Tulichosema kuhusu Kigamboni kimetimia: Tukimbilie wapi?

Kigamboni ni matokeo ya Bush kukaa siku nne Tanzania. Tulijiuliza sana kulikoni kwa bush kukaa hivyo?
 
Jamani mwenye Dta zaidi atuoe ili tuweze kufunguka Macho maana Kila mahali nasiki hili nikigeuka huku nasikia hili.

Naombeni mwenye Full Data azimuvuzishe huku kwenye JF

Hii inachekesha, at any rate,

Maelezo gani mengine unataka yakufungue macho? Nakushauri piga simu, andika barua, au nenda halmashauri ya jiji ukapewe hizo "full data"
 
santa Matata,
Mkuu wangu hata upande wenu nipo vile vile ila jaribu kunielewa nimesimama wapi.
Kuhusu mpango wa mji mpya kama nilivyyousikia unapendeza sana akilini na nakubaliana nao sana..hapa ndipo hoja zangu zinatofautiana na zenu lakini kwa kuel3ewa WATU na MAZINGIRA ya nchi yetu swala la Kigamboni na mji mpya ni changa la macho...
Hata hivyo bado mimi nasema ni bora tuwe n a mpango wa mji mpya, ni bora zaidi kuwa na mpango mzuri wa mji ambao hata mbaadayte unaweza kufanyiowa marekebisho ya umiliki lakini sio kama Kariakoo ama mjini Dar iliojengwa sijui na Wahindi maanake hauwezi kurekebishwa tena zaidi ya kutumia nafasi ndogo zilizokuwepo...
Hao mafisadi kama kweli nia yao ni kuchukua ardhi hizo, wachukue lakini Ishaallah itakuja siku hizo ardhi zitawatokea puani, Tanzania ya leo somo zito...
Hata hizo nyumba walizochukua O'bay, Masaki na Chang'ombe, Ilala Kota bado nina imani ipo siku watafukuzwa kama mbwa koko, Dhulma hata siku moja haina malipo mazuri na mara nyingi hulipwa hapahapa duniani..
 
Watafika Mbwamaji?

Hapana Mkulu,

Hawafiki huko MBWA MAJI.
Wanaishia pale KIBUGUMU B na maeneo ya KIDETE mpaka shamba la NAFCO (shamba la Manji_) kwenye ule mto/sijui mfereji.
Gezaulole na kuendelea pako safi nadhani (in the meantime)
 
Kama kweli wewe ni kiongozi wa Tanzania na si fisadi yaani humiliki eneo kubwa la ardhi Tanzania ukifika Kigamboni utatamani kulia. Ukionyeshwa eneo la wazi amabalo limepingwa fensi kama yale mashamba ya settlers huko Zimbabwe utabaki mdomo wazi!

Yaani wewe vuka tu Mji Mwema, sogea mbele kama kilometa 15 utakutana na eneo la wazi limepigwa fensi majani ni yale yale ya asili (ya mungu) hajaweka chochote kamilikishwa na ardhi ninadhani ana mpango wa kuja kuvuna mafedha toka katika hilo eneo kama serikali italitaka.hilo ni Manji.

Ukisogea mbele zaidi utakutana na matangazo kibao, haya sasa ni ya mhindi mwingine yeye hajaweka fensi lakini eneo lake ni kubwa mara tatu ya la Manji. La Manji ukiliuza, watu wanasema ni heka 800. Huyo yeye kaweka matangazo kuwa ni marufuku hata kukata kuni, kuchunga ng'ombe nk.

Kwa nini viongozi wanaona ni sawa mtu kuchukua ardhi kubwa bila kuiendeleza? Au kwa kuwa wengi wamejitwalia kwa ajili ya future? Tunataka waziendeleze sasa!

Huu ni ubadhirifu greedy etc.
 
