Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Sitashau siku ambayo nilikuwa kijijini kwetu nilienda kwa ajili ya mapumziko likizo. Baada ya siku kadhaa nilianza kuumwa jino sana. sikuwa na huduma yoyote kwani ni kijijini ikabidi nipewe dawa za kienyeji lakini sikupona.

Alikuja bwana mmoja aliniambia kuwa ana dawa kwa hiyo ataniletea. Siku moja mida ya saa 7 mchana akaniletea dawa, Hiyo dawa ilikuwa ni ugoro. Aliniambia nisugue jini linaloniuka kisha niweke ugoro nitapona.

Baada ya muda nikafanya hivyo. Nilikua nipo kwenye mashamba ya migomba, Magimbi na mitimiti ya matunda. Baada ya kuweka ule ugoro hali yangu ilibadirika nikaanza kuona mawenge mara nikadondoka chini nikawa sijielewi.

nililala hapi hadi usiku wa manane huku nikiwa nimetafutwa sana bila mafanikio. usiku huo nilianza kung’atwa na fisi mwilini, baada ya fisi kupiga kelele ule usiku na watu kufuatilia ile milio ndio nikaonekana na kukimbizwa zahanati.

Nilipata matibabu kwa muda wa mwezi mzima na sindano za tetenasi sijui na vichaa vya Umbwa [emoji3][emoji3][emoji3] Lakini nashukuru nikapona maisha yakaendelea.

Hadi leo sijarudi kijijini wala sitaki kusikia labda siku nikazikwe huko na sio mm kujipeleka.
[emoji28][emoji1787][emoji1787][emoji1787]pole mkuu

Fisi hakuondoka na zaga..maana ndo zake yule
 
NILIOKOLEWA NA JIRANI NA WAZUNGUView attachment 1426951

Mimi ilikua siku nikiachwa mwenyewe nyumbn basi hio ndio siku ya kujaribu mengne yote ambayo nakatazwaga,

Siku moja hv wakubwa wote wakaenda shamba kuvuna mahindi nikaachwa mwenyewe, wakati wanaondoka Mama akaniambia "Leo usipotulia litakalo kupata utajisaidia mwenyewe maana kambini watu karbu wote leo wanaenda shamban kuvuna mahindi" (tulikua tunaish kwenye kambi za maliasili na utalii na ipo isolated na vijiji vingne) mtoto wa mamkubwa akacheka akasema "leo sijui tutakuta kituko gani?"

maana wiki iliyopita nilikutwa nimelala kwenye maua baada ya kupanda juu ya bati na kujitia fundi wa antena nikashuka nayo, nilipo angukia ndo hapo hapo nilipokutwa nimejikunyata, wapita njia walikua wananiona ila hawakujua kama nimepattwa na tatzo maana hapo hapo mbuzi wakaja kujilaza kwa kunizunguka, jiran baada ya kuona mbuzi wameondoka wamekuja kuku mimi bado nipo ndo akapigwa na machale akaja kunibeba akanipeleka dispensary,

Sasa basi, baada ya bimkubwa kunipa onyo wakasepa, nikanywa kwanza chai, wakati anaongea vile nilikua nasubr tu amalize lakn kichwan nishapanga leo lazima nijifunze baiskeri.

Nikaenda stoo nikachomoa mphoenix nikakokota mpk barabarani, mimi raha yangu nikokote mpk kwenye mteremko/kilele cha mlima halaf nipande inishushe then nikokote tena nirudie,

Nikaenda mara ya kwanza safi tu, mara ya pili niliumia kdg matakoni baada ya kujibamiza kwenye ule mtalimbo unaounganisha sterring na kiti maana nilikua sikai kwenye kiti ili nifikie sterring na pedal vizuri(tulikua tunaita kuisimamia),

Mara ya tatu ndo kimbembe sasa,
Kwa sbb nilishajihs kuweza mzee nikashuka kwa kasi huku nimekaa kwenye kiti, kitu kikaanza kuyumba, speed ikaongezeka zaid, break nikashndwa kushika maana siwez kutanua vidole nizifikie na nikilazimisha napoteza balance maana huku nyuma nako kiti nimekikalia pale kwenye ncha(pale wanaposema panawatoaga wanawake waendesha baisker bikra) huku nimeinamia sterring,
ule mlima n mrefuu mpk ufke chini, chini ikawa inapanda gari ya watalii wanaenda kule kambini kuchukua kibali ofisini ili waingie porini huku wanachukua video, wakaniona nashuka kwa kasi sanaa ikabd wao ndo wanikwepe,
Sasa pale mwisho wa mlima pana kona kali, juu kuna mto/bwawa kubwa lenye kina hasa, then karavat mbili kubwa hasa, chini maji yanakoshukia ni maporomoko kwenye maweee makubwa na pembeni chaka la miba.

Kona nilijua niwazi kbsa sitaweza kukata na nikilazimisha tuu zile moramu pale chini na mawe mali yangu,

Nikawaza kule juu kwenye bwawa nitakufa bila hata kuonekana nyama, kwenye karavati jinsi yalivyo makubwa na nikisikia yale maji yanavyofoka sikutaka hata kuwaza, kule chini yale maporomoko ndio hata hilo wazo halikunijia, option ikabakia kwenye chaka la miba(miba flan hv mifupi imejikunja halaf inawasha sana ikikuchoma),

Nikalifakamia bwanaaaaa, niliingia mpk kati kati ya lile biwi kubwa la miba, huko ndani kulikua na vicheche, bundi, kware, wanyama flani hv wananuka sana na wale wanaopenda kujisaidia sehem moja hata wakienda mbali watarud pale n.k wote walitoka nduki kila yule kwa mlio wake, nilibananishwa na miba ukijitikisa tu kdg inakuchoma,
kumbe wale wazungu walipigwa na machale, walipaki gari wakarud kuniangalia, wakanikuta nimejaa damu hata kulia siwezi maana nikitanua mdomo tuu nakutana na miba inazidi kupenya, ikawa naangusha tu machozi na migunoo,
mmoja akaenda kwenye gari kuchukua vifaa wakatumia zaid ya masaa mawili kunitoa mule ndani ya lile biwi la miba bila kuniumiza zaidi, wakanipa huduma ya kwanza(walikua na vifaatiba ving),

Wakanipeleka ofisini,
huko tukamkuta mzee na wafanyakaz wenzake, nimejaa ma bandage ofce nzima wakaanza kuitana "jaman njooni mmuone ..... Tena Huku, ya leo kalii"
Yaani baada ya kusununika watu hoi kwa vicheko maana washanizoea sasa,
hapo naonekana tu kijimdomo na macho tu, wale wazungu wakawa marafk zangu kuanzia pale mpk wanaondoka, wakaniachia bonge ya Nokia na PC, niliwashwa siku tatu, kuanzia pale ikawa kuachwa nyumbn mwenyewe n mwiko.
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] bila shaka now utakuwa mpole sana
 
Mimi kaburi liliniita kabisa.
Kifo kilitaka kunimeza...

Kipindi nasoma tulikuwa na masomo ya jioni ...tukitoka saa8 mchana muda wa lunch ,tunaingia saa 10 ,,hapo kutoka saa12..
Nilikua na utararibu wa kurudi nyumbani kwenda kula chakula ili kupunguza gharama za kula shule.
Pia nyumbani ilikua karibu sana Kama dk 5 tu kwa gari nakuwa nimefika.
Kwa hiyo kwenda na kurudi nilitumia sh300.
Nikawa napumzika then saa 10 kasoro narudi shule.

Ikafika siku yangu..
Kama kawaida yangu..wakati narudi shule niligongwa na gari katika harakati za kuvuka barabara....
Ilitokea gari iliovertake ghafla ikaja kunipiga..nilikuwa naelekea mwisho kabisa ..ilinipiga ikanitoa nje kabisa.
Ilikwapua mguu wangu ,,ikaondoka na soksi...nguo zote chakachaka..na zilikuwa mpya maana ilikua mwanzo wa mwaka tu.
Nilijipiga kichwa chini...nikachika Mdomo,Kuna kipande Cha jino kilikatika na juu ya jicho.
Jamani ajali isikie kwa Mtu..isiwe kwako.
Nilizima pale chini dk chache,,

