Tido Mhando atemwa TBC

Tatizo sio ukabila bali ni asili:
Wachaga biashara - TRA& Banks
Wahaya Sheria - Advocates
Wakuria ngangari - Vyombo vya usalama
Wasukuma - maafisa ugani
Wagogo - NGOs
WABONDEI MDOMO- RADIO/TV

Wagogo NGOs....hahaaa

Kwa hiyo na Rutashubyanyuma ni lawyer?
 
greatthinkers
hivi hakuna watanzania wengine wanaoweza kutangaza?
Kwa nini tbc imejaa ukoo mmoja?

Tido kwangu ni kicheff cheff:a s-smoking:

Think.
acha wivu kama na wewe unataka kutangaza soma uaply ukiwa na vigezo utapata mind u hata rushwa ni vigezo bongo
 
Hoja iwe ni je hao akina mhando wanaweza kazi??? Kama hawawezi, tutajua kuwa ajira zao zilitolewa kwa upendeleo. Kama wanadunda kazi basi hakuna tatizo.

My friend kazi ya kutangaza tu na kuandika habari utashindwa? si kazi hiyo bana, look their CV kama hata mmoja wao kafika A-level, wote vilaza wa
Fm4 tena failure, nasema FM 4 failure labda TIDO labda, wanabebana si kujua kazi, period
 
Si anafuata mfano wa rais Mwizi kwani hamkuona wakati wa campaign, Rz1 , Mama JK, JK mwenyewe na vimburu vyote kutoka Chalinze au hamtaki? Ndio Tanzania yenye neema hiyo .... .....
 
Tatizo sio ukabila bali ni asili:
Wachaga biashara - TRA& Banks
Wahaya Sheria - Advocates
Wakuria ngangari - Vyombo vya usalama
Wasukuma - maafisa ugani
Wagogo - NGOs
WABONDEI MDOMO- RADIO/TV

Ongezea hapo:

Wapemba ==> Madaktari wa wanawake na watoto.
 
Kwa hiyo na Rutashubyanyuma ni lawyer?
Kama sivyo basi ni mtetezi wa haki na mwanaharakati kupitia taaluma yake e.g. IT kwikwikwi - just joking!

All in all WATU WASIHUKUMIWE KWA MAJINA AU MAKABILA AU DINI ZAO BALI UTENDAJI WAO!
 
Tukiwakuta ndugu au ukoo mmoja kwenye fani nyingine hatulalamiki! kosa ikiwa kwenye ajira hapo ndo utasikia mambo! Mbona kwenye soka hatujalalamika ukoo wa akina Manara, Kihwelu n.k. Hebu tuwaache wachape kazi! Inawezekana ukoo wao walipomwona ndugu yao Tido anafanya vizuri na wengine wakavutiwa wakaamua kusomea taaluma ya utangazaji au haujui kama utangazaji unasomewa?

Wabondei wangu hebu chapeni mzigo hata kama mnatoka familia moja nani anajali? CV zenu ziliruhusu kuajiriwa TBC bwana!

Mkuu hivi hujui kwamba kuna kitu kinaitwa nepotism katika ajira!!!

Tiba
 
Nimesoma kwa masikitiko katika gazeti la Mwananchi la leo kuwa Tido Mhando hataendelea kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC baada ya mkataba wake kuisha tarehe 15 Desemba 2010.

Tido mwenyewe anakili kuwa mkataba umeisha, lakini hakuridhika na jinsi ujumbe ulivyoletwa kwake.

Watu wengi, wakiwemo wafanyakazi wa TBC, wanalihusisha tukio hili na ushujaa wa Tido kuhakikisha TBC haina upendeleo kwa vyama vyote vya upinzani wakati wa uchaguzi mkuu ulioisha 31 Oktoba 2010.

Kama CCM, nikiwa na maana serikali yake, imefanya hivi, basi anguko lake ni baya. Ni yale ya mfa maji asivyoacha kutapatapa.

Tuliombee taifa letu amani.

Pole Tido, Mungu atakuilipa.
 
hapa kuna neno, eti wanadai ameipendelea chadema,chadema gani, wakati alikuwa anabase ccm
 
Gazeti la Mtanzania limesheheni habari hii ya kuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa TBC ameangushiwa shoka la JK na kutupwa nje kutokana na kulaumiwa na CCM kwa kile kinachodaiwa kuisaidia Chadema kwenye chaguzi hii iliyokwisha hivi karibuni.............


Mamlaka ya Raisi katika kuteua viongozi wa umma yanazidi kuwa na kero kwa sababu yanatumika vibaya.........kwa sababu Bunge halihusishwi katika kuyathibiti..................hii ni hoja nyingine ya kudai katiba mpya itakayopunguza mamlaka ya Raisi katika uteuzi wa watendaji serikalini kwa kuthibitiwa na Bunge.................


Nalo Mwananchi languruma................

Tido Mhando atemwa TBC Friday, 17 December 2010 06:34

Sadick Mtulya, Patricia Kimelemeta
BAADA ya kufanya kazi nzuri ya kuboresha matangazo na uendeshaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), serikali imeamua kuachana na mkurugenzi wa chombo hicho, Tido Mhando baada ya mkataba wake kuisha, lakini mtangazaji huyo maarufu ameielezea uamuzi huo kuwa kuwa ni wa utata.

Kuenguliwa kwake kumefanyika takriban miezi miwili baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu ambao TBC iliripoti kwa kina na bila kupendelea chama chochote na hivyo kujivunia sifa kemkem kutoka kwa watazamaji wa TBC1 na wasikilizaji wa redio hiyo ya umma.

"Hatua hii imenishtua kidogo na hata hivi ninapoongea na wewe wafanyakazi wengi wamepata mshtuko na wengine wanalia," alisema Tido alipoongea na Mwananchi jana. "Ni juzi (Jumatatu) ndio niliandikiwa barua na serikali ya kutakiwa kuondoka.... ilikuwa kinyume kabisa na uratatibu wa serikali.
"Barua ya kutakiwa kuondoka niliipata mara baada ya kukutana na kuzungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Michezo, Utamaduni na Vijana , Seti Kamwanda.''

Tido, ambaye kabla ya kujiunga na TBC alikuwa mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Habari la Uingereza (BBC), alisema kwa mujibu wa taratibu mfanyakazi anayemaliza mkataba wake anatakiwa kujulishwa suala hilo miezi sita kabla.
"Kimsingi (barua) hukumbusha kwamba mkataba unamalizika na kama serikali inakusudia kuuendeleza au la. Sasa hilo halikufanyika kwangu," alisema.
Kwa mujibu wa Tido, hatua hiyo inaweza kutafsiriwa tofauti na wananchi hasa ikizingatiwa kwamba imefikiwa miezi miwili tu tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu.
Wafanyakazi walipata taarifa ya kuondolewa kwa Mhando jana baada ya mkurugenzi huyo kubandika tangazo la kuwataarifu kuwa anaondoka na kwamba ametakiwa akabidhi ofisi kwa Joe Rugabaramu.

"Tangazo linasema kuwa amefanya kazi na sisi kwa miaka minne na sasa mktaba wake umeisha na kwamba ametakiwa akabidhi ofisi kwa Rugarabamu," alisema mmoja wa wafanyakazi wa TBC.
"Baadaye alitushukuru kwa ushirikiano wetu kazini na akatuambia tusubiri hadi hapo mkurugenzi mpya atakapotangazwa."
Mfanyakazi mwingine alisema kuwa walitarajia kuwa Mhando angetimuliwa mapema kabla ya uchaguzi kwa kuwa wanadai kuja kwake nchini kulitokana na uhusiano wake na kigogo mmoja wa CCM ambaye kwa sasa hayuko madarakani.
"Angetimuliwa hata kabla ya Desemba 15, lakini ikaonekana kuwa isingekuwa sahihi," alisema mfanyakazi huyo ambaye alieleza kuwa Mhando aliwasiliana pia kwa simu na mfanyakazi mmoja mmoja kumuelezea uamuzi huo wa serikali.
Habari za Tido kuondoka TBC zilianza kuvuma wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wakati iliposemekana kuwa alikuwa akipigana vijembe vya chinichini na vigogo wa CCM kutokana na vyombo hivyo vya umma kutangaza habari bila ya upendeleo.
Baadhi ya mambo yaliyoibua hisia kuwa mtendaji huyo wa shirika la umma angeondolewa ni msimamo wake wa kuendelea kurusha hewani kipindi cha "Jimbo kwa Jimbo" ambacho kilikutanisha wagombea ubunge wa vyama mbalimbali vya siasa kwenye mdahalo kuhusu maendeleo ya eneo lao.

Kipindi hicho kilichorushwa kwa wakati mmoja na vituo vya televisheni na redio kilianza kwa kushirikisha wagombea wote wa ubunge kwenye jimbo, lakini katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba akaandika waraka wa kuzuia wagombea wa CCM kushiriki kwenye mdahalo huo akidai kuwa chama hicho tawala kina njia zake za kufanya kampeni.
Pamoja na CCM kujitoa, TBC iliendelea kurusha vipindi hivyo hadi kumalizika kwa uchaguzi ambao uliisha kwa CCM kupoteza viti vingi Tanzania Bara, ikiwa ni mara ya kwanza tangu serikali iruhusu mfumo wa vyama vingi.

