Tuliowahi kunywa sumu tukutane hapa

Story ya jamaa aliyebakiwa na buku siku mkewe amejifungua imenikumbusha 2017. Maisha yana tafu sana. Daah, hela......!
 
Mwaka 1975,nikiwa kijana katika kijiji chang u (jina kapuni), nililishwa sumu na bibi moja akimtumia mjukuu wake ambaye nilikuwa nasoma naye. Sumu hii nilipewa kupitia pombe ya kienyeji.
Niliporudi nyumbani muda wa jioni nilitapika sana.
Pamoja na kutapika lakini madhara ya sumu yalinisumbua sana katika kusoma kwangu na kwa kiasi kikubwa yalipunguza uwezo wangu mkubwa darasani ambao ulikuwa katika ngazi ya kitaifa.
Bibi huyu alifanya haya kwa sababu za wivu kwa sababu alitambua ujasiri wangu.
Mwaka 1993 nililishwa sumu tena ofisini kupitia kwenye chai.
Baada ya kujisikia vibaya nilimwita driver wangu ili anirudishe nyumbani. Wakati ananirudisha nyumbani nilikuwa natapika njia nzima. Nililazwa Muhimbili kwa siku tatu na baadaye nilirudi nyumbani.
Niliporudi ofisini, yule Binti aliyenipa chai sikumkuta. Aliacha kazi. Huyu alitumiwa na wabaya wangu kwa sababu nikiwa kiongozi nilipiga vita ufisadi wote uliokuwa unafanywa kwenye shirika ambalo lilikuwa linaendeshwa kwa hasara. Katika uongozi wangu wa miaka mitatu, kila mwaka tulipata faida kubwa.
Mwaka 2013, Mungu aliniepusha na kifo baada ya kupona kuuwawa kwa kutumia Bunduki.
Muda wa saa tatu usiku wakati narudi nyumbani kwa gari ya kukodi, niliona magari mawili yakinifuata kwa nyuma, Nilimuuliza Driver magari yametokea wapi? Alinijibu sijui. Tulikuwa tumekaribia karibu na nyumbani. Nilimwagiza Driver asikate kuingia kwangu mbali anyooshe moja kwa moja.
Magari haya mawili yalisimama getini kwangu na kugeuza. Driver aliendesha gari hadi Ikulu ndogo ya Mkoa. Nilipiga simu kwa rafiki zangu ambao walikuja kunichukua. Siku ya pili nilikwenda kuripoti Polisi. Yote hayo nayo yalisababishwa na Mimi kukataa kuhujumu mali ya umma.
Lakini kwa kifupi, imeandikwa, ukiwa mtu wa haki hata wakitaka kutoa roho yako hawataweza kamwe.
Sijawahi kuweka matukio haya kwa maandishi na hadharani.
Ndugu zangu na rafiki zangu wanayajua.
Wewe ndugu sijui ninakufahamu?visa vyako vinashabihiana na vya mtu ninayemfahamu.
 
Ni kweli mkuu bibi yangu mzaa baba alijiua kwa kunywa sumu miaka ya tisini kutokana na manyanyaso ya mumwe/babu yangu. Pia mjukuu wao/mtoto wa shangazi yangu alienda kujinyongea pale radio safina Arusha bila sababu yoyote ya maana sababu kama ni utajiri alikuwa nao sana tu.
Mimi sio muumini wa dini yoyote lakini katika hili huwa napata mashaka sana!