kulikuwa Kuna gari ya magereza pembeni..wakanibeba wakisaidiana na baadhi ya wanafunzi wenzangu.
Kwenda hospital damu zinanimwagika tu pale...nikapitilizishwa kwenye msaada wa haraka.
Kusafisha vidonda yaani niliona dunia inafika mwisho...Yale maumivu niliyoyapata.
Wakaniuliza km nakumbuka namba za ndugu zangu.
Nimeksriri namba ya mama kuliko nyingine zote..nikataja..
Kumpigia mama anastuka anashangaa.,na mama yangu alikua akiishi wilayani huko,huku nilikua naishi na dada.wakamwambia mwanao yupo hsp ya rufaa...
Mama akampigia dada..dada kupanda gari..akajua niliumia kidogo..akawa anaenda shule..
Haijafika mbali akakuta mama anamwambia eti mtoto Yuko rufaa[emoji16][emoji16][emoji16]
Alishuka hakumlipa konda nauli [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Kufika pale Niko hoi bin taaban nasubiri kwenda x Ray..wapige kichwa mkono na mguu.
Na kipindi hicho madaktar walikuwa na mgomo,shemeji alikua anafahamiana na mtu wa x-ray..hatukupata shida...

sikulazwa nilirudi home..
Kule wazaz wakafunga safari kuja.
Jamani kuugua vidonda usiombe[emoji23][emoji23][emoji23]

Baada ya siku 2 walikuja wale walionigonga..walienda kuuliza shule wakaelekezwa.
Walikuwa bega kwa bega na wazaz Hadi nilipo pona

Ila namba niliisoma vema.
Mwezi mzima sili,sitembei,sioni,siongei.
Kiuno kiliteguka,mguu haufunction,usoni ndio usiseme... nilikua km yule mama kwenye Avatar ya Zero IQ

12.02.2012 hii siku siisahau
thats was a spiritual thing
 
NILIOKOLEWA NA JIRANI NA WAZUNGUView attachment 1426951

Mimi ilikua siku nikiachwa mwenyewe nyumbn basi hio ndio siku ya kujaribu mengne yote ambayo nakatazwaga,

Siku moja hv wakubwa wote wakaenda shamba kuvuna mahindi nikaachwa mwenyewe, wakati wanaondoka Mama akaniambia "Leo usipotulia litakalo kupata utajisaidia mwenyewe maana kambini watu karbu wote leo wanaenda shamban kuvuna mahindi" (tulikua tunaish kwenye kambi za maliasili na utalii na ipo isolated na vijiji vingne) mtoto wa mamkubwa akacheka akasema "leo sijui tutakuta kituko gani?"

maana wiki iliyopita nilikutwa nimelala kwenye maua baada ya kupanda juu ya bati na kujitia fundi wa antena nikashuka nayo, nilipo angukia ndo hapo hapo nilipokutwa nimejikunyata, wapita njia walikua wananiona ila hawakujua kama nimepattwa na tatzo maana hapo hapo mbuzi wakaja kujilaza kwa kunizunguka, jiran baada ya kuona mbuzi wameondoka wamekuja kuku mimi bado nipo ndo akapigwa na machale akaja kunibeba akanipeleka dispensary,

Sasa basi, baada ya bimkubwa kunipa onyo wakasepa, nikanywa kwanza chai, wakati anaongea vile nilikua nasubr tu amalize lakn kichwan nishapanga leo lazima nijifunze baiskeri.

Nikaenda stoo nikachomoa mphoenix nikakokota mpk barabarani, mimi raha yangu nikokote mpk kwenye mteremko/kilele cha mlima halaf nipande inishushe then nikokote tena nirudie,

Nikaenda mara ya kwanza safi tu, mara ya pili niliumia kdg matakoni baada ya kujibamiza kwenye ule mtalimbo unaounganisha sterring na kiti maana nilikua sikai kwenye kiti ili nifikie sterring na pedal vizuri(tulikua tunaita kuisimamia),

Mara ya tatu ndo kimbembe sasa,
Kwa sbb nilishajihs kuweza mzee nikashuka kwa kasi huku nimekaa kwenye kiti, kitu kikaanza kuyumba, speed ikaongezeka zaid, break nikashndwa kushika maana siwez kutanua vidole nizifikie na nikilazimisha napoteza balance maana huku nyuma nako kiti nimekikalia pale kwenye ncha(pale wanaposema panawatoaga wanawake waendesha baisker bikra) huku nimeinamia sterring,
ule mlima n mrefuu mpk ufke chini, chini ikawa inapanda gari ya watalii wanaenda kule kambini kuchukua kibali ofisini ili waingie porini huku wanachukua video, wakaniona nashuka kwa kasi sanaa ikabd wao ndo wanikwepe,
Sasa pale mwisho wa mlima pana kona kali, juu kuna mto/bwawa kubwa lenye kina hasa, then karavat mbili kubwa hasa, chini maji yanakoshukia ni maporomoko kwenye maweee makubwa na pembeni chaka la miba.

