Tukio la Kipa wa Yanga, Diarra kuwaonesha Wanahabari kidole cha kati , imenikumbusha Chuji alivyofanya hivyo akafungiwa

Tukio la Kipa wa Yanga, Diarra kuwaonesha Wanahabari kidole cha kati , imenikumbusha Chuji alivyofanya hivyo akafungiwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
Screenshot 2026-03-22 112131.jpg
Nimeona clip ya Kipa wa Yanga, Djigui Diarra akioneshea kidole cha kati cha mkono wake wa kushoto kuelekea kwa Waandishi wa Habari waliokuwa wakiwarekodi Wachezaji wa timu hiyo wakati wakielekea katika basi ili kuondoka kwenye Uwanja wa Jamhuri baada ya matokeo ya sare ya 1-1 dhidi ya Mtibwa Sugar, jana Machi 21, 2026, na kukumbuka kitu.
Screenshot 2026-03-22 112329.jpg

Screenshot 2026-03-22 112146.jpg
Diarra ambaye pia amekuwa gumzo kutokana na kitendo chake cha kuonekana akimzonga mwamuzi huku akimfokea baada ya mchezo huo, amenikumbusha tukio la kiungo wa zamani wa Yanga, Athumani Iddy “Chuji” alichokifanya Mwaka 2007.

Chuji ambaye alikuwa akiichezea Yanga baada ya usajili wake kutoka Simba kuwa na vuta nikuvute, aliwaonesha kidole cha kati mashabiki waliokuwa wakimzomea kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, tukio ambalo lilisababisha akachukuliwa hatua za kinidhamu na Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), japo sikumbuki adhabu yake ilikuwaje.


Sasa kwa tukio hilo la Diarra sijui itakuwaje.
 
Hata yanga walimchukulia hatua Metacha alipowanyooshea kidole cha kati mashabiki wake tusubiri labda yanga watamchukulia hatua au kuna double standard.
Ukiangalia kwa jicho la tatu ni kama Diarra anafanya vituko vya makusudi ili aondoke yanga baada ya kugundua klabu haiwezi kumuuza.
 
Hata yanga walimchukulia hatua Metacha alipowanyooshea kidole cha kati mashabiki wake tusubiri labda yanga watamchukulia hatua au kuna double standard.
Ukiangalia kwa jicho la tatu ni kama Diarra anafanya vituko vya makusudi ili aondoke yanga baada ya kugundua klabu haiwezi kumuuza.
Hisia.
 
Angewaonyeshea Dole La Pembeni Asingestahili Adhabu...??Na Ni Dole Lipi Ndio Linatikiwa Lionyeshwe Zaidi Kwa Watu Ukitoa Dole La Kati Kwa Majibu Wa Sheria Na Kanuni Za Kuonyesha Ma Dole...??
 
Diara ni mkubwa kuliko TFF,mkubwa kuliko Bodi ya Ligi, mkubwa kuliko Yanga maana amewadharau hadi viongozi walipokuwa wanamzuia asimpige mwamuzi, hivyo hatafanywq chochote kwani ana makosa mengi ya kujirudia rudia na hajawahi kuonywa, kifupi Diara ameuweka mpira wa Tanzania mfukoni mwake.
 
Hata yanga walimchukulia hatua Metacha alipowanyooshea kidole cha kati mashabiki wake tusubiri labda yanga watamchukulia hatua au kuna double standard.
Ukiangalia kwa jicho la tatu ni kama Diarra anafanya vituko vya makusudi ili aondoke yanga baada ya kugundua klabu haiwezi kumuuza.
Yanga haiwezi kufanya lolote. Huyo ndo mchezaji aliyebaki wanajivunia. Wakimgusa tu, watapoteana
 
Hivi ni kwanini huwa wachezaji wa mpira wana hasira sana?! kuna saa unaweza kufikiri ya kuwa uwanjani yupo peke yake.
 
Back
Top Bottom