Beeb
JF-Expert Member
- Aug 18, 2018
- 29,402
- 58,951
Kaka yangu alikua na kigugumizi tulivyokuwa wadogo alikua anapenda kunikorofisha(tumefuatana) ..nikasikiaga ukimfunikia ungo mtu mwenye kigugumizi wakati anaongea anakosa pumzi..siku yake ikafika Bana alinikorofisha nikasema dawa yako inachemka.Ilikuwaje?
Nikambamba siku hiyo anaongea Tena alikua ananiongelesha kwa ugomvi nikakumbuka ungo nikaingia ndani nikachukua ungo vile anaendelea kuongea nikafunika alianza kukata kuongea ametoa tu mimacho ana hema kwa shida Mama anatoka nje ananikuta nimefunika ungo na mwanae ahemi akaniambia wewe utamuua Kaka yako akawahi kufunua ule ungo.
Tangu hapo akunichokoza tena