TANGU 2012 NAPAMBANA ILA BADO BADO...

TANGU 2012 NAPAMBANA ILA BADO BADO...

life255

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2026
Posts
225
Reaction score
576
Tangu 2012 Nimekuwa Nikijaribu Kusimama Tena — Changamoto Niliyonayo Sasa

Wakuu, nimeona leo niandike kitu ambacho kwa muda nimekuwa nikikifikiria sana.

Mwaka 2012 nilifeli masomo. Tangu wakati huo nimepitia vipindi mbalimbali vya maisha—wakati mwingine nikiwa na matumaini, wakati mwingine nikihisi kama nimekwama sehemu moja.

Miaka imepita, lakini bado sijafikia maisha niliyokuwa nimeyafikiria.

Kwa sasa sina ajira wala kipato cha uhakika. Nipo nyumbani na bado natafuta namna ya kuanza upya. Kuna siku mahitaji ya kawaida yanakuwa changamoto, na wakati mwingine hata kiasi kidogo cha fedha kinakuwa na maana kubwa kwa mtu aliye kwenye hali kama hii.

Lakini sitaki huu uwe uzi wa kulalamika.

Nataka kuuliza wale ambao wamewahi kuanzia chini kabisa:

Ukiwa huna kazi, huna mtaji mkubwa, umefeli sehemu fulani ya maisha na unaonekana kama umechelewa kuanza, unaanzia wapi?

Nimekuwa nikifikiria kujiajiri na kuanza kitu kidogo ambacho kinaweza kukua taratibu. Tatizo ni kupata mwanzo na kujua ni wapi niweke nguvu zangu.

Labda kuna mtu hapa amewahi kupitia hali kama yangu na akapata njia ya kusimama tena.

Ningependa kusikia uzoefu wenu—
Ni kitu gani kilikusaidia kutoka kwenye kipindi kigumu?
Uliaanzia wapi bila mtaji mkubwa?
Na ni kosa gani ulifanya ambalo ungependa mtu anayepitia hali kama hii aliepuke?

Mimi bado naamini kwamba kufeli mwaka 2012 hakumaanishi maisha yote yamefeli.

Huenda mtu anayesoma huu uzi akawa na wazo, connection, fursa au hata maneno machache ambayo yanaweza kunipa direction mpya.

Niko tayari kusikiliza.

Safari yangu bado haijaisha.
 
Pambana kufeli shule sio kufeli maisha usichague kazi.
Nimekupata mkuu. Hilo la kutokuchagua kazi nimeanza kulifanyia kazi. Kwa sasa nina wazo la kuanza ufugaji wa kuku, hata kwa mtaji mdogo kabisa. Sitafuti maisha ya mkato; nataka nipate mwanzo ambao utanipa nafasi ya kujisimamia na kukuza hatua kwa hatua.

Kama kuna mtu mwenye uzoefu wa ufugaji au anayoweza kunielekeza kwenye namna ya kuanza kwa mtaji mdogo, nitashukuru sana. Mwanzo mdogo si tatizo, cha muhimu ni kuanza.
 
Tatizo lako linaanzia pale unapochagua cha kufanya.
Tangu mwaka 2012 mpaka sasa ni miaka 14.
Huo ni muda mrefu, ulitakiwa uwe tayari unajua njia ya kupita.
Hata hivyo hujachelewa, kama mapambano yako yalikuwa mijini, sasa jaribu mashambani, huenda utapata kitu cha kufanya.
 
Nguvu zote hizo mkuu? Ingia chaka, Kule ni nguvu zako tu, mtaji kiduchu nguvu kama zote. Ukidhamiria huwezi kosa mtaji maximum 5M per season, unarudi town kufanya mambo unayotaka.

NB. Sio lazma upate mtaji kwenye mambo unayopenda kuyafanya.
Tatizo lako linaanzia pale unapochagua cha kufanya.
Tangu mwaka 2012 mpaka sasa ni miaka 14.
Huo ni muda mrefu, ulitakiwa uwe tayari unajua njia ya kupita.
Hata hivyo hujachelewa, kama mapambano yako yalikuwa mijini, sasa jaribu mashambani, huenda utapata kitu cha kufanya.
Nimekupata mkuu. Hilo la kutokuchagua kazi nimeanza kulifanyia kazi. Kwa sasa nina mpango wa kuanza ufugaji wa kuku kama njia ya kujiajiri.

Nimesomea mifugo na nina uelewa mzuri wa ufugaji, hivyo changamoto yangu kubwa kwa sasa si maarifa, bali ni kupata mtaji wa kuanzia. Sihitaji kuanza na mradi mkubwa; hata mtaji mdogo utanipa nafasi ya kuanza, kuzalisha na kukuza mradi hatua kwa hatua.

Kama kuna mtu mwenye uwezo wa kunisaidia kwa mtaji wa kuanzia, kuku wa mwanzo, au kunielekeza kwenye fursa ya kuanzia, nitashukuru sana. Niko tayari kufanya kazi; ninachohitaji ni nafasi ya kuanza.
 
Nimekupata mkuu. Hilo la kutokuchagua kazi nimeanza kulifanyia kazi. Kwa sasa nina mpango wa kuanza ufugaji wa kuku kama njia ya kujiajiri.

Nimesomea mifugo na nina uelewa mzuri wa ufugaji, hivyo changamoto yangu kubwa kwa sasa si maarifa, bali ni kupata mtaji wa kuanzia. Sihitaji kuanza na mradi mkubwa; hata mtaji mdogo utanipa nafasi ya kuanza, kuzalisha na kukuza mradi hatua kwa hatua.

Kama kuna mtu mwenye uwezo wa kunisaidia kwa mtaji wa kuanzia, kuku wa mwanzo, au kunielekeza kwenye fursa ya kuanzia, nitashukuru sana. Niko tayari kufanya kazi; ninachohitaji ni nafasi ya kuanza.

Tatizo lako ni mindset. Ukifaulu kubadili hyo kitu ni one step ahead. Usipende kupewa/kusaidiwa ili upate, TAFUTA upate.
Hata kazi mbna nyingi sana mtaani umekosa kabisa mkuu? Au unataka kazi soft, kwakua ulifeli shule kazi za kuzipambania ni za jasho na hizo huwezi kukosa.
 
Tatizo lako ni mindset. Ukifaulu kubadili hyo kitu ni one step ahead. Usipende kupewa/kusaidiwa ili upate, TAFUTA upate.
Hata kazi mbna nyingi sana mtaani umekosa kabisa mkuu? Au unataka kazi soft, kwakua ulifeli shule kazi za kuzipambania ni za jasho na hizo huwezi kukosa.
Umesema kweli mkuu. Changamoto yangu kubwa imekuwa mindset na kusubiri msaada badala ya kujisukuma. Nimekupokea, na sasa najaribu kubadilika—kutafuta fursa, kupambana na kazi yoyote halali, na kuanza nilipo bila kuchagua sana. 💪🏽
 
Nguvu zote hizo mkuu? Ingia chaka, Kule ni nguvu zako tu, mtaji kiduchu nguvu kama zote. Ukidhamiria huwezi kosa mtaji maximum 5M per season, unarudi town kufanya mambo unayotaka.

NB. Sio lazma upate mtaji kwenye mambo unayopenda kuyafanya.
Chaka gani? nielekeze vizuri mkuu, na season inachukua mda gani?
 
20260311_141126.jpg
 
Kaka kwanini usitafute hata kazi ya kubeba zege? Mi nilipo disco chuo tu nilijichanganya mji wa serikali Dodoma, kujenga majengo Yale kama kibarua asubuhi nipo pale navizia japo Kuna siku unaingia Kuna siku unakosa, unarudi geto, badae nikajiingiza kwenye ujasiriamali, huku nikifanya kazi hotelini kama mhudumu, nikahamia kwenye ulinzi wa usiku ili mchana nijiajiri, nika hustle hivohivo mdogomdogo, nikaanza kuhama mikoa mpaka sasa nataka kuingia kwenye MZIKI sijakurupuka tu kuingia kwenye MZIKI no, nimeanzia mbali mpaka kufika Leo naingia ngazi mpya mziki kwangu NAIONA kama ngazi mpya mana naenda kutumia kipaji changu nilicho pewa na MUNGU mambo mengine anajua yeye MUNGU kama tawin or lose lakini kumove on muhimu kaka hivo pambana sana 2012 ina mana umri wako si mdogo we ni mtu mzima upo kwenye thirty something kaka, ukitinga 40 bila inshu ya kueleweka dah MUNGU atusimamie, lakini mpaka Leo nataka nianze na label yangu ya mziki nikiangalia niliko Toka just a matter of thanks god
 
Kaka kwanini usitafute hata kazi ya kubeba zege? Mi nilipo disco chuo tu nilijichanganya mji wa serikali Dodoma, kujenga majengo Yale kama kibarua asubuhi nipo pale navizia japo Kuna siku unaingia Kuna siku unakosa, unarudi geto, badae nikajiingiza kwenye ujasiriamali, huku nikifanya kazi hotelini kama mhudumu, nikahamia kwenye ulinzi wa usiku ili mchana nijiajiri, nika hustle hivohivo mdogomdogo, nikaanza kuhama mikoa mpaka sasa nataka kuingia kwenye MZIKI sijakurupuka tu kuingia kwenye MZIKI no, nimeanzia mbali mpaka kufika Leo naingia ngazi mpya mziki kwangu NAIONA kama ngazi mpya mana naenda kutumia kipaji changu nilicho pewa na MUNGU mambo mengine anajua yeye MUNGU kama tawin or lose lakini kumove on muhimu kaka hivo pambana sana 2012 ina mana umri wako si mdogo we ni mtu mzima upo kwenye thirty something kaka, ukitinga 40 bila inshu ya kueleweka dah MUNGU atusimamie, lakini mpaka Leo nataka nianze na label yangu ya mziki nikiangalia niliko Toka just a matter of thanks god
Sina Mtaji Tyu Nawaza Nifuge Kuku
 
Back
Top Bottom