Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Naona mabitozi wa Yanga na afro zao......wachezaji wa zamani walikuwa strong miili mikubwa mikubwa siku hizi miili hii imepotelea wapi?

N.B Thanks Mods
 
Shabaan Dede alihamia Sikinde akitokea Juwata Msondo ngoma ambapo hadithi ni kuwa alinyang'anywa unifomu wakiwa wanapiga mziki.

Mkuu Kishoka,

Heshima mbele, uliyosenma ni sawa kabisa lakini kidogo tu unajua nilifikiri alitoka Msondo Ngoma na kuingia Bima Lee ndio akaenda Sikinde, ambako wimbo wake wa kwanza akiwa Bima Lee ulikuwa "Samaki Baharini Huishi Vipi" akaanzisha na mtindo mpya wa "Magneti Tingisha", hakukaa sana akenda Sikinde, na baadaye kurudi tena Msondo Ngoma,

Anyways ni zamani sana kwa hiyo ninaweza kuwa nimepitiwa mkuu, ila respect kwa kipande chako cha historia.
 
Mchongoma

) kuwa kama wao ni Ogelea Piga Mbizi basi yeye ni chunusi na wasithubutu kuchezea majini tena. Nyimbo zake zilikuwa heavy sana kuliko za hao Marquiz. Hebu chukua nafasi usikilize wimbo kama Marashi ya Pemba au Kesi ya Kanga ndipo ujue kuwa Freddie(RIP) kweli alikuwa Supreme


..ogelea ..ogelea piga mbizi....

wewe na yulee..

ogelea ..ogelea ..piga mbizi...

mimi na wewe..

ogelea ..ogelea ..piga mbizi....

mimi na wewe..eeeh ..mimi na wewe ehh..

then ..

chunusi eeh

eeeeeeeh

chunusi eeh..

eeeeeeh

chika chika !! chika chika!!!

alafu endelea..[dunia msongamano asema maama,nimeyaona leo ..nakubali mie...

OSS chini ya gurumo ...baada ya kisima kuachana na wazairwaa....

akaja na..

usimchezee chatu..ohh..chatu eh..

gongo usimtupie ..utaukosa ushindi...[endelea]

natoa onyo kwa yeyote anayemchezea chatu ni hatari...atakuwa asipate lolote la manufaa..na ajali imkute bila ya kutegemea ...atakuja hadhirika ajute na dunia..[gurumo huyoo..kifaa..sauti isiyoigika..]

...mwisho mwisho kabla marquee du zaire hawajafikia mwisho wa reli..walikuja na....

staili...

chini ya muti ...ale washa washa aa ..ale washa washa a!!
 
WildCard,

Kuna Empire kubwa sana East and Central Africa, inaitwa Bahima kama sikukosea ambayo ni shina ya makabila kadhaa yaliyoko Rwanda, Congo, Burundi, Tanzania, Uganda mpaka Kenya.

Katika ugomvi wa sasa kati ya Museveni na Kagame, chimbuko lake ni hilo la wao wawili kutoka shina moja na ndio maana Museveni anautaka sana ukuu wa EAC!

Sasa kabila la Nyerere Zanaki, inasemekana ni Bahima Empire.

mkuu katika nyanja za siasa za eneo hilo kuna kitu kinachodaiwa kuwepo kwa nia ya kuanzishwa kitu kinaitwa "kilimanjaro republic" ambapo sehemu kubwa itakuwa hiyo bahimba.
hata hivyo kwa makusudi au bahati mbaya wahusika hawataki kabisa kuligusa hili jambo na wakiligusa wanadai ni uzushi tuu sijui kwa nini.
 
Kwikwikwiiiiiii.....Ndivyo Tulivyo!!!

Wengine tulikuwa tunaenda pale posta ya zamani kuangalia meli......

hahahaha umenikumbusha enzi zile wakati wanafunzi wa forodhani sec jamaa
walikuwa wanashangilia wasikiapo honi ya meli/tug boats wakati inaingia au kutoka bandarini. wakati huo utakuta 2/3 ya darasa wana vitabu (passport) na njozi yao ilikuwa kuzamia. kweli miaka yapita
 
Last edited:
enzi za raha nje ya mki ikifika jioni magari ya bendi yanapita ,,,basi la sikinde linapeleka watu DDC MLIMANI PARK...........OSS WANASOMBA WATU HADI KIMARA RESORT.....JUWATA AMANA KAMA KAWAIDA....WATOTO WA MARQUEE PALE PALE LANGATA SOCIAL HALL.......RAHA TU HADI ASUBUHI...

,..BAADAYE DR KHALID ALIKUJA KUIGA HII STAILI YA KUSOMBA WATU WAKALE RAHA MAKONDEKO [PEPONI]AKAFILISIKA....I DONT KNOW WHERE HE WENT WRONG.....

HAPO WAZEE HAMJAWAKUMBUKA......MAKASSY ORIGINAL;...NA MJOMBA WAKE ..DR REMMY ONGALA...[ACHA BWANA HUYU BWANA NAMPENDA SANA ..KAMA BOB MARLEY KWA TUNGO ZAKE..SIO NYIMBO ZA LEO KUTAJANA MAJINA BILA UJUMBE]]..

..WAKATI HUO MAGAZETI YA MZALENDO KAMA LEO ..NI DILI...BENDI ZOTE KARIBU 40 KILA MOJA INASEMA ITAKUWA WAPI.....NA KILA UKUMBI WA SENEMA UNASEMA UNA MOVIE GANI...HADI KIBISA NGOMA TROUPE..ACHA BWANA..RAHA ZIKO WAPI SIKU HIZI KWA MATAJIRI TU!!!..[NANI ANA KIPANDE CHA GAZETI LA MZALENDO ENZI HIZO ...70-80"S ATUWEKEE RATIBA YA BURUDANI,...VIJANA WAONE..]
 
1. Unajua Tanzania, pamoja na siasa zetu enzi zile, lakini bado tulikuwa na nafasi ya ku-socialize hasa kwenye ma-Disco na muziki wa Dance, kwenye hili ni lazima tuwe fair kuwa Mwalimu hakuwa na tatizo kabisaa.

2. Ni kweli kwamba ex- DJ Gerard, au kama alivyokuwa akifahamika kwa jina la "Jerry Kotto", alitokea kuwa mmoja wa the best DJs mjini Dar, na ni kweli kwamba alikuwa na matatizo ya kusoma, lakini Jerry alikuwa na tabia moja nayo ni akipata Album au Tape hukaa chini na kuisikiliza mwanzo mpaka mwisho, akisikia ngoma anayoamini kuwa ni safi basi husimamisha na kuweka alama kwanza kwenye Tape/Album na pia kwenye namba ya ile song, sasa akingia kupiga Disco huzikumbuka nyimbo zote zilipo na ni zipi, tena bila ya tatizo.

3. Kwa kadri ninavyokumbuka tumewahi kuwa na Ma-DJ waliokuwa waburudishaji na wakali, kwa sababu pamoja na kwamba wao yaani ma-DJ walikuwa sio wapigaji hasa wa zile nyimbo, lakini siku zote mchele ni ule ule, ila mapishi ndio hubadili matokeo, hata ma-DJ nao ilikuwa ni hivyo hivyo, kwa kweli ningeomba kuwakumbuka tena kwa nafasi zao, wale wote yaani ma-DJ waliowahi kutuburudisha mjini Dar kama ninavyowakumbuka na pia msaada unakubalika iwapo kuna niliowasahau au kuwaweka kwenye nafasi wasizofaa:-

1. DJ Justin Kusaga - Clouds (Morogoro).
2. DJ Kali Kali (Kalikawe) - YMCA/Mbowe.
3. DJ Ebbo Night Woo Jack! (Bob Rich Mazula) - Msasani Beach.
4. DJ Chris Phaby "The Lover" - Mbowe/Margott.
5. DJ Choggy Sly (Choggo Salum) & DJ JPP (John Peter Pantalakis) - Msasani Beach/Rungwe Beach
6. DJ Roma Pop Juice (RIP) - Mwanayamala.
7. DJ Jerry Kotto (Gerard) - Mbowe RSVP Club.
8. DJ Nigger Jay - YMCA.
9. DJ DC Washington (RIP) - Rungwe Beach.
10. DJ Lucas
11. DJ Tito Jackosn (Tito Kalumanga) - Rungwe Beach.
12. DJ John Bure
13. DJ Joe Kusaga (Joseph Kusaga) & DJ Stewart (Sterwart Chiduo) - Clouds.
14. DJ Kim (Kim) - Rungwe Beach.
15. DJ Kessy (Kessi) - Blue Sky Disco.
16. DJ Eddy - Magomeni.
17. DJ Super Deo (Deo) - YMCA/Margott.

4. Kwa upande wa muziki wa Dance, pia tilkuwa na bendi za wazawa na wageni, hasa kutoka Zaire na wao pia kulingana na nafasi zao kimuziki as I remmember, na time pia lakini pia msaaada unakubalika:-

1. End of The 60s:-

1. Orch. Morogoro Jazz - Mbaraka Mwinshehe (RIP).
2. Orch. Cuban Marimba - Salum Abdallah (RIP).
3. Orch. Nova Success - Baba Gaston (Nairobi).
4. Orch. Nuta Jazz - Muhidini Gurumo (Ilala - Msondo Ngoma).
5. Orch. Tabora Jazz - Wema Abdalalh/Shem Karenga (Tabora).
6. Orch. Western Jazz - Wema Abdallah (Sikukuu street Kariakoo, Dar).
7. Orch. Dar Jazz - Dar.
8. Orch. Unyanyembe Jazz - (Nyanyembe Tabora.)
9. Orch. Kilwa Jazz - Ahmed Kipande/Juma Mrisho (Kilwa).
10. Orch. Police Jazz - Dar.
11. Orch. Atomic Jazz - John Kijiko (Tanga).
12. Orch. Kilombero Jazz - (Kiwanda cha Sukari Kilombero).
13. Orch. Butiama Jazz - Ifakara.
14. Orch. Boma Liwanza - (Zaire/DSM).
15. Orch. Banangenge - Fataki Masumbuko Ya Dunia (Zaire/DSM).

2. In the 70s. to 80s:-

1. Orch. Super Volcano - Mbaraka Mwinshehe (Morogoro).
2. Orch. TK Lumpopo - Juma kilaza (Morogoro).
3. Orch. Afro 70 - Patric Balisidya (DSM).
4. Orch. Urafiki Jazz - Juma Mrisho (DSM).
5. Orch. Nuta Jazz - Muhidini Gurumo (DSM).
6. Orch. Marquiz du Zaire - Chinyama chiyanzi (Zaire/DSM).
7. Orch. Vijana Jazz - Andoro/Maneti (DSM).
8. Orch. Safari Trippers - Marijani Rajabu (DSM).
9. Orch. Mwenge Jazz - George Mpupua (JWTZ- DSM).
10. Orch. JKT Kimbunga - Mzee Zakaria (DSM).
11. Orch. Kimuli muli - Zahiri Zoro (JKT Mafinga/DSM)
12. Orch. Simba Wa Nyika - Wilson & George Peter (Arusha/Nairobi).
14. Orch. Dar International - Abel Baltazari/Marijani Rajabu (DSM).
15. Orch. Police Jazz - Moshi William (DSM).
16. Orch. BarKeys - George Mhando (DSM).
17. Orch. Sola TV - (Temeke - DSM).
18. Orch. Makassy - Mzee Makassy (Zaire/DSM)
19. Orch. Nkashama Nkoi - Ndala Kasheba (RIP) (Zaire/DSM).
20. Orch. Matimila - Remmy Ongalla (Songea/DSM).
21. Orch. Sunburst - Kassim Magati (DSM).
22. Orch. Tanzanite - Nembo (DSM).
23. Orch. Toma Toma - Thomas (DSM).
24. Orch. Mpakani Kyauri Voice - Mzee Khatibu Itei Tei (DSM).
25. Orch. Mlimani Park - Abel Baltazari/Gurumo (DSM).
26. Orch. Doble O - King Kiki (Zaire/DSM).
27. Orch Safari Sound - Mbombo wa Mbombo-Ka/King Kiki/Ndala Kasheba (Zaire/DSM).
28. Orch. Mk Group - Kossongo Mpinda/shem Karenga (DSM).

Huenda kuna niliowaacha, lakini ninaamini kuwa ma-DJ tulionao sasa na bendi za muziki, ni kuanzia in 90s hadi leo ni almost wale wale na bendi ni zile zile ingawa cha kusikitisha sana ni kwamba kama ni bendi zilizopo leo labda hazizidi nne, zingine zote zilikufa kifo cha mende, lakini ni vyema kukumbuka kuwa katika enzi zile za 70s, 80, na mwanzoni mwa 90s pamoja na msiha kuwa magumu kidogo siku zote tulikuwa na burudani kabambe ambazo some of us zilitusaidia sana kuendelea kuyakabili maisha, knowing kwamba kuna weeek end kwenda kula mangoma na kuku za kibongo bongo.

Heshima Mbele Wakuu.

mkuu heshima mbele kwa kumbukumbu kali.

ongezea stc/biashara jazz band

nakumbuka marijani rajabu (RIP) baada ya kutoka olympio primary ambako alikuwa nyanda/golkipa mzuri tuu na mpiga ngoma kubwa katika bendi ya shule
alikwenda bendi ijulikanayo kama stc jazz band na baada ya hapo ndipo akaanzisha safari trippers.

nawakumbuka pia familia ya akina kapinga (george, amato na abraham) ambao wote walikuwa katika timu ya waanzilishi wa bendi ya the barkeys.

kweli tumetoka mbali
 
enzi za raha nje ya mki ikifika jioni magari ya bendi yanapita ,,,basi la sikinde linapeleka watu DDC MLIMANI PARK...........OSS WANASOMBA WATU HADI KIMARA RESORT.....JUWATA AMANA KAMA KAWAIDA....WATOTO WA MARQUEE PALE PALE LANGATA SOCIAL HALL.......RAHA TU HADI ASUBUHI...

,..BAADAYE DR KHALID ALIKUJA KUIGA HII STAILI YA KUSOMBA WATU WAKALE RAHA MAKONDEKO [PEPONI]AKAFILISIKA....I DONT KNOW WHERE HE WENT WRONG.....

HAPO WAZEE HAMJAWAKUMBUKA......MAKASSY ORIGINAL;...NA MJOMBA WAKE ..DR REMMY ONGALA...[ACHA BWANA HUYU BWANA NAMPENDA SANA ..KAMA BOB MARLEY KWA TUNGO ZAKE..SIO NYIMBO ZA LEO KUTAJANA MAJINA BILA UJUMBE]]..

]

...Katika ma convoy ya wakati ule wanamuziki wa ki Zaire wanaingia nchini, enzi za Orch Makassy, Orch Marquize du Zaire, kuna anayemkumbuka GOBBY/GOBBIE?... Huyu naye alikufa kifo cha 'kutatanisha' kama marehemu Zengekala, talking about miaka ya 70's hiyo...

mwenye kumbukumbu ya kisa hicho atuhabarishe tafadhali, nadhani Gobbie alivuma kabla ya Ramadhan Mtoro Ongala hajaanza kuvuma na Orch Makassy


nawakumbuka pia familia ya akina kapinga (george, amato na abraham) ambao wote walikuwa katika timu ya waanzilishi wa bendi ya the barkeys.

...Wow! BARKEYS,...! ...miziki ya kizungu hao, kina TANZANITES, CHEZIMBA,... Son of Alaska, umekumbushia Disco Sansui Seaview wow nasikia dancer mashuhuri enzi hizo, Abdul-CARLOS sasa amekuwa mhubiri jijini London, ama siku hazigandi!...


Disco BIRIBI Salander bridge Club!... Gogo Disco hotel Africana... wakati huo lami (Bagamoyo Road) inaishia maeneo ya kijiji cha makumbusho kijitonyama, kisha vumbi mpaka makutano ya Bahari Beach, Kunduchi Hotels...
 
On a serious note, Environmental/Mazingira;

attachment.php

...Mlima Kilimanjaro wakati huo. Pamoja na kuwa mlima mrefu kuliko yote Africa, ungali upo kwenye Equator, Mlima Kikimanjaro ulikuwa unasifika kwa uoto wake wa asilia, Viumbe hai na wanyama wadogo wadogo pamoja na maji yanayotiririka toka mlimani. Ni kivutio tosha cha utalii nchini Tanzania, hasa kwa kuwa haupandiki kupitia Kenya!

attachment.php

...Mlima Kilimanjaro unavyoonekana sasa, barafu ile ya miaka ile inayeyuka kwa kasi ya kutisha, huenda hivi karibuni ikabaki historia tu kuwa Mlima Kilimanjaro ulikuwa na theluji kwenye kilele chake kama Cpt Nyirenda alivyoonekana akiisimika Bendera ya Taifa.
 
Nondo!...

attachment.php


...katabia ka 'plane-spotting', au kwenda kuangalia meli nadhani kulichangiwa sana za ndoto za "...ipo siku nami nitaukata!", ...kuna walokuwa na daydreaming siku wakizamia melini watabeba chapati na Sun-Vita Orange squash za kusurvive nazo siku kadhaa wakiwa wamejichimbia eti huko Engine room nk!
 
Mkuu Kishoka,

Heshima mbele, uliyosenma ni sawa kabisa lakini kidogo tu unajua nilifikiri alitoka Msondo Ngoma na kuingia Bima Lee ndio akaenda Sikinde, ambako wimbo wake wa kwanza akiwa Bima Lee ulikuwa "Samaki Baharini Huishi Vipi" akaanzisha na mtindo mpya wa "Magneti Tingisha", hakukaa sana akenda Sikinde, na baadaye kurudi tena Msondo Ngoma,

Anyways ni zamani sana kwa hiyo ninaweza kuwa nimepitiwa mkuu, ila respect kwa kipande chako cha historia.



Dede kabla ya kwenda Sikinde alikuwa msondo. Ni mpenzi mkubwa wa Simba, siku hiyo Simba ilikuwa inacheza na Coastal. Dede akakacha onyesho la Msondo akaenda mpirani. Alivyorudi ukumbini baada ya mechi akatimuliwa na kunyang'anywa uniform. Hapo ndio akarudi Mlimani na kutunga nyimbo ya 'Talaka Rejea' yenye kuelezea masahibu yaliyomkuta. Alidai msondo kuna 'msondo-NUTA' na 'msondo-JUWATA'.

Alienda BIMALEE kwa kuwachukua Abdallah Gama (mchawi wa rhythm), Mwanyiro (kompyuta - Bass), na Mulenga (String master - solo) kutoka Mlimani. Kisha Jerry Nashon 'Dudumizi' kutoka Vijana.
 
Ngoja niwarudishe kwenye mpira wa miaka ya sabini tena, kwani wakati huo tulikuwa na kandanada la hali ya juu sana haijapata kutokea. Inawezakana baadhi ya picha zimeshawekwa hapa ila nadhani hakuna tatizo kama nitazirudia, kwani wahenga walitufundisha kuwa jambao jema linastahili kurudiwa tena na tena.




Pan African

attachment.php


kama mtoto wa kariakoo hili ndilo cham langu japo wale wazee wanazidi kutudhulumu kodi la lile jengo
 
1.
Najua una rekodi kubwa sana ya mambo ya wakati huo, ila nakuomba tena upitie kumbukumbu zako vizuri na kwa makini. Ukweli ni kuwa mtindo alioanza nao Marehemu Maneti pale Vijana Jazz ulikuwa ni Koka Koka. Wimbo wa Kamata Sukuma ulitolewa kipindi kimoja na Niliruka Ukuta, na ulipigwa pia katika mtindo wa Koka Koka, ila kutokana na umaarufu ulioambatana na wimbo ule wa Kamata Sukuma, Maneti akapromote wimbo wa "Kamata Sukuma" kuwa mtindo uliorithi Koka Koka mwaka 1976 hivi, na ulidumu muda mfupi sana kabla hajaanzisha Heka Heka.

Mkuu Wangu,

1. Hemedi "Chiriku Tenor'" Maneti, alikuwa ni mmoja wa my favorate singer, kwa hiyo nilikuwa ninamfuatilia sana toka alipoanzia Vijana Jazz, lakini I could still be wrong ila tu ninakumbuka tena very clear kuwa Nyimbo za kwanza za Maneti na mtindo wake wa "Kamata Sukuma" ziko tofauti kabisa na zile za awamu ya pili ya "Koka Koka",

- Kwanza vyombo vilivyotumika kwenye awamu yake ya kwanza sio safi au clear kama za ya pili ambapo alitumia vyombo vizuri zaidi, nyimbo kama za Sabina, Kuruka Ukuta, Magdalena, Zubeda, Maneti specifically anautaja huu mtindo wa Kamata Sukuma kwenye kuziiimba na hii ilikuwa before 1977 kwa sababu kwenye mtindo wa "Koka Koka" ndio kuna wimbo wake wa kuungana kwa TANU Na AFRO, unaoitwa "Muungano Sasa Umekamilika".

- Kwa hiyo mtindo wake wa "Koka Koka" unaanzia mwishoni mwa mwaka 1976 na pia kwenye hizi songs kama kawaida yake anasema sana "wana-koka", na ndani ya hizi nyimbo ndio kuna CCM, Frelimo, Operetion Maduka, Masido, Zuhura (ukiusikiliza kwa makini sana hapa mkuu utakuwa in one statement Maneti anamuuliza Zuhura ataipata wapi tiketi ya "Koka Koka") Zubeda, Belibe, Djogolo Kalulu ni ndani ya hizi nyimbo ndio kwa mara ya kwanza anataja sana "Koka Koka" na "wana-Koka" na hizi alizitoa rasmi wakati wa kuanzishwa kwa CCM, ambapo ndani yake ndipo Mozambique walipata uhuru ndio maana aliimba kupandishwa kwa bendera ya Frelimo.

2.
Kumbukumbu yangu kuhusu wimbo wa "Niliruka Ukuta" ambamo sauti ya Marehemu Maneti ilikuwa haitofautiani na ile ya Marahemu Mbaraka inakuja vizuri sana. Vile vile chini ya mtindo wa Koka Koka, Maneti alipiga wimbo wa "Zuhura Ninaondoka" ambao binafsi nilikuwa nauhusisha sana na mpenzi wangu wa wakati huo Marehemu Zuhura (RIP). Nilikuwa nina T-Shirt moja ya Sunflag iliyokuwa na picha ya kichwa cha tembo kifuani; mgongoni nikaandika pale maneno matatu kwa style ya aina yake: maneno hayo yalikuwa ni Masika, Sokomoko na Koka Koka, ambayo ilikuwa mitindo ya muziki niliyokuwa naizimia sana wakati ule. Marafiki zangu wa wakati huo wa ujingani wakisoma post hii watakumbuka sana ninayosema. Wakati Maneti anatoa wimbo wa "Niliruka Ukuta," Mbaraka naye alitoa wimbo wa "Mshenga" ambapo Marijani naye alikuwa ametoa wimbo uliokuwa unasema "Wapangaji mnawaacha watoto wenu wanavunjavunja milango na madirisha ndani ya nyumba yangu, hivyo ni afadhali muondoke kwani mnaleta sokomoko ndani ya nyumba yangu": jina halisi la wimbo huu silikumbuki tena. Nyimbo hizi zilikuwa kiboko sana wakati huo ndiyo maana kwangu mimi muziki ukawa ni Masika, Koka Koka na Sokomoko.

1. Ni kweli kabisa mkuu unayosema, lakini "Niliruka Ukuta" ulikuwa ni wimbo wa kwanza kumuingiza Maneti kwenye ligi ya juu kimuziki nchini ndio kwa mara ya kwanza wananchi tulianza ku-pay attention kuwa Maneti naye yumo kwenye list,

2. kwenye ule wimbo "kamata Sukuma" aliuutumia kuwataja wanamuziki wenzake wote wa Vijana Jazz, lakini kwenye wimbo wa "Zubeda" ambao ni safu hiyo hiyo ya kwanza na 'Salima" Maneti specifically ndio anathibitisha kuwa Kamata Sukuma ni mtindo sio wimbo tu kama wengi tulivyofikiri kwenye ule wimbo wa "Kamata Sukuma" kwa sababu katika kipindi hicho kizima cha mwanzoni ilikuwa nadra sana kwa Vijana Jazz kusemwa wazi kuwa wanatumia mtindo gani, ni mpaka ukienda kuwaona live as I did ndio ungejua kuwa "Kamata Sukuma" ni mtindo, lakini walipongia kwenye awamu ya pili ya "Koka Koka" ndio kwa mara ya kwanza wakawa kwenye matangazo yao wanasema wazi kuwa wao ni "wana-Koka"


2.
Kuna watu wengine wanaweza pia kuthibitisha hili. Hebu soma hapa:

Marehemu Maneti alipochukua uongozi wa bendi ya Vijana Jazz alianza nao na mtindo wa Kokakoka. Vibao maarufu vya mwanzo mwanzo vya bendi hiyo vilikuwa "Nimeruka Ukuta" uliofahamika na wengi, "Sabina" na Magdalena". Kwenye wimbo wa Sabina alimuomba mpenzi wake Sabina arudi kwani siku nyingi zilikuwa zimepita tangu aondoke na kwenye wimbo "Magdalena" alikuwa analalamika kuzuiwa na wazazi wake kumuoa Magdalena kwa sababu alikuwa na ulemavu wa jicho wakati yeye alikuwa akimpenda sana.

Pamoja na nyimbo hizo, nyimbo nyingine za mwanzo mwanzo za bendi hiyo zilikuwa, "Zuhura Naondoka", "Kamata Sukuma" waliotumia kujitaja majina, "Salima", "Nimeruka Ukuta Namba Mbili" na "Magdalena Namba Mbili" ambamo Maneti alifurahi baada ya wazazi wake kukubali amuoe Magdalena.

Hapa mkuu hata huyu aliyeandika hii article amechemsha big time, kwa sababu kwenye nyimbo zote alizozitaja hapo juu licha ya kwamba niliwaona kwa macho yangu Vijana Jazz wakipiga hiyo miziki, pia bado ninayo kwenye collection yangu ni kwamba, Maneti specifically anatamka neno "Koka Koka" kwenye nyimbo za "Zuhura" na namba mbili za Magdalena na "Kuruka Ukuta" lakini not kwenye nyimbo za before that.

- Mwandishi wa article hii anayo kumbu kumbu kubwa sana na facts nyingi sana za Vijana Jazz, lakini ni hapo tu alipochanganya madawa, hizi nyimbo alizozitaja hapo juu hazikutolewa kwa wakati mmoja, hapana zilitolewa kwa nyakati mbili tofauti:-

- Nyimbo za Sabina, Magdalena, na Kuruka ukuta, mwandishi amesahau wimbo wa "Zubeda" zilitolewa mara ya kwanza Maneti anaingia kwenye taifa kama kiongozi wa bendi ya Vijana na mtindo wa "Kamata Sukuma",

- Na hizi za "Zuhura" na namba mbili za "Kuruka Ukuta" na "Magdalena" ndio kwa mara ya kwanza Maneti anamuuliza Zuhura, ataipata wapi tiketi ya "Koka Koka" hizi zilitoka kwenye awamu ya pili ambapo ndani yake kulikuwemo pia nyimbo za kuipongeza CCM kuungana na Afro, na pia kuwapongeza Frelimo na uhuru wa Mozambique.

