TRA someni hapa: EFD zenu WIZI MTUPU

TRA someni hapa: EFD zenu WIZI MTUPU

Sasa hebu sample wenye maduka ya namna hii uliyoeleza hapa uwaulize kama wameletewa barua ya kununua EFD. Mimi ni mmojawapo, nina kiosk changu mtaani kina-fit kabisa kwenye description hii na nilileletewa barua tangu mwaka jana, na kuna mtu amekuwa akinikumbushia kwa simu mara kwa mara. Ndio maana nasema na nitasema tena na tena, HUU NI WIZI MTUPU.
Tangazo la TRA lipo wazi, kia siku wanasema ikiwa kuna mtu anaamini amepelekewa barua pasipo kustahili basi ni wajibu wake kwenda TRA ili nao wafanye tathimni upya...so, that's ur problem.
 
Mashine zinatumiwa kwa wafanyabiashara ambao anaingiza milion 40 kwa mwaka,na hiyo ni faida,sasa wew unasema wanaonea walala hoi,hivi mtu anaepata faida ya milioni 40 unamwita malala hoi?
Unapopinga jambo usipinge kwa unafiki
 
Haya mambo ya TRA na EFD zao ni WIZI MTUPU. Wanataka mtu mwenye mauzo ghafi ya kuanzia TSh 14,000,000 kwa mwaka anunue hiyo kifaa ambayo bei yake ni kuanzia laki sita na ushee. Twende kimahesabu. Mauzo ya sh 14mil kwa mwaka ni kama wastani wa kuuza sh 38,000 kwa siku. Kwa profit margin ya 10-15% mfanyabiashara kama huyu ana faida ghafi ya kama Tsh 4,000 hivi kwa siku. Akitoa gharama za pango, ulinzi, umeme, usafi, na tukichukulia hana mfanyakazi, huyu mtu faida yake net haizidi 1,000 kwa siku. Watu ambao mmewahi kufanya biashara mnaelewa, mtu mwenye mauzo ya sh 38,000 kwa siku ni mfanyabiashara MDOGO SANA, wa chini kabisa, ni mtu wa kima cha chini huyu. Mtaji wa kuuza 38,000 kwa siku ni mdogo kuliko hiyo laki sita ya kununulia EFD.

TRA wametumia akili gani kudhani kuwa mtu huyu wa kima cha chini anayechuma chini ya sh 1,000 kwa siku anaweza kununua hiyo EFD ya sh 600,000? Mtu anunue kadude hako kwa bei kubwa kuliko mtaji alionao? Halafu wanashangaa kuona watu wanaandamana! Nyie TRA mnashangaa nini kuhusu maandamano? Hamuwajui wanaoandamana? Ni wafanyabiashara ndogondogo wenye mauzo ya sh 38,000 kwa siku, eleweni hivyo. Na hawa wako wengi sana, hawahitaji kutumwa na mtu.

Jamani hivi huko TRA mbona mnataka tudhani kuwa wote mlifeli hesabu? Sh laki sita atazipata wapi mtu anayechuma elfu moja kwa siku? Hata akifanya kazi mwaka mzima bila kula, jumla ya kipato chake itakuwa sh 365,000 bado haitoshi kununua EFD. Mtumie akili jamani. Hicho kiwango hakiwezekani kwa wafanyabiashara mnaowalenga.

Cha kufanya. Rejeeni hicho kiwango mrekebishe, muanzie labda kwenye mauzo ghafi ya sh 100,000,000 kwa mwaka (ambayo ni sawa na wastani wa sh 270,000 hivi kwa siku) hawa angalao wangeweza, na nadhani hawalalamiki maana tunaona zikitumika kwenye maduka. Na hawataandamana.

Hivi mnafahamu kwamba wafanyakazi wanalipa kodi kubwa sana tena bila hata chembe ya kuweza kuikwepa? Hivi mnafahamu kwamba wafanyabiashara ndio wakwepaji wakubwa wa kodi ?

Serikali inapata kodi toka kwa wafanyakazi kwa kutumia mfumo wa Lipa Kadri Unavyopata (PAYE); hapa mfanyakazi ukipata pato tokana na ajira yako unakatwa kodi kulingana na pato hilo. Mfumo huu ndio sawa na huu wa EFD kwa wafanyabiashara. Wanatakiwa walipe kadri wanavyopata. Kama ni hasara si itaonekana.

Hapa suala siyo gharama za EFD hapa suala ni kutaka kuendelea kukwepa kulipa kodi.

Unataka kusema kwamba wafanyabiashara wa Kariakoo hawawezi kununua hizo mashine za EFD? Jiulize wanalipa pango kiasi gani?

Kuna baadhi ya wafanyabiashara kwa sasa wanatoa hizo risti za EFD lakini nasikia wanakupa na usafiri na kijana wa kukusindikiza (kama umenunua mzigo mkubwa). Siyo kwamba wanakupa usafiri kwa mapenzi saaana juu ya mteja wao bali ni kwamba kijana akienda anachukua risti anarudi nayo akija mwingine naye hivyo hivyo! Risti moja inaweza kutumika kuuuzia mizigo mingi. Wanakwepa kodi.

