Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

-Nchi zilizoendelea traffic hawakai barabarani kuongoza magari.
-Traffic wanakuwa Control room/ vituo mbalimbali au Kwenye magari ya patrol na hujitokeza haraka inapotokea ajali barabarani.
-Barabarani hufungwa camera maeneo yote muhimu.
  • Barabarani kuna lane zinazotakiwa kuendesha gari kwa mwendo wa polepole, kawaida au kasi(speed limit inaonyeshwa) ,kwa mfano lane ya kulia ni mwendo kasi, ukiendesha mwendo polepole unapigwa picha na kutozwa faini
  • Bili utakuta imebandikwa mlangoni nyumbani kwako.
-Magari yote au madereva wote ni lazima kuonyesha anuani ya makazi na kitambulisho chako au passport number yako,na taarifa zingine muhimu.
-Kuweka camera barabarani hufanywa mara moja na hufanyiwa service Mara moja au mbili kwa mwaka,na huleta ufanisi na tija badala ya kujaza traffic barabarani.

Ushauri
1). Kwa kuwa Tanzania kuna vitambulisho vya Taifa na anuani za makazi
-Serikali iweke camera za barabarani kwenye maeneo hatarishi (Kona Kali,vivuko etc) badala ya kuweka traffic wengi,( Ili kupunguza gharama za uendeshaji).
2). Serikali iwe na magari mengi ya patrol kwa ajili ya kutoa msaada pindi inapotokea ajali au kuwakamata wahalifu wa makosa wa jinai.
3). traffic waache kutoa au kutoza faini,kwa maana muhimili wenye dhima ya haki au hukumu ni Mahakama.
 
Sio kweli Mkuu !! Mimi ni raia mwema tu ! Najaribu kutoa tahadhari maana mimi nimesafiri sana barabarani nawajua vizuri sana madereva wetu wa sasa huko barabarani akili zao huwa zinahama sijui huwa zinaenda wapi ! Ndio maana utaona kila wakati wanaulizana kwa ishara kama Trafiki wapo mbele au hawapo? Ili tu akanyage mafuta kisawasawa na bila kuchukua tahadhari yeyote !!
Kwani wamekuambia wamewaondoa woote barabarani au wamewapunguza idadi, maana sehemu yenye kutakiwa kuwa na askari watatu wao walikuwa wanajazana mpaka wanane....... Pia ndo walikuwa wanatakatisha rushwa kwa kuhonga viongozi wao ili wabaki kwenye vituo vyenye kupata rushwa kwa wingi na kukataa kwenda kwenye vituo vyenye uchache wa kupata rushwa hususani mikoani. Mfano wa karibu hapa Muheza japo kuwa ni wilaya lakini kuna idadi ndogo mno ya hao wanausalama
Bora hili fagio lipite na liwagawanye kwa usawa kuwapeleka kwenye vituo vingine haswa vile walivyokuwa wanavikataa
 
Sio kweli Mkuu !! Mimi ni raia mwema tu ! Najaribu kutoa tahadhari maana mimi nimesafiri sana barabarani nawajua vizuri sana madereva wetu wa sasa huko barabarani akili zao huwa zinahama sijui huwa zinaenda wapi ! Ndio maana utaona kila wakati wanaulizana kwa ishara kama Trafiki wapo mbele au hawapo? Ili tu akanyage mafuta kisawasawa na bila kuchukua tahadhari yeyote !!
Watakuwepo lakini syo kwa kujazana sehemu 1 matrafik 15+

Ova
 
Kulinda banki,masoko nk hakuna mchongo huko aise

Ova
 
Enzi zetu za Railways bus na KAMATA vidhibiti mwendo ilikuwa ni kawaida kwa kila bus
Hayo mabasi yalikuwa ni mateso kwa mwendo wake wa Kobe...
Mbeya via Iringa kutokea Dar ilikuwa inachukua masaa karibu 20....

Na kama kungekuwa na traffic police kama sasa ingechukua masaa zaidi ya 25
 
Ukienda duniani bara zote zina rada zilizo parmanent computerized, ukija kuzimu mhhhhh
 
1). Kwa kuwa Tanzania kuna vitambulisho vya Taifa na anuani za makazi
-Serikali iweke camera za barabarani kwenye maeneo hatarishi (Kona Kali,vivuko etc) badala ya kuweka traffic wengi,( Ili kupunguza gharama za uendeshaji).
Nakazia;
Wakiinvest kwenye technology serikali itakusanya mapato kuliko kuwategemea traffic police ambao huchukua rushwa na kuzitumia wao kwa mambo yao binafsi
 
Kwani wamekuambia wamewaondoa woote barabarani au wamewapunguza idadi, maana sehemu yenye kutakiwa kuwa na askari watatu wao walikuwa wanajazana mpaka wanane....... Pia ndo walikuwa wanatakatisha rushwa kwa kuhonga viongozi wao ili wabaki kwenye vituo vyenye kupata rushwa kwa wingi na kukataa kwenda kwenye vituo vyenye uchache wa kupata rushwa hususani mikoani. Mfano wa karibu hapa Muheza japo kuwa ni wilaya lakini kuna idadi ndogo mno ya hao wanausalama
Bora hili fagio lipite na liwagawanye kwa usawa kuwapeleka kwenye vituo vingine haswa vile walivyokuwa wanavikataa
Kuna sehemu kama kutoka Mombo kwenda Lushoto; trafiki wa kule nahisi wanaweza maliza hata mwezi bila kupata "chochote" labda fadhila za mabasi, coaster, na fuso on friendship basis.

Kwa jiografia ya kule sioni overspeed au wrong overtaking vikitokea kwa sana makosa muhimu ya trafiki kupiga hela. Wanapigwa baridi hadi wanatia huruma kule.
 
Kuna sehemu kama kutoka Mombo kwenda Lushoto; trafiki wa kule nahisi wanaweza maliza hata mwezi bila kupata "chochote".

Kwa jiografia ya kule sioni overspeed au wrong overtaking vikitokea kwa sana makosa muhimu ya trafiki kupiga hela. Wanapigwa baridi hadi wanatia huruma kule.
Waende likizo ya Kinana wakaote moto washibe
 
Tuliweka uzi humu kuhusu Polisi wa barabara kupunguzwa , huku wengi wao wakipangiwa kulinda Mabenki Usiku , lakini kwa bahati mbaya Moderator akaunga uzi ule kwa mafundo mengi utadhani HIRIZI WANAZOTAPIKA WAUMINI WA MWAMPOSA .

Lakini leo Gazeti la Raia Mwema limeripoti kwamba tayari panga limekwisha tembea , huku MCHEZO WA UPATU waliokuwa wanacheza Trafiki hao kila siku ukibaki njia panda , kwa vile wengi wamepangiwa kazi zingine ambazo haziingizi chochote zaidi ya Mshahara , TAARIFA ZINADOKEZA KWAMBA TRAFIKI WENGINE WALIKUWA NA MCHEZO WA UPATU WA KULIPA HADI SH LAKI MOJA KWA SIKU , ambapo inaelezwa kwamba chanzo cha hela hizo ilikuwa ni Rushwa za barabarani .

Kwa mujibu wa gazeti hilo , Trafiki wengi wanamlaumu Kinana kwa kuibua jambo hilo .

Endelea kubaki JF kwa taarifa zaidi .

Ndio maana jirani alikuwa anaishi nyumb ya 350000 kwa mwezi juzi kahama nasikia kahamia huko goba nyumba ya 180000
 
Back
Top Bottom