Labda niwaombe samahani wananchi kwa kuiendeleza hii habari kwa muda mrefu, lakini nilikuwa na heshima sana na Maneti (RIP), ambaye alipoanza muziki na Vijana Jazz, alituvuta vijana wengi sana then kwa sababu alitumia sana mtindo unaofanana na bendi iliyokuwa maarufu sana enzi zile na vijana ya Orch. Sosoliso toka Zaire, ya kina Matadidi Mabele Mwana Kitoko na Loko Masengo kwenye mtindo wake wa "Kamata Sukuma",

lakini alipobadili tu na kuingia kwenye "Koka Koka", yule mpigaji wake wa Solo Hamza Kalala 'Komandoo" alijitoa Vijana na kuingia UDA JAZZ na ndio maana hata kwenye awamu ya pili ya Maneti, style ya upigaji solo sasa ikabadilika kabisa kwenye mtindo wa "Koka Koka" maana sasa leading solo alikuwa ni Hassan Dalali ambaye upigaji wake wa solo gitaa ulikuwa ni opposite kabisa na Kalala, ingawa baadaye Kalala alirudi tena Vijana, lakini this time alirudi akiwa na style mpya ya solo kama ya Mosesengo Fan Fan, aliyeingia Makassy akitokea kwa Lwambo..

Niliwahi kuhudhuria sana maonyesho yake Maneti live, katika sehemu kama Banana Bar njia panda ya airport, Ukumbi wa Police Chang'ombe, Vijana Social Hall Mwananyamala, na Police Mess Obey, Maneti alikuwa cool na kwa mara ya kwanza nilipata bahati ya kuchati naye one on one, ilikuwa wakati yeye na bendi yake wanasafiri kwenda Bujumbura, ambako walialikwa na bendi moja ya taarabu kule kitongoji cha Buyenzi, Bujumbura. Nilikutana naye nikiwa training ndani ya Meli ya MV. Liemba nice guy na cool pia, alionekana kua na wasi wasi sana kuhusu mashabiki wa muziki wa Bujumbura, wataipokea vipi Vijana Jazz, akiwa na wasi wasi sana akaniambia kuwa "...nasikia huko Bujumbura wao wamezoea wa-Zaire wakali kama kina Papa-Wemba sasa sisi Vijana bongo itakuwaje?..." alikuwa na wasi wasi sana kwenye hilo.

Kwa bahati nzuri tulipofika kule, kilikuwa ni kipindi timu ya maarufu ya mpira ya Intere (International) ambayo then ilikuwa inamilikiwa na rais wao Bagaza, walikuwa ndio kwanza wameajiri wachezaji kadhaa kutoka bongo, ninawakumbuka sana nao ni kina Katwila, Isaack Mwakatika, na George "Best" Kulagwa, Bujumbura ni mji mdogo sana hawa wachezaji walikuwa known na kila mtu kule mpaka watoto wadogo, tena walikuwa maarufu sana kwa hiyo Ads zote za Vijana Jazz zikawa tied na hawa wachezaji, as the results Vijana Jazz wakaweza kuvunja record pale mjini mpaka ikabidi wapigie kwenye uwanja wa taifa wa mpira, on the way back Maneti was happy na ndio akatunga wimbo wa "Bujumbura".

Aliporudi Dar, aliamua kuanza kuutafuta ubunge, infact alikua amesha make a big progress, lakini kwa bahati mbaya akatangulia kwenye haki akiwa ameacha mtoto na dada mmoja pale Mwananyamala Diana (Nafikiri utakumbuka kua aliwahi kuwa na wimbo wa kumsifia sana Diana), next na anapoishi Mkulu DJ JPP (Pantalakis), dada ambaye enzi hizo alikua Air Hostess. Mungu amuweke mahali pema sana peponi Mwanamuziki Hemedi Maneti, na hapa naweka kalamu chini.

Ahsante Wakuu.
 
Dede kabla ya kwenda Sikinde alikuwa msondo. Ni mpenzi mkubwa wa Simba, siku hiyo Simba ilikuwa inacheza na Coastal. Dede akakacha onyesho la Msondo akaenda mpirani. Alivyorudi ukumbini baada ya mechi akatimuliwa na kunyang'anywa uniform. Hapo ndio akarudi Mlimani na kutunga nyimbo ya 'Talaka Rejea' yenye kuelezea masahibu yaliyomkuta. Alidai msondo kuna 'msondo-NUTA' na 'msondo-JUWATA'.

