Aah maisha acha yaendelee.......Baadaye sana ndio unge elewa!
Me mwana chama pia nina bapa moja na nusu nitapigia nyumbani maana bar napo pana msiba!
Huyu ni wale much know.Mkuu huwa najaribu kutaka kujua wewe ni mtu Wa kariba gani nashindwa kukuelewa,una vihoja na vioja vya hapa na pale huku ukijiona wewe ni mjuvi kuwaliko wana jf wote.
Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Mnajitekenya ila ukweli mnaujua.Kuna watu humu wanasema alikuwa anapendwa kwaiyo ni sahihi gharama zote kutumika, kigezo wanachokitumia kupima mtu kupendwa naona ni wingi wa watu wanaomwongelea au mpa sifa
ila niwakumbushe kuwa washangiliaji wa MAN U tz ni wengi kuliko wananachama
Wewe nawe, usimwesabie mwenziyo mabaya.Mungu akiamua ataukipanga ata pangua unaweza uka imagine kabisa mtu anaacha hospital ya taifa muhimbili Anaenda kufia Dispensary ya MZENA !!!!!!!......atakama anateseka nimipango ya Mungu huenda adhabu yake ndo imeanzia hapa kabla kuingia kabrini
Hoja ipi utakayo izungumzia zaidi ya siasa?Wengi wamepotoka sana! Aidha, wengi wanashindwa kuheshimu mawazo tofauti na kushambuliana badala ya kuchambua hoja mbadala. Tunaacha kujadili maudhui na muktadha wa hoja, tunamjadili au kumwelezea mtoa hoja
Au kama vipi wamfanyie mummy kila mtu akijisikia anaenda kumtizama tuKuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...
Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk
Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.
Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali
Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Wazo zuri mkuu au?[emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji848][emoji848][emoji848][emoji2839][emoji2839][emoji2839][emoji2827][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Wengi hawatakuelewa Mshana....ila ukweli ndy huo... msingi ukivurugwa wakati mwingine hata paaa huvurugwa. Kazi Lumumba ni ngumu kuliko vile mtu anaweza fikili. Mambo yamekua si mambo. Mda utasema tusubili...!!Haya ndio majibu kwenye mjadala huu ambao swali hoja kwenye kichwa cha habari halijajibiwa
Iko hivi
Tanzania haijawahi kupata msiba wa kiongozi ngazi ya rais akiwa madarakani tangu uhuru, hivyo ukiachilia mwongozo wa katiba hakuna kingine tujuacho...kwahiyo kwa mara ya kwanza ile practice kwenye vfungu vya katiba ndio inafanyiwa kazi sasa
Hiki kitu kimetokea bila maandalizi ya kutosha(kawaida kifo hakina maandalizi) na hulka ya mwendazake aligeuza mfumo mzima kuufanya ni wake na ndio mwamuzi wa mwisho kwenye kila kitu.. Sasa hapa kuna mambo mengi sana ya kuyaweka sawa, kuna ya lazima na kuna ya muhimu lakini yote yanahitaji muda na muda uliopo hautoshi
Sasa hii ratiba ndefu ya kuaga mwili ni kwa maslahi ya nani? Jibu ni moja tuu... CCM...Ni wakati huu wananchi wakiwa busy na kuaga mwili kwa maelfu huko ndani nyuma ya pazia mambo yanaendelea tena kwa kasi kubwa lakini pia kwa umakini wa aina yake... Wana sacrifice kuuhangaisha mwili ili kudaivate attention ya jamii
CCM inajifahamu position iliyo nayo mbele ya macho ya jamii, IMESHAKATALIWA kitambo.. Uchaguzi huu kama sio wizi mkubwa wa kura ingekuwa Leo hii tunaongea mengine
Sasa ni muhimu sana kupanga timu za ushindi 2025.. Na wakati huo ni sasa, kipindi hiki cha maombolezo...ni katika hili ndio kila timu inajipanga kivyake na kufanya michakato kuwa migumu zaidi
Ni the race against time... Ni kwenye hii kundi lililokabidhiwa msiba linafanya yake pia.. Tutakuja kupeana mrejesho baadae
Huyu marehemu angemuona angeagiza apandishwe cheo
Kiongozi, humo humo kuna wajanja wanapiga mpunga wa maana. Kufa kufaana. Ingekuwa amri yao, kila mkoa angepitishwa.Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...
Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk
Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.
Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali
Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Hoja ipi utakayo izungumzia zaidi ya siasa?
Hili tukio ni la kiroho linasimamiwa kwa misingi ya imani ya Roman Catholic,ambapo kwa wakatoliki si kosa nisha shuhudia misiba mingi tu ya kikaktoliki,inakaa wiki nzima mwili wa marehemu unaletwa nyumbani unaagwa,unapelekwa kanisani unaagwa,unasafirishwa tena unafika ktk mji aliozaliwa unaagwa unapelekwa tena kanisani ktk mji huo unaagwa tena.
Kwa wakatoliki hivi vitu ni kawaida LABDA ULETE SIASA mpaka kwenye vifo kwa ajili ya kutwist agenda ili IENDANE NA MITIZAMO YA KISIASA UPATE CHA KUZUNGUMZA.
Kwa hiyo kama unataka kujenga hoja,jenga hoja ktk misingi inayo liongoza tukio hili na misingi hiyo si mingine bali ni misingi ya imani yake marehemu ya Roman Catholic.
Au sindio?We endelea na maisha hakuna aliekuzuia