Tuliowahi kupewa hela na wanawake

Tuliowahi kupewa hela na wanawake

Jana nmeshangaa sana, tulipanga kuonana na mwanamke mmoja hivi ambae ni rafik yangu kwa takribani miezi miwili, tulitoka jana mida ya saa 11 jioni hivi tukaelekea katika hotel moja pale kinondoni, tukapata vinywaji huku tukiendelea kupiga story, tukala na kusaza, baada ya kutumia nikataka kulipa bill,cha kushangaza binti yule alitoa pesa akalipa yeye nilishangaa sana.

Kwa maisha ya sasa kupata mwanamke anaelipa bill ya zaidi ya elfu 50 ni nadra sana.

Ndio ikawa hivo, tulikula na kusaza bill akalipa, baada ya hapo nikampeleka kwake namimi nikaenda zangu kwangu.

Haya maisha ukiwa na vipesa vya kubadilisha mboga ni matamu sana.
Hujamla kaka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nitoke nje ya mada,

Hii tabia ya wanaume kuomba omba hela imetoka wapi.? Mbona inazidi kushamiri.?
Wanaume kazi ya kuomba omba pesa mtuachie tu siye, ninyi hampendezi walaqhi'..!!
Ni kweli boy kuomba hela kwa girl haipendezi but itawezekan kama boy anashida also remember kuwa mlitaka usawa so nanyie muwajibike dear
 
Basi mie niko tofauti, kama tulikubaliana nimkopeshe na atarudisha na hajarudisha hapo kweli patakauka na kwanza ntampotezea na kuvunja ukaribu.

Ila kama nilimpa kwa ridhaa yangu na ni rafiki yangu, nikionana nae hata sizungumzii hela niliyompa, nazungumzia habari nyingine zinazotuhusu. Pesa makaratasi siku zote huwa najali utu, nimelelewa hivyo.

Pesa ikiwekwa mbele inaharibu mambo mengi sana ya uhalisia.

Mara nyingi nikifahamiana na mtu huwa najali yeye kama yeye huka zake alivyo na tabia kuliko anamiliki nini, atanipa nini au ntampa nini. Ofcourse other factors remain constant.

Kasinde.
Hecko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaparamia makurumembe mzee, mademu yameumizwa kwenye mapenzi hadi mioyo yao imekuwa sugu, Tafuta watoto waliositaarabika mzee, wanaotoka katika familia bora, hawatafuti mwanaume kwa ajili ya kodi bali wanataka mapenzi..

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakika Mkuu
Kudate na team ndingandanga ni hatari sana ila ukipata mtoto yuko smart kichwa kutoka familia safi anaelewa nini anataka kwako ila hawa team of side ni balaa tupu yani ni uparasite mwi mwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jidanganye rafiki.
Mwanaume anatakiwa awe na pesa siku zote awe na za akiba pia.
Ikitokea labda kaumwa, kapoteza kazi ajali n. K hapo hakuna jinsi kumboost.
Lakini mzima kama Extrovert kumpa back up no.
Aende kwa washkaji zake huko au saccoss akakope.
We jifanye mke mwema tu rafiki unampa back up hela yako anaenda lipia room anaenda na mwingine.

mama wawili
Sasa anaejidanganya ni nani hapo kama sio wewe? Yani siwezi dumu na mwanamke ambaye mbinafsi! Wewe pia hela akunyime mpaka siku ukiumwa sio!?
 
Sasa hivi ni dakika chache nimetoka kupokea simu ya mwanamke wangu wa kiha sh 170000..simu imeita akasema njoo chukua hii hela uzungushe.

Huyu dada kunipa hela kwake nikutokana na nisimuache maana anajua mi nina demu mzuri kuliko yeye hivyo anatumia hyo mbinu ili nimuoe mbeleni

Sent using Jamii Forums mobile app
Weka picha ya hela na shemeji
 
I like this
Kuna wanaume nikiwakubali wanakula hela yangu kiroho safi tuu. Nimelelewa maadili ya kuwa, mwanaume ni ikichwa cha familia hivyo akihitaji hela kwangu kama nnayo nampa bila kutaka kujua atairudisha lini, anaifanyia nini.

Ila akikuta nimekaukiwa sina kabisaa hela ya kumpa, daah ntajikuta namwambia usijali ntakupigia simu kukwambia nakupaje hiyo hela, hivyo akiona kimya ajue ndo getegete.

Pesa si kitu mbele ya upendo ila ambacho sifanyi ni kuhonga, pesa yangu sihongi mwanaume ila akiniambia ninahitaji pesa na sauti yake ikapata kibali kutoka moyoni kuwa mpe, pasi shaka namtumia tuu.

K' Matata.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee mmoja wa makamo aliwahi kuniambia, kamwe mwanaume asikubali kupewa pesa na mwanamke, kama atapewa akiwa na shida flani basi ahakikishe anamrudishia hata kama mwanamke akiikataa yeye anapaswa alazimishe aipokee.... Pesa ya mwanamke ina masimango sana, ukizoea kupewa pesa na mwanamke kwa kigezo cha kusaidiana basi kubali kudharauliwa, atakutangaza kwa kila mtu atakayeongea nae, utadharaulika, kwa mwanamke pokea zawadi tu usipokee pesa, Acha mara moja hiyo tabia utaaibika.

Boost your Immune System to fight a Covid-19.
Niliwahi kusoma mahali kuwa hata mpumbavu huzeeka na kuwa mzee wa makamo.
 
Back
Top Bottom