TTCL: Kufungiwa Huduma za Fiber ni bure, wanaodaiwa kuchukua rushwa hatua zitachukuliwa

TTCL: Kufungiwa Huduma za Fiber ni bure, wanaodaiwa kuchukua rushwa hatua zitachukuliwa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kueleza changamoto ya kuunganishwa na Huduma ya TTCL Fiber, kupitia ukurasa wa Instagram baadhi ya waliotoa maoni wamedai kuwa baadhi ya watendaji wamekuwa na tabia ya kuwataka wateja kulipia gharama (Rushwa) za miundombinu ikiwemo nguzo ili waweze kupata huduma.

Kusoma zaidi alichoandika Mdau bonyeza hapa ~ TTCL Fiber kuweni 'serious' na huduma zenu; kama mnaelemewa leteni wawekezaji

Hata hivyo, TTCL wamejibu hoja hiyo kwa kueleza kuwa malalamiko hayo wanayachukua uzito huku wakidai kwamba watachukua hatua kwa yoyote aliyeshiriki, vilevile wamesisitiza kuwa mteja hatakiwi kulipia gharama yoyote ya miundombinu isipokuwa kifurushi kulingana na mahitaji yake.
Screenshot 2025-09-06 110553.jpg

Screenshot 2025-09-04 173518.jpg

ttcl2.jpg

ttcl1.jpg

ttc.jpg

ttcl.jpg
Ikumbukwe kuwa Mdau wa JamiiForums, kupitia hoja yake alidai kumekuwepo na ucheleweshaji wa kupatiwa huduma kwa zaidi ya miezi sita tangu alipokamilisha taratibu zinazotakiwa.

Aidha, alidai kuwa wapo wateja ambao tayari wamekamilisha taratibu na kuunganishwa na huduma hizo, lakini intaneti imekuwa ikikosekana kwa wiki nzima licha ya kulipiwa.
 
rushwa hatuwezi acha , huduma za serikali bila kukaza kuna muda unaishia kuziona kwenye tv tu
 
rushwa hatuwezi acha , huduma za serikali bila kukaza kuna muda unaishia kuziona kwenye tv tu

Sio kweli mkuu.

Wekend ilio pita waliweka kambi Kimara temboni mpaka matosa.

Wanafungia watu Fibre kama hawana akili nzuri.

Wakasema wakitoka huko wanaenda Mbezi.

Kama mtaa ulipo umepitiwa na mkongo wa Taifa, ni chapu tu kifurushi cha chini ndo 55k. HAULIPI GHARAMA NYINGINE YEYOTE
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
TTCL sijui inahujumiwa, mimi nimeomba wafunge months sijawahi hata kujibiwa achilia mbali kufunga hiyo fiber. Kuna fundi kaja kafungia majirani anaowajua nikapewa namba afunge kwangu akagoma nifate utaratibu! Hata yeye hajafanya hata juhudi za kufatilia kama nimefungiwa. Weekend hii namalizana na Halotel
 
Sio kweli mkuu.

Wekend ilio pita waliweka kambi Kimara temboni mpaka matosa.

Wanafungia watu Fibre kama hawana akili nzuri.

Wakasema wakitoka huko wanaenda Mbezi.

Kama mtaa ulipo umepitiwa na mkongo wa Taifa, ni chapu tu kifurushi cha chini ndo 55k. HAULIPI GHARAMA NYINGINE YEYOTE
natumia ttcl fiber mkuu ___ i know them facts ~ lugha kwa hisani ya movie za mabeberu

hizo kambi maalumu sawa wanafunga kwa speed, kuhusu sehemu nje na sehemu maalumu za vikosi kazi wewe penda kutembelea comment section za mitandao yao ya kijamii -- nahitimisha
 
YAS FIBER UNLIMITED INTERNET🛠📡🛜

Kama uko DAR ES SALAAM,
Na unapatikana katika Mitaa ifuatayo tu!
📍Mbweni,
📍Boko,
📍Bunju,
📍Kijitonyama,
📍Urafiki,
📍Mradi Soko Jipya EACL - UBUNGO,
📍Sinza na Mwenge

🔥 YAS FIBER tunakufikia hadi mlangoni
🛠 Installation ni Bure kabisa ✔️
🛵📦 Delivery ni Bure kabisa ✔️
⏰️ Usisubiri tena miezi 3 au 6 ❌️
(Utahudumiwa ndani ya saa 48 tu!)



