Watumishi wa CHADEMA, BILLICANAS wanalipwaje?
Sasa unaanza matusi, Hapo ni wafanyakazi wa umma tu ndo wanaface maisha magumu tanzania, wengine hapana. teh teh teh
Watumishi wa CHADEMA, BILLICANAS wanalipwaje?
Naomba tumsamehe huyu jamaa. Inaonekana bado anaishi enzi za "Zidumu fikra sahihi za mwenyekiti wa ....."!!! Hivi kama ingewezekana, wana CCM wenyewe wangeweza kusema hivyo sasa hivi? Kwani hata fikra zenyewe sizioni, ukiachia mbali hilo suala la usahihi.
Mkuu Masoud, Upo right kabisa, heshima kitu cha bure...baadhi ya watu hawana heshima au malezi mazuri, huwezi kumuongelea Mkuu wa nchi kama unaongea na walevi BILICANAS. Licha ya kuwa tunatofautina na wenzetu wa chama tawala, haimaanishi kuwa tuwakosee heshima pale wao tunapohisi wamefanya hivyo, zaidi ya sisi kuonyesha uungwana wetu kwa watu tukausuta ujinga na uongo wao, viongozi wazuri wa upinzani siku zote huwa kama "mbwa wa kipofu", kuelekeza njia sahihi kwa bwana wake na kuokota alichoangusha. Alichotakiwa kufanya Mbowe si kutoa maneno ya kilevi "eti aondoke ikulu", huu wazimu. Angewaambia wafanyakazi na wananchi wamuondoe ikulu Kikwete maana wao ndo waliomuweka eti!
Hapo anaji kwepa mwenyewe kwa kuwataja senior public officers....The source aionyeshe..! Analeta ujanja ujanja wa maneno ili aonekane yeye ni mwema sana.!!
JuniusMkuu Masoud, Upo right kabisa, heshima kitu cha bure...baadhi ya watu hawana heshima au malezi mazuri, huwezi kumuongelea Mkuu wa nchi kama unaongea na walevi BILICANAS. Licha ya kuwa tunatofautina na wenzetu wa chama tawala, haimaanishi kuwa tuwakosee heshima pale wao tunapohisi wamefanya hivyo, zaidi ya sisi kuonyesha uungwana wetu kwa watu tukausuta ujinga na uongo wao, viongozi wazuri wa upinzani siku zote huwa kama "mbwa wa kipofu", kuelekeza njia sahihi kwa bwana wake na kuokota alichoangusha. Alichotakiwa kufanya Mbowe si kutoa maneno ya kilevi "eti aondoke ikulu", huu wazimu. Angewaambia wafanyakazi na wananchi wamuondoe ikulu Kikwete maana wao ndo waliomuweka eti!
Mzee mwanakijiji inaonesha unataka kisa/mkasa na rais.
Unajuwaje kama TUCTA wamemchagua Kikwete?Mkuu wa nchi ana haki ya kutukana waliomchagua?
Sasa hata kama hawakumchagua,lakini yeye ni Rais wao! so,alistahili kuwatukana?Unajuwaje kama TUCTA wamemchagua Kikwete?
Wapi "wananchi" wametukanwa na Kikwete?
Kuwaambia ukweli kuwa wanawapotosha wafuasi wao kwa kuwa mazungumzo kati yao na serikali hayajafikia mwisho, na kuwa hakukuwa na haja ya kufanya mgomo,alikosea? acheni ushabiki...ukweli siku zote uwe ukweli tu.
Very good answer, kuna watu wanaona bila CCM hawawezi kuishi, hawawezi kupata kazi, watoto wao hawawezi kwenda shule hawana mawazo mbadala, hufikiri watu wote tuko hivyo wanatushangaa sana wanapotuona tuko tofauti kabisa na wao, wanajiuliza tunawezaje kuishi bila CCM? kwa hiyo hawawezi kuisema vibaya CCM au kusema mabaya ya rais hata kama wanaona wazi anakosea, watajikomba waonekane wema kwa heshima ya woga, mimi naona huo ni utumwa wa kifikra na utumwa wa kifikra ni mbaya zaidi kuliko ule wa wakoloni maana unashambulia nafsi, nashukuru Mungu kuniepusha kwa hilo, na sometimes usikute mimi ninayemkosoa rais nafaidika na CCM kuliko yeye anayejikomba, if you cannot express your own views you are as dead as a slave one.mimi si mmojawao wanaomuona Rais kama mfalme wao au baba yao!
Jana mwenyekiti wa CHADEMA bwana Freeman Mbowe alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Wasso huko Ngorongoro alimtaka raisi Jakaya Mrisho Kikwete ajiuzulu na kuondoka Ikulu mara moja. Kisa kushindwa kuwalipa wafanyakazi kiwango cha chini cha sh.315,000!
Kila siku za uchaguzi zinavyokaribia yaonesha watanzania wanazidi kukosa heshima kwa raisi wao. Kumfukuza rais aliyechaguliwa namna hii pia ni kuwakosea heshima mamilioni ya watanzania waliomchagua.
Sababu za kushindwa kuwalipa kazieleza na nyinyi mwawajua wanaofilisi uchumi wa nchi, mbona makucha yenu hamjayakunjua kiasi hicho kwao.
Rais wetu akicheka mwanuna na akinuna kwenu ni nongwa. Nyinyii!