Kwamba TRA inataka kuwabana wafanyabiashara walipe kodi, wanagoma kisha tunasema waendelee na mtindo wao huo ambao ni dhahiri ni ukwepaji kulipa kodi.

Siku wafanyakazi nao wakisema hawataki kulipa PAYE bali wapewe hela zao zote na wao kupeleka kodi TRA itakuwaje?

 
on the other hand nawahurumia wafanyabiashara, kwani wanawatetea watu wasiohitaji utetezi. wanachotakiwa kufanya ni kuongeza bei kwa asilimia 18 kwa kila bidhaa wanayouza,ili hao mabwana kodi waendelee kuchukua 18% bila kuathiri faida.

mahesabu yawe hivi.

mchele umenunua 1000

uza 1200

faida yako 200

kabla mama havintishi hajalipa unamwambia apunguze kasi, muda wa kulipa kodi kujenga nchi.

unajumlisha 18% ya kodi ya jamaa zako wa TRA.

mama havintishi inabidi akung'ute 1416 kwani kuna kashilingi 216 ka TRA hapa kati.

sasa shida ipo hapa, watanzania wangapi wako tayari kulipia hiyo 216 ya ziada ili wapate mchele wao wa 1200?

watanzania wangapi wako tayari kusamehe risiti walipe 1200 wajikate zao?

hizi EFD zitafanikiwa kiutendaji kutokana na mtazamo huo?

jibu la hili swali ndio kazi ya Kamishna wa TRA. kama hana jibuhadi leo, hatakiwi kuwepo kazini.


kuna kitu TRA wanajisahau, kwa makampuni na taasisi, RISITI ni kitu cha muhimu kwa ajili ya kuweka kumbukumbu. Muuza vitumbua wa Kitanzania hahitaji risiti ya kikaangio chake alichouziwa 12000 na muuza vikaangio pale karume. hiyo 2160 ya ziada, ili apewe risiti ingemtosha kufanya nauli, na chenji inayobaki mtoto aendee shule kesho.NDIO maisha ya watanzania wengi.

Kufanikiwa kwa EFD kwenye makampuni yenye mauzo makubwa ni kwa sababu wateja wao si hawa wauza maandazi, si watanzania wa chini, wateja wa haya makampuni ni wale wanaogawana 7% GDP increase ya Tanzania kwa miaka 15 iliyopita. Ingawa hata hawa wanazidoji hizi risiti saa nyengine, lakini hawa hawana jinsi.

Kama kamishna wa TRA halioni hili, sioni sababu ya yeye kuwepo pale.hana ufahamu wa idara anayoiongoza.kugombana na mabosi wake (wafanyabiashara/wananchi) sio njia salama kwake.

Usilolijua kama usiku wa kiza
 
TRA ingetoa hizo mashine za EFD bure ili kukata mzizi wa fitna na unafiki wa wafanya biashara..
 
Wewe rudi primary kabisa maana naona economics zako za "versity" zishakuvuruga. Hiyo sentensi yako ya mwisho inakuhusu wewe mwenyewe kwa 100% maana hakika wewe ni kilaza usiyejijua. Huoni hata haya kujidhihirisha kuwa hujui gharama za biashara, bila aibu unauliza "kama zipi". Ilimradi tu umefika "versity" (hivi ndio wapi huko maana hata kwenye kamusi hakuna neno hili) unajiona mjuaji kumbe bora hata boya kabisa. Hayo maneno machache ya kiingereza hapo sijui gross income, net income...etc ulivyoyakariri basi wajisikiaaaa!

Sasa sikia we kilaza mwandamizi, rudi kajifunze tofauti kati ya "income" na "revenue" halafu uje tuzungumze kulinganisha kati ya biashara na ajira, labda hapo tutaelewana. Maana hizo economics zako za kukariri terminology za kwenye "madesa" zimekuyumbisha sana.
Narudia, wewe ni kilaza...nimekuuliza kama gharama zipi coz' kila unapotoa gharama fulani; unabaki na kitu fulani na ndio maana hata huko kwenye profit kuna profit b4 and after tax depending umetoa gharama ipi na ipi...na kukuonesha ulivyo kilaza wala hufahamu TRA reference yao ni nini...wao reference yao ni annual sales turnover...but in addition to that, acha tabia za kichoko jukwaani...huna sababu za kila wakati kurudia rudia "we wa 'versity" huo ni ushamba. Au kimekuchoma sana kusema nimepiga namba hadi 'versity? we wa wapi wewe?
 
Kulipa kodi nikitendo cha uzalendo

Acha upuuzi watu kama nyie mnapaswa kunyongwa mnaleta hasara duniani. Baba yako na mama yako mwenyewe umeshindwa kumpa hata buku 5 maisha magumu leo umekomalia kupeleka hela TRA zikafanyiwe ufisadi.