Alienda BIMALEE kwa kuwachukua Abdallah Gama (mchawi wa rhythm), Mwanyiro (kompyuta - Bass), na Mulenga (String master - solo) kutoka Mlimani. Kisha Jerry Nashon 'Dudumizi' kutoka Vijana
.

Mkuu Mgirima,

Heshima mbele na shukrani sana, kwa hiyo alienda Bima Lee baada ya kutoka Sikinde, sawa sawa huo wimbo ninaukumbuka sana wa 'Talaka Rejea" lakini sikujua kuwa hiyo ndio ilikuwa maana yake behind it, again shukrani wka marekebisho mkuu, na pia ahsante wka kipande cahko cha historia ya Dede.

Unajua binafsi nilikuwa ninamuona Dede kuwa ni very rough, unajua sometimes jamaa huachia midevu na huvaa rafu rafu sana, halafu ni mkorofi sana akilewa masanga, kwa hiyo sikua mpenzi sana wa nyimbo zake, nilikuwa ninazimia tu na wimbo wake alioutoa akiwa Bima Lee yaani ule wa "Samaki Baharini Huishi Vipi", halafu siku zote nilidhani kuwa Bitchuka, alikuwa akimu over promote mno as opposed na kipaji chake hasa, ingawa sio siri kwua jamaa alikuwa maarufu sana, au?
 
Msimsahau DJ Mzee wa Mji Eddy Saly!

Mkuu Rev,

Uko right, huyu Mkulu niliwahi kumkuta Lusaka, enzi za mwishoni wma 70s, duh! jamaa alikuwa mkali sana alikuwa akipiga ukumbi mmoja maarufusana then huko uliokuwa unaitwa Studio 22, kwenye ghorofa ya 12 downtown Lusaka,

ni huko kwenye Disco pia kwa mara ya kwanza nilikutana na Mkulu wangu Bandawe, sijui kama unampata kwa jina lake la siku hizi "Mzee Pelise Ngwasuma" mklu mmoja town sana Dar, lakini Eddy Sally yes alikwua baabu kubwa sana.

Shukrani kwa this.
 
Ngoja niwarudishe kwenye mpira wa miaka ya sabini tena, kwani wakati huo tulikuwa na kandanada la hali ya juu sana haijapata kutokea. Inawezakana baadhi ya picha zimeshawekwa hapa ila nadhani hakuna tatizo kama nitazirudia, kwani wahenga walitufundisha kuwa jambao jema linastahili kurudiwa tena na tena. Simba

Mkulu Kichuguu,

Again ubarikiwe bro, maana hii ni historia saafi sana kwa mbali kama ninakumbuka vizuri kwenye hii picha ya Simba, kuanzia kushoto ni:-

Kibadeni "King", Mahadhi, Mohamed "Tall", Aloo Mwitu, Daudi Salum "Bruce Lee", Adam Sabu, Mohamed Kajole "Machela", Abas Kuka, Abdalalh Mwinyimkuu, Yusuf Kaungu, Abbas Dilunga, na Willy Mwaijibe.

Duh! saafi sana mkuu, enzi hizo mpira unaanza saa 11 jioni, wananchi tunakuwa uwanjani toka saa 2 asubuhi, sijui kama leo bado yapo hayo!
 
Mwalimu Kichuguu,

Cosmo ya Ilala ilipewa jina baada ya ile Cosmo au Cosmopolitan timu aliyokuwa aikichezea Edison Arantes Do Nascimento-Pele alipokuja kucheza mpira wa miguu Marekani.
 
Cosmo: Sijaelewa jina hili la Cosmo lilikuwa lina maana gani

1. Cosmo mkuu kilikuwa ni kifupi cha Comsopolitan, naamini ni something to do location as a City, sina uhakika sana lakini ninaamini kuwa ina something to do na jiji.

2. Hapo kwenye picha ninawakumbuka watu wanne tu, aliyesimama kushoto kocha wao Mansur Magram, wa kwanza kushoto aliyechuchuumaa Mohamed Msomali, na wa mwisho kulia aliyechuchumaa Jumanne Hassan "Masuminti" aliyesimama mwisho kulia Msuba.

Hawa Cosmo walikuwa chachu sana ya Yanga na Simba, mara kwa mara walikuwa wakiwaadhiri sana timu kubwa, na hawakuwa na tabia ya kutoka toka, kwa mara ya kwanza wachezaji wa Cosmo kutoka na kuingia Simba, ilikuwa ni Mohamed Bakari "Tall" na Jumanne "Masuminti" na baada ya hapo hii timu haikuenda mbali sana ikajifia kifo cha mende tu!
 
Back
Top Bottom