Killing machine
JF-Expert Member
- Jul 24, 2022
- 1,210
- 1,353
Habari wakuu zangu,
Kuna msemo unasema "Jela hakuna mateso ila wanao leta mateso jela ni wajelajela wenyewe."
Hivyo hivyo duniani ni mahala salama, pana maji, vyakula ardhi nzuri, na vyote Mungu alitoa bure. Yaani ule bure, unywe bure, ujenge popote bure, uwinde bure, uvue samaki was baharini bure nk.
Vyoote Mungu alitoa bure kabisa kusudi maisha yawe rahisi na yenye fraha duniani kote, lakini kuna watu wachache walio barikiwa roho za kibinafsi, makatiri, wasiyoipenda katu furaha wala amani wasio iwazia mema dunia yetu nzuri, wala uzao wake wa asili.
Wakajimilikisha mito na maziwa ili wauze maji na kuwalipisha ushuru wavua samaki na wapita na meli juu ya bahari mito na maziwa.
Wakajimilikisha aldhi ili wawalipishe ushuru wakulima walimao juu ya nchi na kuwauzia ardhi wale watakao kujenga na kuishi na wale wafugaji na hata wale wachimbaji wa madini ardhini kama dhahabu, chuma, nk.
Wakajimilikisha anga ili walipwe ushuru kwa wale wapitao na vyombo vya angani. Hawakuishia hapo, wakafikia hatua mpaka ya kutaka ushuru kwa wale walitangazao neno la Mungu, Mungu muumba mbingu na nchi!
Kwa matendo yao wakaipandisha pesa thamani, pesa ikawa na nguvu kuliko utu, pesa ikatawala ikazisimamisha na kuziangusha tawala, ikawasimamisha na kuwaangusha wafalme.
Pesa ikaharibu kabisa nguvu ya upendo kwa dunia yetu pendwa. Wasio na pesa wakakosa ardhi, wasio napesa wakakosa Uhuru, wasio na pesa wakakosa maji, wasio na pesa wakakosa chakula, paku lala, elimu, mavazi, nk, watu wakaitambua thamani ya pesa, wakapania kuitafuta kwa njia yoyote ili wapate heshima, makazi, chakula, maji, mavazi nk.
Kadri watu walivyotafuta pesa kwa nguvu na kwa akili zao zote, wale walioumiliki utajiri wote wa dunia pesa zote za inchi wakapata hofu wakaanza kuwaita; majambazi, matapeli, wakabaji, ombaomba, maskini, mafukara, wadangaji, ma bar maid, wapasua mbao, makapuku wanuka kwapa.
Hawakuishia hapo wakawaita magaidi wakawaua kwa risasi, mabomu, visu, mafuta, magonjwa ya zinaa, nyuklia nk, hawakujipa muda kujiuliza kwanini ujambazi umeshamili, kwanini ngono zimeshamili, kwanini wa watu wanauwana, kwanini migogoro ya ardhi imeshamili!
Hawa kuwa na muda huo, walichojari ni kuongeza ulinzi juu ya mali zao, familia zao, pesa zao, na kuongeza ufanisi katika kutengeneza silaha nzito kwa ajili ya kulinda maslahi yao na utajiri wao.
Leo hii dunia imekuwa uwanja wa vita, magonjwa, visasi, shida, dhiki, ukame, japo maji yapo, kwani hawako tayari kuhakikisha maji yanapatikana kila mahari kwa kuhofia watashindwa kuuza maji ya chupa, wala hawako taya rikuhakikisha kila mmoja ana nyumba ya kulala kwa kuhofia watapoteza mapato kwenye nyumba za kupanga.
Wala hawako tayari kuzalisha umeme wa kutosha kwa kuhofia watashindwa kuuza magenerator, pesa imetufikisha pabaya tumekuwa wanyama! Natokwa na machozi nikiitazama Sudan, Congo, Ukraine, leo hii Palestina na Israel.
Naona kuna mama, watoto, na wazee, wakati wanaoupitia ni mgumu sana na hauelezeki. Yote haya yanatokea kwa sababu ya ubinafsi wa watu wachache ili wauze silaha zao na kuzitangaza biashara zao. Mambo haya yanatupeleka kuelekea Vita ya Tatu ya Dunia kwani nvita zote msingi wake ni ubinafsi.
Vita hii itaanzia pale Irani itakapoingilia kati, bila shaka Mmisri hatasita na vipi nchi nyingine za kiislamu kama Saudi Arabia, nk, na huku pembeni Muingereza na Mjerumani na washirika wengine hawatakaa kimya.