Mkuu Mkandara hatutofautiani kitu kuhusu haja ya kuwa na míji iliyotengezwa kwa mpango badala ya kuwa na miji ambayo inakua kama ni ajali ajali vile(unplanned). Ila hatuna watu wakutufanyia kazi hiyo kwa sasa. Kwa sababu hatuna serikali yenye bongo inayoona mbele. Na maadamu hatuna kitu kama hicho (serikali) ambacho ni muhimu katika kubuni mipango na kuisimamia kikiwa na baraka na imani ya wananchi basi tuiache ardhi ikae kama pori. Kwani itaoza?? Mbona Mwalimu JKN aliacha madini yetu kwa sababu kama hizo. Kama isingekuwa hii mibaka uchumi si wangekuja kufaidi wajukuu zetu?? Hata miji itajengwa tu, ama na kizazi chetu au kijacho. Jambo ambalo sitaki ni kuibiana kimacho macho kama ambavyo wizara ya ardhi (na serikali kwa ujumla) inafanya sasa.
Kuna suala la msingi ambalo tunapaswa kujiuliza.The so called "unplanned miji" imetokana na nini?
Nafikiri ni system yetu ambayo unademand mtu awe na offer,title na permit ya ujenzi halafu zote hizo upatikanaji wake ni mgumu sana, na hata vikipatikana hakuna support systems kama upatikanaji wa MIKOPO kwa ajili ya kufinance hayo majengo yanayotakiwa kwenye michoro ya Jiji.I THINK THE GOVT. SHOULD CREATE THE MARKET FOR THE SAME.

"unademand certain requirements, wakati hakuna support system ya kuwezesha hayo unayodemand yaweze kufanikishwa...NI NGUMU SANA.KESHO UNASEMA MIJI YETU HAINA HADHI....!!!!!!!

KAZI YA SERIKALI NI KUJENGA MAZINGIRA.THEN THE REST WAACHIWE WASWAHILI. HAWATOSHINDWA.
 
Kuna suala la msingi ambalo tunapaswa kujiuliza.The so called "unplanned miji" imetokana na nini?
Nafikiri ni system yetu ambayo unademand mtu awe na offer,title na permit ya ujenzi halafu zote hizo upatikanaji wake ni mgumu sana, na hata vikipatikana hakuna support systems kama upatikanaji wa MIKOPO kwa ajili ya kufinance hayo majengo yanayotakiwa kwenye michoro ya Jiji.I THINK THE GOVT. SHOULD CREATE THE MARKET FOR THE SAME.

"unademand certain requirements, wakati hakuna support system ya kuwezesha hayo unayodemand yaweze kufanikishwa...NI NGUMU SANA.KESHO UNASEMA MIJI YETU HAINA HADHI....!!!!!!!

NI KUJENGA MAZINGIRA.THEN THE REST WAACHIWE WASWAHILI. HAWATOSHINDWA.

KAZI YA SERIKALI



Mkulu,

Nakupa 10/10,maelezo yako yamejitosheleza.
Hakuna cha Kuongeza.
Ila kwa sababu wamezoea kujiwekea wao na familia zao,sisi walala hoi hatuna chetu tena huko.
 
Jamani mwenye details zaidi ya kilicho semwa juu ya hii issue na Waziri leo kwenye mkutano wake na viongozi wa Manispaa,tafadhali weka hapa ilituelewe kwa kina maana taarifa kwenye Luninga hazitoshelezi.
Wana habari tafadhali..................
 
Source: Uhuru 12.12.2008

CHILIGATI AWATOA HOFU KIGAMBONI.
1. Asema ardhi haijauzwa kwa Rais wa Marekani
2. Maslahi ya wananchi ndani ya mradi kuzingatiwa
3. Kufidiwa mali na mazao
4.kupatiwa viwanja vipya.

Waziri wa ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, John chiligati amewatoa hofu wananchi wa Kigamboni, Dar es salaam kuhusu mradi wa uendelezaji wa eneo hilo.
Amesema maslahi ya wananchi walio kwenye eneo la mradi wa uendelezaji wa mji mpya wa Kigamboni yatazingatiwa.

Chiligati alisema hayo jana alipozungumza na viongozi wa Manispaa ya Temeke, wakiwemo madiwani na maofisa watendaji wa kata, kwenye ukumbi wa JKT mgulani.

Mchakato wa mradi huo umeanza na kuwatia hofu baadhi ya wananchi, ambao wamekuwa wakidai kuwa eneo hilo limeuzwa kwa Rais wa marekani anayemaliza muda wake George W. Bush.

Waziri Chiligati alisema katika utekelezaji wa mradi huo, wananchi wenye nyumba na mazao ndani ya mradi huo watalipwa fidia na kupatiwa viwanja ndani ya eneo la mradi .

"Mradi huu ni tofauti na mingine iliyowahi kutekelezwa , ambapo wakazi husika waliondolewa. ktk huu wote watakuwa sehemu ya mradi kwa kupewa viwanja kwa ajili ya uendedelezaji" alisema chiligati.

Kwa mujibu wa taarifa za wizara mradi huo unatajariwa kutekeleza katika eneo la zaidi ya hekta 2,500 ndani ya kata za Kigamboni, Mji mwema, kibada na Vijibweni.

Utajumuisha majengo ya kisasa, huduma za jamii na ujenzi wa miundominu mbalimbali.
Chiligati aliyekuwa amefuatana na baadhi ya maofisa wa wizara hiyo, akiwemo Mkurugenzi wa Mipango miji Albina Burra na kamishna Msaidizi wa Ardhi, kanda ya mashariki Joseph Shewiyo, alisema wananchi watakuwa watekelezaji wa mradi huo kwa kushirikiana na wawekezaji.

Tofauti na miradi mingine alisema huu hautatekilezwa na serikali, bali kazi yake itakuwa kusimamia na kulinda maslahi ya wananchi.

Waziri alisema maslahi ya wananchi yatalidwa kwa kushirikiana ipasavyo kabla na wakati wa utekelezaji wa mradi.

Alisema wananchi walio ndani ya mradi watajenga kwenye viwanja watakavyopewa au kuingia ubia na wawekezaji kujenga kulingana na michoro itakayoandaliwa kwa ajiri ya mji huo.
 
Hivi waungwana wa hapa barazani,hii kitu ndio iliishia hapa hapa eeh.....!?
Nani alipata kumsikia na kumwona Waziri mwenye mamlaka na wizara ya Ardhi na makazi jana alipo kua kwenye kipindi cha PIMA JOTO cha ITV jana?
Alioorodhesha mipango rukuki ya wizara yake na kuhusu hizo mwenyewe aliziita kama Satallite Cities mfano;RUGURUNI na kwengineko katika wilaya zote za JIJI la DSM lakii cha ajabu hakuzungumzia KIGAMBONI kabisa na kama hata kama wana MPANGO wa kujenga hiyo sijui CITY ilaakarukakia kusema wana MPANGO HUU kwa KIMBIJI more than 12-20 kms from DSM.
SASA swala hili lina baki pale pale je KIGAMBONI kuna MPANGO GANI?
 
Jamani kama kuna mtu mwenye access au ujuzi wa kutumia ile website ya MWANAHALISI la jana tarehe 15 mwezi huu wa nne,kuna makara mmoja kwenye page ya 12 inafaa kuwekwa hapa ili wadau wengine wasome kuhusu swala hili.
Napenda kuwakirisha
 
Jamani kama kuna mtu mwenye access au ujuzi wa kutumia ile website ya MWANAHALISI la jana tarehe 15 mwezi huu wa nne,kuna makara mmoja kwenye page ya 12 inafaa kuwekwa hapa ili wadau wengine wasome kuhusu swala hili.
Napenda kuwakirisha

kweli ww mzungu. au mkurya?
 
tatizo hamjajua kosa lenu. "Kikulacho ki nguoni mwako". Kama ilivyokuwa Kibamba wakachagua wabunge, madiwani, wenyeviti wa mitaa n.k kutoka CCM nanyi inaelekea mlifanya hivyo hivyo. Hao hawana ajenda ya kuwatetea wananchi kama ambavyo mbunge wa Jimbo la Ubungo na Diwani wa Kata ya Kibamba walivyokaa kimya wakati ardhi ya wananchi inaporwa kinyemela. Soma katika habari mchanganyiko UPORAJI WA ARDHI.
 
Tena Waziri mwenye mamalaka ya ardhi kwa kuwaongopea wananchi usiseme. Tarehe 25 May 2008 aliwaahidi wakazi wa Kibamba kuwa wizara yake itafanya utafiti wa bei za soko la ardhi na ujnenzi ktk kata ya Kibamba na kisha atakutana nao ili kujadili viwango vitakavyotumika kuwalipa fidia. Hiovyo wawaruhusu wathamini mali wafanye uthamini wakati utafiti wa soko ukiendelea. Wananchi wakaingia mkenge kuruhusu uthamini ufanyike kisha akaingia mitini na wizara ikaimpose viwango inavyotaka ambavyo vilikuwa ni only 13% of the prevailing market prices.

