Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,231
- 9,677
Ndugu zangu Mh Rais mama Samia suluhu Hassani Ni mwanadamu mwenye damu na moyo na mwili wa nyama Kama Tulivyo sisi wengine.
Nikawaida kuona hata watumishi wa umma ikikaribia wikend wanafurahi ili wapate muda wa kupumzisha akili na hata kupata muda wa kukaa na Familia zao, kutokanaa na kazi za wiki nzima zinazowaweka bize na mbali na familia zao.
Ndugu zangu pamoja na kuwa mh Rais wetu Ni mwanadamu, Mama mwenye familia lakini ameamua kutumia nguvu zake zote na muda wake wote kututumikia watanzania kwa utumishi ulio tukuka.
Hana muda wakupumzika, Familia yake kwa Sasa Ni watanzania, watoto wake kwa Sasa Ni watanzania, wajukuu zake kwa Sasa Ni watanzania, Mawazo yake kwa Sasa yapo kwa watanzania tu.
Muda wote ukisikiliza vyombo vya habari au kupita vibanda umiza na kuchungulia TV unaona mh Rais wetu yupo kugusa maisha ya watu, yupo kutatua matatizo na kero, yupo kuzindua miradi ya maendeleo, yupo kutoa matumaini kwa waliokata tamaa, yupo kutoa majibu kwa maswali ya wananchi, yupo kutoa maelekezo kwa watendaji wake, yupo kuhoji juu ya matumizi ya Fedha za umma, yupo kuunganisha watu, yupo kuleta umoja kwa watumishi ili wawatumikie watu bila kiburi Wala majivuno, yupo kuwakumbusha watumishi kuwa vyeo Ni dhamana.
Ni mama kwa maama ya mama kweli kwelii, mlezi Bora ambaye anahitaji kuona Familia yake hii ya watanzania inaboreka siku Hadi siku.
Amedhamilia kuijenga Tanzania iliyo Bora ambayo kila mtu atafaidika na matunda yake, Anataka kuona keki ya Taifa inamfikia kila mtu, Hataki kuona Kuna watu au kundi linabaki nyuma na kujiona kutengwa, anataka kila mtu ajisikie fahari kuzaliwa katika nchi hii.
Anataka kuona mtu akienda hospitali anahudumiwa bila ubaguzi au Hali yake ya kiuchumi, Anataka kuona mwanafunzi aliyemaliza kidato Cha nne au sita anaendelea mbele bila kukwama au kukwamishwa na uchumi wa nyumbani, Ndio maana unaona ameweka Elimu bure Hadi kidato Cha sita na kuongeza bajeti katik Elimu ili wengi wapate mikopo vyuo vikuu.
Ndugu zangu kwa kazi hii kubwa aifanyayo mh Rais wetu tuna kila sababu ya Kuendelea kumtia moyo mh Rais wetu, Tuendelee kumwombea Rais wetu ili mwenyezi Mungu aendelee kumlinda na kumpigania wakati wote.
Uongozi unatoka kwa mungu, hivyo kwa wale wasaidizi wa mh Rais na watendaji wote mliobahatika kupata Nafasi ya kuwa serikalini, Nawaombeni mfanye kazi kwa uadilifu na weledi kuwatumikia watanzania, sisi watanzania hasa sisi vijana tunawategemea Sana mtusaidie.
Muwe wanyenyekevu wenye busara hekima na upendo kwetu, mtangulizeni mwenyezi Mungu katika kazi zenu, Tendeni haki kwa wote Kama anavyo sisitiza Rais wetu, Fanyeni kazi kwa bidii na kujituma kwa kuacha Alama njema hata Kama mtahamishwa kesho au kustaafu.
Ni Bora jina jema kuliko Mali nyingi, hivyo jengeni majina mema kwa kufanya kazi vyema kwa kugusa maisha ya watanzania.