Kwahiyo tujiandae gharama za maisha kupanda zaidi.
Kuna msemo unasema "Jela hakuna mateso ila wanao leta mateso jela ni wajelajela wenyewe."
Hivyo hivyo duniani ni mahala salama, pana maji, vyakula ardhi nzuri, na vyote Mungu alitoa bure. Yaani ule bure, unywe bure, ujenge popote bure, uwinde bure, uvue samaki was baharini bure nk.
Vyoote Mungu alitoa bure kabisa kusudi maisha yawe rahisi na yenye fraha duniani kote, lakini kuna watu wachache walio barikiwa roho za kibinafsi, makatiri, wasiyoipenda katu furaha wala amani wasio iwazia mema dunia yetu nzuri, wala uzao wake wa asili.
Wakajimilikisha mito na maziwa ili wauze maji na kuwalipisha ushuru wavua samaki na wapita na meli juu ya bahari mito na maziwa.
Wakajimilikisha aldhi ili wawalipishe ushuru wakulima walimao juu ya nchi na kuwauzia ardhi wale watakao kujenga na kuishi na wale wafugaji na hata wale wachimbaji wa madini ardhini kama dhahabu, chuma, nk.
Wakajimilikisha anga ili walipwe ushuru kwa wale wapitao na vyombo vya angani. Hawakuishia hapo, wakafikia hatua mpaka ya kutaka ushuru kwa wale walitangazao neno la Mungu, Mungu muumba mbingu na nchi!
Kwa matendo yao wakaipandisha pesa thamani, pesa ikawa na nguvu kuliko utu, pesa ikatawala ikazisimamisha na kuziangusha tawala, ikawasimamisha na kuwaangusha wafalme.
Pesa ikaharibu kabisa nguvu ya upendo kwa dunia yetu pendwa. Wasio na pesa wakakosa ardhi, wasio napesa wakakosa Uhuru, wasio na pesa wakakosa maji, wasio na pesa wakakosa chakula, paku lala, elimu, mavazi, nk, watu wakaitambua thamani ya pesa, wakapania kuitafuta kwa njia yoyote ili wapate heshima, makazi, chakula, maji, mavazi nk.
Kadri watu walivyotafuta pesa kwa nguvu na kwa akili zao zote, wale walioumiliki utajiri wote wa dunia pesa zote za inchi wakapata hofu wakaanza kuwaita; majambazi, matapeli, wakabaji, ombaomba, maskini, mafukara, wadangaji, ma bar maid, wapasua mbao, makapuku wanuka kwapa.
Hawakuishia hapo wakawaita magaidi wakawaua kwa risasi, mabomu, visu, mafuta, magonjwa ya zinaa, nyuklia nk, hawakujipa muda kujiuliza kwanini ujambazi umeshamili, kwanini ngono zimeshamili, kwanini wa watu wanauwana, kwanini migogoro ya ardhi imeshamili!
Hawa kuwa na muda huo, walichojari ni kuongeza ulinzi juu ya mali zao, familia zao, pesa zao, na kuongeza ufanisi katika kutengeneza silaha nzito kwa ajili ya kulinda maslahi yao na utajiri wao.
Leo hii dunia imekuwa uwanja wa vita, magonjwa, visasi, shida, dhiki, ukame, japo maji yapo, kwani hawako tayari kuhakikisha maji yanapatikana kila mahari kwa kuhofia watashindwa kuuza maji ya chupa, wala hawako taya rikuhakikisha kila mmoja ana nyumba ya kulala kwa kuhofia watapoteza mapato kwenye nyumba za kupanga.
Wala hawako tayari kuzalisha umeme wa kutosha kwa kuhofia watashindwa kuuza magenerator, pesa imetufikisha pabaya tumekuwa wanyama! Natokwa na machozi nikiitazama Sudan, Congo, Ukraine, leo hii Palestina na Israel.
Naona kuna mama, watoto, na wazee, wakati wanaoupitia ni mgumu sana na hauelezeki. Yote haya yanatokea kwa sababu ya ubinafsi wa watu wachache ili wauze silaha zao na kuzitangaza biashara zao. Mambo haya yanatupeleka kuelekea Vita ya Tatu ya Dunia kwani nvita zote msingi wake ni ubinafsi.
Vita hii itaanzia pale Irani itakapoingilia kati, bila shaka Mmisri hatasita na vipi nchi nyingine za kiislamu kama Saudi Arabia, nk, na huku pembeni Muingereza na Mjerumani na washirika wengine hawatakaa kimya.
Kwahiyo tujiandae gharama za maisha kupanda zaidi.