Man,Hee! Kumbe nawe akili kama zake au ndio mwenyewe?
Unashindwa kujua kuwa Bunge ndio chombo kikuu cha maamuzi?
Ni wajinga tuu wasio jua hilo ndio maana wanaweza kupeleka wawakilishi kama Msukuma au Kibajaji. Hawajui nguvu ya bunge wakidhani ni kupiga makofi tuu
Nadhani umesahau jinsi katiba yetu ilivyompa rais MAGUVU yasiyopimika!!
Na hata hilo bunge wala sio chombo kikuu cha maamuzi...
Ibara ya 4 inataja VYOMBO VITATU vilivyopewa MAMLAKA ya kutekeleza shughuli za NCHI, navyo ni:-
1. SERIKALI... hii imepewa MAMLAKA YA UTENDAJI,
2. BUNGE... Hili limepewa MAMLAKA ya KUTUNGA SHERIA NA KUSIMAMIA UTEKELEZAJI wa shughuli za umma.
3. MAHAKAMA... Hii imepewa MAMLAKA YA KUTEKELEZA utoaji haki.
Kwahiyo Bunge ni CHOMBO KIKUU cha Kutunga Sheria na Kusimamia Utekelezaji wa Shughuli za Umma!!
Na ndo maana katika huko kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma, ndipo unakuta kuna kamati kadhaa zinazoenda kwenye taasisi kadhaa za serikali kwa gia ya kusimamia utekelezaji wa shughuli za umama lakini wanaishia kugawana posho tu na kuhongwa ili wafiche uozo wanaokuta huko!
Ushawahi kusikia Kamati X imetinga Ikulu kuhoji hili na lile?!
Sasa kutokana na mamlaka ya kila chombo kama ilivyokuwa summarized hapo juu, ndipo inakuja dhana ya MIHIMILI MITATU ya nchi ambayo haipaswi kuingiliana wakati wa kutekeleza mamlaka zao walizopewa na Ibara ya 4(2)!
Kwamba, sawa kiongozi wa serikali ni RAIS! TAASISI YA URAISI inaweza kuwa imejaa MAGWIJI TUPU WA SHERIA, tena waliobobea huku Rais mwenyewe akiwa Harvard Graduate wa LLB, LLM na PhD in Law!!
Lakini pamoja na kuwa na MANGULI WA SHERIA, bado HAMUWEZI kukutana Ikulu na kuanza Kutunga Sheria hata kama uwezo huo mnao kwa sababu MAMLAKA ya Kutunga Sheria ipo mikononi mwa Bunge!
Wewe Rais, na Serikali yako iliyojaa MAGWIJI WA SHERIA kazi yenu inatakiwa kubaki kwenye UTENDAJI, kwa sababu hayo ndiyo MAMLAKA mliyopewa na katiba!!
HALI KADHALIKA, nanyi Bunge, Wabunge wenu WOTE wanaweza kuwa MAHAKIMU NA MAJAJI WASTAAFU na pia MAWAKILI NGULI kama Tundu Lissu kiasi kwamba, mnaweza KUTUNGA SHERIA wenyewe na kisha mkakaa wenyewe kama Mahakimu na Mawakili ili kuanza kuhukumu watu...
CONGRATULATION kwa kuwa na Bunge with such Strong Legal Background but please, hamna MAMLAKA ya kutoa haki kwa sababu Mamlaka hayo yapo invested kwa Mahakama, hata kama Mahakimu wote wamesoma Agriculture and Agronomy, lakini ndo hao waliopewa MAMLAKA kutoa haki!
Ibara ya 4(2) yenyewe inasema:-
Tena ona sasa...Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki vitakuwa ni Idara ya Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Idara ya Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Wabunge huko bungeni tukananeni, tuonaneni macho na meno ili kuhakikisha sheria fulani inapita lakini bado sheria hiyo hiyo haiwi sheria hadi upite mkono wa Rais ambae si ajabu ndo kwanza alikuwa anasuka wakati mnatoana meno! WHY? Kwa sababu Ibara ya 62(1) inasema Bunge litakuwa na sehemu 2, ambayo ni Wabunge na Rais!!
Na 62(3) inasema endapo jambo LOLOTE kinahitaji kuamuliwa na pande 2 basi HALITAHESABIKA kwamba limeamuliwa au kutekelezwa ipasavyo hadi Wabunge na Rais WOTE wamehusika kwenye maamuzi/utekelezaji wa suala husika!
Lakini pamoja na mgawanyo huo wa madaraka, mwishowe kwenye Ibara ya 33(2) wanapigilia msumali kwamba:-
REMEMBER, tulivyotaja hapo juu ni VYOMBO vilivyopewa MAMLAKA YA KUTEKELEZA shughuli za nchi, ambayo mkuu wake ni Rais! Kwani tunaposema Rais amepewa MAGUVU MAKUBWA MNO unadhani msingi wake ni upi?! Of course, kwa mfano Rais HANA MAMLAKA ya moja kwa moja ya KUMFUTA KAZI JAJI hata kama amemteua mwenyewe!Rais atakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.
Lakini MABAVU aliyokuwa nayo Rais, anaweza kumwita Jaji Ofisini, na AKAMLAZIMISHA ajiuzulu na JAJI akaishia kujiuzulu lakini akitoka nje atasema amestaafu kutokana na hili au lile, huku msingiziwaji wa kwanza akiwa "ugonjwa"!
Halafu ngoja... unajua mimi sio mbunge, na nilishaacha mambo ya kufuatilia bunge kwahiyo hata taratibu zao wala sifahamu ! Labda wewe Chakaza, au Mkongwe JokaKuu, kama sio ndugu yangu MALCOM LUMUMBA, au hata Mwanahabari Nguli, msomi wa sheria Ndugu Pascal Mayalla...
Naombeni mnitoe tongotongo kwenye hii FLAG ya MAMLAKA ya Bunge Kutunga Sheria!!
Hivi hawa jamaa huwa wanatunga Sheria kweli au huwa wanajadili na ku-endorse Sheria ZILIZOTUNGWA na Serikali?! Kila nikijaribu kupima ni miswada mingapi kutoka serikalini HUKATALIWA bungeni, na mingapi HUKUBALIWA, nabaki kujiuliza hivi ni nani hasa anayeweza kujigamba kwamba ndie mwenye MAMLAKA ya kutunga Sheria...
Mchakato unakuaje? Au first drafts huwa zinaanzia na brainstorming ya kamati husika za bunge?