Nilijua umeongea point mwishon ukaharibu yaan umehamasisha watu waachane na ukabila, udini na ukanda vzr baadae unawapandikiza chuki kwa kusema rais anapendelea kwao, mbona miaka ya nyuma enzi Msuya akiwa PM alijenga lami kwao mradi ambao haukua wa huko aliongea nani?, pili kuna miradi mikubwa ya maendeleo kwa sasa inayiendelea kujengwa sehemu mbalimbali za nchi hii je kila mkoa ukikosoa kwamba mradi fulan unapaswa kuwa mkoa wao unadhan itakuwaje?, halafu inaonekana kama watu wengi wa kaskazin ndio wanaotoka povu sana awamu hii sijui kwa nn au ubinafsi unawasumbua? Mbona mikoa ya kaskazin imeendelezwa sana toka Uhuru hakuna anayelalamika? Kwa hiyo hamtaki na mikoa mingine ipatiwe hata vimiradi kidogo?. Inasikitisha sana BUT sio mkaz wa kanda ya ziwa wala sio ccm nimeongea kama mtz anayekerwa na watu wabinafsi wanaotaka kila jambo zuri lifanyike mikoa yao tu