Serikali yaomba siku 14 kumjibu Mkulima aliyewashtaki Mawaziri
Na Grace Gurisha
SERIKALI imeiomba Mahakama ya Hakimu MkaziKisutu, Dar es Salaam, muda wa siku 14 kuwasilisha kiapo kinzani katika maombi yaliyofunguliwa na Thomas Nkola, maarufu kama Mkulima, ya kutaka kuwafungulia mashtaka vigogo wa serikali.
Vigogo hao ni Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba, Profesa Makame Mbarawa (Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi), mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mhandisi Rogatus Mativila, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Maombi hayo namba 16 ya mwaka 2023 yaliwasilishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Evodia Kyaruzi, kwa ajili ya kutajwa. Upande wa serikali ulidai kuna baadhi ya nyaraka hujazipata (hati ya wito), hivyo kuomba siku 14 kwa ajili ya kuwasilisha kiapo hicho.
Wakili wa Mkulima, Penina Ernest, alitoa hati mbili na kuukabidhi upande huo na kudai kuwa zingine atazipeleka ofisini. Hakimu Kyaruzi aliahirisha maombi hayo hadi Juni 6, mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama kiapo hicho kimewasilishwa mahakamani hapo.
Katika hati ya maombi hiyo, Mkulima anadai kuwa kwamujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) wakati akitekeleza majukumu yake Dk. Nchemba, Prof. Mbarawa na Mativila katika mwaka wa fedha 2021/2022, walisababishia serikali hasara ya sh 2,914,113,070,000 licha ya kupangiwa bajeti ya ujenzi wa barabara ambayo ni asilimia 99 ya kiasi kilichobaki ambacho kingetekelezwa kwa jumla na kwamba fedha hizo hazijulikani.
Mkulima anadai kuwa pamoja na tuhuma zote zilizoibuliwa na CAG katika ripoti yake ya mwaka 2021/22 kuonyesha hasara kubwa iliyoipata serikali ya Tanzania, walalamikiwa kuwa wanahusika huku Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai na Ofisi ya DPP zikiwa hazijachukua hatua zozote za kisheria dhidi ya viongozi hao kwa kuwahoji.
Pia hati hiyo inaeleza kuwa hata Bunge baada ya kupokea ripoti za CAG, Spika wa Bunge hajalitilia maanani kwa kuwa Bunge limepanga kujadili ripoti hiyo Novemba, mwaka huu hali ambayo jambo hilo litakuwa limepitwa na wakati na watu hao watakuwa wamepokea fedha zingine katika bajeti ya mwaka 2023/24 kwa mradi huo huo.
Chanzo: Gazeti la Nipashe Mei 25, 2023
Na Grace Gurisha
SERIKALI imeiomba Mahakama ya Hakimu MkaziKisutu, Dar es Salaam, muda wa siku 14 kuwasilisha kiapo kinzani katika maombi yaliyofunguliwa na Thomas Nkola, maarufu kama Mkulima, ya kutaka kuwafungulia mashtaka vigogo wa serikali.
Vigogo hao ni Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba, Profesa Makame Mbarawa (Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi), mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mhandisi Rogatus Mativila, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Maombi hayo namba 16 ya mwaka 2023 yaliwasilishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Evodia Kyaruzi, kwa ajili ya kutajwa. Upande wa serikali ulidai kuna baadhi ya nyaraka hujazipata (hati ya wito), hivyo kuomba siku 14 kwa ajili ya kuwasilisha kiapo hicho.
Wakili wa Mkulima, Penina Ernest, alitoa hati mbili na kuukabidhi upande huo na kudai kuwa zingine atazipeleka ofisini. Hakimu Kyaruzi aliahirisha maombi hayo hadi Juni 6, mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama kiapo hicho kimewasilishwa mahakamani hapo.
Katika hati ya maombi hiyo, Mkulima anadai kuwa kwamujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) wakati akitekeleza majukumu yake Dk. Nchemba, Prof. Mbarawa na Mativila katika mwaka wa fedha 2021/2022, walisababishia serikali hasara ya sh 2,914,113,070,000 licha ya kupangiwa bajeti ya ujenzi wa barabara ambayo ni asilimia 99 ya kiasi kilichobaki ambacho kingetekelezwa kwa jumla na kwamba fedha hizo hazijulikani.
Mkulima anadai kuwa pamoja na tuhuma zote zilizoibuliwa na CAG katika ripoti yake ya mwaka 2021/22 kuonyesha hasara kubwa iliyoipata serikali ya Tanzania, walalamikiwa kuwa wanahusika huku Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai na Ofisi ya DPP zikiwa hazijachukua hatua zozote za kisheria dhidi ya viongozi hao kwa kuwahoji.
Pia hati hiyo inaeleza kuwa hata Bunge baada ya kupokea ripoti za CAG, Spika wa Bunge hajalitilia maanani kwa kuwa Bunge limepanga kujadili ripoti hiyo Novemba, mwaka huu hali ambayo jambo hilo litakuwa limepitwa na wakati na watu hao watakuwa wamepokea fedha zingine katika bajeti ya mwaka 2023/24 kwa mradi huo huo.
Chanzo: Gazeti la Nipashe Mei 25, 2023