Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 5,172
- 15,458
Jumatano, 01 Julai 2026
DAR ES SALAAM
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), inapenda kuujulisha Umma kuwa mnamo tarehe 1 Julai 2026, ada ya Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari (Port Infrustructure Development Fee -PID) itaanza kutekelezwa rasmi katika bandari zote za Bahari Kuu.
Ada ya Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari (PID) itatozwa kwa mizigo yote ya ndani itakayoingizwa kwa kupitia Bandari za bahari kuu, isipokuwa mizigo ya vimiminika (Liquid Bulk Cargo).
Aidha Ada hii imegawanywa katika makundi mawili kama ifuatavyo:-
a. Asilimia 4.5% ya kodi kwa mizigo yote ya ndani itakayoagizwa kwa kupitia Bandari za Bahari kuu.
b. Asilimia 1.5% kwa ajili ya malighafi ya viwandani pamoja na mizigo yote isiyotozwa Ushuru wa Forodha (Import Duty).
TPA inatoa shukrani kwa wadau wote kwa ushirikiano wao endelevu na inasisitiza kuwa utekelezaji wa Ada ya Uendelezaji wa Miundombinu ya Bandari (PID) unalenga kuimarisha miundombinu na kuongeza ufanisi wa huduma zinazotolewa katika Bandari za Bahari Kuu nchini.
TPA pia inapenda kusisitiza kuwa, taarifa rasmi zinazohusu utendaji wa bandari, takwimu za shughuli za bandari, changamoto, maboresho na mipango ya maendeleo hutolewa na TPA kupitia njia rasmi za mawasiliano ambazo ni pamoja na Kituo cha Huduma kwa Wateja kilichopo ghorofa ya 6 katika Jengo la Makao Makuu ya TPA (One Stop Centre).
Njia nyingine za mawasiliano ni pamoja na simu ya bure: 0800-110032, Barua pepe: customercare@ports.go.tz, Tovuti: www.ports.go.tz, Mitandao ya kijamii: Instagram, X (Twitter) na Facebook kwa jina @tpa_tz.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu,
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA)