Tumejiandaaje kuishi bila mtandao (internet)🛜 kuanzia kesho hadi tarehe 3 November, 2025

Tumejiandaaje kuishi bila mtandao (internet)🛜 kuanzia kesho hadi tarehe 3 November, 2025

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
15,774
Reaction score
35,994
Wahuni na mafisadi wanampago wa kuzima mtandao ili kufanya uchafuzi wao gizani, wameona kuwa mitandao itaeneza haraka mipango ya maandamano, kura fake, rushwa katika uchafuzi huo, na uonevu na matendo ya kinyama ya poliCCM dhidi ya raia Wema

Naona hawa wahuni na mafisadi wanajipalia Mkapa wenyewe, hii utatufanya hata sisi ambao hatuko interested na siasa kuona Nia Yao mbaya na kuamua kuandama

Athari za network shutdown

1. Kuuwa fursa za ajira na kipato
Vijana wanategemea mitandao ku post bidhaa Kwa wateja, na bidhaa sio zao, wao wanafanya tu freelancing
Ikizima mtandao unataka kuwauwa na njaa, na hii inaweza kuona hawana option zaidi ya kuandama

2 kuharibu mawasiliano
Yaani wahuni mpange kuwaweka Watanganyika gizani kisa ubinafsi wenu wa madaraka,
Hii itakuwa approach mbaya na mtaamsha hasira na kusababisha maandamano makubwa

3 hasara katika biashara
Biashara ndogo na za kati (SME) zinategemea mitandao kwa masoko, malipo mtandaoni, mawasiliano na wateja. Shutdown inazuia hesabu zao za siku za kawaida.

Ripoti zinaonyesha kwamba nchi zilizo na shutdowns zimepata hasara kubwa ya

4 Uzalishaji wa Taifa (GDP)
Kwa kila siku ya shutdown, nchi inaweza kupoteza asilimia fulani ya uzalishaji wao wa kila siku; ripoti zinaonyesha kwamba hata shutdown ya muda mfupi inaweza kupunguza uzalishaji.

5 network shutdown inasababisha ugumu wa wanafunzi kusoma na kupata maarifa

Mafisadi naona mnajichanganya vibaya mno
 
Msijali , tarehe 29_10 nisiku ya kukirejesha kila kilichopotea .

Wakuu nawahakikishia tarehe 29_10 inakwenda kuwa moja ya tarehe muhimu sana kwenye Taifa letu.

Mkitaka kuamini angalieni namna serikali kupitia taasisi na vitengo vyake vya usalama vinavyohaha kuhakikisha wanapamana kwa nguvu zote kuzima kila aina ya jaribio .

Hiyo maana yake ni nini?

Maana yake nikwamba serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama wameshapeleleza na kukutana na matokeo hasi kuhusu usalama wao hivyo eneo pekee wanalolitwgemea ni propaganda.

Kunawakati wanatamani hata wangelikuwa mod ili wahakujishe kila post inayohamasisha maandamano iwe inafutwa kabla haijaonekana jukwaani .

Wakuu haijitaji unabii kujua kuwa tarehe 29_10 Kuna jambo lisilo la kawaida linakwenda kutokea kwenye Taifa letu .
 
Back
Top Bottom