo limbukeni anajisifia kuwa ana damu ya wakenya, duh.
 
Awe makini kuhusu maswali ya mtego kuhusu Korona.

Wakenya wanataka kumtumia Lissu kipropaganda kuhusu ishu ya Korona ili ionekane sisi watanzania tumefanya ujinga tulivyopambana na Korona halafu wao Wakenya eti wamefanya vyema na malockdown yao...

Wakati wa Kampeni bado haujafika kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi na katazo alilotoa Mh. John Magufuli kuwa ni marufuku kufanya siasa mpaka siku za kampeni zitakapoanza baada ya August 25 2020.

Wana wa mtaa wa Lumumba muwe na subra .
 
Basi kama ninawaona wajumbe flani wana-jam frequency za redio husika kwenye eneo la Tanza ya wenye nia.

Watanza we nye nia wengi hawana uwezo wa kumiliki ving'amuzi vya digital vyenye redio ambako SITIZENI wanaweza kurusha matangazo yakafika kote Tanza ya Wenye nia.

Kampeni hizi bila redio na TV za ndani ni changamoto sana kwa TL.

Short Wave Frequency broadcasting haina audience siku hizi hasa hapa Tanza ya wenye nia.
 
Wakati wa Kampeni bado haujafika kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi na katazo alilotoa Mh. John Magufuli kuwa ni marufuku kufanya siasa mpaka siku za kampeni zitakapoanza baada ya August 25 2020.

Wana wa mtaa wa Lumumba muwe na subra .
Kampeni bado lakini aliruhusu siasa za majukwani au hadharani ambazo alitoa katazo zamani. Alitoa onyo kusiwe na matusi tu.
 
Lissu na Membe wao wanapiga kampeini za hasira binafsi dhidi ya Magufuli; hilo linajulikana kabisa; siyo kuwa wanashindana na sera za CCM. Sasa awe makini atakapokuwa anatumia vyombo vya nje kumtukana Magufuli kama alivyokuwa anafanya alipokuwa Ulaya. Watangazaji wa Kenya wanaweza kabisa kumwuliza maswali yanayoelekea huko, na akishindwa kuwa makini atajikuta anatoa matusi tena, jambo litakalokuwa inakiuka kanuni za uchaguzi.
 
Huyu anataka kuongoza hii nchi.. huku akikimbilia kutuonyesha hataki kutumia.. vyombo vya habari vya nchini.. huyu angeuza nchi yetu kama angebahatika kuchaguliwa kuwa Rais.

Anaonyesha yupo radhi.. media za nchi za nje ziendelee kuliko za nchini, mpenda mabeberu hajali uchumi wa nchi yetu, wala kusaidia kutengeneza ajira.. kwa sababu kawaona bora Kenyans waendelee, poleni washabiki wake.

Magufuli 💯 Mzalendo
 
John Shibuda - Mtoto wako akiwa 'chokoraa' huwezi lalamika, hujamlea.



Video Source: Watetezi TV

Sheria mbovu ndiyo zinafanya vyombo vya habari kutotaka kuhoji wanasiasa wapinzani na hili ni zao baya la CCM Mpya hivyo lawama zote zibebwe na CCM Mpya, ni wajibu wa viongozi wa dola walio madarakani kulea na kukuza demokrasia. " mwisho wa nukuu.


Sio penye mifarakano ndo tunaanza kukumbuka mambo ya baba wa Taifa kuhusu uzalendo. Hii sheria ni kwa vyama leo vipo kesho havipo..........Why do we create our emperor?

Sheria hii inadhalilisha CCM. Itafika kipindi utaambiwa kuhama dini moja kwenda nyingine lazima ukae mwaka mmoja ndio uoe. Hebu tuuenzi wosia wa Mwl. Nyerere

Je sheria hii ina changisho la historia ya Tanzania. Maana ya Siasa ni rufaa ya sauti ya jamii. Vijana mlio kwenye maamuzi msiwe na mihemko ya kukomoana. Ukoloni mamboleo tunaunda. Huwezi kuwa mwanasiasa bila kupigwa unyago wa elimu ya uraia.

Sijwahi kuona Askofu anawatengenezea sheria za waislamu, na kamwe sijawahi kuona waislamu wakiitengenezea sheria wakristo.... Tunakwenda wapi?

Huu muswada ni haramu huwezi kuondoa uwe halali. Shame upon us! Nyama ya nguruwe uitie viungo gani iwe halali?

Maagano ya Tanganyika na Zanzibar ilikuwa ni vijana wawe na amsha amsha kama Zitto na Polepole na Mnyika.

Tushindanishe busara na hekima zetu. Kila shilingi ina pande mbili. Dhamira ya huu muswada ni nini?

Nguvu ya chama cha siasa ni hisia za umma. Chama cha siasa sio chama cha kutegemea Polisi na msajili.
 
Back
Top Bottom