Tuliowahi kunywa sumu tukutane hapa

Tuliowahi kunywa sumu tukutane hapa

Kiukweli watu hujiua kutokana na kukosa suluhisho ya kile wanachokiona ni tatizo kwao, ambacho kwa wengine huenda ikawa ni kitu cha kawaida kabisa lakini wao hukiona kama kitu kikubwa sana.
Ndio maana ni vizuri mtu ukiwa na kitu kinakusumbua jaribu kutafuta mtu wa karibu unaemuamini mzee au Kijana mwambie tatizo lako na jinsi linavyokutesa, naamini atakushauri na kukutia moyo.
Pia nawashauri pia wale wanaofuatwa kuombwa ushauri ni vizuri waoneshe ushirikiano kwa watu hao, kuwatia nguvu na moyo, na usikione wanachopitia ni kama kitu cha kijinga sana hasa kwa kujionesha mbele yao.
Kuna mtu anahitaji maneno machache tu ili arudi Kwenye hali yake tena, Kuna mtu anataka kupewa confidence tu ili ajione yuko sawa kama wengine, katika maisha haya nimegundua wengi kuna vitu vinawatesa na wanaumia navyo moyoni either vya kimaumbile au kisaikolojia tu ambavyo wakishauriwa wanaweza kuviona ni vya kawaida.
Imagine kama mleta Uzi alitaka kujiua tu sababu ya Kukojoa kitandani, naamini alikosa mtu wa kumpa confidence na kinyume chake wanafamilia wengi huanza kueneza habari nje, na kumfanya mhusika aathirike vibaya kisaikolojia. Wapo watu huwa wanawaza mbali mpaka kufikia hatua ya kutaka kujiua eti tu sababu Pua yake iko hivi, mdomo wake uko hivi, sura yake iko hivi, mfupi sana, miguu yake....na vitu chungu mzima vya kimaumbile, hii huanzia mashuleni mpaka mitaani.
Ni vizuri tujijengee utaratibu wa kuwafichia siri wenzetu katika familia au mashuleni huko, pengine wewe ni mwalimu unaona mwanafunzi wako anakasoro flani na wenzake humtania, hujui tu ni namna gani mtoto huyo anapitia mateso ya kifikra na kuathiri uwezo wake darasani. Kuna wanafunzi hawatamani kabisa kuja shule sababu ya kutaniwa, anakuja tu basi hana la kufanya lakini concentration yake Kwenye masomo ni ndogo sana, Jitahidi kuwatia moyo watu kama hawa Ndugu mwalimu au mwanajamii yeyote.
Kuna ndugu yako anatatizo fulani ambalo ni la aibu, mtunzie siri usimtangaze, mtie nguvu. Kuna mtu anatatizo flani msaidie, mtie nguvu mpe japo ushauri kama huwezi kumpa pesa au kitu. Kuna watu hujiua sababu tu anadaiwa elfu kumi! Elfu Kumi ni nini ukifananisha na uhai? Pengine alitakiwa mtu wa kumshauri tu labda ukakutane na anayemdai umuombee ampe muda kidogo zaidi, au waandikishane amlipe kidogo kidogo.....
Kiufupi Tujitahidi kutowadhalilisha au kutowanyanyapaa Binaadamu wenzetu, Tuwatie nguvu. Kingine watu wa waliosomea Mambo ya Saikolojia au ushauri wanahitajika sana hawa wawepo na kutushauri kuhusu yale tunayopitia katika maisha yetu ya kila siku.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana brother umemaliza kila kitu. Nimejifunza hata mtoto wangu kutopuuza chochote hata liwe jambo dogo. Kwanza kabisa ni kuonyesha upendo alafu ndio mengine yanafuata
 
