Tujikumbushe kuhusu Hoteli ya Alkael Mbowe kutumia umeme wa wizi

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,901
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoani Kilimanjaro limeikatia umeme hoteli ya Aish hotel inayomilikiwa na Mbunge wa Hai (CHADEMA), Freeman Mbowe kwa madai kuwa wamebaini inatumia umeme wa wizi na kuisababishia Serikali hasara ya shilingi milioni 10.8.

Akiungumza, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Kilimanjaro, Mahawa Mkaka, Shirika hilo limebaini jana Septemba 14 kuwa wamejiunganishia umeme na kuharibu miundo mbinu yake.

“Baada ya kupata taarifa kutoka vyanzo vyetu tulienda kwenye hoteli hiyo kufanya ukaguzi, tukabaini wameharibu mita na kujiunganishia umeme kinyemela. Hasara hiyo ya milioni 10.8 ni kwa tathmini ya awali na sasa hivi tunasubiri hesabu kutoka Tanesco makao makuu,” amesema Mkaka.
 
Hivi walikosa mwanasheria wa kuidai fidia serikali kwa kusema uongo au ni kweli walikuwa wanaiba?
 
Wakati fulani early 2003 kipindi hiko naishi Mabibo wakati bado tanesco wanatumia yale mamita analogue kuna nyumba ya mwenyekiti wa mtaa alikutwa amewapiga nyoka Tanesco so haya mambo yapo tu.

Na alikuwa mwana-ccm
 
Ukianza kukumbushia maujinga mliyokuwa mnawafanyia wapinzani Enzi za jiwe utaharibu! Nakutahadharisha tu kaa kwa kutulia. Maujinga yenyewe haya master minder eti Sabaya, Mnyeti na Makonda.

Usiwakumbushe watu machungu. Watu wameamua kukaa kimya kupisha maridhiano na siasa Safi, mkitaka kuwakumbusha na kuwachokonoa hamtaweza kuendelea kuwatawala
 
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoani Kilimanjaro limeikatia umeme hoteli ya Aish hotel inayomilikiwa na Mbunge wa Hai (CHADEMA), Freeman Mbowe kwa madai kuwa wamebaini inatumia umeme wa wizi na kuisababishia Serikali hasara ya shilingi milioni 10.8.

Akiungumza, Meneja wa Tanesco Mkoa wa Kilimanjaro, Mahawa Mkaka, Shirika hilo limebaini jana Septemba 14 kuwa wamejiunganishia umeme na kuharibu miundo mbinu yake.

“Baada ya kupata taarifa kutoka vyanzo vyetu tulienda kwenye hoteli hiyo kufanya ukaguzi, tukabaini wameharibu mita na kujiunganishia umeme kinyemela. Hasara hiyo ya milioni 10.8 ni kwa tathmini ya awali na sasa hivi tunasubiri hesabu kutoka Tanesco makao makuu,” amesema Mkaka.
Mtu wa namna hii ndio mnataka awe kiongozi wa kitaifa sijui itakuwaje?
 
Subiri uone vipofu wanavyoibuka🤣 yaani mauchafu yao hawayaoni na bado wanakomaa eti awe kiongozi
 
Tupe muendelezo wa hii habari, hilo deni lilipwa? au wahusika walichukuliwa hatua gani?
 
Back
Top Bottom