Trust katika Mahusiano

Trust katika Mahusiano

ha haaa, ndo maana sikutaka kabisa kuzungumzia uongo kuhusu mipango ya kando..... kwenye hilo, wooooteeeee tunasema uongo. siwezi kubali kwa mpenzi wangu kuwa nina mpango wa kando, labda anikamate, lol!

Shosti post imeniacha mbaali...but nitaifuatilia yoote and i will give my opinion....

Ila hapa nimeweka nukta nikacheka kwanza bold hyooo
 
then unatakiwa kuwa muongo uliyepindukia, maana baada ya uongo wa kwanza kuna wa pili......... ili kuokoa mahusiano yasivunjike
Kwa kifupi uongo huwa haufai kabisa na uaminifu ni kitu kidogo sana lkn kikipotea huwezi kukirudisha. Ni heri kusema ukweli kwa gharama yoyote ili ujijengee sifa ya uaminifu ktk jamii na watu wa aina hiyo huaminiwa sana na mara nyingi watu husema flani akikwambia kitu jua ni kweli kwani hua hadanganyi.
 
Unajua mimi huwa nashindwa kuelewa inakuaje mwanaume kukuambia juu ya ex wake anaona sawa ie kama vile amekutana nae leo ofisi flani na anakuambia hata maendeleo ya huyo ex wake na mama unaona hakuna shida. Lkn wewe ukimwambia leo nimekutana na ex wangu mahala flani na pia kumwambia maendeleo yake , mwanaume anajisikia vibaya ni kwanini.


Kwenye mambo ya mahusiano, wanaume hujiona kana kwamba wako juu ya sheria. Pia sometimes wanawachukulia wenzao for granted...

Ni kawaida mwanamume kusimula habari za wapenzi wake wote, mwingine hata kama ni 20. Ila wewe anza kumweleza, ukifikisha hata 5-10 hajadondoka basi huyo siyo wa sayari hii!!

Muwaelewe tu na kuwasaidia...vinginevyo mtaongeza idadi ya wajane bure!!

Babu DC!!
 
Kwa kifupi uongo huwa haufai kabisa na uaminifu ni kitu kidogo sana lkn kikipotea huwezi kukirudisha. Ni heri kusema ukweli kwa gharama yoyote ili ujijengee sifa ya uaminifu ktk jamii na watu wa aina hiyo huaminiwa sana na mara nyingi watu husema flani akikwambia kitu jua ni kweli kwani hua hadanganyi.

Ukweli katika mambo gani lakini??

Kama ni mambi ya msingi na ambayo yanagusa centre ya mahusiano yetu, basi hapo tuko pamoja...!!

Ila kama ni mambo yasiyo na tija....sidhani kama ni lazima kuyaongelea.

Na hata ikibidi...unaweza kuyapotezea tu!

Babu DC!!
 
Hao achana nao, ingawa wanaboa kwani wanaongea uongo kwenye vitu ambavyo hata mhusika hana maslahi navyo!!


Linalogomba ni pale ambapo mtu anajaribu kusema uongo ambao hata hauna tija...

Mfano unataka kwenda kuonana na shoga yako FP pale Kinondoni kwa akina G (ambaye pia ni shoga yenu) na hakuna mpango wowote wa maangamizi...badaya ya kumweza baba mapacha ukweli unamwambia kuwa una safari ya ghafla kwenda kumwona ndugu yako mgonjwa Temeke hospitali...

Huo si upuuzi kweli?

Kwa watu unpredictable kama mie, naweza kukupa offer ya sympathy na kuamua twende wote kumwona mgonjwa..lol!!

Babu DC!!
babu shkamoo! mimi mtu kama huyo hata kuishi naye naona tabu sana! anaweza kukudanganya sanaaaaa, mpaka siku akikuambia ukweli, utahisi labda ni ile hulka yake imekomaa, jamani jamani TUPUNGUZE UONGOOOOOOO! MTU UNAKUWA MUONGOOOOOOOO, utasikia mimi nakaa kwenye bonge la ghorofa mbezi baharini, umepata mgonjwa ghafla, tumekuja kwako, kumbe unakaa kwenye kota za polisi! jamaniiiiiiiiiiiiiiiii! puuuuuuuuuuuuu!
 
wangu mzima lakini? mapacha wakubwa sanaaaaaaa sasa! namnyonyesha baba yao tu! naomba kuchangia kama ifuatavyo!

kuna watu WAONGOOOOOOOOO, YAANI ANAKUDANGANYA LIVE MPAKA UNASHTUKA! Mtu anadiriki kusema aliolewa bikra wakati woteeeeeeeee tunajua ana mtoto mkubwaaaaa wa nje ya ndoa! labda alimaanisha bikra ya ukuta wa nyuma! kwi kiw kiw kwi, huo ni mfano tu! kuna watu kwa kifupi wana masters ya uongo, sasa wanafanya PHD zao!
ha haaaa, mbavu zangu mimi rafikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii....
hivi snowhite keshaenda kulala? maana naona najifaidia peke yangu tu, lol!
haya hizo phd supervisor ni ke au me?
mwenzangu, haya mambo yanazidiana etiiiii...... sasa itabidi na sisi tuanze hata certificate tu, unaonaje rafiki, tutagraduate kweli?
 
