Toa ushuhuda wowote ambao unadhani bila Mungu usingetoboa

Toa ushuhuda wowote ambao unadhani bila Mungu usingetoboa

Corona ya kwanza ile Kaliiii, daktari anamuogopa mgonjwa, ambulance iko silence , akipatikana mgonjwa tu. Uelekeo Mlonganzila.

Bila mkono wa MUNGU nisingetoboa ILINIPIGA hosp ya kwanza wamepima kila kitu HAKUNA ugonjwa , naulizwa je? Unajisikia kukereketa Kooni , nawajibu HAPANA kumbe hali hiyo NAISIKIA .Anapewa dawa narudi nyumbani hali ile ile.

Hosp nyingine hivyohivyo. Hali yangu vikawa tete!! Hakika NILIMUOMBA MUNGU, maombi ambayo NINA UHAKIKA MWENYEZI MUNGU MUWEZA WA YOTE, aliyasikia na WEMA NA FADHILI ZAKE ZIKANIFUATA.
Jamaa ile ya kwanza iliondoka na mama yangu 🥺🥺🥺🥺


Zab 125:1 SUV​

Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.
 
2012 nilikuwa naishi Mbagala naungaunga maisha feri
Huko nnapoishi sikuwa na chochote ni kwa mshkaji nilikuwa nachangia kodi na sometimes nakosa
Siku moja sikuwa na kitu niliishia kula mihogo ya mia tatu asubuhi na sikupata kula chochote tena mpaka usiku niliamua kurudi Mbagala
Lakini mfukoni nilikuwa na jero tu ilibidi kwenda Mbagala na kesho lazima nirudi feri

Nilitega dcm limejaa nikadandia nyuma ndiyo nikaenda Mbagala ili ile jero inifae kesho kurudi feri nauli ilikuwa ni mia tatu kipindi hicho
Nimefika home mshkaji yupo na shemeji mpya
Nikaishiwa pozi inatakiwa nitafute pa kulala huwa narudigi feri kulala kwenye miboti

Nikaskuti kama nusu saa hivi pale ikabidi niage nikaondoka nikapanda gari tena kurudi feri usiku huo
Nilipofika feri huwa sehemu nzuri ya kulala ni upande wa kigamboni nikawa naenda kwenye kivuko kuna namna ya kuingia pale bila kulipa lakini siku hizi sijajua pakoje

Magari yako foleni kusubiri kivuko kije natembea pembeni ya foleni nikaona hela imekunjwa kunjwa elfu 10
kama mita mbili tu mbele kuna mama alikuwa amesimama anaongea na jamaa aliyeko ndani ya gari
Nilivyookota hela aliona kuna kitu nimeokota lakini hakujua ni nini nilivyofika mbele ilikuwa ni elfu 25 nilimshukuru Mungu kwa kila namna siku hiyo na nlibaki na maswali sana kwa kilichotokea






Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Mungu hufanya njia pasipo na njia 😍😍🤣🤣🤣 barikiwa sana jamaa
 
Askofu GWAJIMA Huwa ni mtu wa tofaut sana.....

Ingia YouTube Kuna somo alifundisha jumapil ya hii wiki pata muda sikiliza......

KUSUDI LA KUCHAGUA LITASIMAMA

mwenyez MUNGU haangalii matendo yako mazuri au mabaya....yeye hum bariki amtakaye...
Mwenyez MUNGU hum hurumia amtakaye Kwa sabab amemchagua.....
Kuna watu Mungu amewabarik na hawajawai kupiga goti hata hawaja mwomba chochote.....

Watoto Esau na yakobo walishindana tumboni.....
Na MUNGU alimpenda Yakobo........
Kabla hata hawajazaliwa....Mungu alimchagua Yakobo tangu tumboni hajazaliwa... kusema Mungu alimchukia Esau...ina maana Mungu ana upendeleo...Hasha......
Sio Kwa mazuri au mabaya Mwenyezi MUNGU humchagua amtakae Ili kusudi la MUNGU litimie...

