Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Tukisema kwa lawama dhidi ya serikali ambazo zinatolewa na wananchi mbalimbali hii ni haki yao kabisa hakuna mtu anayepingwa kwa kutoa lawama zozote zile lakini tunapotoa lawama ni vizuri tuwe na vitu vya ziada yaani unatoa lawama huku ukiwa na suluhisho la suala hilo au ukiwa na mchango wa aina yoyote ambao unaweza kusaidia suala hilo .
Tukio la mabomu la gongo la mboto na mbagala limetukumbusha mengi haswa suala la watu kuhamia sehemu za karibu na makambi ya jeshi hebu kwanza tuone historia fupi ya kambi hizi .
Kambi ya gongo la mboto wakati inajengwa enzi hizo ilikuwa mbali sana na raia ila raia walikimbilia maeneo ya jirani na kambi hiyo kwa ajili ya kujihifadhi na shuguli zingine lakini wakati inajengwa ilikuwa mbali sana .
Kambi ya lugalo nayo ilikuwa mbali sana pamoja na magorofa ya jeshi mwenge nayo yalijengwa kwa ajili ya wafanyakazi lakini yakaonekana yako mbali kwa wafanyakazi wa serikali ndio maana wanajeshi wakamwekwa hapo lakini ona sasa hivi wananchi walivyojaa pembeni mwa magorofa hayo .
Kambi ya changanyikeni kuna rada ndio maana ni ngumu kwa baadhi ya sehemu raia kusogelea kwa sababu wanaweza kuonwa au kunasana kwenye mitego mengine ya maeneo hayo .
Kambi ya mabibo nayo wakati inajengwa ilikuwa mbali na mji wakati ule soko la kariakoo linajengwa raia waliohamishwa kule walipewa nafasi maeneo ya mabibo unaweza kuona jinsi gani wakati kambi hizi zinajengwa zilivyokuwa mbali enzi hizo .
SUALA LA KUHAMISHA KAMBI KUWA MBALI NA RAIA
Kila mwananchi mwelewa anatakiwa ajue kwamba kambi hizo zimejengwa kwa gharama kubwa sana na kuhamisha kwenda sehemu nyingine pia inahitaji gharama kubwa pengine zaidi kutokana na gharama hizo basin a uwezo wa nchi yetu katika masuala mbalimbali yanayohusu fedha tusihoji kwanini kambi hazipelekwi mbali je nchi ina uwezo wa kujenga kambi zingine mbali zaidi na kama zikienda huko kwa maslahi ya nani ?
SUALA LA WATU KUJIUZURU
Kama nilivyosema hapo juu watu wengi hawajui mambo yanayoenda na kuendeshwa ndani laiti wangejua gharama za kuhifadhi mali hizo na kiasi cha bajeti kilichowekwa kwa ajili ya bidhaa hizo kama zinaendana sawa au la kama hazitoshi itasaidiwaje na sio kujiuzuru hata wakijiuzuru wale wanaokuja watapata wapi fedha na uwezo wa kuendesha shuguli hizo tukumbuke hii ni sekta nyeti kwa usalama na maslahi ya nchi yetu sio ya kuchezewa chezewa hovyo .
KWA WASIOJUA .
Hifadhi ya silaha inahitaji aina Fulani ya mazingira , hewa na matumizi mengine kama Grisi na mafuta mfano mzinga mmoja ile midigo iliyookotwa inatumia karibu lita 20 za mafuta kwa ajili ya kuosha kama una mizinga kama ile alfu 4 tu unaweza kupiga gharama za mafuta , grisi matunzo mengine .
Halafu kuna hili tatizo la mgao wa umeme
SULUHISHO .
Matukio kama haya yanagusa sekta muhimu katika taifa yasitumiwe katika kujinufaisha kisiasa hata kidogo , wazalendo haswa wanasiasa kwenye vyama mbalimbali tumieni wataalamu na wajuzi wenu katika kuleta suluhisho mbadala la matatizo haya na sio kupiga domo bila suluhisho la msingi .
