Tulipokuwa primary,unakumbuka?

Kuna wanaokumbuka 'Someni Kwa Furaha' kitabu cha kwanza mpaka cha nne. Wagagagigikoko, Lizabeta na Bulicheka? Vitabu vya Alfu Lela U Lela, Abdul etc etc??
 
Chang'ombe Primary School Dar 1971/72 - Viatu vilikuwa 'Maklipa','Tiger' na 'Bata', PE ndio kipindi kilichokuwa kikipendwa zaidi kwa vile ilikuwa ni dakika 45 za kucheza mpira!
Nje pale wakati wa mapumziko alikuwa anakuja mzee mmoja na tenga lake lenye mihogo ya kuchemsha tuliyoipa jina la 'Likembe'!
Kitabu cha kumsaidia mwanafunzi masomo ya Darasa la Saba kilikuwa ni 'Mwandani wa Wanafunzi'! kitabu cha kiswahili kilikuwa 'Tujifunze Lugha Yetu-kitabu cha 7' kwenye kiingereza kulikuwa na hadithi za 'Kalagesye' na kadhalika! Wanafunzi tulikuwa tunajisomea wenyewe vitabu vya hadithi kama 'Mashujaa', 'Roza Mistika', 'Visa vya Ajabu', 'Mashimo ya Mfalme Suleiman', 'Hadithi ya Allan Quaterman' na kadhalika na kadhalika...!
Those were really the beautful Days.....!!
 
Bulicheka na mkewe Lizabeta....(unaishaje huu wimbo wa Wagagagikoko?)

Na ule wa 'Makari hodari....yo yo yo '? unaishaje?


Bulicheka na mkewe Eliza, Eliza,
Walikwenda Mombasa kuiona nchi,
Katikati ya bahari chombo cha kikazama,
Wakaogelea wote wakaokokaa,
 
kweli enzi zinapita jameniiii, hayo mafuta ya Rays tena rangi zake zilikuwa zile kali sana kama njanoooooo na nyekundu. Ah tumetoka mbali sana. Na vikopo vile vilikuwa vikiisha mafuta basi vilitumika kama container za kuhifadhi mahindi yaliyokaangwa na kulowekwa na sukari. darasani huko ni kula kwa kwenda mbeleeeeeee.
 
Jamani wengine tunakumbuka enzi zile tunapo rudi shule pale karume tunarudi na kuuza dawa za mbu jioni na kibatari huku wagambo wakitusumbua aah kweli tumetoka mbali hizi dawa zilikuwa za aina mbili kijani na nyekundu lakini kijani ndio zilikuwa mali yaani zinawaka kuliko hizi nyekundu sijuwi zilikuwa zinatengenezwa wapi hizi
Halafu tuna sema tunenda shule kumbe tunaishia sokoni kariakoo au feri mhh makubwa yamepita.
 
Kuna wanaokumbuka 'Someni Kwa Furaha' kitabu cha kwanza mpaka cha nne. Wagagagigikoko, Lizabeta na Bulicheka? Vitabu vya Alfu Lela U Lela, Abdul etc etc??

Hapo umenipata natafuta hivyo vitabu nitapata wapi
 

Nilidhani hii shairi litasahauliwa nilitoe. NAkumbuka Muhisika hapa alikuwa naitwa Dadi, mwenge ulikaribishwa kijijini Mahurunga! Yaani hadithi za vitabu vile niliamini ni kweli kabisa!
 
Duh, yaani sijui kwa nini nilkuwa sijaipitia hii thread wandugu.

Nakumbuka Simulizi za Allan Quaterman na Bwana Gudi, na Mashimo ya Mfalme Selemani yaani utafikiri ni kweli kabisa.

Vinara wa Allan Quatrman ni Msolopa Gasi na Shoka la Ajabu liitwalo Inskoskazi, Namkumbuka Faulata, na Bibi Gagula
 

Nilikisoma kitabu hiki miaka mingi sana iliyopita, ila nilikuwa mdogo kuweza kukumbuka kila kitu. Nimesahau yaliyo mengi, ila nakumbuka sana "Mashimo ya Mfalme Suleiman na kadithi za "Twaingia katika nchi ya Wakukuana"
 
Ama kweli huko tulikotoka kulikuwa kutamu,

Nakumbuka shuleni kwetu tulikuwa na mwalimu mmoja mnoko sana, wiki ya zamu yake alikuwa anafika shuleni saa 11 Alfajiri ili agonge kengere ya kuhesabu namba saa 12 kamili. Basi mdogo wangu alikuwa mzembe sana wa kuamka mapema, siku moja akatoa mpya, aliamua kupiga mswaki usiku kabla ya kulala na akavaa uniform kabisa ili akikurupuka asubuhi ni mbio tu ili awahi namba. Kweli siku hiyo alifanikiwa kuwahi namba, lakini bado akapata adhabu maana uniform zake zilikuwa zimekunjamana sana kwa vile alilala amevaa. Mmeipata hiyo!!!!!!!!!!!!!!.

