Tukutane hapa watumishi ambao hawategemei mishahara, tuelezane changamoto na mbinu

Mimi ni mtumishi nimekua nikinunua bidhaa zangu online kupitia kwenye company ya www.digxam.co wako Japan na Tanzania

Kiukweli waga sigusi mshahara wangu nimenunua member ship wakinutumia mzigo wa milion moja wa laptops nikiuza Napapata milioni kwa muda wa week moja, mzigo wa simu napata vile vile
Hebu fafanua kidogo kuhusu hiyo Kampuni kama haina longolongo. Ofisi zao kwa Tanzania zinapatikana wapi?

Na hizo bidhaa ni used, au ni brand new?
 
Mimi binafsi sio mtumishi serikalini ila ntachangia machache ninayoweza wakuu

Kwanza, ukiajitiwa iwe serikalini au sekta binafsi usikimbile kuoa au kuolewa, au kuzaa mtoto au watoto. Wekeza kwanza kwenye uchumi angalau miaka 5 nipo uanze hayo mengine.

Pili, ukiajiriwa popote ple usibadili mfumo wako wa maisha kwa zaidi ya 40%,ni kweli ulikwa umechakaa sasa unatakiwa upendeze kiasi na ule vizuri ila sasa unapoanza kutoka usiku kwenda club au bar kisa una uhakika wa mshahara ndipo unapoanza kuharibu uchumi wako.

Tatu, unapoajiriwa popote pale jitahidi sana kuona fursa za kiuchumi nje ya ajira zichambue kisha kusanya mtaji wako baada ya miaka miwili anza kuifanya fursa moja wapo.

Nne, kamwe sinunue gari la mkopo hata kama utashawishiwa vipi hapo kazini kwenu. Ukiona unanunua kwa mkopo jua huwezi kulimliki hilo gari fuata kanuni ya nunua kitu unachoweza kukinunua mara mbili.

Mwisho kabisa, uisubiri ukastaafu ndipo ukaanza biashara yoyote, hautaiweza. Kama umeshastaafu au unaelekea kustaafu na una vijana wakubwa fanya utaratibu wa kufungua biashara ya familia wewe usimamie fedha wao waifanye hiyo biashara na muheshimianekama wafanyabiashara sio baba/mama na wanawe maana mtafeli.

Vikubwa vya kuepuka ni;
1. Starehe
2. Kuiga maisha ya watu
3. Uwizi kazini
4. Kuridhika na mshahara
Ahsante ingawa Ww mkuu unaongea theory sana kuliko mtoa mada, Yeye kaonyesha vitu vinawezekana. Vyako ni vigumu kutekelezeka cause sometimes family inakuja automatically hata kabla ya kazi so tell us what we can do after.....
 
Nimefungua huu uzi kwa ajili ya kuwakutanisha watumishi wote wenye idea ya ujasiriamali, wanaofanya biashara,kilimo,ufugaji na wanaotarajia kufanya biashara, kilimo na ufugaji n.k

Kwa ugumu wa maisha jinsi ulivyo mfumuko wa bei ni ndoto kwa sisi watumishi wa halmashauri kutoboa, Kuna clip moja wasira alisema "mshahara unakupa pesa ya kula tu na kuvaa" na huo ndio ukweli. Bei ya mchele inapepea, sukari juu mafuta juu, Mwisho wa mwezi unabaki na madeni na kuishi kwa kuomba omba na kubangaiza kwanini tusidharaulike na waendesha bodaboda?

Nimetembea mazingira mengi kabla ya kuajiriwa kama Mwalimu na baada ya kuajiriwa, nimeona watumishi wengi waliofanikiwa humu humu kwenye ajira ya serikali, Nawasifu walimu na watumishi wengine waliopo mijini, Kuna Shule moja nilienda nikakuta magari yamepaki japo ni IST Lakini ni sign mojawapo ya kuanza kujikwamua kiuchumi, at the same time wewe unaenda kwenye kituo chako Cha kazi na baiskeli na sio kwamba umeamua kununua baiskeli kwa sababu ya mazoezi hapana ni kwa sababu ya ugumu wa maisha, kwanini bodaboda asitudharau?

Kwenye Maofisi huko unaona kabisa nyuso za watu zikiwa zimekata tamaa kabisa, furaha hakuna maisha Magumu, je ni kweli duniani tumekuja kuteseka? Je wenye biashara mijini/ vijijini ni smart sana kuliko sisi? Tunakwama wapi?