💬 Tuma ujumbe/Piga simu Leo
☎️ +255717245161
📍 DODOMA & DAR ES SALAAM

(GHARAMA ZA VIFURUSHI SOMA HAPA👇)
FB_IMG_1757062680516.jpg
FB_IMG_1757062680516.jpg
 
sasa kwanini hamtufungii? kila unapokwenda kwenye ofisi zenu tunaambiwa vifaa havipo
 
Baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kueleza changamoto ya kuunganishwa na Huduma ya TTCL Fiber, kupitia ukurasa wa Instagram baadhi ya waliotoa maoni wamedai kuwa baadhi ya watendaji wamekuwa na tabia ya kuwataka wateja kulipia gharama (Rushwa) za miundombinu ikiwemo nguzo ili waweze kupata huduma.

Kusoma zaidi alichoandika Mdau bonyeza hapa ~ TTCL Fiber kuweni 'serious' na huduma zenu; kama mnaelemewa leteni wawekezaji

Hata hivyo, TTCL wamejibu hoja hiyo kwa kueleza kuwa malalamiko hayo wanayachukua uzito huku wakidai kwamba watachukua hatua kwa yoyote aliyeshiriki, vilevile wamesisitiza kuwa mteja hatakiwi kulipia gharama yoyote ya miundombinu isipokuwa kifurushi kulingana na mahitaji yake.
Ikumbukwe kuwa Mdau wa JamiiForums, kupitia hoja yake alidai kumekuwepo na ucheleweshaji wa kupatiwa huduma kwa zaidi ya miezi sita tangu alipokamilisha taratibu zinazotakiwa.

Aidha, alidai kuwa wapo wateja ambao tayari wamekamilisha taratibu na kuunganishwa na huduma hizo, lakini intaneti imekuwa ikikosekana kwa wiki nzima licha ya kulipiwa.

Kwa mtazamo wangu, tatizo lipo makao makuu ya ttcl Tanzania; wala mikoani na wilayani katika sakata hili la kutofungwa huduma za intaneti.

Mgogoro mkubwa ni vifaa havipatikani ofisi za mikoa na wilayani, na vikipatikana vichache ni changamoto kuvipata wateja kutokana ni wingi wa wateja waliomba kufungiwa huduma za faiba kwa muda mrefu wakisubiri.

Kwa mfano leo, kuna ofisi zimesitisha kupokea maombi ya wateja wapya mpaka wazamani wafungiwe huduma kwanza.
 
Baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kueleza changamoto ya kuunganishwa na Huduma ya TTCL Fiber, kupitia ukurasa wa Instagram baadhi ya waliotoa maoni wamedai kuwa baadhi ya watendaji wamekuwa na tabia ya kuwataka wateja kulipia gharama (Rushwa) za miundombinu ikiwemo nguzo ili waweze kupata huduma.

Kusoma zaidi alichoandika Mdau bonyeza hapa ~ TTCL Fiber kuweni 'serious' na huduma zenu; kama mnaelemewa leteni wawekezaji

Hata hivyo, TTCL wamejibu hoja hiyo kwa kueleza kuwa malalamiko hayo wanayachukua uzito huku wakidai kwamba watachukua hatua kwa yoyote aliyeshiriki, vilevile wamesisitiza kuwa mteja hatakiwi kulipia gharama yoyote ya miundombinu isipokuwa kifurushi kulingana na mahitaji yake.
Ikumbukwe kuwa Mdau wa JamiiForums, kupitia hoja yake alidai kumekuwepo na ucheleweshaji wa kupatiwa huduma kwa zaidi ya miezi sita tangu alipokamilisha taratibu zinazotakiwa.

Aidha, alidai kuwa wapo wateja ambao tayari wamekamilisha taratibu na kuunganishwa na huduma hizo, lakini intaneti imekuwa ikikosekana kwa wiki nzima licha ya kulipiwa.
@ttcl ni waste of money and time...
 
Back
Top Bottom