Sina haja ya kufafanua ila nadhani ulitakiwa kusoma vizuri mada na sio kukurupuka na kuleta hoja za lumumba
 
kwa biashara ya kawaida mauzo ya 38,000 sio mapato. These are sales not gross revenues. Mtu aliyeuza 38,000 amenunua hiyo bidhaa ili aiuze. kwa mahesabu ya kuinunua kwa kuiuza kwa faida ya asilimia 10, basi huyu bwana amenunua mzigo kwa dealer/distributor/wholesaler kwa 34,000 yeye anauza 38,000. mapato ya huyu bwana kwa siku ni 4,000 tu!!
kama kweli hii ndio cutoff ya TRA waache hawa jamaa walalamike, mfanaybiashara mwenye mapato ya 4,000/= kwa siku bado ni mtu wa kipato cha chini sana. Kwa nini? hii 4,000 inaitwa gross revenue. kwa maana kuwa baadae ataondoa gharama za umeme/kodi za pango la eneo la biashara etc/ Net revenue ya huyu bwana haiwezi kuzidi 2,000 kwa siku.

Hii anarudi nayo nyumbani, huko sasa anakutana na matumizi ya kila siku ambayo hata mfanyakazi anakuwa nayo. na yeye anatakiwa anunue umeme nyumbani, anunue maji, anunue chakula, watoto waende shule.huyu mtu kama hajaiba basi atafilisika baada ya kipindi kifupi, kwani atakuwa anakula kamtaji kadogo alikonako bila yeye kujua.


Tukirudi kwa wafanyakazi wanaolalamia PAYE, naomba niseme kuwa hii wanayokatwa wao mwisho wasiku wanapewa NET PAY. hii wanarudi nayo nyumbani.wakiwa makazini kwao, hawalipi kodi ya ofisini, hawalipii umeme ofisini, hawalipii hata hela ya mlinzi. Mapato ya mfanyakazi anayepata net pay ya 180,000 kwa mwezi ni zaidi ya mapato ya mfanya biashar aanayeuza 14M kwa mwaka. Hili liko wazi kwa yeyote ambaye hesabu hazimpigi chenga.kwani Mfanyabiashara kabla hajaenda nyumbani ana net income ya 2,000. mfanyakazi ana net income ya 6,000. ni zaidi ya mara tatu.
na wanaosema laki 600,000 kwa mwaka ni pesa kidogo, kun amtu yoyote anayelipwa 180,000 anayetumia laki 6 kununua kitu asichokihitaji na kisichomuongezea kipato chake kwa namna yoyote?

Serikali iongeze cuttoff point ya hayo mapato ya mwaka. Serikali ibuni njia mpya za kukusanya mapato. tumewasema wanategemea sigara na pombe basi wameona wahamie kwenye kukusanya kodi za watu ambao kodi zenyewe hazikusanyiki.tunarudi kulekule kwenye mambo ya kodi ya kichwa. wagawe hizo machine bure, wawaelimishe wafanyabiashara, kama zinafaida kwao, nina uhakika watazichukua.

TRA wanaona wafanyabiashara ni wezi kwa kuwa wao ni majambazi nambari wani, hivyo si ajabu.bahati mbaya hii mbinu yao haitaongeza mapato.waiobereshe.
Kimweri,
ume-challenge ili mradi tu u-challenge au unaamini ulikuwa na base za ku-challenge? What do you mean unaposema mfanyakazi mwenye salary ya TSh. 180K hiyo ni net salary? Unless kama unataka kuniambia hujawahi kuajiriwa maishani mwako otherwise think twice. Na hata kama hujawahi kuajiriwa, tafuta salary slip(S.L) ya yeyote kisha iangalie. Juu kabisa ya S.L panaandikwa Basic Salary...ndiyo hiyo 180K. Chini yake wana-list non-taxed income ambayo ni 10-15%. Normally hii ni kwa ajili ya NSSF na wenzake. Wakishakata hiyo 10-15% from 180K, kinachobaki ni taxed income kwa ajili ya PAYE. Kinachobaki ndiyo Net Salary mfanyakazi anayoenda nayo nyumbani! So how come unasema kwamba hiyo 180K ni net pay? Ningekuelewa endapo ungesema KCC sio 180K otherwise ulichosema ni completely FALSE.

Hiyo hoja ya 38K kwa siku nimeshasema sana hapa! Tusijitie upofu na kujifanya hamnazo...narudia, tusijitie upofu na kujifanya hamnazo ili mradi tuweze kupinga kwavile ndicho tunachopenda kufanya! Wale wanaogoma pale Kariakoo si kweli hata kidogo kwamba ndio wanaofanya mauzo ya sh. 38,000/- kwa siku. Sh.38,000/- ni mchele 10kg@1500+maharage 10kg/2000+unga 15kg@1000=50,000/-....yaani tayari kuna excess ya sh. 12K. Maduka kama hayo yapo mitaa ya ndani ndani huku uswahilini ambayo in most cases yana sifa zifuatazo....mteja anasimama dirishani huku akigonga nondo kwa sarafu kwavile muuzaji yupo chumbani; haya ni yale maduka yanayouza mafuta ya taa na ya kula ya mia mia; haya ni yale yanayouza majani kwa sh.50/-, haya ni yale maduka ambayo wanakuwa na vidaftari vya kuandika waliochukua sukari robo kilo na kuahidi watalipa next time...in most cases, maduka haya ni yale yanayohudumia wakazi ambao wapo within 100m radius. Tuwe wakweli, hata kama TRA wamesema ni kwa ajili ya wafanyabiashara wenye annual sales ya TSh. 14m; hawa wengi wao hawajaguswa...
 
