Tuliowahi kupewa hela na wanawake

Tuliowahi kupewa hela na wanawake

Zamaani wakati bado mtoto kuna kijana nilikuwa na mahusiano nae, siku moja alienipigia simu akasema ameenda kwao amekuta wamekatiwa umeme mita ilikuwa na deni sijui ilikuwaje sikumbuki vizuri. Inatakiwa walipe elfu themanini kama sikosei na yeye pesa hana.... akasema niazime pesa nitakurudishia mshahara ukitoka. Nikamtumia na nilipanga nimpe tu ila yeye sikumwambia, kama mkosi vile ndani ya kipindi kifupi mahusiano yakaanza kuyumba na pesa yangu hata hajaonesha nia ya kurudisha, nikamkumbusha akaanza kupiga chenga ooh sina hela sasa hivi hela yako nitakulipa, nikamwambia nilipe sasa hivi. Akaanza kutoa povu nikasema hata sijali, fanya unilipe. Ooh basi ngoja nikope nikulipe,nikasema fanya hivyo. Alinirudishia huku ananisimanga, ndio tukawa tumemalizana. Hapo sikumhesabia elfu tano tano alizokuwa 'anaazima' bila kurudisha.

Alaa kumbe wameulizwa wanaume


Sent using Jamii Forums mobile app
We kwamwene una shida sana aisee 🤣🤣🤣 yani nusura umtoe roho kijana wa watu. Sasa kutoa si moyo lakini? Mbona kudaiana hivyo na alikuwa mtu wako.🤣🤣🤣
 
Kuna kipindi mtoto wa kigogo aliniletea mafungu yote ya kikoba yeye ndo mweka hazina kwamba niizungushe izae afu tuje tuirudishe,nikaona huu mtego huu unaweza ukahama mji...mwanamke akipenda na akaona una akili anaweza kukuhonga hata nyumba ya baba ake😁
Hahahaha kweli kabisa, mi nikikwama nachukuaga hata 2M nafanya mishemishe narudishia. shida iko kwa hizi mbuzi ambazo zinajua kupokea tu.
 
Basi mie niko tofauti, kama tulikubaliana nimkopeshe na atarudisha na hajarudisha hapo kweli patakauka na kwanza ntampotezea na kuvunja ukaribu.

Ila kama nilimpa kwa ridhaa yangu na ni rafiki yangu, nikionana nae hata sizungumzii hela niliyompa, nazungumzia habari nyingine zinazotuhusu. Pesa makaratasi siku zote huwa najali utu, nimelelewa hivyo.

Pesa ikiwekwa mbele inaharibu mambo mengi sana ya uhalisia.

Mara nyingi nikifahamiana na mtu huwa najali yeye kama yeye huka zake alivyo na tabia kuliko anamiliki nini, atanipa nini au ntampa nini. Ofcourse other factors remain constant.

Kasinde.
Wewe sina wasiwasi kabisa na familia uliotoka. Naweza nikaoa hata ndani ya mwezi mmoja. Shida ni zile mbuzi zingine zenye covid 19 🤣🤣🤣🤣🤣 zinawaza hela tu!
 
Wewe sina wasiwasi kabisa na familia uliotoka. Naweza nikaoa hata ndani ya mwezi mmoja. Shida ni zile mbuzi zingine zenye covid 19 🤣🤣🤣🤣🤣 zinawaza hela tu!


Wee Mjuba acha uchokozi.

Unamwaga kuku kwenye shamba la mchele aahahahhaaaa.
 
Hao wengine..alafu mpenzi si mti wa pesa kwamba muda wote anakuwa nazo muda wote anipe tu..no..Kuna muda mnaishiwa na mnahitaji tafu kutoka kwa Wandani wenu (sisi)
Now you are talking! 👏
 
Hayo ndio mapenzi ya kweli sasa, hongera sana umepata demu mwenye roho ya kizungu. Wanawake wengi ni wabinafsi by nature wana mkono wa kupokea tu ila akikupa hata buku atakusimanga kishenzi ila kunao wale wazungu wa roho mtu anakupa hata M ila hakuwazi.

Huyo mwanamke usije kumuacha, ni wa shida na raha huyo hakika.

Kweli mkuu, amenipa pesa zake nyingi sana mpaka kuna kipindi alinitumia nauli kutoka Point A-E ili nikam****, na bado nikapewa na nauli ya kurudi + Matumizi.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom