Mzigua90
JF-Expert Member
- Sep 23, 2014
- 38,405
- 88,864
Mpanda miti mwenzio audacious
Poleee sana,
Kwa upande wangu, kuna simbilis moja almanusra inifanye nipak vitu vyangu niondoke duniani, shenzi sana, mapenzi haya
Anyway.. tuyaache hayo
miaka ya Nyuma kidogo hapo, nikiwa kama standard three hv au two, nikiwa kwa babu mzaa mama moshi vijijin huko, siku moja nimepanda juu ya mti wa mmerez, (kwa wanao ifahamu hii miti ukiwa umekomaa n mrefu sana) nilikua naupunyua matawi, bwana wee huku na huko nimekata tawi lina kama V hv, hiyo V si ikaja ikanivaa shingon kama tai hv... nilijaribu kulivua weee lakn wapi, huku na huko wapi (nilikua bado mdogo, chini ya miaka 10) so uamuz wa haraka ukanijia nijiachie tu nidondoke nalo, nikaachia panga likatangulia kwanza... Yaan ilitokea kama miujiza vile, ile nataka kujiachia tu likanivuka lenyewe, niko hoi bin taaban hapo, nguvu zenyewe zalisha anza kuisha, nikashuka nikaenda kulala