Mimi sasahivi nilishawaambia hata ndugu. Rafiki yangu kwenye shida hata kama sio ndugu yangu, namuheshimu kuliko hata ndugu wa tumbo moja. Kuna jamaa hatukuwa na urafiki hata ule wa kusalimiana na kwao zipo kidogo, alikuwa rafiki yangu ghafla mpaka kuna muda alikuwa anawatuita mimi wife na watoto tukapige stori kwake maana tulikuwa majiranu (baadaye nimekuja kugundua alikuwa anatuita tukale kiaina maana alikuwa anatuita wakati mkewe akiwa jikoni. Yaani ilikuwa inaanza hv, mkewe akanakuja anamuita wife ampe kampan jikoni ana stori ampe, mara kidogo watoto wanaitana wanaenda kucheza, halafu baadaye unasikia fulani mwite baba aje tukae huku aikae mwenyewe) huyu hata akikosea namsamehe haraka bila hata kuomba msamaha.
Dah!huyo jamaa yuko na moyo safi sana na hekima
 
Mwaka 1975,nikiwa kijana katika kijiji chang u (jina kapuni), nililishwa sumu na bibi moja akimtumia mjukuu wake ambaye nilikuwa nasoma naye. Sumu hii nilipewa kupitia pombe ya kienyeji.
Niliporudi nyumbani muda wa jioni nilitapika sana.
Pamoja na kutapika lakini madhara ya sumu yalinisumbua sana katika kusoma kwangu na kwa kiasi kikubwa yalipunguza uwezo wangu mkubwa darasani ambao ulikuwa katika ngazi ya kitaifa.
Bibi huyu alifanya haya kwa sababu za wivu kwa sababu alitambua ujasiri wangu.
Mwaka 1993 nililishwa sumu tena ofisini kupitia kwenye chai.
Baada ya kujisikia vibaya nilimwita driver wangu ili anirudishe nyumbani. Wakati ananirudisha nyumbani nilikuwa natapika njia nzima. Nililazwa Muhimbili kwa siku tatu na baadaye nilirudi nyumbani.
Niliporudi ofisini, yule Binti aliyenipa chai sikumkuta. Aliacha kazi. Huyu alitumiwa na wabaya wangu kwa sababu nikiwa kiongozi nilipiga vita ufisadi wote uliokuwa unafanywa kwenye shirika ambalo lilikuwa linaendeshwa kwa hasara. Katika uongozi wangu wa miaka mitatu, kila mwaka tulipata faida kubwa.
Mwaka 2013, Mungu aliniepusha na kifo baada ya kupona kuuwawa kwa kutumia Bunduki.
Muda wa saa tatu usiku wakati narudi nyumbani kwa gari ya kukodi, niliona magari mawili yakinifuata kwa nyuma, Nilimuuliza Driver magari yametokea wapi? Alinijibu sijui. Tulikuwa tumekaribia karibu na nyumbani. Nilimwagiza Driver asikate kuingia kwangu mbali anyooshe moja kwa moja.
Magari haya mawili yalisimama getini kwangu na kugeuza. Driver aliendesha gari hadi Ikulu ndogo ya Mkoa. Nilipiga simu kwa rafiki zangu ambao walikuja kunichukua. Siku ya pili nilikwenda kuripoti Polisi. Yote hayo nayo yalisababishwa na Mimi kukataa kuhujumu mali ya umma.
Lakini kwa kifupi, imeandikwa, ukiwa mtu wa haki hata wakitaka kutoa roho yako hawataweza kamwe.
Sijawahi kuweka matukio haya kwa maandishi na hadharani.
Ndugu zangu na rafiki zangu wanayajua.
Mkuu wachana nazo hizo mambo,usifanye masikhara utauwawa kweli,fikiria familia yako kwanza,aisee ni hatari sana.
 
ama kwa hakika kizuri hakikosi kasoro. pole zake na zako maana upendo wake kwako ulifanya aafanye lolote kwa ajili yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu napenda kutofautiana na wewe huo si upendo, changamoto zinatakiwa kukabiliwa kwa namna ambayo haizai changamoto nyingine. Wapo baadhi ya wanawake wanapenda mkato katika kufikia malengo jambo ambalo ni sawa.
 
mi kuna miaka nilipitia kipindi kigumu ikatikia hatua nikaenda kulala barabarani ili gari inipitie ilikuwa nyakati za usiku,lakin cha ajabu gari lilikuw likifika karbu yangu linasimama dereva na konda wake wanakuja kunitoa na maneno juu."hili lijamaa limelewa pombe za bure".

