Tunakoelekea ni kubaya, vikundi vya uasi vinakiri kuhusika na mauaji ya mwenyekiti wa CCM na polisi, hii sio tamaduni yetu watanzania, this must stop

Tunakoelekea ni kubaya, vikundi vya uasi vinakiri kuhusika na mauaji ya mwenyekiti wa CCM na polisi, hii sio tamaduni yetu watanzania, this must stop

Kama unatumia mitandao nadhani umewaona TFF (Tanganyika freedom fighters) wanakiri kuhusika na kumkata kata mapanga mwenyekiti wa CCM kijiji cha mkoani Mbeya na kumshambulia polisi hadi kifo.

Sikuwahi kufikiria hata siku moja tutafikia huku na cha kushangaza nimesoma baadhi ya comments wakifurahia huo ukatili na kuonyesha utayari wa kuwa sehemu ya hao TFF.

Haya sio mambo ya kubeza hata kidogo, kwa sasa yanaweza kuonekana kama cheche lakini yakianza kushika moto this will be dangerous, very dangerous,
Wanaobeza wana kosa gani?
Don't you know that ccm is the root cause??
 
Kiuchumi na kijamii na wao serikali si inapoteza au kuchafuka, watalii na wawekezaji watajua nchini hakuna usalama kutisha na hata raia watajawa na sitofahamu mwisho siku hawafanyi kazi zao Kwa urahisi na uhuru....
Refer mauaji kishirikina ya albino na kukata watu koromeo Kwa Ajili Uchaguzi mkuu, hasa Kanda ziwa kule, nilikuwepo mkoa moja kule, Kwa hofu ya kukatwa koromeo, mwisho saa12 jioni wananchi umejifungia ndani kwako, sasa hapo tutafanya biashara Gani ya maana, watu wakijua wanaishi Kwa kuviziwa wauwe kisa wao ni Ccm au Chadema, so na hao serikali wanaoleta hizo propaganda waangalie upande pili shilingi.
Serikali chafu zote duniani, haziogopi chochote na hawajali usalama Wala uhai wa watu wao zaidi ya kutunga mbinu za kubaki madarakani.

Unakumbuka Lowasa alivyotukanwa anajinyea, kisha akarudi wakampokea. Walimchafua kisha wakampokea.

Hivi vyama vya siasa wakati vinaanzishwa 1992 vilipandikizwa.

Hakuna vyama makini hapo. Wote ni TISS kasoro Lissu anayeishi kwa muujiza wa MUNGU.

Siiamini hata kwa bahati mbaya hiyo TFF feki. Watawavuta watu kisha watawachoma wakamatwe.

Shida kubwa ya Mwafrica ni uroho wa maliasili na kukosa utashi wa maendeleo kwa watu wake.
 
Back
Top Bottom