Tuliowahi kunywa sumu tukutane hapa

Tuliowahi kunywa sumu tukutane hapa

Sijawai kufikiria kujitoa uhai ila kupotea niende kusiko julikana ambako simjui mtu yeyote nikae 20 yrs bila kurudi home, sio kwamba home kubaya ila natamani tuu
Toka nimemaliza chuo sijawai rudi home zaidi kukiwa na matatizo na kunakipindi nilienda kufanya interview, kwa sehem home kunakila kitu ambacho ukifanya uwezo wa kutoboa ni mkubwa ila sipendi kukaa jilani na ndg zangu
Ndugu zangu karibia wote waliopo home wana good life, hadi leo sijapotea kwa sababu nilikuwa nafauru darasani na sijawa kwama hata darasa moja pia toka nifike secondary ( form 2) nimekuwa mtu wa church sana hadi leo, kuna kipindi nilipo kwa form 1 nilikwa mkorofi (mtukutu niliyekaribia kushindikana) sana school nilitaka kutoroka niende chunya migodini sema nilichokosea niliwashirikisha jamaa zangu wawili mpango wangu wakutoroka walinibembeleza ile mbaya nibaki shule na nilitaka kufanya iv cos kuna teachers fulani iv nilikuwa naona kama hawanipendi kila nikiharibu najikuta natumbukia mikononi mwao nachapwa na kusemwa sana ila home hawajui na nikirudi rikizo nikifanya msala tu mvua ya maneno inanyesha kwangu so akili ya kupote kusipo julikana ilikuwa kubwa sana.
Nilivo fika form 2 nilibadilika kabisa nikawa mtu wa church hadi leo nyumban hawa amini kama nimebadilika hadi shule watu hawa amini kwa sababu napitaga mara nyingi kuwapa hi na kuna watu hawaamini hadi leo
 
Nilishawahi kufikiria kujiua.
Sababu nilikuwa ni kukosa upendo kutoka kwa ndugu zangu.
Na hasa kipindi nikiwa mja mzito wa first born wangu sijui chochote ,
Kwa msaada wa Google...nilifatilia kila hatua na nikaweza.
Nilikuwa na mimba ya miezi 8 nilikuwa nakaa mwenyewe ,mwanaume alikuwa ni mtu wa kusafiri,Na alikuwa hana wasiwasi kwa vile ndugu zangu walikuwa karibu akajua watanisaidia.
Nilikuwa naumia sana.nikasema kwa nn nisijiue tu mimi na mwanangu tumboni.
Ila upendo ulinifanya nighairi.maana nilikuwa nashauku ya kumwona mwanangu.
Nimekaa mwenyewe mpaka siku uchungu unanishika nikamwomba house girl wa ndugu yangu nilale nae.
Alihamndulilah.nilijifungua salama.
Nampenda mwanangu na huwa namwambia..
Kwa sababu yake,ntahakikisha ntakuwepo duniani mpaka ahadi itakapofika..
Haijalishi ntapitia magumu gani....
 
mi kuna miaka nilipitia kipindi kigumu ikatikia hatua nikaenda kulala barabarani ili gari inipitie ilikuwa nyakati za usiku,lakin cha ajabu gari lilikuw likifika karbu yangu linasimama dereva na konda wake wanakuja kunitoa na maneno juu."hili lijamaa limelewa pombe za bure".

Maisha ni mtihani mzito ndo maana siwez kumdharau mkubwa au mdogo,


maisha yalitight kinoma had wale wanaokuzunguka huwaoni yan.fikiria mwanaume unamaliza hata week huna buku wala jero mfukoni,root za kijiweni nikapunguza ikawa ni Mimi na kitanda kitanda na mm had mwili ukapungua .

umaskini usikie kwa jirani mana hata wasichana walipotea kwenye anga yangu,inafikia hatua unamtizama msichana yuko uchi ila humuoni.simu yangu ya mkononi ikawa inamaliza hata week 3 Hamna sms yoyote iliyoingia ,nafkiri hata voda walinisusia (kidding).
nakumbuka ilikuwa jmoc asubuh nataka niamke nikachote maji nikapokea SMS ya ujumbe kutoka kwa aliyekuwa kama demu wangu ikisomeka hivi."najua unapitia kipindi kigumu cha maisha ila pambana maisha yapo nakuombea kila la kheri kwa mpenz mwngne utakayempata mi nimeamua niwe single.". Aseeeee hii SMS ilinivuruga nikarudi kitandani nikalala licha ya kutokuw na usingiz tena.


lakini cha ajabu mwaka huo huo kuna Siku nilipishana na jamaa njian macho mekunduu AF mweusii tii.akantoa salam kisha akaniomba aniulize kitu pemben ,kumbe anashida na sehem wanapouza bangi ,nikamjibu yeah napafaham ila inaweza niamin lete ela nikufatie ,jamaa akachomoa buku 5 nikaenda ,kufika njian nikawaza sijui nizame ndichi nmpotezee ila roho nyingine ikasita. Nikaamua kumfatia tu kibish.

Maisha yalivyokuwa sasa baada ya kumletea weeder ,jamaa alitokea kuwa mshikaj knoma akawa anantuma kumbe n dreva wa shirika flan kambini huko kigoma ,miez kadhaa mbele akaniunganisha nikapata job tena mshahara wa kutosha.HADI LEO NIPO HUKU NAKULA LIFE

REST IN PEACE RASTA nakukumbuka kwa mchango wako mkubwa kwenye maisha yangu.



OVER
"Nina certificate ya nursing ila nashindwa kupangilia mwandko"

Sent using Jamii Forums mobile app
Mungu hamtupi mja wake. Pole mkuu na hongera sana maana ulishasahau machungu ya wakati huo
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, ni kwamba katika maisha tunakutana na changamoto ambazo wakati mwingine huwa kubwa kwelikweli, au huwa kubwa kulingana na mhusika atakavyoitafsiri changamoto yenyewe ndani ya ubongo wake kitu ambacho hupelekea mhusika kukata tamaa kwa asilimia zote hadi kuona bora kufa kuliko kuendelea kuishi.

Wengine huwa ni changamoto za kutatulika lakini hushindwa kuchukua hatua stahiki kutokana na ujinga au kutokana na kuathirika kisaikolojia kutokana na muda wa changamoto husika.

Sasa basi naomba nisimulie kisa changu kilichonipelekea kutaka kuutoa uhai wangu ndani ya Dar es Salaam na kingine ndani ya Kilimanjaro, japo katika visa vyote sikufanikiwa na ndio maana nipo hai hadi muda huu.

Ieleweke thread kama hizi ni kuwasaidia wengine wenye wanaopita matatizo kama ya waliotangulia, ili wasikate tamaa bali wajue ni hatua gani za kuchukua ili watoke kwenye matatizo waliyonayo na mwisho wabaki wakiusifu na kufurahia uzuri wa kazi za Mungu aliye chanzo chao.

Twende kwenye kisa cha kwanza ambacho almanusra kiondeke na uhai wangu!
Nilipomaliza elimu ya msingi moja kwa moja nikatakiwa kwenda kwa shemeji kufanya kazi ya kuuza kitimoto Arusha huku nikiendelea kusubiri matokeo, lakini safari yangu nilikuwa na wasiwasi maana nilikuwa na tabia ya kukojoa kitandani, sasa nikawa nawaza huko mjini nitakaaje na hii tabia yangu?

Nikajipa moyo tu potelea mbali liwalo na liwe. Sasa nilipofika Arusha, kwa bahati nzuri sikupangiwa kulala na yeyote ila nilipangiwa nitakuwa nalala kwenye makochi ofisini.

Kwa kifupi pale niliishi kijanjajanja na tabia yangu hiyo japo mbeleni waliijua tabia yangu ila wakawa wananisitiri tu

Mdogomdogo mara nikafaulu kwenda kidato cha kwanza lakini sikukubali kuendelea na shule japo nilibembelezwa sana lakini nikawa sitaki kabisa. Hivyohivyo mpaka ilipotimu mwezi wa 7 mwaka 2010 kaka yangu akapiga simu kwa dada Arusha sasa katika kumsalimia akataka niende Dar nikakae dukani. Ile kaka kutaka niende Dar kulinichanganya kabisa mpaka nikaanza ujeuri kazini maana nilitaka niache kazi shemeji na dada wakakataa sababu nilikuwa nimeshakuwa mtu wa muhimu na mzoefu pale ofisini.

Kweli nilizidisha ujeuri hadi wakayasikia madai yangu wakanilipa changu nikasepa.
Nakumbuka nilipita kwanza nyumbani Rombo nikiwa na kiasi kama laki tatu na chenchi ila mpaka naondoka nilikuwa nimebakiwa na 125,000 wakati nilikaa siku tatu tu nyumbani.

Baada ya siku tatu mimi huyoo Dar es Salaam. Nilitoka asubuhi saa kumi na mbili lakini tulienda kufika saa mbili usiku kwa sababu kuna gari lilipata ajali mbele yetu kulekuke Rombo kabla hata hatujafika mashati. Nilipofika Ubungo nikapokewa na jamaa wa tax aliyetumwa na kaka ndio akanipeleka hadi dukani. Nilipofika nakumbuka tulisalimiana tu akaniingiza dukani usiku uleule. Kuna laki moja ilibaki mfukoni baada ya kutoa nauli nikampa aniwekee mimi nikaendelea na kazi yeye akaketi hapo mlangoni akinielekeza bei ya vitu na namna ya kufanya kazi maana ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuuza dukani.

Sasa bahati yangu nikawa nalala kwenye chumba changu mwenyewe tena, hivyo ikawa chansi ya kuficha aibu yangu ya kukojoa kitandani maana nilikuwa nikitandika nailoni usiku na asubuhi nalificha.

Kipindi hicho tulikuwa tandika ila baada ya miezi michache akahamia kwake Tabata, hivyo ikawa nikifunga duka tunalala sehemu moja!

Kimbembe kikaanza. Kipindi hicho nilikuwa najitahidi hata sinywi soda hovyohovyo na maji hasa ile mida ya jioni kuelekea usiku lakini wapi! Nilikuwa nikijitahidi sana naweza kukosa siku 2 ndani ya wiki. Mambo yakawa magumu kwangu.

Lile jambo liliniathiri kisaikolojia kwa wakati huo kuliko wakati mwingine wowote tangu kuzaliwa. Nimajiona sifa na nikaanza kulaumu kwanini hata nilizaliwa?

Yani nalala na mtu msafi, asiyependa uchafu, nyumba safi, kitanda kisafi, mashuka masafi, nina akili timamu lakini nakojoa kitandani? Nikawa sina amani na mawazo ya kutaka kujiua yakaanza kumea kwenye akili yangu maana nilijiona nikifa nitakuwa na amani na hakuna chochote kitakachoendelea.

Kaka alikuwa hapendi kabisa hiyo tabia yangu na tangu utotoni alikuwa hapendi
Kadri siku zilivyokuwa zinaenda mimi nikawa naanza kufikiri mbinu nzuri ya kuniondoa chapu, ilipofika mwezi wa pili mwaka wa 2011, nakumbuka siku hiyo nilifata bia na baiskeli nikakutana na jamaa anatembeza sumu za panya, mende, kunguni nk; nikamsimamisha nikamuuliza sumu ya bei ghali kabisa ni sh ngapi? Akajibu kuwa ni buku.

Nikamwuliza sifa zake akasema hiyo sumu huua panya fasta na akishakufa hanuki. Sikuongea sana nikamwambia anifungie.

Niliporudi dukani nikaendelea na mambo yangu kama kawaida huku lengo langu likiwa ni kwenda kujiulia mbali na eneo la nyumbani. Kesho yake asubuhi nikadamka nikaenda kwenye kimsitu fulani kiko pale Tabata kisukuru kwa pembeni sijui eti ni wa jeshi, maana mission yangu ilipofeli kule, muda wa kutokea barabarani kuna mbaba aliniambia we mtoto unafanya nini kwenye huo msitu wa jeshi?

