Usiyoyajua Kumhusu Le Mutuz Super Brand!, Je Wajue Alijitabiria Kifo Chake Kabla?. Aliandika Kila Kitu. Could He Be The Top Most JF Celeb Wetu?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,498
113,604
Wanabodi,
JF bado tuko kwenye maombolezo ya kumlilia member mwenzetu William Malecela, kwa jina maarufu Le Mutuz Super Brand ambaye kesho Jumatano saa 9:00 Adhuhuri ndipo atapumzishwa kwenye nyumba yake ya milele, kwenye makaburi ya familia ya Malecela pale Mvumi Mission, Dodoma.

Kuna mengi kumhusu mtu huyu ambayo wengi hawayajui, miongoni mwa mengi hayo ni alijiandaa kwa kila kitu kwa kuandika kila kitu kuhusu maisha yake ikiwemo kujitabiria kifo chake kama alivyoandika hapa Le Mutuz: Historia ya kweli juu ya maisha yangu (My American experience)

Mange anawawakilisha baadhi ya Maadui zangu wa Maisha ambao wangependa kusikia nimekufa kwa sababu wana wasi wasi kua nitawadhulumu urithi wa Baba yetu ambaye bado yupo hai na huenda hata tukaondoka sisi tukamuacha ....hahahahha....

Ama kweli kauli huumba!. Na mimi naomba kuuliza, jee kuna uwezekano William Malecela, Le Mutuz Super Brand akawa ndiye the top most celeb wetu humu JF?.

Kwa wale mtakao penda kumfahamu zaidi, unaweza kujua each and everything kumhusu Le Mutuz kwa kutembelea bandiko hili Le Mutuz: Historia ya kweli juu ya maisha yangu (My American experience)

RIP WJSM Tribute to Mwana JF Mwenzetu William Malecela Le Mutuz, Alikuwa Mtu wa Watu

Paskali
 
Uungwana wake ulimpelekea kutafuta bila kuchoka suluhu baina yake na wanae waliopo Marekani.

Bahati mbaya sana sana mke wake na Mange walijitahidi kutumia fursa hiyo kumdhalilisha wakiamini wanafanya vyema.

Atabaki muungwana daima kwa sababu hapa mwisho aliamua kuwa muungwana.

Mungu Mpokee Mja wake
 
Uungwana wake ulimpelekea kutafuta bila kuchoka suluhu baina yake na wanae waliopo Marekani.

Bahati mbaya sana sana mke wake na Mange walijitahidi kutumia fursa hiyo kumdhalilisha wakiamini wanafanya vyema.

Atabaki muungwana daima kwa sababu hapa mwisho aliamua kuwa muungwana.

Mungu Mpokee Mja wake
Yule Mange mwisho wake atakuwa Mbaya sana, ubaya una mwisho.

Ila Neema na Watoto wake wamelaaniwa na hasa Watoto wana laana ya milele.
 
My dad did me wrong. You know what i do? I call him halaf namwambia baba nakupenda ujue? Najisikia raha sana kuongea na wewe. Na sometimes we go for the date. Sitaki ajisikie vibaya ama kujutia alishanikosea. Sitaki akose amani. Nampenda kwa kweli. Sitaki afe kwa msongo wa mawazo. Amekosea. Amehua alikosea na life must go on. Hakunaga kitu nakichukuliaga maanani kama mtu kuniomba radhi. Hata kama asipotamka lakini matendo yake yakawa yanaashirua kwamba anajutia namhug na kumsamehe. Wazazi ni baraka. Wanakosea lakini sasa tufanyeje?
 
Screenshot_20230516-135349_Chrome.jpg
 
sema jamaa alikua anachukiwa na watu wengi huko mtandaon, na watu wenyewe walikua hawana sababu ya kumchukia ni vile tu walipandikizwa chuki kupitia watu wao waliowapenda(kina mangekimambi)

wa bongo tunapenda kununua ugomvi sana
 
Kuna watu wana matatizo yako obvious na daktari alishawaambia they won't live longer than muda fulani.

Mnakumbuka kauli za nikifa atamalizia nani? Nimejitoa uhai wangu kwa ajili ya nchi yangu? It was obvious they wouldn't exceed a certain period of time hence "unabii".
 
Back
Top Bottom