Swali kwako
Sasa mkuu kama kukojoa kwangu kitandani ulikuwa ni ugonjwa mbona tatizo liliisha lenyewe?
Alafu mkuu sijapendezwa na kauli yako ya mwisho kuwa pombe zinatuharibu warombo sababu wakaazi walioko kule ni asilimia ndogo sana ya warombo wote. Wengi wapo nje ya rombo alafu wale wanaolewa hovyo kule ni wale walioshindwa maisha mijini wakarudi kule
Niwie radhi kwa kauli ya mwisho ulimi umeteleza hata hivyo unaonekana muungwana.
Nashukuru umetamka historia ya ukoo wenu.Mimi ni mtaalamu wa saikolojia sasa cha kufanya mjaribu kuondoa hili pepo huwa linarithiwa hata kizazi cha nne kama sio muumini wa dini yeyote kuna njia za kimila za kutoa laana za ukoo.
Unajua kwanini watu wa mkoa flani wanasifika kwa kujinyonga?ni kiongozi wao mkuu kufanya hivyo.
Sisi kwetu kila baada ya miaka mi2 tunafanya dua maalum kufuta madhambi yao babu zetu wa kale kuua vitoto vichanga kisa mapacha.
 
Niwie radhi kwa kauli ya mwisho ulimi umeteleza hata hivyo unaonekana muungwana.
Nashukuru umetamka historia ya ukoo wenu.Mimi ni mtaalamu wa saikolojia sasa cha kufanya mjaribu kuondoa hili pepo huwa linarithiwa hata kizazi cha nne kama sio muumini wa dini yeyote kuna njia za kimila za kutoa laana za ukoo.
Unajua kwanini watu wa mkoa flani wanasifika kwa kujinyonga?ni kiongozi wao mkuu kufanya hivyo.
Sisi kwetu kila baada ya miaka mi2 tunafanya dua maalum kufuta madhambi yao ya kale kuua vitoto vichanga kisa mapacha.
Bahati mbaya mila katika ukoo wetu ni kama zimesahaulika.
Yani laana naamini zipo sababu kuna maneno alitamka huyo bibi na ikawa kama alivyosema.
 
Ukweli ni kwamba sumu za panya nyingi zinazouzwa hazina madhara kiivyo kwa binadamu. Hata mie nlijaribu pakti 4 tofauti sikufa nliishia kuharisha na kutapika

Nakuja PM mkuu unipe jina na rangi ya hiyo sumu iliyokupelekesha nami niitafute.
Brother please...
 
Ukweli ni kwamba sumu za panya nyingi zinazouzwa hazina madhara kiivyo kwa binadamu. Hata mie nlijaribu pakti 4 tofauti sikufa nliishia kuharisha na kutapika

Nakuja PM mkuu unipe jina na rangi ya hiyo sumu iliyokupelekesha nami niitafute.
Acha bangi braza.
 
Kujiua kunanasibishwa na aina flani ya magonjwa ya akili!

Tunahitaji tiba.

Tiba kuu na ya mwanzo kabisa ni kufungua kifua na kuliongea tatizo linalokusibu!

Ukiamua kukaa kimya unazungumza na kichwa chako na kujijibu kwa moyo wako, basi kujiua ndio hatua inayofata!

"TUZUNGUMZE CHANGAMOTO ZETU, HAIJALISHI ZITATAFASIRIWA à NA TUNAOZUNGUMZA NAO"
 
Sijasoma mada ila heading nilivyoona tu ngoja nichangie...

Huku nilipo mtu akinywa sumu na akapona (akanusurika kufa) basi wanamuita MABAKI YA SUMU
 
Mm ninahis kama sijarogwa siwez pata hata chembe ya kujiua hata kidogo. Maana kama maisha yamekua magumu ninao uwezo wa kurudi kijijini nile na kunywa bure na uwezekano upo ila si kujiondo hapa.
 
