Tumia Nguvu zako kupata Pesa

Kasomi

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
11,036
20,337
SAFARI YA KUTAFUTA PESA.

TUMIA NGUVU ZAKO KUPATA PESA.

Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, walisema wahenga.

Kubagua kazi ni kauli za wasio na maono.

Kuishi bila kazi na kuridhika kuwa duniani bila kujishughulisha na chochote wakati Mungu amekupa Uhai, akili, na afya njema UNAKUWA MZIGO KWA TAIFA.

Katika sehemu ya tano tuliona jinsi ya kutumia akili kuzalisha mawazo makubwa yanayoweza kumpa mtu pesa.

Katika sehemu ya sita nakukumbusha kwamba

Kuna siraha kuu 3 zinazoweza kukupatia pesa

1.Akili 2.Mikono 3.Mazingira.

Katika kipengele cha mikono nataka leo ujiulize swali hili

Je unaweza kufanya nini?

Kama unaweza kulima, LIMA upate pesa

Kama unaweza kubeba mizigo BEBA upate pesa

Kama unaweza kubeba tofali kwa mafundi au kuchanganya zege CHANGANYA upate pesa.

Kama unaweza kuchimba mitaro CHIMBA upate pesa.

Kwenye kitabu cha THE SCHOOL OF MONEY Mwandishi anasema kwamba Pesa zimejificha kwenye matatizo.

Hivyo basi ili upate pesa kwa kutumia nguvu zako ni muhimu kujiuliza kwamba

Je unaweza kutatua tatizo gani ili upate pesa?

Jijini Dar es salaam mvua ikinyesha daraja likabomoka kwenye mtaro au kijito fulani

Watu wanajitolea kutengeneza daraja la muda mfupi, au wakati mwingine wanapanga tofali kisha wanaweka kitambaa kwa mbele kidogo

Ukitaka kupita kwenye matofali waliyopanga kwa kuwa hutaki kulowa, ni LAZIMA utoe pesa.

Hivyo ndivyo maisha yalivyo, ukitatua matatizo ya watu, HAKIKA watakupatia pesa.

Tumia nguvu ulizonazo, kama mtaji wa kupata unachokitafuta.
 
Huyo mwandishi anayesema pesa zimejificha kwenye matatizo ni mpuuzi mkuu!

Pesa imejificha kwenye anasa na starehe tu. Unless anamanisha anasa na starehe ndiyo matatizo
 
Huyo mwandishi anayesema pesa zimejificha kwenye matatizo ni mpuuzi mkuu!

Pesa imejificha kwenye anasa na starehe tu. Unless anamanisha anasa na starehe ndiyo matatizo
Hata hayo ni matatizo pia
 
SAFARI YA KUTAFUTA PESA.

TUMIA NGUVU ZAKO KUPATA PESA.

Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, walisema wahenga.

Kubagua kazi ni kauli za wasio na maono.

Kuishi bila kazi na kuridhika kuwa duniani bila kujishughulisha na chochote wakati Mungu amekupa Uhai, akili, na afya njema UNAKUWA MZIGO KWA TAIFA.

Katika sehemu ya tano tuliona jinsi ya kutumia akili kuzalisha mawazo makubwa yanayoweza kumpa mtu pesa.

Katika sehemu ya sita nakukumbusha kwamba

Kuna siraha kuu 3 zinazoweza kukupatia pesa

1.Akili 2.Mikono 3.Mazingira.

Katika kipengele cha mikono nataka leo ujiulize swali hili

Je unaweza kufanya nini?

Kama unaweza kulima, LIMA upate pesa

Kama unaweza kubeba mizigo BEBA upate pesa

Kama unaweza kubeba tofali kwa mafundi au kuchanganya zege CHANGANYA upate pesa.

Kama unaweza kuchimba mitaro CHIMBA upate pesa.

Kwenye kitabu cha THE SCHOOL OF MONEY Mwandishi anasema kwamba Pesa zimejificha kwenye matatizo.

Hivyo basi ili upate pesa kwa kutumia nguvu zako ni muhimu kujiuliza kwamba

Je unaweza kutatua tatizo gani ili upate pesa?

Jijini Dar es salaam mvua ikinyesha daraja likabomoka kwenye mtaro au kijito fulani

Watu wanajitolea kutengeneza daraja la muda mfupi, au wakati mwingine wanapanga tofali kisha wanaweka kitambaa kwa mbele kidogo

Ukitaka kupita kwenye matofali waliyopanga kwa kuwa hutaki kulowa, ni LAZIMA utoe pesa.

Hivyo ndivyo maisha yalivyo, ukitatua matatizo ya watu, HAKIKA watakupatia pesa.

Tumia nguvu ulizonazo, kama mtaji wa kupata unachokitafuta.
Wewe unatumia nn kupata pesa???
 
Huyo mwandishi anayesema pesa zimejificha kwenye matatizo ni mpuuzi mkuu!

Pesa imejificha kwenye anasa na starehe tu. Unless anamanisha anasa na starehe ndiyo matatizo
Hujui kama hujui, na bado hutaki kujifunza. Ukiweza kutatua changamoto na matatizo ya watu wanaokuzunguka ndio fursa nzuri kwako ya kupiga pesa.
 
SAFARI YA KUTAFUTA PESA.

TUMIA NGUVU ZAKO KUPATA PESA.

Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, walisema wahenga.

Kubagua kazi ni kauli za wasio na maono.

Kuishi bila kazi na kuridhika kuwa duniani bila kujishughulisha na chochote wakati Mungu amekupa Uhai, akili, na afya njema UNAKUWA MZIGO KWA TAIFA.

Katika sehemu ya tano tuliona jinsi ya kutumia akili kuzalisha mawazo makubwa yanayoweza kumpa mtu pesa.

Katika sehemu ya sita nakukumbusha kwamba

Kuna siraha kuu 3 zinazoweza kukupatia pesa

1.Akili 2.Mikono 3.Mazingira.

Katika kipengele cha mikono nataka leo ujiulize swali hili

Je unaweza kufanya nini?

Kama unaweza kulima, LIMA upate pesa

Kama unaweza kubeba mizigo BEBA upate pesa

Kama unaweza kubeba tofali kwa mafundi au kuchanganya zege CHANGANYA upate pesa.

Kama unaweza kuchimba mitaro CHIMBA upate pesa.

Kwenye kitabu cha THE SCHOOL OF MONEY Mwandishi anasema kwamba Pesa zimejificha kwenye matatizo.

Hivyo basi ili upate pesa kwa kutumia nguvu zako ni muhimu kujiuliza kwamba

Je unaweza kutatua tatizo gani ili upate pesa?

Jijini Dar es salaam mvua ikinyesha daraja likabomoka kwenye mtaro au kijito fulani

Watu wanajitolea kutengeneza daraja la muda mfupi, au wakati mwingine wanapanga tofali kisha wanaweka kitambaa kwa mbele kidogo

Ukitaka kupita kwenye matofali waliyopanga kwa kuwa hutaki kulowa, ni LAZIMA utoe pesa.

Hivyo ndivyo maisha yalivyo, ukitatua matatizo ya watu, HAKIKA watakupatia pesa.

Tumia nguvu ulizonazo, kama mtaji wa kupata unachokitafuta.
vipi miguu si muhimu mkuu?
 
Unahimiza ujambazi!!
Sio nguvu za ujambazi mkuu

 
Back
Top Bottom