Last edited by a moderator:
TRA ingetoa hizo mashine za EFD bure ili kukata mzizi wa fitna na unafiki wa wafanya biashara..
Mkuu wangu, umesema jambo sahihi kabisa...ili kutoa mzizi wa fitina wapewe bure though am certain bado watakataa coz' base ya madai yao haipo kwenye bei bali ni kwamba hawataki tu hizi mashine kv wanafahamu udanganyifu wao utakuwa unaelekea mwisho.
 
Mtoa mada yupo sahihi, nimeshawahi kufanya biashara fulani kwa mtaji wa laki4 lakini kwasiku nikawa nauza mwastani wa elfu 40, lakini ukifika mwisho wa mwezi nikipiga mahesabu yangu najikuta faida niliyobaki nayo ni kama Tsh 36,000/=. Japo sizielewi terminology za uchumi mtoa mada anazosema ila yupo sahihi.
 
Kinachotusumbua watz ni kitu ki1. Wengi wetu tuna uelewa mdogo sana kiasi kwamba chochote tunachoambiwa tunakubali tu hata kama kinatuumiza. Yani tumekuwa kama watu ambao tumechukuliwa msukule, hatu-reason, tunapelekwa pelekwa tu kama upepo. Kwa ujumla TRA ambayo ndiyo serikali wanawaibia wananchi kwani kodi wanazotoza haziendani na kipato halisi cha yule anayetozwa. Kodi tunalipa huduma za afya, elimu hovyo, rasilimali za nchi kibao watu masikini wa kutupwa 33.6%(extremely poor), matumizi mabaya ya fedha za umma mfano kuna vigezo gani kumlipa mbunge wa bunge la katiba 700,000/= kwa siku huku wagonjwa pale muhimbili wodi za majeruhi wanalazwa chini na huku wengi wakikosa matibabu?

Wanachotaka kukifanya kwa wafanyabiashara walishaanza kukifanya kwa wafanyakazi. Kuna makato mengi sana yasiyoelezeka. Swali ni kwamba; fedha hizi zote zinaenda wapi? bajeti yenyewe asilimia zaidi ya 50 ni wahisani, miradi mingi sana ya maendeleo ni wahisani(wafadhili), PESA zetu zinaenda wapi. Unyonyaji mtupu TZ.

Bado kuna pesa nyingi tu zinazofisidiwa waziwazi na wahusika hawachukuliwi hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kutaifishiwa mali zao kufidia wizi na hujuma wanzofanya. Wizi kuanzia juu mpaka chini. The country will remain extremly poor for ever and ever, na wananchi tusitegemee miujiza yoyote ile unless people decide to bring changes kwa gharama yoyote ile.

Nilishangaa sana kuona TANGA nao wakigoma kufungua maduka. Kumbe nao uvumilivu umewashinda.
 
on the other hand nawahurumia wafanyabiashara, kwani wanawatetea watu wasiohitaji utetezi. wanachotakiwa kufanya ni kuongeza bei kwa asilimia 18 kwa kila bidhaa wanayouza,ili hao mabwana kodi waendelee kuchukua 18% bila kuathiri faida.
Mkuu wangu inaonesha wazi kwamba hii mada umeikurupukia bila kufanya utafiti hata kidogo!! Hiyo 18% uliyoisema ni VAT wakati hawa wafanyabiashara wanaogoma sasa wala hawahusiki na hiyo VAT ingawaje kuna watu wanapotosha na kuwaambia kuna VAT wakati si kweli!! Hao wa 18% wameanza kutumia hizi mashine since 2010 na wala hawakugoma; na hadi leo wanazitumia ingawaje kuna wengine wanafanya ujanja wa hapa na pale ambao kwa kiasi kikubwa unatokana na Watanzania wenyewe kutojali masuala ya kuchukua risiti!! Hawa wa sasa wanachokatwa ni income tax na wal sio Value Added Tax uliyoisema.
 
Tatizo nilionalo ni bei ya EFD na hiyo ya kuchukua 18% ya mauzo. Kama wangesema wanachukua 18% ya faida sawa lkn ya mauzo wamekula hadi mtaji wangu.

Mfano kg 1 ya mchele kwa sasa ni 1,000 kwa bei ya jumla. Ukienda kuuza dukani bei ni 1,200. Halafu anakuja mtu wa EFD anachukua 18% ya mauzo ya 1200 sawa na 216/- ukifanya hesabu ya kutoa 1200-216#984. Hapo hujalipa kodi ya chumba, hujala, hujalipa umeme na maji.

Pamoja na kwamba kodi hizo hazichukuliwi, ukifanya utafiti utabaini kuwa kila baada ya mwaka mmoja mfanyabiashara anaachia chumba sawa na kufilisika kwani anashindwa kulipa pango la chumba. Kinachosababisha watu wasione haya, ni kile kitendo cha anatoka mmoja, anaingia mwingine. Na huyu aliyeingia hajisumbui kuuliza kwa nn mwenzake katoka, kwa kuwa anamtaji tayar na pesa ya kulipa pango anayo mkononi, analipa na kuanza biashara. Mkataba ukiisha anajijuta hajakusanya pesa ya kulipa kodi ya chumba hivyo anaamua kuhama. Kila mwaka kuhama hadi mtaji wote kwisha.