Sasa baada ya kuingia kwenye hicho kimsitu nikapanda juu ya mikorosho huku nikifikiria namna nitakavyoingia makazi mapya ambayo ni ya kufikirika zaidi. Baada ya muda nikaibugia ile sumu yote ambayo ilikuwa kama vile vitambi vya kwenye packet ndogondogo.

Baada ya kuibugia nikashuka zangu juu ya ule mkorosho ili nisije kuanguka saa ya kufa. Nikakaa pale chini ya mti muda mrefu bila kuhisi chochote ndio nikaamua kutafuta njia ya kutoka ndani ya ule msitu baada ya njaa kuwa kali kwenye mida ya saa nane mchana, nikatokeza barabarani ndio huyo dingi akakutana na mimi akaniuliza, wee mtoto umetoka kufanya nini ndani ya huo msitu wa jeshi? Nikamwambia nimetoka kujisaidia.

Tukaachana mimi nikaelekea na njia ya kupandia Tabata migombani ili nikavizie chakula dukani kwa rafiki wa kakaangu ambaye pia ni rafikiangu ili nikampange endapo akiulizwa na kaka nilikuwa wapi aseme nilikuwa kwake. Kweli mpango wangu ukaenda fresh ila misheni yangu ya kuwahi kwa father God ikafeli.

Niliporudi kwa kaka nikamkuta anapambana na kazi huku anafua mashuka niliyokojolea usiku huo kitendo ambacho kiliniumiza mara dufu. Katika kuniuliza nilikoamkia asubuhi nikamdanganyadanganya ikabidi anivungie tu sababu akishaanza kuona kama dishi lango haliko poa.

Tukaendelea vizuri tu shetani wangu akawa ndio kanikomalia vizuri yani hata asubuhi najikuta nakojoa kitandani kama mtoto mdogo wakati mimi ni mkaka wa miaka 20 kabisa. Hazikuisha hata wiki mbili nikanunua sumu nyingine ya panya nikainywea bafuni muda ambao nilikuwa mwenyewe usiku lakini yenyewe niliitapika tu wala sikuhisi chochote kibaya wala nini.

Nikaona huu sasa ni uduanzi, kesho yake mchana nikashuka ile sumu ya kuulia mbu nikaipulizia kwenye kikombe alafu nikaenda kununua sindano zile za mahospitalini nikainyonya kwa ile sindano kisha nikajidunda mguuni alafu nikaionja kidogo lakini matokeo yake pale nilipojidunda pwlivimba alafu pakawa panauma sana lakini sikupatwa na tatizo lingine.

Nilitokewa na kidonda lakini kilipona chenyewe bila hata mtu kujua Mwezi wa tatu mwaka huohuo nikaenda kununua sumu nyingine ya panya ambayo ni kapakt kadogo sana kalikofungwa na karatasi mbili, nikakaweka kwenye juice fulani zilizokuwa zinaitwa juice za glass au pride juice nikanywa usiku wa saa tano ambapo muda huo kaka alikuwa anakunywa bia na marafiki zake kibarazani nje ya duka.

Ile nimeinywa tu nikahisi kuzunguzngu na dalili ya kutapika, nikajikaza nikatoka kama naenda kuoga na nilipofika nyuma ya nyumba tu nikatapika chakula chote cha mchana alafu nikaishiwa nguvu kiasi. Nikadaka ukuta nikadondokea kwa jamaa mmoja ambaye muda mwingi anakuwa hayupo nyumbani huja usiku kwa usiku na usiku huo alikuwa ameshalala ila mimi nikadondokea pembeni kidogo ya gari lake nikawa natapika maji na kujiharishia mfululizo mpaka nikaishiwa nguvu kiasi kwamba nilikuwa nikitazama balbu iliyokuwa juu yangu naiona kama imesambaa.

Muda mfupi baadae nasikia kaka akiita hadi kwa baadhi ya majirani akiniulizia maana niliacha ndoo ya kuogea kule na sabuni kule bafuni alafu hajui nilipo na ni usiku sana.

