Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,278
- 10,378
mtu mwenye mawazo ya kibaguzi hangojei thread yoyote ile wala haitaji kushawishiwa. Kwa sababu racism na other forms of discrimination are irrational ndivyo ilivyo hata kwenye hili. Hivyo usishangae kuona watu wanaleta hisia za rangi n.k Wanaofanya hivyo ni wazi wanajionesha motivation yao ni nini.
Lakini kwa vile mtu ana rangi au kabila tofauti basi haina maana kuuliza Utanzania wake ni kujaribu kuuliza rangi yake. Rostam siyo Mtu wa kwanza mweeenye asili ya nje ya Afrika Tanzania. Wapo Watanzania wengi na waliofanikiwa (au kutofanikiwa sana) ambao uraia wao hauhojiwi kwa sababu watu wanawajua. Utaona watu kama kina Manji (hakuna mtu anayeleta maswali juu ya asili yao kwani watu wengi wanawajua); watu kama kina Bakhresa, Premji n.k
Hadii hivi sasa hakuna mtu ambaye ameweza kuweka hata historia fupi ya RA kabla ya 1994. Forget alizaliwa wapi (kwani kwenye uraia wetu hiyo ni irrerelevant, kwetu ni uraia wa wazazi na miaka ulizaliwa ndiyo inaingia). Mtu anaweza kuzaliwa Kigombero na asiwe Mtanzania na aliyezaliwa London akawa Mtanzania. Baba yake Rostam ni Muiran na hajawahi kuwa Mtanzania, Rostam amekuwa vipi Mtanzania?
Kuwa na passport haina maana mtu ni Mtanzania kwani Jenerali aliwahi kuwa na passport na akavuliwa Utanzania wake vile vile na kulazimishwa kuomba tena.
Tusiwatie hofu kwamba kwa kuhoji background ya RA tunataka kuleta mambo hate mongering n.k mtu anayetaka kuwa na hayo haitaji sababu.
Mkuu, with all due respects, I stand by my statement. Hakuna wakati katika ambapo tumehoji uraia wa mtu bila kuwa na nia ya kumbomoa au kumkomoa huyo mtu. Tumewadhalilisha wazalendo kama Jenerali Ulimwengu kwa misingi hiyo hiyo. Na ni hicho hicho kinachofanyika humu.
Kusema kuwa hakuna mtu aliyetokeza kuweka wazi historia ya Rostam ni kutupotosha. Hilo swali limeulizwa katika media ambapo ni sehemu ndogo mno ya watanzania wenye access nayo. Mpaka leo sijasikia mtu anaetoka katika jimbo la uchaguzi la Rostam ambae ameweza kusema wazi wazi kuwa Rostam hana mizizi katika jimbo hilo.Huyu jamaa hakuteuliwa kuwa mbunge, aligombea. Tena katika jimbo ambalo anadai alizaliwa. Unataka kuniambia kuwa hao wapinzani wake huko jimboni walishindwa kweli kuhoji uhalali wake? Hao walioshindana nao hawakuweza kweli kupata wazee wa kijiji ambao hawana kumbukumbu ya uzaliwa au kuwepo kwa Rostam nchini mpaka hivi karibuni? Walishindwa kuwapata watu ambao wangeweza kuthibitisha kuwa Rostam alikuja kumtembelea mjomba wake (kama ilivyodaiwa na baadhi yenu) ndipo akahamia! Hata sasa hivi, hao investigative journalists wa magazeti yetu wanashindwa nini kufuatilia katika mahospitali, shule, archives za mitihani ya shule ili kuonyesha kweli huyu jamaa ni imposter? Hamfanyi yote hayo badala yake mnatuuliza sisi, the privileged few, kama tunaweza kuthibitisha historia yake! Ignoring the fact kuwa wengi wetu hata kuipata hiyo Igunga kwenye ramani itakuwa ni shida. Unadai baba yake ni miran kwa hiyo hakuwa raia! Una maanisha kuwa baba yake hakuwahi kuja Tanzania? Kama alikuja Tanzania, alikuja lini humu nchini na sheria inasema nini kuhusu wale waliokuja nchini kabla ya uhuru? Again, unaleta insinuations bila kuzi-substantiate. Kwa kujua kuwa inawezekana kuwa Rostam kweli alizaliwa Tanzania basi unasogeza magoli kwa kuhoji uraia wa baba yake. Kitu gani kitafuata baada ya hapo? Uraia wa babu yake? Kwa mtazamo wako basi wale wote ambao ni dhahiri kuwa waliowatangulia walitoka nje ya Afrika watakuwa suspect. Kuanzia wakina marehemu Jamal hadi wakina Issa Shivji!
Kama nilvyosema hapo awali. Tunafanya hivi kwa ville ya chuki. Jenerali hakuvuliwa utanzania ati kwa sababu uzalendo wake ulitiliwa mashaka. La hasha. Alikosana na wakubwa na akafanyiwa hivyo kushikishwa adabu. Asingetumia haki yake ya kuhoji matendo ya waliomzidi angeendelea kupeta. Hao wakina Bakhresa, Manji, Premji, unaodai tunawajua, nani ana uhakika wa uraia wa wazazi wao?
Kama kweli tunataka kuhakikisha kuwa tunawakilishwa na watanzania tu basi tudai kuwa wabunge WOTE watueleze uzaliwa wao, wa baba zao na wa babu zao. Kwa kufanya tunavyofanya, ni dhahiri kuwa kinachotuongoza si uzalendo bali ni chuki na nia ya kutaka kumkomoa mhusika! Ndiyo maana kuna mtu/watu wanazungumzia kuwachoma moto wahindi wote na sote tunakaa kimya!
Kama vile alivyofanya Lee Atwater nanyi mnamtumia ( pengine bila kujua) huyu na wahindi wengine ( kwa wengi wetu Rostam ni mhindi) waliotajwa na Mengi kuthibitisha uhalali wa chuki zetu dhidi ya wahindi. Rostam anakuwa Willie Horton wenu.
Amandla........