Last edited by a moderator:
Kwenye mambo ya mahusiano, wanaume hujiona kana kwamba wako juu ya sheria. Pia sometimes wanawachukulia wenzao for granted...

Ni kawaida mwanamume kusimula habari za wapenzi wake wote, mwingine hata kama ni 20. Ila wewe anza kumweleza, ukifikisha hata 5-10 hajadondoka basi huyo siyo wa sayari hii!!

Muwaelewe tu na kuwasaidia...vinginevyo mtaongeza idadi ya wajane bure!!

Babu DC!!
Hapo nimekuelewa aisee manake nilikua nashinwa kuelewa mtu atakuambia mpaka meseji aliyotumiwa na ex wake lkn wewe ukijaribu kusema bwana leo nimepata number ya ex wangu . Hapo panakua hapatoshi. Kuna rafiki yangu mumewe humuonyesha sms zilizotumwa na ex wake na kila alipowasiliana lazima alimjuza mkewe. Sasa mwanamama akasema isiwe shida akaitafuta number ya cm ya ex wake nae akaja kumshirikisha mumewe kua leo nimepata number ya ex wangu , mwanaume akaona ameonewa na kuanza kufoka. Aliponiambia nilisikitika sana na kumuuliza kwanini aliitafuta iyo no akaniambia alichoka kuambiwa habari ya ex wa mumewe kila mara kana kwamba yeye hakua nae.
 
Unajua mimi huwa nashindwa kuelewa inakuaje mwanaume kukuambia juu ya ex wake anaona sawa ie kama vile amekutana nae leo ofisi flani na anakuambia hata maendeleo ya huyo ex wake na mama unaona hakuna shida. Lkn wewe ukimwambia leo nimekutana na ex wangu mahala flani na pia kumwambia maendeleo yake , mwanaume anajisikia vibaya ni kwanini.
ha haa, jibu la hii naona ukimsoma babu Dark City hapo post na 161 unaweza ona sababu.....
 
Last edited by a moderator:
Hao achana nao, ingawa wanaboa kwani wanaongea uongo kwenye vitu ambavyo hata mhusika hana maslahi navyo!!


Linalogomba ni pale ambapo mtu anajaribu kusema uongo ambao hata hauna tija...

Mfano unataka kwenda kuonana na shoga yako FP pale Kinondoni kwa akina G (ambaye pia ni shoga yenu) na hakuna mpango wowote wa maangamizi...badaya ya kumweza baba mapacha ukweli unamwambia kuwa una safari ya ghafla kwenda kumwona ndugu yako mgonjwa Temeke hospitali...

Huo si upuuzi kweli?

Kwa watu unpredictable kama mie, naweza kukupa offer ya sympathy na kuamua twende wote kumwona mgonjwa..lol!!

Babu DC!!
ha haaa, umeona eeeh!
au mwulize cacico kilichotokea pale Kebbys...... hivi ningesema uongo lile jahazi nani angeliokoa? si ningeumbuka?
 
Last edited by a moderator:
Yes kuna kweli zingine ni very unpleasant au damaging. Mzazi mwenzangu aliniambiaga baada ya kuona jinsi gani nilivyohonest kuwa "kutosema ukweli wote hakumaanishi unasema uongo", so kwa couple sio vizuri kudig sana past za mtu maana waweza sababisha akudanganye kwa ajili ya kuprotect relationship yenu. Kuna vitu kama mtoto ni muhimu kuuliza lakini sijui umeshatembea na wanawake wangapi it is irrelevant IMO.

daaaa hata anaye uliza swali kama hili lazima anategemea kudanganywa.
 
ha haaaa, mbavu zangu mimi rafikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii....
hivi snowhite keshaenda kulala? maana naona najifaidia peke yangu tu, lol!
haya hizo phd supervisor ni ke au me?
mwenzangu, haya mambo yanazidiana etiiiii...... sasa itabidi na sisi tuanze hata certificate tu, unaonaje rafiki, tutagraduate kweli?
tena snowhite awe supervisor wetu! na @gfsonwhite atuongoze kwenye dessertation, jamani mbona majangaaaaaaaa?? yaani kuna watu ni waongoooooo wamevuka mipaka! mi hubby wangu Asprin anasemaga uongo mtamu!
 