Kwahiyo ili hizo EFD zifanye kazi yafuatayo yafanyiwe kazi:-
1. Wapange kuchukua 18% ya faida na si mauzo ya siku.
2. Mashine bei ipungue kwani baada ya muda ni kukusanya faida tu.
3. Kodi za vyumba vya biashara zizibitiwe. Lisiachwe mikononi mwa mwenye nyumba tu, serikali ipange kiwango cha kodi hizo na wasimamie.

La sivyo tutarajie kuona kila siku kuibuka kwa wajasiria mali halafu baada ya mwaka wanapotea wanakuja wengine
Mkuu ntamaholo,
Ni kwamba bado hufahamu suala zima la hizi mashine...ni bahati mbaya sana watu wenye malengo wanayofahamu hao wamekazana kupotosha na Watanzania kwavile hatupendi kutafuta ukweli; tumeumeza upotoshaji huo kama ulivyo. Unaposema TRA wanachukua 18% maana yake ni kwamba hawa wafanyabiashara wanatakiwa kulipa VAT ndiyo hiyo 18%. Be informed that, hiyo si kweli...hawa wafanyabiashara wa sasa wala sio VAT Registered. Waliosajiliwa na VAT wameanza kutumia hizi mashine since 2010 na wala hawakugoma. Hawa wa sasa wanachotakiwa ni kulipa Income Tax kama ile inayolipwa na wafanyakazi na wala sio VAT.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu, umesema jambo sahihi kabisa...ili kutoa mzizi wa fitina wapewe bure though am certain bado watakataa coz' base ya madai yao haipo kwenye bei bali ni kwamba hawataki tu hizi mashine kv wanafahamu udanganyifu wao utakuwa unaelekea]


Tatizo kubwa na la msing hapa ni zaidi ya Machine za EFD ni mfumo mzima wa kodi... Wafanyabiashara wana madai zaidi ya machine za EFD ambazo kwa sababu za makusudi serikali chini ya TRA ndio inachokishililia.. IKUMBUKWE Wafanyabiashara hawa ni walipa kodi wazuri wa kodi zao walizokuwa wanakadiliwa.


Madai ya wafanya biashara ni haya..


  1. Kwanza ni BEI ya machine ulikinganisha na BEI ya soko ya machine husika kwa soko la sehemu nyingine duniani.. kenya tu mashine zinapatikana kwa chininya TZS 350,000. ukienda china na kwingineko ni chini ya $80.
  2. Gharama kubwa na usumbufu unaotokana na machine hizo ukilinganisha na cash flow za mlengwa yaani mfanyabiashara anayeingiza 38,000 Kwa siku... Gharama za karatasi moja ni 6000 na gharama za maintenance ambazo ni zaidi ya laki 3 kwa mwaka na usumbufu wa kuripoti TRA NA KWA WAKALA kila machine inapoaharibika...
  3. Utaratibu wa faini kwa amabaye atashindwa kutumia machine hizo unatoa mwanya kwa wafanayakazi wasio waaminifu wa TRA( ambao ni wengi) na Askari waliozoea Rushwa kuleta taabu kwa wafanyabiashara.
  4. Machine za EFD hazionyeshi gharama za manunuzi na gharama za uwendeshaji ambapo hapo hasa ndio penye tatizo kubwa... Gharama nyingi za manaunuzi ama hazina risiti ama zina risiti ambazo hazilingani na gharama halisi... HILI LITAPELEKEA mfanyabiashara kutozwa kodi kubwa kuliko hanavyostahili kutokana na kukosekana na kumbukumbu za manunuzi.
  5. Mfumo mzima wa biashara ama zimetoka nje ya nchi ambazo ulipiwa kodi custom.. kodi ya import duty and VAT...Au zimenunuliwa kwa wakulima na wavuvi ama wafugaji ambao hawatoi risiti...Kwa zinazopita Customs ukadiliaji umekuwa shida kubwa... mzigo huo huo amabo haupishani hata miezi mitatu unaweza kuwa na kodi tofauti na tena yenye tofauti ya kutisha ... hii imeleta mianya ya rushwa kwa watumishi wa TRA na kupelekea wafanyabiashara kulipa malipo mengi yasiokuwa na risiti... amabayo yatakuja kumfanya alipe malipo mengi ya kodi ya mapato.
  6. Kodi zinazotozwa na TRA Customs hazinlingani na thamani halisi ya bidhaa zinazoingizwa na kushawishi wafanaya biashara kukubali kutoa rushwa ili angalau aweze kuuza bidhaa yake kwa gharama nafuu.
  7. kwa mazao yanaotka kwa wakulima mengi hayana risiti na kwa stahili hii mfanyabiashara atalazimaika kulipa zaidi kodi za mapato.
  8. Kwa ujumla mfumo mzima wa kodi unatakiwa kuangaliwa upwa ili uwe wazi na unaoshawishi wafanyabiashara kulipa kodi stahiki na kupunguza mianya ya Rushwa .... GHARAMA Nyingi za uendeshaji hazina risiti na hili ni tatizo la kuangalia ..
  9. Mfumo hauruhusu uingizaji wa mzigo wa pamoja ( sharing importation) ambapo kila mfanyabiashara aliyeshare container atalipa stahiki yake na mzigo wake kuwa na thamanai ya manaunuzi...
  10. kwa ujumla kufanya baishara Tanzania hasa kwa sekta zisizo rasmi zimekabiliwa na kodi nyingi zisizo na kichwa wa miguu... kodi za pango... kodi ya takataka.. kodi za fire... kodi za mabango... kodi za hamashauri... nk nk...