Akawa anahangaika bahati nzuri baadaye sijui alifikiria nini akapanda juu ya ule ukuta akaniona, akaja fasta akamwamsha na yule jirani huku mimi nawasikia tu ila siwezi kufanya chochote hata kutoa sauti au kukunja hata kidole cha mkono siwezi.
Wakaja mbiombio wakaenda kuleta mabarafu wakaniwekea ila nikawa hata sitingishiki ila masikio yangu yakawa yanasikia kuliko kawaida. Mara nasikia wakisema, ameshakufa, hahemi huyu, kafanyaje? Nini kimemkumba?.

Basi nilishangaa kaka akisema amekunywa sumu huyu. Kauli ile ilinishtua japo nilikuwa marehemu 90% Wakashauriana mara wakanibeba wakanitupa kwenye gali wakaniwahisha hospitali ya amana, lakini katika kunibeba kule kote nilikuwa naelewa nimebebwa lakini sihisi/yani mwili wangu ulikuwa hauhisi chochote tena hata walinifinya nikajua nimefinywa lakini sikuhisi maumivu.

Kufika amana nikapokelewa fasta nikawekewa maji tu kumbukumbu zikakomea pale hadi asubuhi nilipozinduka nimezungukwa na marafiki wa kaka wengi na mirija ya maji.

Kila mtu akawa anataka kujua nilipatwa na nini lakini nikasema sielewi ilikuwaje.
Kikubwa pale nilipona bila bata kutumia dawa tofauti na maji niliyowekewa.
Kingine nilipotoka hospitali nilipoteza uwezo wa kuonja kwa muda wa karibu mwezi mzima na kuna namna nilikuwa nikiisikia ile harufu ya sumu kwa muda huohuo ikaja kupotea Kifupi kaka alihonga pale nisipelekwe polisi kwa kosa la kujiua ndio tukaondoka. Sasa mpaka leo najiuliza madaktari na kaka walijuaje nimekunywa sumu?

Sijawahi kupata jibu ila mwaka 2016 ndio nilimwambia kaka ukweli.
Tatizo la kukojoa kitandani lilikuja kuisha baada ya kuacha mchezo wa kujichua, na hii niligundua baada ya kukaa muda wa mwezi sijajichua likaisha lenyewe ndio nikajua kumbe ndio dawa ya tatizo.

Na nashukuru baada ya kujua nilikuwa nakojoa kitandani kwa sababu ya kujichua kulikopitiliza, ilibidi niache huo mchezo mara moja!

Kisa cha pili nitakileta maana vidole vimechoka kutyp

KISA CHA PILI KIPO COMMENT YA 43
"Nikamwuliza sifa zake akasema hiyo sumu huua panya fasta na akishakufa hanuki. Sikuongea sana nikamwambia anifungie"

Bwashee isije ikawa hii ndiyo dawa pekee ambayo ilikuponya. Kwa nini usiipigie promo kwa vikojozi wengine?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini baadhi ya watu wanaojiua wakifikia Ile steji ya kukata roho kama wanajuta.
Kuna documentary niliiona jamaa alitaka kujiua sijui alimeza sumu gani matokeo yake baadhi ya organ zake zilivurugika kufa hakufa. Alifanyiwa operation akawa na ulemavu na akila chakula kinamchukua karibu 1 hour kumaliza chakula kidogo tu.sehemu ya koo haipo vizuri tena na sehemu ya kusagia chakula haipo vizuri alijuta
 
