umeufanya ubongo wangu, uchanganyike na kukumbuka ya nyuma .
niliwah siku kumsifia mwanaume mmoja ambaye walisoma nae na out of my own understading nlimwambia mwanamke atakaye olewa na MW..... atafurah sana, huuby akinyunyuka na kuelekea chumban na msosi ambao alikuwa anakula alisusa. to be fair as a lady nilijua nimekosea ingawa kimsingi sio kosa kivile. basi nili kuwa mpole nikamwangukia hubby kwa samahani hadi akarudisha moyo nyuma na kula msosi wake alokuwa kaususa.
kimbembe kikaja siku moja nilikuwa naenda sokoni nikakutana na huyu shemeji, tukasalimiana vizuri kweli tukadondosha stori moja mbili, basi akanipatia kadi ya mchango wake wa harusi. mm kuikataa kuipokea nilishindwa manake ningemwambiaje?? nikaichukua nikaiweka mfukoni, njian narudi nawaza nitamwambiaje mume kwamba nimekutana na huyu mtu na wakati alishanikanya nisimuongelee huyu mtu mbele yake?? dah uanamke kazi niliumwa kichwa kwa mawazo mwisho nikasema to hell with everything nitamwambia ukweli ila nitatafuta pozi la kushuka ili asiniwie mbogo. mweeeeh!
basi jion hubby karudi mie tabasamu la kulazimisha ile mbaya pole nk vikafuata, baada ya mapumziko kaoga, kala tukaingia chumban basi kitandani nawaza naazaje kusema?? kumbe bwana nikiwa nawaza naazaje kusema hubby alikuwa kesha chungulia ndani ya pochi yangu akiwa anatafuta nail cut akaiona na yeye aliuchuna ili ajue kama nitasema kweli ama nitamficha. si nikaanza mume wangu mpenzi niko chini ya miguu yako baba nisamehe usinigombeze naomba unisikilize. hahah...........alichonijibu mbona unatubu sana mie unachotaka kuniambia nakijua wala usipate shida ya kuungama ila tu niambie ukweli umekutana wapi na mw...............???
mmh! yaani ilikuwa kama maji yaliyopatiwa njia ya kupita, nilijieleza kana kwamba natolewa roho kwa heshima utafikiri kashikilia digrii yangu ama anataka kuchana cheti changu. alichonijibu ni neno moja tu alisema yaani D ungenificha hili ungenitambua ila umesema ukweli sion shida nimekuelewa.
mm ndo presha ikashuka nikalala mtoto wa kike.
mpaka leo sijui kwann lakini binafsi huwaga nasema mwanaume ni mwanaume tu aisee hata kama ni mtoto mdogo wa kiume mi saluti kwake. na ndio maana hunikuti nashindana nae milele.