Tubadilike nchi ni yetu sote... sekta hii nayo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa... iundwe tume maalumu ya kurekebisha mfumo mzima wa ulipaji kodi na kuwaka fair ness kwa pande zote.... na kusitisha zoezi la EFD

Muonamambo

A town
 
ukitaka kumtawala mtu kirahisi mnyime elimu,mwenye elimu mnyime kazi,hapobutakuwa umefanikiwa ccm oyeeeeeee!!!
 
Acha kuongea kama unamatatizo ya akili, raia yoyote kwa kuishi tu lazima unalipa kodi kwa namna moja au nyingine, bado wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo nyie si mliwaambia waache kutegemea kuajiriwa ila wajiajiri wenyewe na sasa kumbe mnataka kuendelea kuwatoza kodi ili muendelee kutumia ma V8 na kuishi maisha ya luxury. kwanza hii serikali imekosa uhalali wakukusanya kodi. Kwa sababu haiwezekani wao waendelee kuneemeka na kodi za walalahoi huku kwenye huduma za msingi kuna mapungufu kibao na ubadhirifu ndio usiseme.

tatizo wafanyabiashara wengi hawana mazoea ya kulipa kodi na wamezoea kuwaibia wateja kwa ajili ya kutengezeza milima ya faida...jamani lipeni kwani mnategemeaje Tz kuwa kwenye nchi zilizoendelea bila ya kumpa kaisari cha kwake
 
Tatizo kubwa na la msing hapa ni zaidi ya Machine za EFD ni mfumo mzima wa kodi... Wafanyabiashara wana madai zaidi ya machine za EFD ambazo kwa sababu za makusudi serikali chini ya TRA ndio inachokishililia.. IKUMBUKWE Wafanyabiashara hawa ni walipa kodi wazuri wa kodi zao walizokuwa wanakadiliwa.

Madai ya wafanya biashara ni haya..


  1. Kwanza ni BEI ya machine ulikinganisha na BEI ya soko ya machine husika kwa soko la sehemu nyingine duniani.. kenya tu mashine zinapatikana kwa chininya TZS 350,000. ukienda china na kwingineko ni chini ya $80.
  1. Tatizo watu mnachanganya mambo...badala ya kunitajia hiyo bei, ulitakiwa kwanza unitajie aina ya mashine wanazotumia! Unless wawe wame-change siku za karibuni otherwise hiyo be unayosema wewe ni ya ETR ambazo hazifanyo remote transmission na badala yake data zinakuwa stored kwenye fiscal memory. Wakati Kenyan ETR hazifanyi remote transmission, hizi zilizokuwa approved na TRA zinafanya remote data transmission automatically to TRA. Kwa upande mwingine, ukija hilo la $ 80 hapa ndo wala haliingii kabisa coz' this's not all about having EFD but EFD ambazo moja kwa moja zita-communicate ni TRA. Sasa hizo za $ 80 ni just for general use. Huwezi hiyo ya $ 80 leo hii ukainunua, kisha zika-transmit data to TRA. Ukitaka kufahamu vizuri hizi mashine, unatakiwa kuchukua mfano wa calculator. IKiwa umesoma sayansi hususani zama hizi, bila shaka umeshaitumia sana Scientific Calculator! Nadhani unafahamu, wakati unanunua hizi calculator isn't all about scientific calculator...ingawaje zote ni scientific lakini bei zinatofautiana kutegemeana na functions na mambo mengine kama hayo...lakini zote ni scientific calculators!

Gharama kubwa na usumbufu unaotokana na machine hizo ukilinganisha na cash flow za mlengwa yaani mfanyabiashara anayeingiza 38,000 Kwa siku... Gharama za karatasi moja ni 6000 na gharama za maintenance ambazo ni zaidi ya laki 3 kwa mwaka na usumbufu wa kuripoti TRA NA KWA WAKALA kila machine inapoaharibika...
hili la sh.38,000/- nishalisema sana hadi linatia uvivu! Kwa hayo mengine wala sidhani kama yana msingi. IKiwa unataka kuuza nafaka lazima utanunua mizani; mbona hamgomi na kulazimisha kupima kwa makopo/pishi kama zamani? Hizo mizani zikiharibika hamsumbuki kumtafuta fundi? Ikiwa una baa, mnaweka viti na meza...kwanini msiweke mabenchi kama kwenye pombe za kienyeji? Kwanini nongwa iwe kwenye EFDs peke yake? Hakuna biashara isiyo na gharama ambayo burden moja kwa moja inaenda kwa mfanyabiashara!
Utaratibu wa faini kwa amabaye atashindwa kutumia machine hizo unatoa mwanya kwa wafanayakazi wasio waaminifu wa TRA( ambao ni wengi) na Askari waliozoea Rushwa kuleta taabu kwa wafanyabiashara.
Ili hao wezi wasipate mwanya basi mnawajibu wote kutumia hizo mashine...mbona majibu unayo wewe mwenyewe!!
Machine za EFD hazionyeshi gharama za manunuzi na gharama za uwendeshaji ambapo hapo hasa ndio penye tatizo kubwa... Gharama nyingi za manaunuzi ama hazina risiti ama zina risiti ambazo hazilingani na gharama halisi... HILI LITAPELEKEA mfanyabiashara kutozwa kodi kubwa kuliko hanavyostahili kutokana na kukosekana na kumbukumbu za manunuzi.
Na ndio maana kuna kitu kinaitwa Cash Book! Mfanyabiashara smart, lazima atakuwa na cash book ikiwa anaona kuna mapungufu huko kwenye mashine.
Mfumo mzima wa biashara ama zimetoka nje ya nchi ambazo ulipiwa kodi custom.. kodi ya import duty and VAT...Au zimenunuliwa kwa wakulima na wavuvi ama wafugaji ambao hawatoi risiti...Kwa zinazopita Customs ukadiliaji umekuwa shida kubwa... mzigo huo huo amabo haupishani hata miezi mitatu unaweza kuwa na kodi tofauti na tena yenye tofauti ya kutisha ... hii imeleta mianya ya rushwa kwa watumishi wa TRA na kupelekea wafanyabiashara kulipa malipo mengi yasiokuwa na risiti... amabayo yatakuja kumfanya alipe malipo mengi ya kodi ya mapato.
Mara zote huwa mnajisahau kwamba mnapotoa tuhuma kwa watumishi wa TRA kwamba wanadai rushwa; mnaacha kusema kwamba nanyi ni watoa rushwa wakubwa! Mnaenda kwa watumishi wa TRA huku mmebeba sura za kirushwa rushwa tu na kuwa easily approachable coz' mtoa rushwa anajulikana tu hata anavyo-approach desk lako!! Kwa kila mfanyakazi mshenzi mmoja wa TRA mla rushwa, pembeni yake kuna at least mfanyabiashara mshenzi mmoja mtoa rushwa.
Kodi zinazotozwa na TRA Customs hazinlingani na thamani halisi ya bidhaa zinazoingizwa na kushawishi wafanaya biashara kukubali kutoa rushwa ili angalau aweze kuuza bidhaa yake kwa gharama nafuu.
No justification katika kutoa rushwa kama ambavyo no justification ya mshahara mdogo kwa muomba rushwa! By the way, any smart business person lazima aangalie tax regulation za biashara anayotarajia kuifanya. Kama unauza nguo na kukwaza na kodi, badili bishara na kuuza mbepejeo za kilimo zisizo na kodi..
kwa mazao yanaotka kwa wakulima mengi hayana risiti na kwa stahili hii mfanyabiashara atalazimaika kulipa zaidi kodi za mapato.
Yangekuwa na list ingekusaidia nini wakati TRA wanafanya mahesabu kwa kuangalia mauzo yako? Jambo la msingi ni wewe kuwa na cash book itakayokuwa na particular zote for your future use. Likewise, kama zamani ulikuwa unanunua mchele kwa sh.1000 na hulipi income tax na hivyo unauza hata kwa sh.1200; sasa unatakiwa kufahamu kwamba ukiuza utalipa income tax so, either huo mchele ununue chini ya sh.1000 au uuze zaidi ya 1,200/-. Msijifanye mnatuhurumia end users; kadanganyeni wengine.
Kwa ujumla mfumo mzima wa kodi unatakiwa kuangaliwa upwa ili uwe wazi na unaoshawishi wafanyabiashara kulipa kodi stahiki na kupunguza mianya ya Rushwa .... GHARAMA Nyingi za uendeshaji hazina risiti na hili ni tatizo la kuangalia...
Noted with thanks, i hope wahusika wamekusikia.
Mfumo hauruhusu uingizaji wa mzigo wa pamoja ( sharing importation) ambapo kila mfanyabiashara aliyeshare container atalipa stahiki yake na mzigo wake kuwa na thamanai ya manaunuzi...



  1. kwa ujumla kufanya baishara Tanzania hasa kwa sekta zisizo rasmi zimekabiliwa na kodi nyingi zisizo na kichwa wa miguu... kodi za pango... kodi ya takataka.. kodi za fire... kodi za mabango... kodi za hamashauri... nk nk...