Unaweza kusoma mpk PhD na usiweze kumilik hata bajaji.... Mwingine hakusoma Wala nini akawa na maisha Bora kabisa kuliko wewe...
Una weza kua na akili nyingi za darasani lakini sio Kwa kutenda mazuri au mabaya Mwenyezi Mungu humchagua amtakaye...

KUSUDI LA MUNGU KUCHAGUA LITASIMAMA

Yer 1:5 SUV​

Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

========

Nalikuchagua kabla sijakuumba
 
mwaka wa 8 huu sina ajira.. kujiajiri nako imekua kimbembe!

ila nipo!

nina Afya njema nazidi kupambana!

naamini bila Mungu nisingekua hivi
Wakati wa Mungu utakufikia soon, keep believing
 
Askofu GWAJIMA Huwa ni mtu wa tofaut sana.....

Ingia YouTube Kuna somo alifundisha jumapil ya hii wiki pata muda sikiliza......

KUSUDI LA KUCHAGUA LITASIMAMA

mwenyez MUNGU haangalii matendo yako mazuri au mabaya....yeye hum bariki amtakaye...
Mwenyez MUNGU hum hurumia amtakaye Kwa sabab amemchagua.....
Kuna watu Mungu amewabarik na hawajawai kupiga goti hata hawaja mwomba chochote.....

Watoto Esau na yakobo walishindana tumboni.....
Na MUNGU alimpenda Yakobo........
Kabla hata hawajazaliwa....Mungu alimchagua Yakobo tangu tumboni hajazaliwa... kusema Mungu alimchukia Esau...ina maana Mungu ana upendeleo...Hasha......
Sio Kwa mazuri au mabaya Mwenyezi MUNGU humchagua amtakae Ili kusudi la MUNGU litimie...

Unaweza kusoma mpk PhD na usiweze kumilik hata bajaji.... Mwingine hakusoma Wala nini akawa na maisha Bora kabisa kuliko wewe...
Una weza kua na akili nyingi za darasani lakini sio Kwa kutenda mazuri au mabaya Mwenyezi Mungu humchagua amtakaye...

KUSUDI LA MUNGU KUCHAGUA LITASIMAMA
Tuseme Amen ,Sometimes inashangaza sana kuna wakati unamuasi sana Mungu kusali kwa tabu lakini inashangaza pale ambapo unapiga goti na kumuomba unashangaa boom umekipata .

Wakati nasoma nakumbuka nlikua mkorofi sema nikienda kanisani naomba kweli basi Mungu aliamua kunidhirihishia miujiza yake kipindi kile unakuta umelala unaota mitihani kesho ukiingia unakuta ni ileile ulioiota au unakuta bado dakika 5 lakini kuna roho inakulazimisha ufungue ukurasa usome na kweli ukiingia unaukuta

Miujiza yake Aisee ni Mingi yani wakati mwengine unapata tatizo lakini ghafla anatokea mtu ambaye hutegemei anakuja kukusaidia
 
Akika ayo yote aliyonitendea Mungu ni mfano wa punje ya haradali hii pumzi nayo jidai nayo inatosha kabisa kuwa ushuhuda kamili bila ya kuniuliza juu ya ushuhuda wa Mungu kwangu na kwa wengine
 
Mungu hakuna alilowahi kunisaidia, kikubwa anakula pesa zangu kila siku,

Mimi ndo namsaidia maana nampa pesa.

Nilikuwa na shida akanitupa halafu saivi eti nimtolee, kweli?

Kila nilichonacho nimekipata kwa jasho langu.

Kwanza hayupo na kama yupo hana nguvu yoyote, kiufupi mimi namzidi uwezo.
Watakupinga na kukubeza but i think I UNDERSTAND this feeling you express here...
Sisemi nakuunga mkono ila NIMEKUELEWA SITUATION YAKO and i dont judge you at all.

Wengi ni wanafik wakikuponda hapa au pengine Mungu KAWAPENDELEA SANAA but guys kuna watu wana mateso sana na kuna wakat tunateseka sana..Anyway Mungu sijui huwa anakua wapi.

Namuamini Mungu ila kuna wakat NAPATA MASHAKA MAKUBWA SANA
 
Amani ya Bwana iwe juu yenu.