Maisha ni mtihani mzito ndo maana siwez kumdharau mkubwa au mdogo,


maisha yalitight kinoma had wale wanaokuzunguka huwaoni yan.fikiria mwanaume unamaliza hata week huna buku wala jero mfukoni,root za kijiweni nikapunguza ikawa ni Mimi na kitanda kitanda na mm had mwili ukapungua .

umaskini usikie kwa jirani mana hata wasichana walipotea kwenye anga yangu,inafikia hatua unamtizama msichana yuko uchi ila humuoni.simu yangu ya mkononi ikawa inamaliza hata week 3 Hamna sms yoyote iliyoingia ,nafkiri hata voda walinisusia (kidding).
nakumbuka ilikuwa jmoc asubuh nataka niamke nikachote maji nikapokea SMS ya ujumbe kutoka kwa aliyekuwa kama demu wangu ikisomeka hivi."najua unapitia kipindi kigumu cha maisha ila pambana maisha yapo nakuombea kila la kheri kwa mpenz mwngne utakayempata mi nimeamua niwe single.". Aseeeee hii SMS ilinivuruga nikarudi kitandani nikalala licha ya kutokuw na usingiz tena.


lakini cha ajabu mwaka huo huo kuna Siku nilipishana na jamaa njian macho mekunduu AF mweusii tii.akantoa salam kisha akaniomba aniulize kitu pemben ,kumbe anashida na sehem wanapouza bangi ,nikamjibu yeah napafaham ila inaweza niamin lete ela nikufatie ,jamaa akachomoa buku 5 nikaenda ,kufika njian nikawaza sijui nizame ndichi nmpotezee ila roho nyingine ikasita. Nikaamua kumfatia tu kibish.

Maisha yalivyokuwa sasa baada ya kumletea weeder ,jamaa alitokea kuwa mshikaj knoma akawa anantuma kumbe n dreva wa shirika flan kambini huko kigoma ,miez kadhaa mbele akaniunganisha nikapata job tena mshahara wa kutosha.HADI LEO NIPO HUKU NAKULA LIFE

REST IN PEACE RASTA nakukumbuka kwa mchango wako mkubwa kwenye maisha yangu.



OVER
"Nina certificate ya nursing ila nashindwa kupangilia mwandko"

Sent using Jamii Forums mobile app
Katika zote hii imenigusa sana, kitu nilichojifunza ni mtu yeyote unayemuona mbele yako anaweza akawa msaada kwako regardless macho yako yanamuonaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilishawahi kupiga mixer ya dozi moja na nusu ya fragile na nusu ya cetrin (sina uhakika kama inaandikwa hivyo) kisha nikashushia bia bingwa. Kabla bia yenyewe sijaimaliza demu wangu akaingia ghetto, aliona siko sawa, halafu pembeni akakuta makaratasi kibao ya dawa basi akajua tayari mana alikua anajua napitia kipindi kigumu mno, akapiga kelele wapangaji wenzangu wakajaa wakaninywesha mchanganyiko wa maji na majivu nikatapika kinoma pale.

Demu akanichukua tukaenda kwake, muda huo m najiona niko sawa tu. Akatuma mtoto wake akanunue maziwa nayo nikapiga huku natapika sio poa. Basi bwana baadae kidogo cha moto ndo nikaanza kukiona, nikawa najisikia hovyo mno yan muda wote nataman niwe natapika. Tumbo linavuruga hatari, mwili hauna nguvu hata kidogo. Sikulala ile siku

Kesho yake mambo yakazidi kuwa hovyo zaidi. Tumbo linauma kinoma yan utafikiri ndani linakatwa katwa, nikienda haja natoa tu vibonge bonge vya damu. Haja ndogo mkojo una mchanganyiko wa damu kama yote asee! Huku hamu ya kula sina nakunywa tu uji. Mungu ambariki yule manzi popote alipo, alinipigania sana. Hali ikaenda hivyo kama siku nne hivi kisha nikawa sawa.

