Tuliokulia vijijini tukafanikiwa kusoma soma kisha babu au bibi zetu wakatuasa tusipendelee kurudi vijijini tukutane hapa

FAJES

JF-Expert Member
Oct 29, 2017
714
628
Kama unavyojua buana, ukizaliwa kijijini enzi hizo, ni shida sana kufaulu kwenda Sekondari miaka hiyo ya 2000 mwanzoni mwanzoni maana enzi hizo shule za kata zilikuwa bado hazijaanza.

Sasa ukifanikiwa kufaulu lazima kijiji kizima kijue. Mungu ni mwema buana, akatujalia na akina sisi wa mavumbini tukafaulu na kwenda kusoma soma mpaka tukatoboa kufikia vyuo vikuu.

Shida ikaanza pale Babu yangu alipokuwa akiniasa kabisa kuwa nisipendelee sana kurudi kijijini wakati wa likizo. Na akawa anasema kuwa ikitokea nimerudi basi nisikae sana na nikitaka kuondoka nisipendelee kuaga watu wengi na wala nikitaka kwenda kijijini wakati wa likizo nisiwe natoa taarifa.

Yanai niwe nafanya kushtukiza tu. Kwakweli nilipata wakati mgumu sana kumuelewa Babu yangu ila ndio hivyo akishasema inabidi kutii.

Nina dhani jambo hilo linahusiana na imani za kishirikina. Japo Babu yangu alianza kuwa mtu wa Church ukubwani kuelekea uzeeni ila bado naona alikuwa anafahamu na kuamini sana mambo mengi kuhusu tunguri.

Bahati mbaya mpaka Babu anafariki sikufanikiwa kukaa naye na kumuuliza kwa undani kuhusu kauli zake enzi hizo. Vipi wewe Babu ama Bibi yako amewahi kukwambia jambo kama hili? Unaweza ku-share?
 
Mambo mengi kijijini babu anakwambia usije bila kutoa taarifa lazima akuruhusu yani sasa unawezq kuja ukienda bila taarifa unaweza kuamka unaumwa vibaya mno na umekuja mzima wa afya mimi sipendi kwenda yani miaka hata 7 sigusi ingawa sijazaliwa huko ila napaogopa tu.
 
Mkuu kijijini Kuna Mambo bhana

Kipindi tu nimefaulu kwenda elimu ya juu

Nilienda kwa babu bhana mwanza kwanza akasema hakuna kwenda kuogelea utaenda na mamba
Ukitaka kwenda kwa ndugu inabidi uende nae
Hakuna kumtarifu au kuaga kesho naondoka
La sivyo umekwisha
Tangu babu afariki Kuna baadhi ya ndugu unaogopa kuwatembelea
 
Mkuu kijijini Kuna Mambo bhana

Kipindi tu nimefaulu kwenda elimu ya juu

Nilienda kwa babu bhana mwanza kwanza akasema hakuna kwenda kuogelea utaenda na mamba
Ukitaka kwenda kwa ndugu inabidi uende nae
Hakuna kumtarifu au kuaga kesho naondoka
La sivyo umekwisha
Tangu babu afariki Kuna baadhi ya ndugu unaogopa kuwatembelea
Ha ha haaa. Hapo kwenye mamba mkuu umenena. Hiyo story ipo hasa huko Ukara-Ukelewe. Ukicheza Mamba anakufata mpaka home kwenu.
 
Fanyeni utafiti vizuri,siku hizi mjini ndio kubaya kuliko vijijini.maduka yote makubwa mjini yanaendeshwa kwa ndumba,wafanyakazi maofsini wanasiasa Hali kadhalika.kwa hiyo msiogope kurudi vijijini
 
Kwanini Babu au bibi akuzuie kurudi nyumbani baada ya kufanikiwa huwenda labda na yeye alikuwa mruka usiku mbona mwaka 2000 juzi tu mie nimemaliza miaka ya ya 90s na nilifaulu vizuri nachojua mashuleni ndio kulikuwa na ushirikina sana na hata nilipomaliza bado wazee waliniasa nikumbuke kurudi nyumbani na kusaidia wadogo zangu
 
linenwalo lipo
Kwanini Babu au bibi akuzuie kurudi nyumbani baada ya kufanikiwa huwenda labda na yeye alikuwa mruka usiku mbona mwaka 2000 juzi tu mie nimemaliza miaka ya ya 90s na nilifaulu vizuri nachojua mashuleni ndio kulikuwa na ushirikina sana na hata nilipomaliza bado wazee waliniasa nikumbuke kurudi nyumbani na kusaidia wadogo zangu
 
Back
Top Bottom