Leo twende na confessions ya yale unahisi bila Mungu au Allah usingekuwa hapo ulipo.

Leo sianzi mimi

Twenden kazi watoto wa Mungu/Allah uwanja ni wenu hebu shuhudia matendo makuu ya Mungu/Mola

Zaburi 71:16 BHN

Nitataja matendo yako makuu, ee Bwana Mwenyezi-Mungu; nitatangaza kuwa ndiwe mwadilifu peke yako.

Zaburi 23:1-6 SRUV​

BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Ilikua mwaka jana kwa mambo haya ya ulevi cku hiyo nilizima watu wakaja niokota nilikaa ICU wiki moja nilikuwa sitambui chochote.Mama mkwe na wife walikua bega kwa bega nami mpaka nikapata nafuu namshukuru Allah maana ningeweza poteza maisha mwenyez mungu naomba umpe maisha marefu mama mkwe nampenda sana alinipigania mpaka nikawa sawa
 
Ilikua mwaka jana kwa mambo haya ya ulevi cku hiyo nilizima watu wakaja niokota nilikaa ICU wiki moja nilikuwa sitambui chochote.Mama mkwe na wife walikua bega kwa bega nami mpaka nikapata nafuu namshukuru Allah maana ningeweza poteza maisha mwenyez mungu naomba umpe maisha marefu mama mkwe nampenda sana alinipigania mpaka nikawa sawa
Ashukuriwe Allah kwa kukuokoa na mauti🙏🏻🙏🏻🙏🏻
 
Pole sana ndugu.
Asante mkuu, she went in a week hapo Mloganzira it was February 4th 2021 ila uzuri na uhakika na lipo.

I'm very sure of it👇🏻👇🏻👇🏻👇🏻

Ufu 14:13​

Ufu 14:13 SUV​

Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.
 
nipo nae mi huwa siachagi mke hata akiniwekea sumu nikipona naendelea nae mimi sipo kama mungu shetan kakosea kidogo kamfukuza mimi naangalia hadi mwisho kitakuwa nini, yaani mm ndio mwisho wa matatizo yote
Kwaio umemzidi Mungu 🤣🤣
 
Tuseme Amen ,Sometimes inashangaza sana kuna wakati unamuasi sana Mungu kusali kwa tabu lakini inashangaza pale ambapo unapiga goti na kumuomba unashangaa boom umekipata .

Wakati nasoma nakumbuka nlikua mkorofi sema nikienda kanisani naomba kweli basi Mungu aliamua kunidhirihishia miujiza yake kipindi kile unakuta umelala unaota mitihani kesho ukiingia unakuta ni ileile ulioiota au unakuta bado dakika 5 lakini kuna roho inakulazimisha ufungue ukurasa usome na kweli ukiingia unaukuta

Miujiza yake Aisee ni Mingi yani wakati mwengine unapata tatizo lakini ghafla anatokea mtu ambaye hutegemei anakuja kukusaidia
Sasa usifanye dhambi kizembe

Rum 6:1-7​

Rum 6:1-7 SUV​

Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.
 
Akika ayo yote aliyonitendea Mungu ni mfano wa punje ya haradali hii pumzi nayo jidai nayo inatosha kabisa kuwa ushuhuda kamili bila ya kuniuliza juu ya ushuhuda wa Mungu kwangu na kwa wengine
Mungu akupe miaka mingi tena uone wajukuu zako
 
Amani ya Bwana iwe juu yenu.

Leo twende na confessions ya yale unahisi bila Mungu au Allah usingekuwa hapo ulipo.

Leo sianzi mimi

Twenden kazi watoto wa Mungu/Allah uwanja ni wenu hebu shuhudia matendo makuu ya Mungu/Mola

Zaburi 71:16 BHN

Nitataja matendo yako makuu, ee Bwana Mwenyezi-Mungu; nitatangaza kuwa ndiwe mwadilifu peke yako.

Zaburi 23:1-6 SRUV​

BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.
Siku kama ya leo mwakani nitakuwepo tena ofisini kwangu kama ilivyo leo; ni ushuhuda ulio mbele kwa sababu nina agano na Mungu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom