Tunataka wawekezaji, mara wanyang'anyeni leseni!

Nchi ilishafanya makosa mengi. Na marekebisho mengine lazima yatapnekana ya kipuuzi kwa wapuuzi. Na yatakuwa na maumivu au gharama. Hata Mh Rais amesema hilo wazi. Kuwa lazima watu wengine (wachache) waumie.

Sasa katika kutafakari hili, ni kujiuliza, mwekezaji tunamhitaji kwa ajili ya nini? Pato la taifa. Pato la taifa kwa ajili ya nini? Kuwaletea watu huduma za kimaendeleo. Huduma hizi ni wazi maji safi na salama na huduma za afya ni vipaumbele. Maji ni uhai. Sasa, kama kitaalam (kama alivyojibu mhandisi wa maji alipoulizwa) akasema kila kitu kiko sawa isipokuwa tu mahali pa kuweka tank la maji kuna mwekezaji!!! Hivi kuna mtu anaelewa adha ya maji kwa baadhi ya maeneo ya nchi hii?? Kuna watu wananyang'anyana maji na mifugo kwenye madimbwi!!! Sasa what is the point ya kuwa na mwekezaji anaingiza pato la taifa kisha watu walioeneo alilipo yeye ndio kikwako kwamba hawapati maji wanataabika na kufa na magonjwa?? Hata kama ni mimi ningefanya alichoamua Mh Rais. Si lazima tubembeleze mwekezaji. Tusitafute huruma. Aondoke, kama kuna gharama zilipwe tu kama kuzilipa watu watapata maji. Tumeshalipishwa mambo mangapi kila siku umeme nchi inalipa 452Mil? Aondoke!! Mwalimu alisema madinu hayaozi.

Nimetumia uhuru wangu kujieleza. Tafadhali niambie ikiwa maji hayapatikani mpaka tu tank liwekwe hapo kwa mwekezaji, wewe ungeshauri nini? Don't take lightly watu wanataabika hili suala la maji ndugu!

Kama ni makosa ni process nzima ya mpaka kuruhusu awekeze hapo, jambo la juzi wakati shida ya maji ina miaka na miaka!

PRIORITY.

Hivi kitaalamu kweli lazima tank la maji likae hapo, hakuna alternative nyingine ya kuweka tank mpaka hapo?? tujadili kiupana zaidi, wataalamu mwisho wao ulikuwa hapo lazima tank likae hapo??,, siamini kama hapo mahala au hilo eneo halina mahala pengine pa kuweka tank ila ni hapo tu siamini kabisa...wataalam wafanye kazi yao na mh ashauriwe vizuri..

Unaweza ukala hasara ya kujitakia na hii ni hasara ya kujitakia kwa kutofanya mambo yetu kitaalamu baadala yake tunarahisisha...
 
Duh tunasafari ndefu sana,..
Hilo eneo ndio penye chanzo cha maji.??
Tumeshindwa kuwa na eneo la kuweka tank
mpaka mahala hapo tu.., wataalam wameshindwa kabisa pakuweka tank?..
Tulimpaje huyo muwekezaji eneo tukijua tutalihit aji?, na tuna kazi nalo??
Gharama zake za exploration na maandaliza ya uchimbaji huku tukiwa tumempa leseni kihalali nani atazilipa???
Tumefikiria kiasi gani cha ajira kitakosekana kwa watu wetu na mapato kwa nchi yatapotea eti kwa sisi kushindwa na kukosa mahala pa kuweka tank la maji mpaka tukafunga shughuli za uchimbaji kweli tank ???

Tujaribu kufikiri kiundani sana katika kutatua matatizo ya wananchi na kuleta shughuli za maendeleo baadala yake hatutoenda mbele,, " eti tumekosa mahala pa kuweka tank la maji na kumyang' anya muwekezaji eneo atakalochimba nickel na sisi kutumia ekari moja tu kwa tank la maji na kuacha ekari nyingi zikiwa iddle.." kuna solution nyingi kiasi cha kuweka tank la maji mahala popote pale..