Unakuta mtumishi Kadi ameiacha kwenye hizi ofisi ndogo za kukopesha ambao hawajali 1/3 ya mashahara. Yoote ni ugumu wa maisha na pesa amechukua alichofanyia hakionekani, tunavaa na tunakaa kwenye nyumba kama vile hatulipwi mishahara.

Nafahamu humu Kuna watumishi ambao walijiongeza/ wanajiongeza je waliwezaje? Kipi kifanyike kwa mtumishi kujikwamua kiuchumi?. Wanawezaje kusimamia? Vipi kwa walioko halmashauri ya Kijijini wafanye nini!

Idea yangu ni hii kwa watumishi, Naanza na estimation ya mtaji wa million 5 ambayo Kila mtumishi anaweza kuimudu.

1. Kufungua duka la nafaka mbalimbali (5million unaweza Anza)
2. Duka la simu na vifaa vyake
3. MPESA, TIGOPESA, WAKALA WA BANK ZOTE (wengi wanafanya)
4. Duka la viatu vya kike aina zote za viatu
5. Duka la vinywaji baridi (it depend na location na mkoa ulipo)
6.kilimo (Kuna mabonde ambayo yana maji na hawategemei mvua ekari 300,000)....

Ongeza na za kwako na changamoto yako, action na implementation ni muhimu tuache ngojera, na tukimbie dharau ndogo ndogo.
Mimi sio mtumishi mkuu, ni wapi huko kuna mabonde hawategemei mvua ili tukalime...
 
Mkuu hizo Habari unaingia hapo unawauliza Kuna namba ya simu ya Japan na Tanzania

Misiwezi kuwaelekeza watumishi wenzangu sehemu ambayo sio sahihi
Hapa sasa ndiyo umenipa walau mwanga wa kitu cha kufanya.
 
Nami nasubir ukianza kutoa Elimu ya hiyo company
Hapo kuna platforms ambazo wauzaji wa bidhaa wakikwa sehemu mbalimbali ikiwepo Japan South Africa Dubai Tanzania wamejisajili pale kwenye online platform wengi ni Watanzania wanaushi nje ya nchi na wanatangaza na kuuza bidhaa zao kupitia pale.

Unaweza kumtafuta seller moja ukamwambia unataka nini akakutafutia kuweka order Kisha ulalipa kwa njia za kawaida bank kama CRDB NMB au kwenye simu unaingia kwenye menu unachugua kampuni unalipa

Ukifanya malipo weka kumbukumbu namba ya Jina unalotumia kwenye website yao.

Mizigo ikijaa wanapakia kwenye container wasafirisha na kule huku Kisha wanalipoa ushuru wa custom wanakupigia unawapa maelekezo mzigo wako utafikaje
 
Mimi binafsi sio mtumishi serikalini ila ntachangia machache ninayoweza wakuu

Kwanza, ukiajitiwa iwe serikalini au sekta binafsi usikimbile kuoa au kuolewa, au kuzaa mtoto au watoto. Wekeza kwanza kwenye uchumi angalau miaka 5 nipo uanze hayo mengine.

Pili, ukiajiriwa popote ple usibadili mfumo wako wa maisha kwa zaidi ya 40%,ni kweli ulikwa umechakaa sasa unatakiwa upendeze kiasi na ule vizuri ila sasa unapoanza kutoka usiku kwenda club au bar kisa una uhakika wa mshahara ndipo unapoanza kuharibu uchumi wako.

Tatu, unapoajiriwa popote pale jitahidi sana kuona fursa za kiuchumi nje ya ajira zichambue kisha kusanya mtaji wako baada ya miaka miwili anza kuifanya fursa moja wapo.

Nne, kamwe sinunue gari la mkopo hata kama utashawishiwa vipi hapo kazini kwenu. Ukiona unanunua kwa mkopo jua huwezi kulimliki hilo gari fuata kanuni ya nunua kitu unachoweza kukinunua mara mbili.

Mwisho kabisa, uisubiri ukastaafu ndipo ukaanza biashara yoyote, hautaiweza. Kama umeshastaafu au unaelekea kustaafu na una vijana wakubwa fanya utaratibu wa kufungua biashara ya familia wewe usimamie fedha wao waifanye hiyo biashara na muheshimianekama wafanyabiashara sio baba/mama na wanawe maana mtafeli.