"Ilikuwa aondoke kabla kampeni hazijaanza ingawa mkataba wake ulikuwa umalizike Desemba 15. Lakini serikali ilikuwa inarekebisha mambo yake na kumtafuta mtu anayeweza kurithi nafasi yake," chanzo cha habari cha ndani serikalini kilidokeza.
Chanzo kingine alisema: "Kuna watu wanaajiriwa pale TBC ambao malipo yao yanayotokana na Saccos ya shirika hilo, kitu ambacho ni kinyume na taratibu za serikali zinazotaka mwajiriwa alipwe na Hazina."
Jitihada za gazeti hili kumpata katibu mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Seti Kamhanda hazikuzaa matunda.
Alipoulizwa endapo atakubali kurejee kwenye wadhifa huo ikitokea serikali ikamwita tena, Mhando alijibu: "Nitalazimika kuchukua muda zaidi kutafakari hilo kwa kina.

"Nitafanya maamuzi ya kazi ya kufanya kulingana na wakati utakavyokuwa, lakini itanichukua muda kidogo kutafakari hilo kwa kuwa nimefanya kazi mfululizo.'
Kuhusu utendaji wa shirika hilo, Tido alisema amefarijika kwa kiasi kikubwa na mafanikio ya kiutendaji yaliyofikiwa.
"Nilikuwa na mipango mikakati mingi ya kuendeleza shirika hili hususani kulifanya lijiendeshe kwa kujitegemea bila ya kuhitaji ruzuku serikalini," alisema na kuendelea:

"Lakini nimefarijika vya kutosha na utendaji wangu na mafanikio yaliyofikiwa na TBC hadi wananchi kukiamini chombo hiki na ‘reaction' imekuwa nzuri kutoka kwao na kwa vyama vya siasa.''
Mbali na kurusha taarifa za kampeni katika njia iliyoonekana kuwa si ya upendeleo hata kwa chama tawala, TBC ilifanikiwa sana katika urushaji wa moja kwa moja wa matangazo ya mechi za mpira wa miguu na matukio makubwa ya kisiasa na kijamii.

Mechi za michuano mbalimbali ya kimataifa na ya ndani, urushaji wa matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge, urushaji wa moja kwa moja wa matukio makubwa na staili ya utangazaji ulilifanya shirika hilo kuwa na mvuto mpya na hivyo kuweza kupambana na vituo vingine vya redio na televisheni vya kampuni binafsi.
 
Jamani Tido ni kichwa kizuri sana kile kwenye ile fani yake,tunapoteza mtu potential,mi nafikiri kama kuna redio na TV zinazoweza kumlipa hapa bongo achukue kazi au kama vp afungue yake
 
Hii ni hatari kwa nchi yetu.Ukisha fanya kinyume na matakwa ya CCM hata kama ni haki unakuwa hatarini hii kazi kwelikweli. CCM sasa tumewachoka. MULO naye umemuundia zengwe na mimi naomba umniundie zengwe kwani nyie ni mizengwe tu.
 
Wandugu,
tusisitize mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni!. Hao Mhando's ni majina tuu. Tido angkuwa na nepotism, angemuajiri last born wa familia yake, Jane Mhando (RIP) ambaye alikuwa very competent kwenye broadcasting.
By the way, Tido anastaafu rasmi tarehe 31/12/2010. Hivyo kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma, sasa hivi lazima atakuwa likizo ya lazima na atakuwa tayari ameisha kabidhi ofisi kwa mtu wa chini yake akikaimu kusubiri mteuliwa mpya.
 
Tido nenda Tido, huna haja ya kutafakari what next kwani umeacha legacy itakayokujemgea heshima.
Big up Tido.
 
Sidhani kama Tido hukulijua hili, hata kama hukulijua awali lakini makala kadhaa ziliandikwa kuhusu kibarua chako. Anyway, bado cv yako ipo juu sidhani kama utakosa kazi hata ya uhariri wa vijarida vyetu uchwara hapa bongo
 
Jamani Tido ni kichwa kizuri sana kile kwenye ile fani yake,tunapoteza mtu potential,mi nafikiri kama kuna redio na TV zinazoweza kumlipa hapa bongo achukue kazi au kama vp afungue yake
Kweli Tido ni kichwa kama ni kweli alishawishiwa kurudi nchini enzi za "Boys II Men", then he is still safe, ABC inamsubiri.
 
Back
Top Bottom