Kwanini huyo mwekezaji asitumie technology itakayo saidia vyote kwa pamoja?

Hiyo aliyosema Mh. Rais ya kutafuta technology muafaka uliisikia? Basi Nikueleze tu Mh. Rais ame ingiza social costs kwa huyo private investor ili tuwe wote better off...Hiyo safari ya mbali niafadhali iwepo kuliko social distress zilizosababishwa na investor ambao hawajali maslahi mapana ya raia wetu.
 
Hivi kitaalamu kweli lazima tank la maji likae hapo, hakuna alternative nyingine ya kuweka tank mpaka hapo?? tujadili kiupana zaidi, wataalamu mwisho wao ulikuwa hapo lazima tank likae hapo??,, siamini kama hapo mahala au hilo eneo halina mahala pengine pa kuweka tank ila ni hapo tu siamini kabisa...wataalam wafanye kazi yao na mh ashauriwe vizuri..

Unaweza ukala hasara ya kujitakia na hii ni hasara ya kujitakia kwa kutofanya mambo yetu kitaalamu baadala yake tunarahisisha...

Yes. Swali jingine ni kwenye utaalam. Na utaalam wa watu wetu walio wengi umeshaligharim taifa maeneo mengi. Na utaalam mwingine ni wa kudanganya hesabu ili watu kupata faida binafsi na familia zao.

Kinachotakiwa ni hiki;

Utalaam wa kweli + Uzalendo.
 
la msingi uchaguzi ujao ufanywe kwa njia ya kielektroniki na usimamiwe na jumuiya za kimaitafa zikiongozwa na Russian Federation
 
Kwanini huyo mwekezaji asitumie technology itakayo saidia vyote kwa pamoja?

Hiyo aliyosema Mh. Rais ya kutafuta technology muafaka uliisikia? Basi Nikueleze tu Mh. Rais ame ingiza social costs kwa huyo private investor ili tuwe wote better off...Hiyo safari ya mbali niafadhali iwepo kuliko social distress zilizosababishwa na investor ambao hawajali maslahi mapana ya raia wetu.
Itategemea aina ya mkataba muwekezaji aliyoingia na serekali na kama atakua tayari kuwa flexible. Otherwise inaweza kuwa kesi ingine ya mahakama ya kimataifa.
 
Kwanini huyo mwekezaji asitumie technology itakayo saidia vyote kwa pamoja?

Hiyo aliyosema Mh. Rais ya kutafuta technology muafaka uliisikia? Basi Nikueleze tu Mh. Rais ame ingiza social costs kwa huyo private investor ili tuwe wote better off...Hiyo safari ya mbali niafadhali iwepo kuliko social distress zilizosababishwa na investor ambao hawajali maslahi mapana ya raia wetu.

Muwekezaji anapokuja haji kienyeji, anapokuja anapitia hukohuko serikalini na serikali ndio humpa mkataba baada ya kupitia taratibu, pia ukumbuke muwekezaji husimamiwa na serikali kwa kila jambo alifanyalo. Kama ni mkataba usio na tija kwa wananchi basi wa kuraumiwa ni serikali sio muwekezaji, muwekezaji ni mfanya biashara ambaye anatafuta faida na mianya ya kupata faida. Kama mianya tunaitengeneza wenyewe kwa kupokea rushwa unawezaje kumlaumu muwekezaji ambaye si mtanzania???

Rais kama mkuu wa nchi hakutakiwa kuchukua maamuzi ila alitakiwa atoe amri kwa wataalamu kutafuta eneo lingine la tank la maji, pia atoe amri ya kupitia mkataba wa muwekezaji kama upo na kama haupo wataalamu wauandae ili unufaishe wananchi..
 