Vikubwa vya kuepuka ni;
1. Starehe
2. Kuiga maisha ya watu
3. Uwizi kazini
4. Kuridhika na mshahara
Safi sana mkuu!

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Hili tangazo
Mimi ni mtumishi nimekua nikinunua bidhaa zangu online kupitia kwenye company ya www.digxam.co wako Japan na Tanzania

Kiukweli waga sigusi mshahara wangu nimenunua member ship wakinutumia mzigo wa milion moja wa laptops nikiuza Napapata milioni kwa muda wa week moja, mzigo wa simu napata vile vile
Hili ni Tangazo tu kama matangazo mengine..
 
Vijana subilia niwambie msiishi katika nadharia suala la kujikwamua kiuchumi ni wazo zuri Ila mtambue mafanikio si kwa wote Kwenye kila jambo iwe siasa, biashara, elimu nk hapa tuambiane ukweli watumishi wengi wa umma huingia katika huu mtego wa kuamini wakikopa wakiwekeza kwenye biashara ndio njia sahihi ya matumizi ya mkopo Ila akikopa akinunua kiwanja au akijenga si njia sahihi, anasahau yeye kashapoteza umri kwenye kusoma nk

Kipindi wewe upo shule wenzako wapo mtaani Wana pitia uzoefu na changamoto za biashara so wanaheshimu kipato Cha biashara sababu ndio ajira zao ndio elimu zao Kama wewe unavyotamba na ujuzi wako so nachotaka kusema nini

Vijana wa Sasa mnao ajiliwa mnaharaka na maisha hizo haraka haraka zenu ndio unajikuta unakosa vyote na kuona ajira haina maana bora biashara kwanini unataka biashara sababu uijui unataka kilimo kwa sababu ukijui kuwa uko napo Kuna changamoto zake hivyo basi Kama wewe mtumishi wa umma usikope ukabeti pesa ya mkopo kwenye biashara narudia usikope ukaenda kubeti kwenye biashara utalia nachokushauri

Kopa mapema pesa kidogo kwa mda mdogo nunua kiwanja, samani za ndani tulia utachekwa Ila tulia ishi usiwe na haraka na maisha kikubwa uhai sawa, tulia mkopo ukiisha huo wa miaka miwili, kopa tena miaka mitatu endeleza kiwanja chako inua boma lako mpaka usawa wa kupaua, tulia ishi, kula vizuri vaa vizuri achana na story za ujenzi hiyo miaka mitatu ipite, sawa miaka mitatu ikipita mkopo wako ukiisha nenda sasa kakope ule mkopo wa kinua mgongo yani mkopo wa miaka nane vuta mzigo wote Kisha nenda kapaue nyumba yako weka milango madilisha piga ripu, weka umeme, maji Kisha hamia kwako, ukishamia kwako hapo Sasa ndio anza kamali na pesa zile za top up million tatu nne unapeleka uku ikipotea unatulia unatafuta nyingine tena sijui kwenye kilimo nk yani unabeti upo kwako kumbuka hapo upo kwako ndani ya miaka mitano ya ajira ujaishi kwa shida ulikua unafurahia maisha na una mipngo yako na upo kwako so ndani ya miaka kumi utaishi katika ndoto zako cause una mji wako pia una deal zako zinazokupa pesa ya kusukuma maisha

Sasa wewe chukua mkopo wa kinua mgongo yani mkopo wa miaka nane kabeti kwenye biashara au kilimo hiyo pesa kikipotea uko majanga unatulia miaka Saba unakopa tena inaanza plan zako kumbuka hapo yule mwenzako aliyekopa kidogo akaanza na ununuzi was kiwanja ndani ya hiyo miaka Saba ambayo wewe ulibeti yeye yupo kwake na anafanya ambacho wewe ukitaka awali kikaferi, na hiyo miaka Saba mwenzako aliishi vizuri bila stress maana anajua pesa ilienda wapi Ila wewe una stress maisha pesa huna maisha huna

Asikwambie mtu maisha ya kibongo makazi Yani nyumba kwanza ambao hawamini nyumba kwanza wanazo nyumba za urithi za baba zao na mama zao
 
Back
Top Bottom