Tubadilike nchi ni yetu sote... sekta hii nayo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa... iundwe tume maalumu ya kurekebisha mfumo mzima wa ulipaji kodi na kuwaka fair ness kwa pande zote.... na kusitisha zoezi la EFD

Muonamambo

A town
Ni matumaini yangu kwamba haya hayana uhusiano na EFDs; sana sana yanawakilisha ile simulizi ya Mbwa Mwitu na Mwana Kondoo! Mbwa Mwitu kamjia juu Mwana Kondoo kwamba kwanini anachafua maji wakati anamuona yeye (mbwa mwitu) anakunywa maji! Mbwa Mwitu alitoa madai haya wakati yeye amekaa upande wa juu wa mto na Mwana Kondoo yupo kwa chini. Mwanakondoo akajibu, nayachafua vp wakati mimi nipo upande wa bondeni na wewe kwenye mwinuko? Mbwa Mwitu akakaza, "usibishe wewe, ilikuwa mwaka juzi ile!!! Mwana Kondoo akajibu, mbona mie nimezaliwa mwaka huu?! Mbwa Mwitu kv shida yake ilikuwa ni kitoeo; akaja na lingine...kama hukuwa wewe basi baba ako, kama si baba ako basi mama ako; kama c mama ako basi kaka ako, kama si......ili mradi tu Mmbwa Mwitu apate kitoweo! Mbwa Mwitu ana visa!
 
Acha kuongea kama unamatatizo ya akili, raia yoyote kwa kuishi tu lazima unalipa kodi kwa namna moja au nyingine, bado wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo nyie si mliwaambia waache kutegemea kuajiriwa ila wajiajiri wenyewe na sasa kumbe mnataka kuendelea kuwatoza kodi ili muendelee kutumia ma V8 na kuishi maisha ya luxury. kwanza hii serikali imekosa uhalali wakukusanya kodi. Kwa sababu haiwezekani wao waendelee kuneemeka na kodi za walalahoi huku kwenye huduma za msingi kuna mapungufu kibao na ubadhirifu ndio usiseme.
Kuna nchi za watu ambazo kodi ni asilimia 40 - 45 ya pato la mtu kwa mwezi, sasa kwetu sisi ambao ni chini ya 30 % kwa mfanyakazi na mfanya biashara mbona inakuwa vigumu kwa mtu kuelewa kwamba ni wajibu wake kulipa kodi. Ieleweke kwamba mfanyibiashara analipa kodi kutokana na faida - profits na sio mauzo - sales, ina maana baada ya kutoa gharama zote za huduma au bidhaa, sasa kwa wafanyibiashara wetu wengi nnaowajua shule zao ni za kuungaunga tu. Mwisho wa siku ilitakiwa tulalamike sisi kw vile ndio tunabeba mzigo wote, umeona wapi upendo wa mfanyibiashara kiasi cha kugoma kwa niaba ya mtumiaji, nashikilia pale pale kila mtu ana wajibu wa kuchangia maendeleo ya nch yake iwe kwa kodi au njia nyingine yeyote.
Tatizo naona kwa vile serikali yetu mara kwa mara imekuwa na sifa mbaya- kila kitu kinaonekana kwa mtindo huo wa kifisadi lakini mwenye akili timamu anatakiwa aweze kutenganisha, sasa sijui wewe utakua na akili timamu au pumba tu
 
mi ni mfanyakazi lakini nawasapoti wafanyabiashara.hata wakinunua hizo mashine bado mzigo ni kwetu sisi walaji.kama ujuavyo biashara za bongo ni maelewano.hatujafika hatua ya kuwa na fixed price.nguo ya elf 40 utainunua kwa 15000.just imagine wauza mitumba wa karume au mchikichini wawe na efds unategemea walalahoi tutavaa?.suruali ya ekf 10 utainunua kwa elf 25.ile ya dukani ya elf30 utainunua kwa 50.mshahara wenyewe laki 4 utaweza kuishi?usiwe na myopic minded.kabla ya kuropoka uwe unafikiria matokei ya kitu kwa mapana yake.sio tu ushabikie wafanyabiashara kulipa kodi bila kujua position yako itakuwaje kama mlaji katika mzunguko wa kibiashara.
kwa wafanyabiashara kulipa kodi ni sawa kabisa kakini kuwepo na utaratibu ambao hautaleta madhara kwaa end user.bei ya umeme imepanda maji nayo yamepanda kutoka50 kwa ndoo moja hadi 100 tsh.kwa uelewa wako mdogo hapo muathirika ni nani?unadhani ni tanesco au serikali?acha ushabiki usiokuwa na tija kijana
kama hujui kaka omba kujulishwa..
mfanyabiashara ya mitumba na EFD wapi na wapi????
mauzo ghafi na 14,000,000 zinapatikana wapi kwenye biashara ya mitumba??? nina wasiwasi wewe sio mfanyakazi, lakini ungekuwa ni mfanyakazi halafu uka jumlisha makato yako yooote ya kodi kwa mwaka then ukaenda kujilinganisha na mfanyabiashara anayelipa kiwango hichohicho cha kodi kwa mwaka!! then utaona tofauti ya kipato na kimaisha kati yako na mfanyabiashara. mfanyabiashara anayelipa kodi kwa kiwango ninacholipa mimi kwa mwaka ni tajiri mwenye mabilioni ya shilingi.
DAMN IT!!! after all, kodi za wafanyabishara hulipwa na wateja wao
 
Back
Top Bottom