NENO LA LEO
USALAMA WA NCHI NA WATU WAKE UNAHUSU TAIFA LOTE LA WATANZANIA NA MALI ZAKE SIO CCM WALA JWTZ – WEWE TIMIZA WAJIBU WAKO KWA KULETA SULUHISHO LA KUDUMU KWA VITENDO http://www.mnyonge.blogspot.com/
Tukio la mabomu la gongo la mboto na mbagala limetukumbusha mengi haswa suala la watu kuhamia sehemu za karibu na makambi ya jeshi hebu kwanza tuone historia fupi ya kambi hizi .
Kambi ya gongo la mboto wakati inajengwa enzi hizo ilikuwa mbali sana na raia ila raia walikimbilia maeneo ya jirani na kambi hiyo kwa ajili ya kujihifadhi na shuguli zingine lakini wakati inajengwa ilikuwa mbali sana .
Kambi ya lugalo nayo ilikuwa mbali sana pamoja na magorofa ya jeshi mwenge nayo yalijengwa kwa ajili ya wafanyakazi lakini yakaonekana yako mbali kwa wafanyakazi wa serikali ndio maana wanajeshi wakamwekwa hapo lakini ona sasa hivi wananchi walivyojaa pembeni mwa magorofa hayo .
Kambi ya changanyikeni kuna rada ndio maana ni ngumu kwa baadhi ya sehemu raia kusogelea kwa sababu wanaweza kuonwa au kunasana kwenye mitego mengine ya maeneo hayo .
Kambi ya mabibo nayo wakati inajengwa ilikuwa mbali na mji wakati ule soko la kariakoo linajengwa raia waliohamishwa kule walipewa nafasi maeneo ya mabibo unaweza kuona jinsi gani wakati kambi hizi zinajengwa zilivyokuwa mbali enzi hizo .
SUALA LA KUHAMISHA KAMBI KUWA MBALI NA RAIA
Kila mwananchi mwelewa anatakiwa ajue kwamba kambi hizo zimejengwa kwa gharama kubwa sana na kuhamisha kwenda sehemu nyingine pia inahitaji gharama kubwa pengine zaidi kutokana na gharama hizo basin a uwezo wa nchi yetu katika masuala mbalimbali yanayohusu fedha tusihoji kwanini kambi hazipelekwi mbali je nchi ina uwezo wa kujenga kambi zingine mbali zaidi na kama zikienda huko kwa maslahi ya nani ?
SUALA LA WATU KUJIUZURU
Kama nilivyosema hapo juu watu wengi hawajui mambo yanayoenda na kuendeshwa ndani laiti wangejua gharama za kuhifadhi mali hizo na kiasi cha bajeti kilichowekwa kwa ajili ya bidhaa hizo kama zinaendana sawa au la kama hazitoshi itasaidiwaje na sio kujiuzuru hata wakijiuzuru wale wanaokuja watapata wapi fedha na uwezo wa kuendesha shuguli hizo tukumbuke hii ni sekta nyeti kwa usalama na maslahi ya nchi yetu sio ya kuchezewa chezewa hovyo .
KWA WASIOJUA .
Hifadhi ya silaha inahitaji aina Fulani ya mazingira , hewa na matumizi mengine kama Grisi na mafuta mfano mzinga mmoja ile midigo iliyookotwa inatumia karibu lita 20 za mafuta kwa ajili ya kuosha kama una mizinga kama ile alfu 4 tu unaweza kupiga gharama za mafuta , grisi matunzo mengine .
Halafu kuna hili tatizo la mgao wa umeme
SULUHISHO .
Matukio kama haya yanagusa sekta muhimu katika taifa yasitumiwe katika kujinufaisha kisiasa hata kidogo , wazalendo haswa wanasiasa kwenye vyama mbalimbali tumieni wataalamu na wajuzi wenu katika kuleta suluhisho mbadala la matatizo haya na sio kupiga domo bila suluhisho la msingi .
NENO LA LEO
USALAMA WA NCHI NA WATU WAKE UNAHUSU TAIFA LOTE LA WATANZANIA NA MALI ZAKE SIO CCM WALA JWTZ – WEWE TIMIZA WAJIBU WAKO KWA KULETA SULUHISHO LA KUDUMU KWA VITENDO http://www.mnyonge.blogspot.com/