Kwani lazima tank likae hapo mlimani?,
afterall hilo tank linachukua heka elfu ngapi mpaka wamtoe mwekezaji?,
maana kwa uzoefu hakuna tank la kuzidi robo heka,
hata matank ya nuclear power hayawi makubwa kihivyo
Sasa huyo mwekezaji alikataa kuwekwa tank ili iweje?

Alafu watanzania wengi ni wajinga pamoja na kwenda shule, wawekezaji wa nchi hii huwa wanakuwa kama miungu watu, na tumelalamika kweli, leo ten wanatetewa loh!
 
Humu kuna watu kila siku ni kuwaza siasa za kupinga tu, yani madini ya kwetu mlima wa kwetu wananchi wakose maji kisa mlima kwani hakuna sehemu zingine.
 
Mkuu wawekezaji wengi hukopa kwenye mabenki sasa najiuliza mtu aliyepewa leseni kafanya exploration ina maana huo mkopo ataurudisha vipi naona tunajiweka kwenye hatari kushitakiwa na kulipa pesa nyingi zaidi
Nenda kawasaidie kuli basi, yani inafikia mtanzania unamtetea mgeni badala ya mtanzania mwenzio kisa upinzani? Huu ni upuuzi kabisa.
 
Kuna mtu aliota ati mpaka kipindi cha Mtukufu huyu kiishe tutakuwa tumetengeneza kesi lukuki.
 
Wawekeza chenga, ni bora wananchi wapate maji kuliko mgodi utakaosabisha vifo vya risasi kutokea.
 
Huyo jamaa kalipa fidia ya mabilioni kwa wananchi kuchukua maeneo,kafanya exploration kwa mabilioni ya shilingi,kaweka wafanyakazi,kaagiza mitambo

Tujiandae kulipa fidia ya mabilioni,escrow na IPTL inaikumba nchi,tutalipa fidia GEITA na huko ngasamo na kwingine

Fidia mpaka sasa itafika trilioni kadhaa ikijumuisha loss of profit and business

Pia wakienda mahakamani tutashindwa na kuwafidia na eneo kubaki lao

Hawajapewa hata haki ya kusikilizwa kabla ya kunyanganywa,kesi rahisi sana kuishinda

Unajifanya kuwapenda wananchi halafu unawatwisha zigo la fidia!!!
Huyo jamaa, mwekezaji unayemsema ni nani? Je, ana leseni gani ya uchimbaji madini kuna aina 3) na mashrti ya leseni yake ni yapi? amewekeza nini, na chenye thamani gani katika kilima hicho kinachogombewa? ripoti ya ESIA inasemaje/inatoa ufumbuzi gani kuhusiana na matumizi ya kilima hicho kwa ajili ya kusambaza maji? Kama ripoti ya ESIA haisemi kitu juu ya matumizi ya kilima kwa kusambaza maji katika wilaya nne za mkoa wa Simiyu, kwa nini hivyo? Je cost-benefit analysis (opportunity cost) ya kuchimba nickel au kusambaza maji kwa zaidi ya watu milioni 1.5 (going forward) inatuelekeza kufanyika kitu gani? Kuna maswali mengi ya kiufundi yanayohitaji majibu kabla ya kujiingiza kwenye mijadala ya yenye shutuma na lawama. hapa ni JF, GT.
 
Halafu baadae mnaanza kulalamika na kulaumu madini yenu yanachukuliwa,sijui mnanyonywa ,mara hiki mara kile

Wa Tz wanafki sana
Mkuu mimi sishabikii kwamba madini yachimbwe kiholela, ninachopingana na hao jamaa ni huo utetezi mfu eti wamekosa mahali pa kujenga tanki la kupeleka maji bariadi kisa kwenye kilima cha Ngasamo kuna mwekezaji kapewa kuchimba madini! Ni upumbavuuu wa kiwango cha PhD. Hata kama wanataka kuvunja mkataba na mwekezaji hakukuwa na namna nyingine ya kuvunja huo mkataba? Kwenye huu mkataba tukipelekwa mahakama za usuluhishi wa biashara lazima tutage!
 
Back
Top Bottom