This is Rostam I know... The Story Behind the Man

This is Rostam I know... The Story Behind the Man

I wish you all the best of luck Prince! Leave no stone unturned in exposing these fisads. We look forward to hearing more from you. Great man! SAA YA UKOMBOZI NI SASA![/QUOTE]

Ili ukombozi upatikane tunahitaji kuwa na rais ambaye ni adui wa RA and the Co. Kwahiyo ndugu zangu, hasa sisi tuliotoka kule vijijini tufanye juu chini twende huko tukawaelimishe na kuwahamasisha ndugu zetu wasiendelee kuipigia CCM kura tena. YES WE CAN.
 
unajua unachokisema ni kikubwa mno kuliko unavyoashiria..

a. Inawezekana vipi kijana wa miaka 25 kutoka asikojulikana kuweza kugombea Ubunge na kushinda?

b. Akiwa na miaka 30 hivi kijana huyo huyo anakuwa mtu mwenye nguvu kabisa nchini kiasi cha kuitwa na jarida mojawapo kuwa ni "King Maker"?

c. Akiwa chini ya miaka 40 anaweza kuwafanya watu kama kina Ruhinda, Kingunge, Mkapa, Mwang'onda, n.k kuweza kukaa chini na kugwaya mbele zake?

d. Inakuwaje mtu huyo kuweza kupanga safu yake ya mashambulizi kuanzia Ikulu.. na hakuna mtu anayeweza kumnyoshea kidole hata gizani?

Asili ya nguvu zake ni nini? Watu wengi wanafikiri ni fedha yake... Hili si kweli kwani watu wenye fedha wamekuwepo wengi kabla yake kuna watu waliokuwa waitikise nchi hii kama wangetaka.. kina Rajpar (wengine hata hawamkumbuki huyu), kina Somaia (yule wa Tanga), na wengine wengi.

Mzee Mengi aliwahi kuuliza swali ambalo lina umuhimu kweli, "kiburi chake anatoa wapi"?

Sasa MM unataka kusema nini hapa? Jamaa ni expert Kalumanzila au? Maana nasikia warabu wamo na impact yao tunaiona Mlingotini.
 
I have completed reading the radar thesis I will share with you the SFO findings in London, before Monday next week.

Yesterday I had a very good time her although it is very chilly to read the findings by SFO.

Lord have mercy! Kwanza death bed confessions halafu sasa SFO wanakupa ripoti yao juu ya dili ya rada. Haya, tunasubiri ripoti.

Amandla........
 
Marehemu Amir Jamal na Alnur Kasum walikua wadanganyika nao? mbona mmoja maziko yalikua Canada, au ndio yale yale ya Balali kupigwa kiberiti? Huyu kaka RA ni mdanganyika wa msimu, msimu ukiisha he will reveal his true colour and citizenship.
 
Anamiliki makampuni kama uyoga

Lakini jina lake halionekani popote

Na Saed Kubenea

MwanaHALISI​


ROSTAM Aziz, mbunge wa Igunga, anamiliki makampuni mengi ambamo jina lake halionekani, MwanaHALISI limegundua.

Hata pale anapokiri hadharani kuwa anamiliki kampuni fulani, bado kampuni hiyo haina jina lake kamili la Rostam Abdulrasul Aziz kama linavyofahamika katika kumbukumbu za bunge.

Rostam anatajwa kumiliki makampuni 10 yaliyoanzishwa jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, lakini jina lake linaonekana katika kampuni moja tu, kwa mujibu wa fomu za Wakala wa Usajili wa makampuni na Leseni za Biashara (BRELA).

Kampuni ambako jina lake linatajwa ni African Trade Development (T) Limited (ATDL) ambako pia limeongezewa jina jingine "Sakarri" kwenye safu ya majina ya ukoo, ambalo hata hivyo halifahamiki kwa wengi.

Katika ATDL, orodha ya waanzilishi wenye hisa inaonyesha kuna Rostam watano (5) huku jina "Rostam" likiwa ama limekosewa au limebadilishwa herufi kadhaa au wahusika wakiwa na ubini tofauti.

Hata katika ununuzi wa magazeti ya Rai, Mtanzania, The African, Dimba, Bingwa na "chuo" cha uandishi wa habari – MAMET, kutoka kampuni ya Habari Corporation Limited (HCL), hakuna jina lake.

MwanaHALISI linaweza kuripoti kuwa magazeti hayo yaliuzwa kwa kampuni inayoitwa Isenegeja Limited ya Dar es Salaam ambako jina la Rostam halionekani.

Aidha, ni Rostam Aziz aliyekiri mbele ya waandishi wa habari, 3 Mei mwaka huu katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski, kuwa anamiliki magazeti hayo kupitia kampuni ya New Habari Limited ambayo pia bado ni kitendawili.

Siku tatu kabla ya kauli yake kwamba anamiliki kampuni hiyo, gazeti lake la Rai liliripoti kuwa "inasadikika kwamba Rai linamilikiwa na Rostam."

Kwa mujibu wa barua ya Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi ya HCL, Shaaban Kanuwa ya 30 Aprili mwaka huu, bado wamiliki wa sasa wa magazeti hayo hawajayalipia.

Barua hiyo inayoandikwa kwa Isenegeja Company Limited, kupitia New Habari (2006) Limited (NHL), ambayo Rostam Aziz anadai kumiliki, inasema MAMET na magazeti ya Dimba na Bingwa, bado hayajalipiwa.

Kanuwa anasema katika barua hiyo, kwamba wakurugenzi wa HCL wanapendekeza zilipwe mara moja Sh. 100 milioni ambazo walikubaliana wakati wa ununuzi wa kampuni hiyo.

Wakati huohuo, Kanuwa anaelekeza kuwa iwapo Isenegeja haijawa tayari au imeshindwa kulipia magazeti mawili ya Dimba na Bingwa na MAMET, basi iache kuvitumia, kwa maana ya kuyachapisha na kuendesha chuo.

Habari Corporation iliuzwa miaka mitatu iliyopita. Haijafahamika magazeti ya Rai, Mtanzania na The African yaliuzwa kwa kiasi gani.

Lakini barua ya bodi ya HCL inasema gharama ya magazeti ambayo hayajalipiwa ilikuwa kama ifuatavyo: Dimba Sh.40 milioni, Bingwa Sh. 30 milioni na chuo Sh. 10 milioni na ilitaka kiasi hicho kilipwe ifikapo 29 Mei mwaka huu.

MwanaHALISI haikuweza kufahamu majengo ya HCL yaliuzwa kwa kiasi gani. Kanuwa alipoulizwa iwapo Isenegeja wamekwishawalipa, alisema swali hilo aulizwe mwenyekiti wa bodi, Jenerali Ulimwengu ambaye imefahamika yuko nje ya nchi na hakuweza kufikiwa.

Uchunguzi wa gazeti hili haukuweza kubaini faili la NHL ambako ulitegemea kukuta jina la Rostam Aziz aliyesema anamiliki kampuni hiyo na magazeti yake.

Lakini miezi miwili iliyopita, kulikuwa na andishi kwenye mtandao wa jamiiforum.com lililokuwa linaenda kwa Rostam Aziz kumtahadharisha kuwa alikuwa anaendesha kampuni ya NHL bila kusajiliwa na bila mwelekeo wowote.

Andishi lililosainiwa kwa jina moja la Salva, halikujulikana iwapo lilikuwa linatoka kwa mmoja wa wakurugenzi wa HCL na ambaye hivi sasa ni mkurugenzi wa mawasiliano ikulu, Salva Rweyemamu.

Mwandishi alikuwa anaonya juu ya kutozingatia sheria za nchi, kushindwa kuendesha kampuni kwa misingi bora ya menejimenti ambako kulikuwa kunaelekea "kuua kampuni."

Haijafahamika pia uhusiano wa NHL na Isenegeja, na uhusiano wa Rostam na makampuni yote mawili – NHL na Isenegeja. Waanzilishi na wamiliki wa Isenegeja ni Hassani Haidari na Gulam Abdulrasul wote wa anwani za Dar es Salaam.

Katika umiliki wa kampuni ya African Trade Development (T) Limited (ATDL) ndiko kuna vimbwanga vya majina yanayohusiana na Rostam.

Majina yaliyotumika kusajili kampuni hiyo ni Rostom A. Sakarri, Rostam Sakarri, Rustom Aziz Sakarri, Rustam Sakarri na Rustam Sakaari.

Wanahisa wengine wa kampuni hii waliojiandikisha BRELA, ni Gulam Abdulrasul Chakaar, Bahram Abdulrasul Chakaar na Abdulkadir Mehrab.

Rostam hakupatikana kuthibitisha iwapo Rustam, Rustom, Rostom na Rostam Sakarri yalikuwa majina yake, kulikuwa na jina lake au yalikuwa ya ndugu zake wa karibu. Simu yake ilijibu wakati wote kuwa haipatikani.

Kwenye muhutasari wa kikao cha kampuni ya ATDL cha 17 Machi 1993, kuna saini mbili za Rustam Chakaari (mkurugenzi) na Bahram A Chakaar (mwenyekiti).

Kubadilikabadilika kwa tahajia (spelling) za jina Rostam na mwingiliano wa majina ya ukoo, ni mambo yanayoacha kitendawili kigumu kutegua.

Kwa mfano, siyo rahisi kujua iwapo majina haya yameparanganyishwa kwa makusudi: Rustam Sakarri na Rustam Sakaari.


Mwanasheria aliyezungumza na MwanaHALISI kuhusu utata huu, amesema ni vigumu kumhusisha Rostam na majina hayo matano iwapo kunazuka matatizo ya kisheria kwenye kampuni hizo.

Amesema akihusishwa ataweza "kuruka kihunzi" na kudai hahusiki kwa kuwa nchi nzima, na labda vyeti vyake, kama anavyo, vinaonyesha anafahamika kwa jina la Rostam Abdulrasul Aziz.

Mwanasheria huyo alisema labda mtu wa aina hiyo anaweza kunaswa kwa kutumia ushahidi wa mazingira.

Makampuni ambayo yanatajwa kumilikiwa na Rostam, lakini jina lake halionekani BRELA, ni pamoja na Africa Tanneries Limited, Tanzania Leather Industries Limited na Wembere Hunting Safaris Limited.

Mengine ambako jina lake halionekani ni Tanzania Packages Manufacturers Limited na Caspian Construction Limited ambayo anwani zake zilikuwa zinatumiwa na kampuni tata ya kufua umeme ya Dowans.

Gazeti hili lina orodha ya makampuni ambayo yanadaiwa kuwa ya Rostam, wale wote waliotajwa kuwa waanzilishi na baadhi ya ofisi za makampuni haya ambako inadaiwa alikuwa anakwenda binafsi kuhimiza utendaji au kufuatilia malipo.

Madai ya Rostam kumiliki kampuni zisizo na majina yake yalianza kujitokeza lilipozuka sakata la yeye kuhusishwa na kampuni kadhaa zenye kashfa, zikiwamo Dowans na Kagoda.

Rostam mweyewe alikiri kuwa na uhusiano na Dowans, lakini akadai hamiliki kampuni hiyo isipokuwa anuani na barua pepe za kampuni yake ya Caspian Construction zilikuwa zinatumiwa na kampuni hiyo ya Dowans.

Jina la Rostam linatajwa katika umiliki wa kampuni tata ya Kagoda. Wakili wa Mahakama Kuu, Byidinka Michael Sanze amenukuliwa katika hati yake ya kiapo, akisema kwamba Rostam ndiye aliyemtaka kushuhudia hati za mikataba ya Kagoda

Kampuni ya Kagoda ilichota zaidi ya Sh. 40 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
 
Anamiliki makampuni kama uyoga

Lakini jina lake halionekani popote

Na Saed Kubenea

MwanaHALISI​


ROSTAM Aziz, mbunge wa Igunga, anamiliki makampuni mengi ambamo jina lake halionekani, MwanaHALISI limegundua.

Hata pale anapokiri hadharani kuwa anamiliki kampuni fulani, bado kampuni hiyo haina jina lake kamili la Rostam Abdulrasul Aziz kama linavyofahamika katika kumbukumbu za bunge.

Rostam anatajwa kumiliki makampuni 10 yaliyoanzishwa jijini Dar es Salaam kwa nyakati tofauti, lakini jina lake linaonekana katika kampuni moja tu, kwa mujibu wa fomu za Wakala wa Usajili wa makampuni na Leseni za Biashara (BRELA).

Kampuni ambako jina lake linatajwa ni African Trade Development (T) Limited (ATDL) ambako pia limeongezewa jina jingine “Sakarri” kwenye safu ya majina ya ukoo, ambalo hata hivyo halifahamiki kwa wengi.

Katika ATDL, orodha ya waanzilishi wenye hisa inaonyesha kuna Rostam watano (5) huku jina “Rostam” likiwa ama limekosewa au limebadilishwa herufi kadhaa au wahusika wakiwa na ubini tofauti.

Hata katika ununuzi wa magazeti ya Rai, Mtanzania, The African, Dimba, Bingwa na “chuo” cha uandishi wa habari – MAMET, kutoka kampuni ya Habari Corporation Limited (HCL), hakuna jina lake.


MwanaHALISI linaweza kuripoti kuwa magazeti hayo yaliuzwa kwa kampuni inayoitwa Isenegeja Limited ya Dar es Salaam ambako jina la Rostam halionekani.

Aidha, ni Rostam Aziz aliyekiri mbele ya waandishi wa habari, 3 Mei mwaka huu katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski, kuwa anamiliki magazeti hayo kupitia kampuni ya New Habari Limited ambayo pia bado ni kitendawili.

Siku tatu kabla ya kauli yake kwamba anamiliki kampuni hiyo, gazeti lake la Rai liliripoti kuwa “inasadikika kwamba Rai linamilikiwa na Rostam.”

Kwa mujibu wa barua ya Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi ya HCL, Shaaban Kanuwa ya 30 Aprili mwaka huu, bado wamiliki wa sasa wa magazeti hayo hawajayalipia.

Barua hiyo inayoandikwa kwa Isenegeja Company Limited, kupitia New Habari (2006) Limited (NHL), ambayo Rostam Aziz anadai kumiliki, inasema MAMET na magazeti ya Dimba na Bingwa, bado hayajalipiwa.

Kanuwa anasema katika barua hiyo, kwamba wakurugenzi wa HCL wanapendekeza zilipwe mara moja Sh. 100 milioni ambazo walikubaliana wakati wa ununuzi wa kampuni hiyo.

Wakati huohuo, Kanuwa anaelekeza kuwa iwapo Isenegeja haijawa tayari au imeshindwa kulipia magazeti mawili ya Dimba na Bingwa na MAMET, basi iache kuvitumia, kwa maana ya kuyachapisha na kuendesha chuo.

Habari Corporation iliuzwa miaka mitatu iliyopita. Haijafahamika magazeti ya Rai, Mtanzania na The African yaliuzwa kwa kiasi gani.

Lakini barua ya bodi ya HCL inasema gharama ya magazeti ambayo hayajalipiwa ilikuwa kama ifuatavyo: Dimba Sh.40 milioni, Bingwa Sh. 30 milioni na chuo Sh. 10 milioni na ilitaka kiasi hicho kilipwe ifikapo 29 Mei mwaka huu.

MwanaHALISI haikuweza kufahamu majengo ya HCL yaliuzwa kwa kiasi gani. Kanuwa alipoulizwa iwapo Isenegeja wamekwishawalipa, alisema swali hilo aulizwe mwenyekiti wa bodi, Jenerali Ulimwengu ambaye imefahamika yuko nje ya nchi na hakuweza kufikiwa.

Uchunguzi wa gazeti hili haukuweza kubaini faili la NHL ambako ulitegemea kukuta jina la Rostam Aziz aliyesema anamiliki kampuni hiyo na magazeti yake.

Lakini miezi miwili iliyopita, kulikuwa na andishi kwenye mtandao wa jamiiforum.com lililokuwa linaenda kwa Rostam Aziz kumtahadharisha kuwa alikuwa anaendesha kampuni ya NHL bila kusajiliwa na bila mwelekeo wowote.


Andishi lililosainiwa kwa jina moja la Salva, halikujulikana iwapo lilikuwa linatoka kwa mmoja wa wakurugenzi wa HCL na ambaye hivi sasa ni mkurugenzi wa mawasiliano ikulu, Salva Rweyemamu.

Mwandishi alikuwa anaonya juu ya kutozingatia sheria za nchi, kushindwa kuendesha kampuni kwa misingi bora ya menejimenti ambako kulikuwa kunaelekea “kuua kampuni.”


Haijafahamika pia uhusiano wa NHL na Isenegeja, na uhusiano wa Rostam na makampuni yote mawili – NHL na Isenegeja. Waanzilishi na wamiliki wa Isenegeja ni Hassani Haidari na Gulam Abdulrasul wote wa anwani za Dar es Salaam.

Katika umiliki wa kampuni ya African Trade Development (T) Limited (ATDL) ndiko kuna vimbwanga vya majina yanayohusiana na Rostam.

Majina yaliyotumika kusajili kampuni hiyo ni Rostom A. Sakarri, Rostam Sakarri, Rustom Aziz Sakarri, Rustam Sakarri na Rustam Sakaari.