Mimi Lucas Mwashambwa ninaungana na mamillion ya watanzania kumuombea mh Rais wetu katika majukumu yake ya Urais.
Nikawaida kuona hata watumishi wa umma ikikaribia wikend wanafurahi ili wapate muda wa kupumzisha akili na hata kupata muda wa kukaa na Familia zao, kutokanaa na kazi za wiki nzima zinazowaweka bize na mbali na familia zao.
Ndugu zangu pamoja na kuwa mh Rais wetu Ni mwanadamu, Mama mwenye familia lakini ameamua kutumia nguvu zake zote na muda wake wote kututumikia watanzania kwa utumishi ulio tukuka.
Hana muda wakupumzika, Familia yake kwa Sasa Ni watanzania, watoto wake kwa Sasa Ni watanzania, wajukuu zake kwa Sasa Ni watanzania, Mawazo yake kwa Sasa yapo kwa watanzania tu.
Muda wote ukisikiliza vyombo vya habari au kupita vibanda umiza na kuchungulia TV unaona mh Rais wetu yupo kugusa maisha ya watu, yupo kutatua matatizo na kero, yupo kuzindua miradi ya maendeleo, yupo kutoa matumaini kwa waliokata tamaa, yupo kutoa majibu kwa maswali ya wananchi, yupo kutoa maelekezo kwa watendaji wake, yupo kuhoji juu ya matumizi ya Fedha za umma, yupo kuunganisha watu, yupo kuleta umoja kwa watumishi ili wawatumikie watu bila kiburi Wala majivuno, yupo kuwakumbusha watumishi kuwa vyeo Ni dhamana.
Ni mama kwa maama ya mama kweli kwelii, mlezi Bora ambaye anahitaji kuona Familia yake hii ya watanzania inaboreka siku Hadi siku.
Amedhamilia kuijenga Tanzania iliyo Bora ambayo kila mtu atafaidika na matunda yake, Anataka kuona keki ya Taifa inamfikia kila mtu, Hataki kuona Kuna watu au kundi linabaki nyuma na kujiona kutengwa, anataka kila mtu ajisikie fahari kuzaliwa katika nchi hii.
Anataka kuona mtu akienda hospitali anahudumiwa bila ubaguzi au Hali yake ya kiuchumi, Anataka kuona mwanafunzi aliyemaliza kidato Cha nne au sita anaendelea mbele bila kukwama au kukwamishwa na uchumi wa nyumbani, Ndio maana unaona ameweka Elimu bure Hadi kidato Cha sita na kuongeza bajeti katik Elimu ili wengi wapate mikopo vyuo vikuu.
Ndugu zangu kwa kazi hii kubwa aifanyayo mh Rais wetu tuna kila sababu ya Kuendelea kumtia moyo mh Rais wetu, Tuendelee kumwombea Rais wetu ili mwenyezi Mungu aendelee kumlinda na kumpigania wakati wote.
Uongozi unatoka kwa mungu, hivyo kwa wale wasaidizi wa mh Rais na watendaji wote mliobahatika kupata Nafasi ya kuwa serikalini, Nawaombeni mfanye kazi kwa uadilifu na weledi kuwatumikia watanzania, sisi watanzania hasa sisi vijana tunawategemea Sana mtusaidie.
Muwe wanyenyekevu wenye busara hekima na upendo kwetu, mtangulizeni mwenyezi Mungu katika kazi zenu, Tendeni haki kwa wote Kama anavyo sisitiza Rais wetu, Fanyeni kazi kwa bidii na kujituma kwa kuacha Alama njema hata Kama mtahamishwa kesho au kustaafu.
Ni Bora jina jema kuliko Mali nyingi, hivyo jengeni majina mema kwa kufanya kazi vyema kwa kugusa maisha ya watanzania.
Mimi Lucas Mwashambwa ninaungana na mamillion ya watanzania kumuombea mh Rais wetu katika majukumu yake ya Urais.