Ajenda yake ni kufanikisha utwaaji wa ardhi kutoka mikononi mwa wananchi by all dubious means. Kajifunzeni Kibamba. Mkakati sahihi wa kuhakikisha ardhi uliyoanayo inakukwamua kiuchumi ni kwa fedha mbele makaratasi nyuma. Watu kutoka ardhi wakija kwako kwanza waulize bei gani kabla ya kuweka sahihi yako popote pale. kwa mtindo huo hawana ubavu. Mkiingia mkenge mkafanya tamaa kama watu wa Kibamba mkasaini kwanza documents zozote kabla ya bei kutangazwa wazi wazi mmekwisha
 
Tena Waziri mwenye mamalaka ya ardhi kwa kuwaongopea wananchi usiseme. Tarehe 25 May 2008 aliwaahidi wakazi wa Kibamba kuwa wizara yake itafanya utafiti wa bei za soko la ardhi na ujnenzi ktk kata ya Kibamba na kisha atakutana nao ili kujadili viwango vitakavyotumika kuwalipa fidia. Hiovyo wawaruhusu wathamini mali wafanye uthamini wakati utafiti wa soko ukiendelea. Wananchi wakaingia mkenge kuruhusu uthamini ufanyike kisha akaingia mitini na wizara ikaimpose viwango inavyotaka ambavyo vilikuwa ni only 13% of the prevailing market prices.

Ajenda yake ni kufanikisha utwaaji wa ardhi kutoka mikononi mwa wananchi by all dubious means. Kajifunzeni Kibamba. Mkakati sahihi wa kuhakikisha ardhi uliyoanayo inakukwamua kiuchumi ni kwa fedha mbele makaratasi nyuma. Watu kutoka ardhi wakija kwako kwanza waulize bei gani kabla ya kuweka sahihi yako popote pale. kwa mtindo huo hawana ubavu. Mkiingia mkenge mkafanya tamaa kama watu wa Kibamba mkasaini kwanza documents zozote kabla ya bei kutangazwa wazi wazi mmekwisha



Moja ya tatizo kubwa ni wengi wetu (me included) kutozifahamu sheria. Wiki iliyopita kwenye KipimaJoto ilielezwa kwamba thamani ya ardhi unayopaswa kulipwa fidia sio ya soko la sasa. Ardhi itathaminishwa kwa kuzingatia thamani yake kabla ya serikali kutangaza azma ya kuendeleza makazi au miji mipya.
Sheria inaelekeza tofauti na watu wanavyofikiri.
 



Moja ya tatizo kubwa ni wengi wetu (me included) kutozifahamu sheria. Wiki iliyopita kwenye KipimaJoto ilielezwa kwamba thamani ya ardhi unayopaswa kulipwa fidia sio ya soko la sasa. Ardhi itathaminishwa kwa kuzingatia thamani yake kabla ya serikali kutangaza azma ya kuendeleza makazi au miji mipya.
Sheria inaelekeza tofauti na watu wanavyofikiri.

Ergo.... sheria ya ardhi ina hitlafu kubwa na inahitaji marekebisho! Akina Tundu Lissu wameipigia kelele sana, wakaonekana ni wakorofi, mi nawashauri wakazi wa huko Kigamboni na Kibamba wamtafute Tundu Lissu au LEAT wawatetee mahakamani.
 
Ergo.... sheria ya ardhi ina hitlafu kubwa na inahitaji marekebisho! Akina Tundu Lissu wameipigia kelele sana, wakaonekana ni wakorofi, mi nawashauri wakazi wa huko Kigamboni na Kibamba wamtafute Tundu Lissu au LEAT wawatetee mahakamani.

Mkulu,

Kidogo mawazo yako yanatoa mwanga katika hili sakata,insited ya kuandamana na kugomea mikutano ni UBORA tukafungua KESI mapema tukapambana nao MAHAKAMANI.
Kwa wachangiaji wengine,tatizo hapa sio KUUZA ardhi yetu,mimi binafsi siuzi ya kwangu hata kwa BILIONI 2,nitakacho ni kuwa na haki na ardhi yangu ambayo ndio itakua makazi yangu ya kudumu kwangu na wajuu wangu.Serikali inanitaka nisimamishe ujenzi mwaka jana mwezi wa 12,wakati wao kwa mujibu wa WAZIRI na MAKALA ILE YA MWANAHALISI watatoa tamko rasmi mwezi wa kumi (10) mwaka huu.Ila mwaka jana walisema wangetoa hilo tamko mwezi wa kwanza (1)
 
Back
Top Bottom