Nilishawahi kufikiria kujiua.
Sababu nilikuwa ni kukosa upendo kutoka kwa ndugu zangu.
Na hasa kipindi nikiwa mja mzito wa first born wangu sijui chochote ,
Kwa msaada wa Google...nilifatilia kila hatua na nikaweza.
Nilikuwa na mimba ya miezi 8 nilikuwa nakaa mwenyewe ,mwanaume alikuwa ni mtu wa kusafiri,Na alikuwa hana wasiwasi kwa vile ndugu zangu walikuwa karibu akajua watanisaidia.
Nilikuwa naumia sana.nikasema kwa nn nisijiue tu mimi na mwanangu tumboni.
Ila upendo ulinifanya nighairi.maana nilikuwa nashauku ya kumwona mwanangu.
Nimekaa mwenyewe mpaka siku uchungu unanishika nikamwomba house girl wa ndugu yangu nilale nae.
Alihamndulilah.nilijifungua salama.
Nampenda mwanangu na huwa namwambia..
Kwa sababu yake,ntahakikisha ntakuwepo duniani mpaka ahadi itakapofika..
Haijalishi ntapitia magumu gani....
Hii dunia ina mambo yake. Mimi mmoja kati ya watoro wetu wa3 siku anazaliwa nilikuwa nimebakiza buku tu baada ya kumrudisha wife home kutoka hospital. Kwakuwa ilikuwa usiku nikaona sio ishu, atakula kwa ndugu niliyekuwa naishi nae nyumbani. Ili kupunguza zile za "mzazi hali hiki na hiki" nikapotea nyumbani kama masaa mawili huku nawaza asubuhi itakuwaje. Poda, sabuni, nguo za kumshikia mtoto wakati wa baridi, chakula cha mzazi n.k. hapo hata unga hakuna ndani maana uliisha siku moja kabla hajaenda kujifungua. Nikazuga mpaka saa tatu nikasema ngoja nipande home nikalale mimi mwanaume nitajikaza hadi kesho. Lahaula!! Kufika home kachanga kanalia mama mtu anabembeleza lakini ukisikiliza sauti yake ni kama analia pia. Nikawaza imekuwaje, nikabisha mlango nikafunguliwa. Nikauliza kulikoni, wife aliponijibu sikutaka hata kumwangalia maana nilihisi aibu. Aliniuliza "mbna umeondoka bila kuacha hata chakula, nina njaa tangu nilipokula ule mkate mchana hospital sijala mpaka sasa" nikamuuliza kwann hujala si ungekula kwa bro? "Wamepika wakamaliza wakaenda kulia ndani mwao hata hawajanisemesha." Nyumba niliyokuwa naishi ndio hiyohiyo ilikuwa na chumba kinachotumika kama jiko, fikiria nini kilikuwa kikiendelea. Kwa huzuni kabisa nikamwambia wife nina buku hapa na hukoama ntilie wote wamefunga. Akaniambia atakikaza ila maziwa ndio hamna. Asubuhi niliamka mapema sana kuhangaika nione wataishije. Ajabu ni kuwa hakuna aliyejali zaidi ya kuambiwa "usiku tulipika kaugali kadogo tukaona mzazi hatashiba" sikuwajibu. Mungu alisaidia nikajipanga kwa mbinde maisha yakasonga mpaka mtoto akawa mkubwa. Narudia tena NDUGU ZAKO UNAWAPATA WAKATI WA SHIDA. Fikiria mzazi kabisa, hili mpaka nazama chini sitalisahau na huwa namwangalia mtenda nasema yamepita.
 
Sumu ni za panya na wanatangaza kabisa "sumu ya panya, kunguni, viroboto na mende"" sasa hapo unategemea itakua na effect kubwa kwako, huenda kua hata hao wanaotengeneza wanajua kuna watu wana akili za namna hiyo hivyo hata ile makali yake kwako inakua ndogo...

Niliwai kujaribu kitu kama hiko ila sio kwa sumu... Dah asikwambie mtu unavofanya kile kitu kuna kipindi mambo yanakua heavy.. Haya mambo yapo jamani hasa ukikosa hata mshauri
 
Hii dunia ina mambo yake. Mimi mmoja kati ya watoro wetu wa3 siku anazaliwa nilikuwa nimebakiza buku tu baada ya kumrudisha wife home kutoka hospital. Kwakuwa ilikuwa usiku nikaona sio ishu, atakula kwa ndugu niliyekuwa naishi nae nyumbani. Ili kupunguza zile za "mzazi hali hiki na hiki" nikapotea nyumbani kama masaa mawili huku nawaza asubuhi itakuwaje. Poda, sabuni, nguo za kumshikia mtoto wakati wa baridi, chakula cha mzazi n.k. hapo hata unga hakuna ndani maana uliisha siku moja kabla hajaenda kujifungua. Nikazuga mpaka saa tatu nikasema ngoja nipande home nikalale mimi mwanaume nitajikaza hadi kesho. Lahaula!! Kufika home kachanga kanalia mama mtu anabembeleza lakini ukisikiliza sauti yake ni kama analia pia. Nikawaza imekuwaje, nikabisha mlango nikafunguliwa. Nikauliza kulikoni, wife aliponijibu sikutaka hata kumwangalia maana nilihisi aibu. Aliniuliza "mbna umeondoka bila kuacha hata chakula, nina njaa tangu nilipokula ule mkate mchana hospital sijala mpaka sasa" nikamuuliza kwann hujala si ungekula kwa bro? "Wamepika wakamaliza wakaenda kulia ndani mwao hata hawajanisemesha." Nyumba niliyokuwa naishi ndio hiyohiyo ilikuwa na chumba kinachotumika kama jiko, fikiria nini kilikuwa kikiendelea. Kwa huzuni kabisa nikamwambia wife nina buku hapa na hukoama ntilie wote wamefunga. Akaniambia atakikaza ila maziwa ndio hamna. Asubuhi niliamka mapema sana kuhangaika nione wataishije. Ajabu ni kuwa hakuna aliyejali zaidi ya kuambiwa "usiku tulipika kaugali kadogo tukaona mzazi hatashiba" sikuwajibu. Mungu alisaidia nikajipanga kwa mbinde maisha yakasonga mpaka mtoto akawa mkubwa. Narudia tena NDUGU ZAKO UNAWAPATA WAKATI WA SHIDA. Fikiria mzazi kabisa, hili mpaka nazama chini sitalisahau na huwa namwangalia mtenda nasema yamepita.
Pole sana mkuu. Nilijifunza wakati wa shida ili upate upenyo, inatakiwa ujichanganye na watu ambao hawakufahamu kabisa au ambo hawajui historia yako
Nilijifunza pia watu wa karibu ukikumbwa na misukosuko mibaya wanachekelea kimyakimya
 
Pole sana mkuu. Nilijifunza wakati wa shida ili upate upenyo, inatakiwa ujichanganye na watu ambao hawakufahamu kabisa au ambo hawajui historia yako
Nilijifunza pia watu wa karibu ukikumbwa na misukosuko mibaya wanachekelea kimyakimya
Mimi ukata umenipa funzo kubwa sana na nikisema niandike hapa kila kitu, ntawachosha na kunawatakaosema ni chai. Humu jf kuna mtu mmoja ambaye katika kuongea naye wakati huo alinitia moyo (ile ya kuona kabisa ameguswa na aliendelea kunishauri nini cha kufanya) wengine ukiongea naye anakuuliza mawili matatu ukiwa mwepesi ukafunguka ndio na pm anakublock na simu hapokei.
 
Nilishawahi kufikiria kujiua.
Sababu nilikuwa ni kukosa upendo kutoka kwa ndugu zangu.
Na hasa kipindi nikiwa mja mzito wa first born wangu sijui chochote ,
Kwa msaada wa Google...nilifatilia kila hatua na nikaweza.
Nilikuwa na mimba ya miezi 8 nilikuwa nakaa mwenyewe ,mwanaume alikuwa ni mtu wa kusafiri,Na alikuwa hana wasiwasi kwa vile ndugu zangu walikuwa karibu akajua watanisaidia.
Nilikuwa naumia sana.nikasema kwa nn nisijiue tu mimi na mwanangu tumboni.
Ila upendo ulinifanya nighairi.maana nilikuwa nashauku ya kumwona mwanangu.
Nimekaa mwenyewe mpaka siku uchungu unanishika nikamwomba house girl wa ndugu yangu nilale nae.
Alihamndulilah.nilijifungua salama.
Nampenda mwanangu na huwa namwambia..
Kwa sababu yake,ntahakikisha ntakuwepo duniani mpaka ahadi itakapofika..
Haijalishi ntapitia magumu gani....
Dah ulifanya jambo la msingi sana
 
Back
Top Bottom