Zamaani wakati bado mtoto kuna kijana nilikuwa na mahusiano nae, siku moja alienipigia simu akasema ameenda kwao amekuta wamekatiwa umeme mita ilikuwa na deni sijui ilikuwaje sikumbuki vizuri. Inatakiwa walipe elfu themanini kama sikosei na yeye pesa hana.... akasema niazime pesa nitakurudishia mshahara ukitoka. Nikamtumia na nilipanga nimpe tu ila yeye sikumwambia, kama mkosi vile ndani ya kipindi kifupi mahusiano yakaanza kuyumba na pesa yangu hata hajaonesha nia ya kurudisha, nikamkumbusha akaanza kupiga chenga ooh sina hela sasa hivi hela yako nitakulipa, nikamwambia nilipe sasa hivi. Akaanza kutoa povu nikasema hata sijali, fanya unilipe. Ooh basi ngoja nikope nikulipe,nikasema fanya hivyo. Alinirudishia huku ananisimanga, ndio tukawa tumemalizana. Hapo sikumhesabia elfu tano tano alizokuwa 'anaazima' bila kurudisha.
Alaa kumbe wameulizwa wanaume
Sent using
Jamii Forums mobile app