Mkuu wangu, umesema jambo sahihi kabisa...ili kutoa mzizi wa fitina wapewe bure though am certain bado watakataa coz' base ya madai yao haipo kwenye bei bali ni kwamba hawataki tu hizi mashine kv wanafahamu udanganyifu wao utakuwa unaelekea]
Tatizo kubwa na la msing hapa ni zaidi ya Machine za EFD ni mfumo mzima wa kodi... Wafanyabiashara wana madai zaidi ya machine za EFD ambazo kwa sababu za makusudi serikali chini ya TRA ndio inachokishililia.. IKUMBUKWE Wafanyabiashara hawa ni walipa kodi wazuri wa kodi zao walizokuwa wanakadiliwa.
Madai ya wafanya biashara ni haya..
- Kwanza ni BEI ya machine ulikinganisha na BEI ya soko ya machine husika kwa soko la sehemu nyingine duniani.. kenya tu mashine zinapatikana kwa chininya TZS 350,000. ukienda china na kwingineko ni chini ya $80.
- Gharama kubwa na usumbufu unaotokana na machine hizo ukilinganisha na cash flow za mlengwa yaani mfanyabiashara anayeingiza 38,000 Kwa siku... Gharama za karatasi moja ni 6000 na gharama za maintenance ambazo ni zaidi ya laki 3 kwa mwaka na usumbufu wa kuripoti TRA NA KWA WAKALA kila machine inapoaharibika...
- Utaratibu wa faini kwa amabaye atashindwa kutumia machine hizo unatoa mwanya kwa wafanayakazi wasio waaminifu wa TRA( ambao ni wengi) na Askari waliozoea Rushwa kuleta taabu kwa wafanyabiashara.
- Machine za EFD hazionyeshi gharama za manunuzi na gharama za uwendeshaji ambapo hapo hasa ndio penye tatizo kubwa... Gharama nyingi za manaunuzi ama hazina risiti ama zina risiti ambazo hazilingani na gharama halisi... HILI LITAPELEKEA mfanyabiashara kutozwa kodi kubwa kuliko hanavyostahili kutokana na kukosekana na kumbukumbu za manunuzi.
- Mfumo mzima wa biashara ama zimetoka nje ya nchi ambazo ulipiwa kodi custom.. kodi ya import duty and VAT...Au zimenunuliwa kwa wakulima na wavuvi ama wafugaji ambao hawatoi risiti...Kwa zinazopita Customs ukadiliaji umekuwa shida kubwa... mzigo huo huo amabo haupishani hata miezi mitatu unaweza kuwa na kodi tofauti na tena yenye tofauti ya kutisha ... hii imeleta mianya ya rushwa kwa watumishi wa TRA na kupelekea wafanyabiashara kulipa malipo mengi yasiokuwa na risiti... amabayo yatakuja kumfanya alipe malipo mengi ya kodi ya mapato.
- Kodi zinazotozwa na TRA Customs hazinlingani na thamani halisi ya bidhaa zinazoingizwa na kushawishi wafanaya biashara kukubali kutoa rushwa ili angalau aweze kuuza bidhaa yake kwa gharama nafuu.
- kwa mazao yanaotka kwa wakulima mengi hayana risiti na kwa stahili hii mfanyabiashara atalazimaika kulipa zaidi kodi za mapato.
- Kwa ujumla mfumo mzima wa kodi unatakiwa kuangaliwa upwa ili uwe wazi na unaoshawishi wafanyabiashara kulipa kodi stahiki na kupunguza mianya ya Rushwa .... GHARAMA Nyingi za uendeshaji hazina risiti na hili ni tatizo la kuangalia ..
- Mfumo hauruhusu uingizaji wa mzigo wa pamoja ( sharing importation) ambapo kila mfanyabiashara aliyeshare container atalipa stahiki yake na mzigo wake kuwa na thamanai ya manaunuzi...
- kwa ujumla kufanya baishara Tanzania hasa kwa sekta zisizo rasmi zimekabiliwa na kodi nyingi zisizo na kichwa wa miguu... kodi za pango... kodi ya takataka.. kodi za fire... kodi za mabango... kodi za hamashauri... nk nk...
Tubadilike nchi ni yetu sote... sekta hii nayo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa... iundwe tume maalumu ya kurekebisha mfumo mzima wa ulipaji kodi na kuwaka fair ness kwa pande zote.... na kusitisha zoezi la EFD
Muonamambo
A town
Naona kila mtu anasema amefanya 'UTAFITI' juu ya hii EFD lakini sifahamu kama ni kweli wamefanya au wamesikia tu watu wakizungumza tu mabarazani..
1. Watu wanachanganya kati ya
Electronic Cash Register (ECR)
Na Electronic Fiscal Device
(EFD). Hizi ni mashine aina
mbili tofauti kimadhumuni
Hizo ECR unaweza nunua
popote na kuzitumia, na ndizo
hizo ukienda China watu
huzikuta na kuja kuleta madai
ya bei.
EFD huwezi ikuta dukani
kiholela na kuinunua ili
uitumie sababu inatengenezwa
kwa matakwa maalum ya kila
nchi husika,na si kila
mtengenezaji anatengeneza
2. Kuhusu Kenya,
kwanza hakuna EFD kenya ipo
chini ya 600000 TZS.
Pili EFD za kenya zipo tofauti
kiutendaji ukilinganisha na za
hapa,Wao walikuwa wa kwanza
kutumia hizi mashine,
na ilikuwa haina mfumo wa
kutuma Z Report kwenda KRA,
sisi tulichofanya kwa za kwetu
ni kuziongezea uwezo wa
kutuma hiyo Z Report kila siku
kwenda TRA
(hapa ushamuongezea kazi ya
ziada mtengenezaji » bei
itapanda),,
baada ya sisi kufanya hili KRA
iliikubali TRA na wakaja
kujifunza,Na wao siku si nyingi
wataanza zoezi upya liwe
kama la TRA.
3. Kila nchi inaagiza itengenezewe
EFD vile inavyotaka iwe, ndiyo
maana hata bei hazifanani
4. Ushauri:
Hizo kodi nyingine
wafanyabiashara wanazolipa
inabidi wakae na wanaowatoza
kujua jinsi gani ya kuweza
kuzipunguza, mfano kodi ya
jengo,takataka,zimamoto,n.k
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums