Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Thomas Nkola maarufu kama Mkulima afungua kesi 5 ambazo zimesikilizwa jana tar 29/5/2023 katika mahakam ya hakimu Mkazi Kisutu, dhidi ya viongozi mbalimbali ikiwemo Mwigulu, Mkurugenzi PCCB, Mkurugenzi wa Mashtaka wa Serikali, Mkurugenzi wa Upelelezi Makosa ya Jinai, January Makamba, Makame Mbarawa, Justine Jutsine, Emmanuel Tutuba na wengine wengi ambao wamehusishwa na ubadhilifu wa fedha wa Tsh. Trilioni 8.4 kupitia ripoti ya CAG.
Wakili wa Mkulima amesema katika kesi 5 kati ya 7 ambazo zilifunguliwa na kusajiliwa, jana tar 29 ilikuwa kesi namba 17 mbele ya Mh. Mrio ambapo Mawakili wa Serikali wameomba wapatiwe nakala za maombi pamoja na viambatanisho walivyokuwa hawajapatiwa na kesi kuhairishwa mpaka tar 12/6/2023 saa 4 asubuhi.
Pia kuna kesi namba 13 ya 2023 mbele ya Mh. Mazengo vilevile wameomba Mahakama kupatiwa kupatiwa nakala za maombi na viambatanisho, ambapo Mahakama imeamuru waweze kupatiwa nakala hizo na kesi imehairishwa mpaka 4/6/2023 saa tatu asubuhi
Pia kesi namba 14 ya 2023 Mawakili wa Serikali wameomba baadhi ya wajibu maombi (respondent) kupatiwa nakala na viambatanisho walivyokuwa hawajapatiwa na hivyo kesi kuhairishwa mpaka 8/6/2023 saa 3 asubuhi.
Akisema kuwa mtanzania ana haki kumstaki mtu ikiwa ameona kuna mtu amefanya ubadhirifu au amesababisha harasa katika taifa, na ibara ya 27, 1 na 2 ya Katiba ya Tanzania inampa haki hiyo.
Mkulima kwa upande wake amsema kuwa hii siyo kwa ajili yake pekee bali ni kwa watanzania wote, yeye amekuwa muwakilishi tu, hivyo anahitaji kuungwa mkono na watu wengine sababu peke yake hatoweza.
Pia Mkulima akaongeza kuwa amefayanya hivyo kama hamasa sababu walifundishwa uzalendo toka wakiwa shuleni chini ya Mwl. Nyerere sababu mpaka sasa yeye bado ni mzalendo, na kuwaasa wazee wengine wawe wazalendo.
Mkulima awaomba pia walimu wafudishe uzalendo shuleni kwani mtu akikuona unafungua kesi kama alivyofanya anashangaa na kuhoji kama atawaweza waliofunguliwa kesi.
Pia soma:
Wakili wa Mkulima amesema katika kesi 5 kati ya 7 ambazo zilifunguliwa na kusajiliwa, jana tar 29 ilikuwa kesi namba 17 mbele ya Mh. Mrio ambapo Mawakili wa Serikali wameomba wapatiwe nakala za maombi pamoja na viambatanisho walivyokuwa hawajapatiwa na kesi kuhairishwa mpaka tar 12/6/2023 saa 4 asubuhi.
Pia kuna kesi namba 13 ya 2023 mbele ya Mh. Mazengo vilevile wameomba Mahakama kupatiwa kupatiwa nakala za maombi na viambatanisho, ambapo Mahakama imeamuru waweze kupatiwa nakala hizo na kesi imehairishwa mpaka 4/6/2023 saa tatu asubuhi
Pia kesi namba 14 ya 2023 Mawakili wa Serikali wameomba baadhi ya wajibu maombi (respondent) kupatiwa nakala na viambatanisho walivyokuwa hawajapatiwa na hivyo kesi kuhairishwa mpaka 8/6/2023 saa 3 asubuhi.
Akisema kuwa mtanzania ana haki kumstaki mtu ikiwa ameona kuna mtu amefanya ubadhirifu au amesababisha harasa katika taifa, na ibara ya 27, 1 na 2 ya Katiba ya Tanzania inampa haki hiyo.
Mkulima kwa upande wake amsema kuwa hii siyo kwa ajili yake pekee bali ni kwa watanzania wote, yeye amekuwa muwakilishi tu, hivyo anahitaji kuungwa mkono na watu wengine sababu peke yake hatoweza.
Pia Mkulima akaongeza kuwa amefayanya hivyo kama hamasa sababu walifundishwa uzalendo toka wakiwa shuleni chini ya Mwl. Nyerere sababu mpaka sasa yeye bado ni mzalendo, na kuwaasa wazee wengine wawe wazalendo.
Mkulima awaomba pia walimu wafudishe uzalendo shuleni kwani mtu akikuona unafungua kesi kama alivyofanya anashangaa na kuhoji kama atawaweza waliofunguliwa kesi.
Pia soma: