Augustoons
JF-Expert Member
- Oct 31, 2007
- 409
- 55
I say! Thanks, nilikuwa sijui asili ya neno hilo, ingawa ktk gwaride la kiskauti tulikuwa tunayatumia maneno "as you were".Ati neno ajuwa linatokana na neno "as you were"
Nimesoma yoooote na nimefarijika sana kukumbuka enzi hizo. Lakini furaha yangu haitaweza kamilika bila ya kukumbuka kitabu kinachitwa MWANDANI WA MWANAFUNZI. hiki kitabu kilikuwa kiboko. ukiweza ku-solve maswali yake yaaani wewe ni kwenda sekondari tu.
Duh, kweli tunatoka mbali.
Jamani msisahau kuwa enzi za Waziri mkuu Sokoine watu tulivaa mashati yenye rangi za mawingu! Sijajua yalikuw yanazalishwa wapi, ila nina uhakika ilikuwa ni Tanzania hapa hapa..QUOTE]
Nadhani unazungumzia yale mashati yaliyokuwa yakiitwa "YEKE-YEKE", nadhani k/sbb yaliibuka wkt ule wimbo wa Yeke-yeke (wa Mori Kante) ulipokuwa hot cake. Nadhani wkt huo akida dada walikuwa wakijidai na viatu vya plastiki vilivyokuwa vinaitwa "SANDAK".
Sasa naona wengi mmesahau suala la kuvaa vijinsi chini ya sare, ama suala la kuvaa kaptura mbili mbili ili kuzuia fimbo kwenye makalio! Mie nilikuwa hodari sana wa kuvaa nguo za namna hiyo ili kupunguza makali ya fimbo za mwalimu "WALKING". Alipewa jina hili na wanafunzi wa darasa la tatu akiwa anafundisha somo la Kiingereza.
Sasa kioja ni kwamba kuna mwalimu alikuwa akijulikana kama "Twinkle" huyu yeye alikuwa anachapa nyuma ya ugoko ama mikononi. Hapa ikwa vijinsi chini ya sare havina deal tena. Huyu yeye alipewa jina hili la Twinkle kufuatia ule wimbo wa
Twinkle Twinkle Little Star
How I wonder what you are
Up above the World is so High
Like a Diamond in the Sky
Nakumbuka wimbo huu ulikuwa katika kitabu cha Kiingereza cha darasa la sita.
Tunatoka mbali sana kwa kweli.
Nakumbuka nililamwa viboko vitatu kwa kukutwa nasoma huku natoa tabasamu la nguvu kitabu cha Hesabu cha KIONGOZI CHA MWALIMU
Kamanda leo nimekumbuka mbali....
Nakumbuka nililamwa viboko vitatu kwa kukutwa nasoma huku natoa tabasamu la nguvu kitabu cha Hesabu cha KIONGOZI CHA MWALIMU