Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...
Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk
Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.
Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali
Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Ngoja tuwekane sawa katika jambo hili, na tuwe waadilifu.
Hapa nagusia nukta mbili au tatu na nukta ya mwisho itakuwa ni nasaha kwangu na kwenu.
1. Kiimani hasa kwetu sisi Waislamu jambo hili ni jambo baya na limekemewa vikali sana, na kiistilahi tunaita KUOMBOLEZA(Kuomboleza ni miongoni mwa mambo manne ya kijinga,ambayo hayataisha mpaka Kiyama kinasimama). Kiimani tunaamini ya kuwa Mtu ni wa aidha motoni au peponi,na akifa anatakiwa kuzikwa haraka ili akaanze kuishi maisha mapya kaburini, kama mtu wa kheri basi kaburi ni katika bustani miongoni mwa mabustani ya Peponi, na kaburi ni katika mashimo miongoni mwa mashimo ya motoni. Kwahiyo kitendo cha kumchelewesha maiti kumzika ni kuzidi kumpa dhiki na kumtesa kama ni wa motoni, na kama ni wa kheri basi mnamchelewesha kwenda kupata mazuri yake,kama alitoa usia mapema basi mzigo wa madhambi unakiwa ni juu yenu na si juu yake. Hitimisho ni kuwa,ni wajibu wetu na ni jambo jema kuwahisha kumzika maiti,tena huwa bora zaidi kutomsafirisha.
2. Wasia, ni jambo la dharura sana kwa mtu makini, tena ukiacha wasia mzuri juu ya maziko yako yaweje,huwa bora zaidi. Ila si kila wasia hufanyiwa kazi.
3. Hapa lazima tuelezane ukweli, mtoa mada nina hakika hali wa shani (Hii ni dhana ya hakika kabisa, kwayo inahukumu hili, sababu imevuka kiwango cha uzani wa asilimia Hamsini),umeandika uzi huu au haya kwa sababu ya chuki yako juu ya mwenda zake, lakini swali la msingi ni , Je angekuwa amekufa kipenzi chako tena katika wadhifa huo wa mwendazake ungeyaandika haya au na wewe ungekuwa katika kundi la hawa ambao wako dhidi yako na mlengo wako ambao wewe unawaita wapigaji ?
4. Hii ni nasaha ambayo kwayo,nimeigusia hapo awali ya kuwa baada ya kumaliza nukta mbili au tatu inayofata ni nasaha kwangu,kwako mtoa mada na kwa wale wasio kuwa mimi na wewe. Nasema hivi
"Hutosha mtu kuwa MUONGO kusema au kuandika juu ya kila anachokiona au kukisikia". kiasili haya si maneno yangu.
Ziada :
"Hajutii yule aliyekaa kimya kwenye fitina/fitna au kila wa kala."