Wanahisa wengine wa kampuni hii waliojiandikisha BRELA, ni Gulam Abdulrasul Chakaar, Bahram Abdulrasul Chakaar na Abdulkadir Mehrab.

Rostam hakupatikana kuthibitisha iwapo Rustam, Rustom, Rostom na Rostam Sakarri yalikuwa majina yake, kulikuwa na jina lake au yalikuwa ya ndugu zake wa karibu. Simu yake ilijibu wakati wote kuwa haipatikani.

Kwenye muhutasari wa kikao cha kampuni ya ATDL cha 17 Machi 1993, kuna saini mbili za Rustam Chakaari (mkurugenzi) na Bahram A Chakaar (mwenyekiti).

Kubadilikabadilika kwa tahajia (spelling) za jina Rostam na mwingiliano wa majina ya ukoo, ni mambo yanayoacha kitendawili kigumu kutegua.

Kwa mfano, siyo rahisi kujua iwapo majina haya yameparanganyishwa kwa makusudi: Rustam Sakarri na Rustam Sakaari.

Mwanasheria aliyezungumza na MwanaHALISI kuhusu utata huu, amesema ni vigumu kumhusisha Rostam na majina hayo matano iwapo kunazuka matatizo ya kisheria kwenye kampuni hizo.


Amesema akihusishwa ataweza “kuruka kihunzi” na kudai hahusiki kwa kuwa nchi nzima, na labda vyeti vyake, kama anavyo, vinaonyesha anafahamika kwa jina la Rostam Abdulrasul Aziz.

Mwanasheria huyo alisema labda mtu wa aina hiyo anaweza kunaswa kwa kutumia ushahidi wa mazingira.

Makampuni ambayo yanatajwa kumilikiwa na Rostam, lakini jina lake halionekani BRELA, ni pamoja na Africa Tanneries Limited, Tanzania Leather Industries Limited na Wembere Hunting Safaris Limited.

Mengine ambako jina lake halionekani ni Tanzania Packages Manufacturers Limited na Caspian Construction Limited ambayo anwani zake zilikuwa zinatumiwa na kampuni tata ya kufua umeme ya Dowans.

Gazeti hili lina orodha ya makampuni ambayo yanadaiwa kuwa ya Rostam, wale wote waliotajwa kuwa waanzilishi na baadhi ya ofisi za makampuni haya ambako inadaiwa alikuwa anakwenda binafsi kuhimiza utendaji au kufuatilia malipo.

Madai ya Rostam kumiliki kampuni zisizo na majina yake yalianza kujitokeza lilipozuka sakata la yeye kuhusishwa na kampuni kadhaa zenye kashfa, zikiwamo Dowans na Kagoda.


Rostam mweyewe alikiri kuwa na uhusiano na Dowans, lakini akadai hamiliki kampuni hiyo isipokuwa anuani na barua pepe za kampuni yake ya Caspian Construction zilikuwa zinatumiwa na kampuni hiyo ya Dowans.
Jina la Rostam linatajwa katika umiliki wa kampuni tata ya Kagoda. Wakili wa Mahakama Kuu, Byidinka Michael Sanze amenukuliwa katika hati yake ya kiapo, akisema kwamba Rostam ndiye aliyemtaka kushuhudia hati za mikataba ya Kagoda.

Kampuni ya Kagoda ilichota zaidi ya Sh. 40 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

- Sometimes hawa huwa wanachukua habari hapa JF, hizi si tumezisema sana huko nyuma kwamba huyu Rostam hajasajili jina lake kama owner wa kampuni mahali popote, naona habari zinajirudia tena.

FMES!
 


Lakini miezi miwili iliyopita, kulikuwa na andishi kwenye mtandao wa jamiiforum.com lililokuwa linaenda kwa Rostam Aziz kumtahadharisha kuwa alikuwa anaendesha kampuni ya NHL bila kusajiliwa na bila mwelekeo wowote.

Angalia hapo juu Mkuu.
 
huyu hajakoma sio, tindikali haikumtosha, safari hii watakuua.
 