Vile vile nakumbuka enzi hizo tulikuwa hatuvai chupi wengi wetu wavulana kwa wasichana, sasa utamu ulikuwa pale ambapo kiranja unatoa adhabu ya wanafunzi kuruka kichura na wakati huo wewe (mimi) kiranja nimekaa mbele yaani wanaruka kuelekea kwangu nilipo. Yaani tilikuwa tunaona picha za bure kabisa.......

Nakumbuka baada ya muda wa shule au siku za jumamosi tunaenda kuchanja/kutafuta kuni, kama wewe ni kijana mkubwa una ka-demu kako, basi mtawafukuza watoto wadogo ili mcheze mchezo wa baba na mama kwenye kichaka. Basi wakuu, ni enzi hizo wengine tulianza kupata uzoefu.
 
Nakumbuka shuleni kwetu tulikuwa kila siku ya jumatatu kwenye gwaride la usafi tulikuwa tunaimba wimbo huu kabla ya ukaguzi wa Mkuu wa shule.

(1) Sisi ndio vijana wako Mwalimu Nyerere,
Tutakao kilinda chama cha mapinduzi

Kiitikio: Hongera Mwenyekiti wa CCM,
Hongera na makamu wa Mwenyekiti.

(2) Chama kilizaliwa visiwani Unguja,
Na sherehe za mwanzo mkoani Dodoma


Kiitikio: Hongera Mwenyekiti wa CCM,
Hongera na makamu wa Mwenyekiti.
 
Mkuu anayekumbuka huu wimbo auweke sawa basi:

(1) Chama chetu kimetuongoza, hadi uhuru tulioupata,
Kinaendelea kuongoza kufikia lengo ujamaa.
Mwenyekiti Mwalimu Nyerere mwenye hekima na wingi wa sifa, Tanzania

Kiitikio
Ewe chama chombo chetu mathubuti kwa hakika, ndio wewe nguzo yetu muongozi wa Taifa, Mwenyekiti Mwalimu Nyerere mwenye hakima na wingi wasifa, Tanzania.

(2) Ilifika wakati mgumu wananchi walifadhaika, utumwa ukoloni ni sumu sisi sote tuna ............


(?) Na mtu asiyejua kufa mwambieni aone kaburi.........

Mie siukumbuki vizuri
 

Ebwana we wewe utakuwa Alumni wangu unamkumbuka Marehemu Mwalimu motomoto? Sabuni ( soap ) Mwalimu Muhsin?

U made my day mate na story ya kuuza dawa za Mbu na kulangua sigara..
 
Ninakumbuka pia wimbo huu wa kuusifu Ujamaa
na kuupinga ubepari (ukoloni)


Wito umekwisha tolewa,
Njoni tuishi kijamaa,
Sasa twamkomiesha mchawi,
Naye ndiye ubinafsi;
Tulitawaliwa,
na hayo mawazo,
ya ubinasi kama;
Liwe jembe, eti langu,
liwe duka eti langu,
kiwe kiwanda eti changu,
chochote kile eti changu;
Lo! lo! loooooooo!

Hiyo hiyo ni kasumba,
ni makovu ya mkoloni,
ubinafsi,
ni kichochoro cha maendeleo,
chapindapinda,
nao ujamaa,
barabara ya lami,
ukipita hapo,
kichwa mbele haraka.
 
Duh!
Mnatukumbusha mbali sana kwa nyimbo hizi.
Long live JF!
 
Duh! Mnakumbuka enzi hizo 2kienda shule 2napaka mafuta ya kupikia KORIE? Yaani mguu ulikua unameremeta na uso unawaka mpaka basi. Unajibandika layer ya mafuta.

Ukikosa mafuta hayo unapata
Rays. Yalikua yakiuzwa sh 100 tu.
 




Think Pad,

Ulicopy hapa zile posts zako kuleeeeee kwa Kabanga ampiga mkoloni....sawa?
 
I remember kila siku jioni kabla ya kuondoka tunaenda parade then tunaimba wimbo ufuatao:

Bendera ya Tanzania,
ndiyo ya kujivunia
Ilianza kupepea,
mwaka sitini na moja,

Hapo tunashuhudia
Tunavyojitegemea
Hapa kwetu Tanzania,
Uhuru umechanua,
Muumba wetu rabuka,
Zijaze zako fanaka......!

....nimesahau sahau vimaneno vingine.....but was very very emotional aiseee.......!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…