Ukweli kuhusu "Kaskazini kuendelezwa na Wanakaskazini"
Ukweli tunataka kupandikiza ukabila udini na ukanda awamu hii kuliko kipindi chochote .
Serikali inapandikiza Ukanda, wananchi wanapandikiza ukabila
Dini zinapandikiza udini kwa kuleta mpaka CV za waslamu jamii forum sijui ndio zitusaidie nini.
Tumeamua kuondoa utaifa na kuwa wabaguzi lakini makosa makubwa yapo kwa rais wetu ambaye anaonekana wazi wazi kupendelea chato halafu kuna watu wanamsapoti.
Tatizo lipo tena kwa watanzania kuamini kutoendelea kwao ni kwa sababu kumesababishwa na watu wa kasikazini maana wao wameendelea yaani watu wa kasikazini kwa ujumla.
Leo hii tunashangilia uwanja wa ndege wa kiwango cha kimataifa kujengwa kwenye population ya ya watu 17,000 hii haijawai fanyika duniani kote.
Ukabila ukabila ukabila Nyerere hatukumuelewa alipokuwa akipigania utaifa kwanza.
Hivi wahaya,wachaga na wasukuma tukijifanya nchi hii ni yetu makabila mengine yakiungana nini kitatokea?
Waislamu hii nchi wakijifanya ni yao Christians wakiungana nini kitatokea
Christian hii nchi wakijifanya ni yao waislamu wakiungana nini kitatokea?
Huku mtaani tunaishi na watu wa kila aina mwingine mmakonde,Mjaluo,Waha wanyamwezi tunacheka tunakunywa tunafurahia lakini unaamka asubuhi unaanza kueneza ukabila kwa vile unatumia I'd fake jamii forum wakati ukute wewe ni kiongozi wa kitaifa au chama.
Wengine kama mimi ni wakatoriki lakini tulisoma shule za waislamu. Vijini waislamu na dini zingine wanashirikiana sana tena kwa upendo mkubwa .
Lakini mijitu misomi ndio inashinda jamii forum kupandikiza chuku na uhasama wa kidini ukanda na ukabila.
Lazima tukubali ukweli kuwa Rais anapopendelea kwao tuungane kama taifa tumshauri ajirejebishe.
Serikali inapotutangazia kuwa mkoa wa Kagera ni mkoa masikini wakati una umeme kila kijiji tena kila nyumba karibu ina luku lazima tutafakari kuwa kwanini watangaze kagera ni mkoa masikini?
Kumbukeni makabila yote ya Tanzania Tanzania sio kwenu ni waamihaji walio wengi ukiondoa wagogo ndio wazawa .
mimi nadhani tanzania hakuna ukabila ila wapo wanaojifanya kupinga ukabila kumbe wao ndio wanajenga hisia za chuki na fitina katika vichwa vya watu.
akitaka kupinga jambo fulani anaweka ukabila, anaweka udini ndio hoja yake ibebwe na hayo lakini matokeo yake anajenga hisia za ukabila vichwani mwa watu.
mfano kuna watu vi viwembe kupindukia, msichana hakatizi mbele yake, ametembea na watu idadi haihesabiki lakini watu wakiingia katika stori za kawaida unamkuta mtu huyu anasema kabila fulani ni malaya? Sasa unajiuliza hivi huyu anayoyaongea anayajua? je yeye anajitambua? je ana ushahdi kuwa lile kabila analolisema ameona tabia za kipekee katika hoja hiyo? kwa utafiti wangu nimebaini hakuna anayejenga hoja hizi kwa ushahidi bali kuna misemo watu wamezoea kusema ndio wanabeba na unakuta analolisema mtu kutuhumu wengine yeye kakubuhu.
wito wangu tutoke kwenye hadithi tunazorithishana tutafute ukweli. tusikimbilie kujenga hoja ya kaskazini wamependelewa wakati wewe huoni mwenyewe unaogopa hata kujenga nyumbani kwenu ukiogopa kurogwa sasa waliofanya juhudi na kwa ku play their role na serikali ikawaunga mkono tusifanye unafiki kuwafitini bali tuige.
yawezekana kweli huko nyuma walikuwepo viongozi wengi kutoka huko wakapeleka miradi mingi huko lakini hizo ndizo zilikuwa tawala za huko nyuma kila anayechaguliwa anakimbilia kufanya kwao.
kwa sasa tutazame tunakwendaje lakini sio kuvurugana kwa kusakiziana hoja za udini na ukabila.
hakuna jamii inayoweza kuvumilia kupakwa matope mda wote kila anayeibuka akitokea jamii isiyoendelea anadhani hojua ni kupaka matope jamii zilizombele. Zipo sababu nyingi za kihistoria, kijiografia na kitamaduni zinazoweza kusababisha jamii zisiwe sawa na anayetaka kutafuta maendeleo kwa jamii yake azitazame hizo na aangalie ni wapi pa kurekebisha.