Last edited by a moderator:
Hapo nimekuelewa aisee manake nilikua nashinwa kuelewa mtu atakuambia mpaka meseji aliyotumiwa na ex wake lkn wewe ukijaribu kusema bwana leo nimepata number ya ex wangu . Hapo panakua hapatoshi. Kuna rafiki yangu mumewe humuonyesha sms zilizotumwa na ex wake na kila alipowasiliana lazima alimjuza mkewe. Sasa mwanamama akasema isiwe shida akaitafuta number ya cm ya ex wake nae akaja kumshirikisha mumewe kua leo nimepata number ya ex wangu , mwanaume akaona ameonewa na kuanza kufoka. Aliponiambia nilisikitika sana na kumuuliza kwanini aliitafuta iyo no akaniambia alichoka kuambiwa habari ya ex wa mumewe kila mara kana kwamba yeye hakua nae.

Mwanamume anashindana na wanae kwa mkewe sasa ndo ulete habari za ex si ndiyo patachimbika??

Tuacheni jamani...Mungu mwenye ndiye katuumba hivyo...

Just loves and get us not into competition...

Babu DC!!
 
I say trust but verify. Kuamini amini tu bila kushirikisha common sense na bongo yako haihusiki kabisa.



Mi sioni ubaya wa kumwambia mwenza wako saluni gani unaenda maana kama unaenda kweli kwa nini usimwambie? Ni vizuri kumwambia mwenzio ili hata ukipatwa na mabaya na usirudi nyumbani yeye angalau atakuwa anajua pa kuanzia.



Hivi kwanza mtu unaanzaje kumwambia mpenzi wako kwamba umekutana na ex wako? Ni kwamba out of the blue unaanza 'habibti/ habibi leo nimekutana na ex wangu pale Shoppers Plaza au'?
umeufanya ubongo wangu, uchanganyike na kukumbuka ya nyuma .

niliwah siku kumsifia mwanaume mmoja ambaye walisoma nae na out of my own understading nlimwambia mwanamke atakaye olewa na MW..... atafurah sana, huuby akinyunyuka na kuelekea chumban na msosi ambao alikuwa anakula alisusa. to be fair as a lady nilijua nimekosea ingawa kimsingi sio kosa kivile. basi nili kuwa mpole nikamwangukia hubby kwa samahani hadi akarudisha moyo nyuma na kula msosi wake alokuwa kaususa.

kimbembe kikaja siku moja nilikuwa naenda sokoni nikakutana na huyu shemeji, tukasalimiana vizuri kweli tukadondosha stori moja mbili, basi akanipatia kadi ya mchango wake wa harusi. mm kuikataa kuipokea nilishindwa manake ningemwambiaje?? nikaichukua nikaiweka mfukoni, njian narudi nawaza nitamwambiaje mume kwamba nimekutana na huyu mtu na wakati alishanikanya nisimuongelee huyu mtu mbele yake?? dah uanamke kazi niliumwa kichwa kwa mawazo mwisho nikasema to hell with everything nitamwambia ukweli ila nitatafuta pozi la kushuka ili asiniwie mbogo. mweeeeh!

basi jion hubby karudi mie tabasamu la kulazimisha ile mbaya pole nk vikafuata, baada ya mapumziko kaoga, kala tukaingia chumban basi kitandani nawaza naazaje kusema?? kumbe bwana nikiwa nawaza naazaje kusema hubby alikuwa kesha chungulia ndani ya pochi yangu akiwa anatafuta nail cut akaiona na yeye aliuchuna ili ajue kama nitasema kweli ama nitamficha. si nikaanza mume wangu mpenzi niko chini ya miguu yako baba nisamehe usinigombeze naomba unisikilize. hahah...........alichonijibu mbona unatubu sana mie unachotaka kuniambia nakijua wala usipate shida ya kuungama ila tu niambie ukweli umekutana wapi na mw...............???

mmh! yaani ilikuwa kama maji yaliyopatiwa njia ya kupita, nilijieleza kana kwamba natolewa roho kwa heshima utafikiri kashikilia digrii yangu ama anataka kuchana cheti changu. alichonijibu ni neno moja tu alisema yaani D ungenificha hili ungenitambua ila umesema ukweli sion shida nimekuelewa.

mm ndo presha ikashuka nikalala mtoto wa kike.

mpaka leo sijui kwann lakini binafsi huwaga nasema mwanaume ni mwanaume tu aisee hata kama ni mtoto mdogo wa kiume mi saluti kwake. na ndio maana hunikuti nashindana nae milele.
 
Shosti post imeniacha mbaali...but nitaifuatilia yoote and i will give my opinion....

Ila hapa nimeweka nukta nikacheka kwanza bold hyooo
ha haaaa, hapo kwenye bold ni kweli shosti.....
hivi ntaanzaje kusimulia kuwa nina mpango wa kando? au yeye ataanzia wapi kunisimulia? hapo ni kudanganyana tu....
ila sasa inapotokea nadanganya kuwa naenda hosp wakati naenda kwenye kibao kata hapo sasa ndo kuna tatizo
 
Back
Top Bottom