Hii dunia ina mambo yake. Mimi mmoja kati ya watoro wetu wa3 siku anazaliwa nilikuwa nimebakiza buku tu baada ya kumrudisha wife home kutoka hospital. Kwakuwa ilikuwa usiku nikaona sio ishu, atakula kwa ndugu niliyekuwa naishi nae nyumbani. Ili kupunguza zile za "mzazi hali hiki na hiki" nikapotea nyumbani kama masaa mawili huku nawaza asubuhi itakuwaje. Poda, sabuni, nguo za kumshikia mtoto wakati wa baridi, chakula cha mzazi n.k. hapo hata unga hakuna ndani maana uliisha siku moja kabla hajaenda kujifungua. Nikazuga mpaka saa tatu nikasema ngoja nipande home nikalale mimi mwanaume nitajikaza hadi kesho. Lahaula!! Kufika home kachanga kanalia mama mtu anabembeleza lakini ukisikiliza sauti yake ni kama analia pia. Nikawaza imekuwaje, nikabisha mlango nikafunguliwa. Nikauliza kulikoni, wife aliponijibu sikutaka hata kumwangalia maana nilihisi aibu. Aliniuliza "mbna umeondoka bila kuacha hata chakula, nina njaa tangu nilipokula ule mkate mchana hospital sijala mpaka sasa" nikamuuliza kwann hujala si ungekula kwa bro? "Wamepika wakamaliza wakaenda kulia ndani mwao hata hawajanisemesha." Nyumba niliyokuwa naishi ndio hiyohiyo ilikuwa na chumba kinachotumika kama jiko, fikiria nini kilikuwa kikiendelea. Kwa huzuni kabisa nikamwambia wife nina buku hapa na hukoama ntilie wote wamefunga. Akaniambia atakikaza ila maziwa ndio hamna. Asubuhi niliamka mapema sana kuhangaika nione wataishije. Ajabu ni kuwa hakuna aliyejali zaidi ya kuambiwa "usiku tulipika kaugali kadogo tukaona mzazi hatashiba" sikuwajibu. Mungu alisaidia nikajipanga kwa mbinde maisha yakasonga mpaka mtoto akawa mkubwa. Narudia tena NDUGU ZAKO UNAWAPATA WAKATI WA SHIDA. Fikiria mzazi kabisa, hili mpaka nazama chini sitalisahau na huwa namwangalia mtenda nasema yamepita.
Daaah, maisha haya tuliopitia shida tumshukuru Mungu tumeyaona maisha halisi
 
Huu uzi unaweza ukaonekana hauna maana lakini haya mambo yapo. Mimi kuna muda nilipitia hali ngumu sana kwenye maisha, kuliko niliyonayo sasa. Nilikuwa nawaza kujiua ili nipotee maana hata ndugu wanakuona kituko. Wazo moja tu lilikuwa linafanya nikomae, familia. Nikawaza mimi ndio baba na mume katika familia, kama mimi nimekoswa kazi na hela ilhali nakomaa Je! Itakuwaje kwa mke wangu ambaye ananitegemea 100% katika kutimiza mahitaji ya familia? Vp watoto watakapoona nafukiwa shimoni na wasinione tena? Kwann nisisubiri siku yangu ifike ili angalau nisiihuzunishe familia mara mbili. Wakose chakula najua hapa wanawake hufanya lolote ili waishi na watoto wengine mpaka hufanya mambo haramu, nabado wakose ile faraja yangu ya ngoja nikatafute angalau ya uji. Nilikuwa nikiwaza hayo yote halafu unaenda ndugu anatumbua bia unamuomba hata buku anakunyima anakwambia hana pesa😭😭. Umasikini usikieni tu kwa watu. Kiukweli kama isingelikuwa familia huenda ningeshajifia kitaaambo. Mshana Jr aliwahi kuelezea humu kuhusu tiba za kiroho. Nilikuwa nikisoma mada zake nahisi 90% nina shida. Katika kosa sifanyi sasahv nikuwambia mtu mipango yangu ya sasa na baadaye. Nikiulizwa unafanya nn, nawaambia niko nyumbani nasubiri ajira. Maisha ni mtihani mkubwa sana kwa binadamu, ukiona dogo kwa mwenzio ni mateso.
Yan unawaza Kama buku wameshindwa kukupa ukiwa hai ili ukajitetee na watoto wako vipi ukifa hao watoto watawajali pengine unawaza hivi buku tuu wamekataa kunipa vipi jeneza watanunua kweli?

Duniani changamoto nyingi Sana nimechukua maneno yako baadhi naahid kuyafanyia kazi
 
Huyu jamaa hajamalizia kisa chake cha pili nimekasirika mpaka nikaamua kujiua. Nmechukua maziwa glass mbili nikachukua na mayai matano nikakaanga nmekula nipo nasubiria hapa nife
 
Hii dunia ina mambo yake. Mimi mmoja kati ya watoro wetu wa3 siku anazaliwa nilikuwa nimebakiza buku tu baada ya kumrudisha wife home kutoka hospital. Kwakuwa ilikuwa usiku nikaona sio ishu, atakula kwa ndugu niliyekuwa naishi nae nyumbani. Ili kupunguza zile za "mzazi hali hiki na hiki" nikapotea nyumbani kama masaa mawili huku nawaza asubuhi itakuwaje. Poda, sabuni, nguo za kumshikia mtoto wakati wa baridi, chakula cha mzazi n.k. hapo hata unga hakuna ndani maana uliisha siku moja kabla hajaenda kujifungua. Nikazuga mpaka saa tatu nikasema ngoja nipande home nikalale mimi mwanaume nitajikaza hadi kesho. Lahaula!! Kufika home kachanga kanalia mama mtu anabembeleza lakini ukisikiliza sauti yake ni kama analia pia. Nikawaza imekuwaje, nikabisha mlango nikafunguliwa. Nikauliza kulikoni, wife aliponijibu sikutaka hata kumwangalia maana nilihisi aibu. Aliniuliza "mbna umeondoka bila kuacha hata chakula, nina njaa tangu nilipokula ule mkate mchana hospital sijala mpaka sasa" nikamuuliza kwann hujala si ungekula kwa bro? "Wamepika wakamaliza wakaenda kulia ndani mwao hata hawajanisemesha." Nyumba niliyokuwa naishi ndio hiyohiyo ilikuwa na chumba kinachotumika kama jiko, fikiria nini kilikuwa kikiendelea. Kwa huzuni kabisa nikamwambia wife nina buku hapa na hukoama ntilie wote wamefunga. Akaniambia atakikaza ila maziwa ndio hamna. Asubuhi niliamka mapema sana kuhangaika nione wataishije. Ajabu ni kuwa hakuna aliyejali zaidi ya kuambiwa "usiku tulipika kaugali kadogo tukaona mzazi hatashiba" sikuwajibu. Mungu alisaidia nikajipanga kwa mbinde maisha yakasonga mpaka mtoto akawa mkubwa. Narudia tena NDUGU ZAKO UNAWAPATA WAKATI WA SHIDA. Fikiria mzazi kabisa, hili mpaka nazama chini sitalisahau na huwa namwangalia mtenda nasema yamepita.
Mzee umenikumbusha au unanisema

Mie mwanangu wa tatu kipindi Cha kujifungua Ile wife kaamka asubuh gafla anasema tumbo linamuuma na inawezakana mambo yameiva kujicheki nna buku 2 nikamfata bwana mdogo nikamueleza akasema hana hata kumi Ila kiuhalisia alkua vizuri nikapiga baiskel kwa ile kauli alioniambia huku choz zikinitoka nikaenda kwa jamaa mmoja nae akanichomolea ikanibid kibishi nikamchukua bodaboda akampeleka wife hospital huku wale madogo wawili nikiwaandaa waende nyumban mana nlifulia kiasi Cha kutoka jijini hadi wilayan Yan nlirudisha Mpira kws kipa Ila nilipanga nyumba basi nikatoa buku nikanunua chapati za madogo nikabak na buku.

MUNGU saidia kufika hospital muda tuu wife akajifungua inshu anatokaje pale hospital home maza hayupo na ndie mkombozi kiunganishi bad nikarud home mpaka jion nikasema liwalo naliwe nikamchukua buku nikaweka tigopesa nikaweka mbet nikapet buku izae 45k kesho ake asubuh kuchek simu nishinda Ile bet nikatoa pesa kwenda hospital nikakuta yule bwana mdogo kaona aibu akalipa hospital na usafir kurud home Ile hela ya bet ndo ukanisaidia kuanza maisha ya dogo mpya.

Mie nae Nina mapichapicha Hadi najiwaza aisee
 
Back
Top Bottom