Kamari sio poa jamani, haifai

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi mkuu, pole Sana kwa changamoto. Samahani nimevutiwa na Lisa chako, naomba kuhoji yafuatayo.
1. Huyo binti bado upo nae?
2. Kwa faidi ya jamvi hili ungefafanua kilichokupelekea huko japo hata kwa codes,tuzidi kujifunza.

Siku njema


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Twin angu alijiua kwa sumu..ikanisumbua balaa hiyo hali..! Ilinisumbua kwasababu toka tunazaliwa hatujawahi achana naye hata kwa lisaa...pia dada yangu nayemfata zilikua haziivi..nilikua nampiga balaa...bas akaambiwa asicheze na mimi..kwahyo na mimi kwa hasira nikama nikamblock...sikumjali kabs ni dada au ndugu..mdogo wangu wa mwisho nimeachana aye miaka mingi sana naye nikawa namuona mtoto..so mtu niliyeamua kuwa naye benet ni twin wangu sikua mtu wa marafikia

Alipojiua wenyeji wakaanza kusema akifa pacha mmoja mwingine hachukui round! Ile hali ikawa inaniboa sana.alafu hom wakawa kama wamenitenga fulani( walikua wananiogopa maana niligeuka kama kichaa kbs..nilikua natembea na panga naona kila mwanafamilia ndo chanzo cha twin kujiua!) Two months later nikaamua kunywa piriton 20! Nilienda tu dispensary nikasema mama kanituma umpe piriton ..nikanywa zote...lol.niliamka niko hosp! Na drip za kutosha..nakumbuka nililala tu sema tumboni kulikua kunavuruga! Sikufa...! Nikapewa mshauri akaniweka sawa kias chake .since then sijapata mawazo hayo .!Mungu alinipa utashi tena!rip B!
Dah afadhali mwishoni story yako inaonesha hukufa maana nilikua na hofu kweli (jokes)

Mimi pia nilipatwa na situation fulani kwenye maisha mpaka nikatamani kufa lakini kilichoniokoa ni kufikiria familia yangi jinsi walivyo na matumaini juu yangu nikaamua kukomaa til now angalau.

Au Modds mnasemaje?
 
Dah afadhali mwishoni story yako inaonesha hukufa maana nilikua na hofu kweli (jokes)

Mimi pia nilipatwa na situation fulani kwenye maisha mpaka nikatamani kufa lakini kilichoniokoa ni kufikiria familia yangi jinsi walivyo na matumaini juu yangu nikaamua kukomaa til now angalau.

Au Modds mnasemaje?


Sitajaribu tena...ni kupambana na changamoto hata iweje kubwa vip!😍😍😍
 
Vipi mkuu, pole Sana kwa changamoto. Samahani nimevutiwa na Lisa chako, naomba kuhoji yafuatayo.
1. Huyo binti bado upo nae?
2. Kwa faidi ya jamvi hili ungefafanua kilichokupelekea huko japo hata kwa codes,tuzidi kujifunza.

Siku njema


Sent using Jamii Forums mobile app
Swali la kwanza nimeshalijibu katika comments chini hapo, ila hili la pili nimepanga kuliandikia thread kabisa. Nitaku tag mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilimpoteza rafiki yangu wa damu hivi hivi kisa sumu, alijiua namuona ile sumu hadi leo naikumbuka inaitwa “THIODAN” dah sitasahau alikunywa namuona, kinachoniumiza zaidi nilikua na uwezo wakuipiga na mkono ile chupa kabla hajanywa kwasababu alikua karibu yangu lakini sikufanya vile.


Sent from iPhone 6s Plus

Duh kwanini huksaidia??????
 
Back
Top Bottom