Kona nilijua niwazi kbsa sitaweza kukata na nikilazimisha tuu zile moramu pale chini na mawe mali yangu,

Nikawaza kule juu kwenye bwawa nitakufa bila hata kuonekana nyama, kwenye karavati jinsi yalivyo makubwa na nikisikia yale maji yanavyofoka sikutaka hata kuwaza, kule chini yale maporomoko ndio hata hilo wazo halikunijia, option ikabakia kwenye chaka la miba(miba flan hv mifupi imejikunja halaf inawasha sana ikikuchoma),

Nikalifakamia bwanaaaaa, niliingia mpk kati kati ya lile biwi kubwa la miba, huko ndani kulikua na vicheche, bundi, kware, wanyama flani hv wananuka sana na wale wanaopenda kujisaidia sehem moja hata wakienda mbali watarud pale n.k wote walitoka nduki kila yule kwa mlio wake, nilibananishwa na miba ukijitikisa tu kdg inakuchoma,
kumbe wale wazungu walipigwa na machale, walipaki gari wakarud kuniangalia, wakanikuta nimejaa damu hata kulia siwezi maana nikitanua mdomo tuu nakutana na miba inazidi kupenya, ikawa naangusha tu machozi na migunoo,
mmoja akaenda kwenye gari kuchukua vifaa wakatumia zaid ya masaa mawili kunitoa mule ndani ya lile biwi la miba bila kuniumiza zaidi, wakanipa huduma ya kwanza(walikua na vifaatiba ving),

Wakanipeleka ofisini,
huko tukamkuta mzee na wafanyakaz wenzake, nimejaa ma bandage ofce nzima wakaanza kuitana "jaman njooni mmuone ..... Tena Huku, ya leo kalii"
Yaani baada ya kusununika watu hoi kwa vicheko maana washanizoea sasa,
hapo naonekana tu kijimdomo na macho tu, wale wazungu wakawa marafk zangu kuanzia pale mpk wanaondoka, wakaniachia bonge ya Nokia na PC, niliwashwa siku tatu, kuanzia pale ikawa kuachwa nyumbn mwenyewe n mwiko.
Haki ya Mungu toka nizaliwe sijawahi kucheka hivi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji86][emoji86]

Yaan mkuu niko kwenye jam hapa tazara imebidi nichepukie BAKHRESA hapa nicheke nisije gonga magari ya watu[emoji1787][emoji1787]

Eti" njoeni mumuone huyu" means uligeuka kituko kila kona[emoji28][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
thats was a spiritual thing
Hakika
Shetani yupo kazini
MUNGU pia yupo,halali wala hasinzii kwa ajili ya maisha ya kwetu [emoji120]

Na hii kitu niliwahi onyeshwa(huwa naota na napata mafunuo kwa njia ya mawazo)
Lakini kwa umri niliokuwa nao sikuelewa,pengine kwa sababu ya utoto na imani yangu ilikuwa ndogo nadhani.
Ila Mungu yupo, Mungu wetu ni Mungu wa vita...ana nguvu.
God heals everything
All the pains i passed through yet He was there for me [emoji120]




Kuna wakati anafanya pasi na kumuomba..
Huwa nashangaa Sana kuna watu huwa hawaoni sababu ya kumshukuru Mungu,wameelekeza sana malalamiko kwa Mungu kuliko shukrani,hawajui wao kumaliza siku wakawa wazima wa afya,wanakula,wanaona,wanatembea,wanaongea ni sababu tosha za kumshukuru Mungu.
 
Hakika
Shetani yupo kazini
MUNGU pia yupo,halali wala hasinzii kwa ajili ya maisha ya kwetu [emoji120]

Na hii kitu niliwahi onyeshwa(huwa naota na napata mafunuo kwa njia ya mawazo)
Lakini kwa umri niliokuwa nao sikuelewa,pengine kwa sababu ya utoto na imani yangu ilikuwa ndogo nadhani.
Ila Mungu yupo, Mungu wetu ni Mungu wa vita...ana nguvu.
God heals everything
All the pains i passed through He was there for me [emoji120]




Kuna wakati anafanya pasi na kumuomba..
Huwa nashangaa Sana kuna watu huwa hawaoni sababu ya kumshukuru Mungu,wameelekeza sana malalamiko kwa Mungu kuliko shukrani,hawajui wao kumaliza siku wakawa wazima wa afya,wanakula,wanaona,wanatembea,wanaongea ni sababu tosha za kumshukuru Mungu.
Mkuu najua kidogo wewe unaweza nielewa nikisema mambo mengi yanakuwa yamepangwa au kuna mambo huwa shetani anajua yatatokea vipi na hatua utakayopiga, ila Mungu husimama bila hata sisi kujua kuna mda unaweza dhurika na kuna mda hata hilo jambo halitokei kwamfano unataka uende kazini ila unaghairi kumbe kuna tukio baya ilibidi litokee kwako....

Pole sana madam, Mungu anakusudio nawewe na bado halijatimia ndio maana upo hai....
 
Mkuu najua kidogo wewe unaweza nielewa nikisema mambo mengi yanakuwa yamepangwa au kuna mambo huwa shetani anajua yatatokea vipi na hatua utakayopiga, ila Mungu husimama bila hata sisi kujua kuna mda unaweza dhurika na kuna mda hata hilo jambo halitokei kwamfano unataka uende kazini ila unaghairi kumbe kuna tukio baya ilibidi litokee kwako....

Pole sana madam, Mungu anakusudio nawewe na bado halijatimia ndio maana upo hai....
Watu wengi huwa hawaelewi hilo mkuu.
Hawajui kuwa Kuna muda Mungu anatuepusha na mengi pasi na sisi kujua.

Amen,naamini hivyo pia
"Mungu amenihurumia,
Jambo hili kubwa Sana,
Sikustahili Jambo hili,
Nimelipata bure tu.

Sasa najua haya yote,nasifu huruma Yake"
 
Watu wengi huwa hawaelewi hilo mkuu.
Hawajui kuwa Kuna muda Mungu anatuepusha na mengi pasi na sisi kujua.

Amen,naamini hivyo pia
"Mungu amenihurumia,
Jambo hili kubwa Sana,
Sikustahili Jambo hili,
Nimelipata bure tu.

Sasa najua haya yote,nasifu huruma Yake"
Amen mkuu Mungu ni mwema....i believe hiyo ndo point ya wewe kuamini zaidi kwenye ukuu wake...
 
Amen mkuu Mungu ni mwema....i believe hiyo ndo point ya wewe kuamini zaidi kwenye ukuu wake...
"Je!mwanamke aweza kumsahau Mtoto wake anyonyaje,hata asimhurumie mwana wa tumbo lake?
Naam,hawa waweza kusahau,lakini mimi sitakusahau wewe.Tazama nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu;kuta zako ziko mbele zangu daima"
Isaya 49:14-16

Hii mistari huwa naielewa kuliko kawaida.
Mungu anatukumbuka zaidi ya tunavyodhani.

"Nimeweka walinzi juu ya kuta zako,Ee yerusalemu;hawatanyamaza mchana wala usiku;
Isaya62:6@


"Maana Mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana,ili nikuokoe"
Yer1:19b
 
"Je!mwanamke aweza kumsahau Mtoto wake anyonyaje,hata asimhurumie mwana wa tumbo lake?
Naam,hawa waweza kusahau,lakini mimi sitakusahau wewe.Tazama nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu;kuta zako ziko mbele zangu daima"
Isaya 49:14-16

Hii mistari huwa naielewa kuliko kawaida.
Mungu anatukumbuka zaidi ya tunavyodhani.

"Nimeweka walinzi juu ya kuta zako,Ee yerusalemu;hawatanyamaza mchana wala usiku;
Isaya62:6@


"Maana Mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana,ili nikuokoe"
Yer1:19b
Amen na asante kwa mistari mizuri....isaya ni kitabu ninachokipenda sana
 
Back
Top Bottom