Sijui kwa habari hiyo hapo juu kuna ubaya gani kisheria. Labda kama directors/shareholders hawa-exist, au less than 18 years old. To register a company you need an address and the names of shareholders and directors (living). Kwa shughuli alizonazo Rostam sitashangaa kama ana kampuni hata mia. THis is a guy who have been also playing offshore, especially Cyprus, Isles Man etc he must be having more companies there.
 
huyu hajakoma sio, tindikali haikumtosha, safari hii watakuua.
Silence in issue we ought to speak against, means agreement, participation or both.Tatizo la most Tanzanians ni hiyo tabia ya uoga and unnecessary silence.
 
- Sometimes hawa huwa wanachukua habari hapa JF, hizi si tumezisema sana huko nyuma kwamba huyu Rostam hajasajili jina lake kama owner wa kampuni mahali popote, naona habari zinajirudia tena.

____________________________

Field Marshall ES:

Inawezekana wanachukuwa vyanzo hapa lakini wao wamekwenda mbali zaidi. Isitoshe inabidi tuwashukuru kwa kuzimwaga habari kwenye gazeti hilo (Mwanahalisi) lenye circulation kubwa kuliko magazeti yote nchini -- nasikia huchapa nakala 75,000 kila wiki. Wanaoingia humu JF sidhani kama wanafika robo ya hao.

Lakini pia ni dhahiri kabisa kwamba huyu RA daima amekuwa na dhamira zisizo takatifu dhidi ya nchi hii na wananchi wake -- ama sivyo atueleze sababu hasa ya kujificha nyuma ya majina ya wengine iingawa mimi naamini mengi ya majina hayo ni feki tu -- yaani hakuna watu halisi..

Kama ilivyoandikwa huko nyuma hawezi kuthibitisha kinagaubaga majigambo yake kwamba kampuni zake zimeajiri watu 6,000 au kwamba analipa mabilioni kila mwaka kama kodi serikalini. Hawezi, maana tunaweza ku-allege, bila wasiwasi kwamba hizo kampuni siyo zake, na hawezi kulazimisha kusema ni zake wakati hakuna ushahidi wa kimaandishi. Nasikia hata ofisi hana -- anababaisha tu mara hapa, mara kule.

Ni tapeli mkubwa hapa nchini na inasikitisha kuona vyombo vyetu vya dola vinakosa fyoko ya kumgusa.

Kwa mfano, inaaminika kwamba iwapo Mengi angewataja tu "mapapa" wa kizalendo (yaani siyo hao wenye asili ya Kiasia), sidhani kama akina Mkuchika, Maelezo, TCRA etc wangemsumbua Mengi. Kilichomponza Mengi ni kuwagusa wasiogusika katika nchi hii -- hao weupe.

Hawa na wengine wanaomtetea RA wanadhihirisha kweli ule usemi "Miafrika ndiyo tulivyo!" Hatutaendelea daima kwani bado tuko wanyonge sana. Nyerere angalau alijaribu kuondoa unyonge huu lakini sasa unarudi kwa kasi.
 
Wanamapinduzi wa kweli nchi hii wako wapi wale wasiofuata itikadi lakini ukweli? Hakuna watu wanaoweza kujitolea kufa kwa kukataa upuuzi huu wa RA na watu wake by using any means?
 

"huyu hajakoma sio, tindikali haikumtosha, safari hii watakuua."

________________________________

Omr:
kawaida huwa ni hivyo, ni lazima atokee mmoja shujaa kutoa shingo yake kwa ajili ya kuokoa mamilioni wengine "mabwege". Hiyo imo ktk historia duniani na haitafutika daima.
 
"Sijui kwa habari hiyo hapo juu kuna ubaya gani kisheria. Labda kama directors/shareholders hawa-exist, au less than 18 years old. To register a company you need an address and the names of shareholders and directors (living). Kwa shughuli alizonazo Rostam sitashangaa kama ana kampuni hata mia. THis is a guy who have been also playing offshore, especially Cyprus, Isles Man etc he must be having more companies there."

______________________

Interested Observer:

Kuwa kisheria au la si suala hapa. Suala ni jee dhamira ya kujifichajificha namna hii ni takatifu ndani ya shuguli zake? Kikubwa kinachojitokeza mara moja ni kwa yeye mwenyewe kuwa tayari kuruka kimanga inapotokea jinai katika makampuni yake hayo -- kwani huikana hapo hapo kuwa siyo yake -- eg Richmond, Kagoda.

Mimi nadhani sambamba na kampuni zake zote hizo zisizokuwa na jina lake ni bora angekuwa na nyingine kadha ambazo kuna jina lake na kujaribu kuziendesha kihalali -- kama onyesho kuwa "Si mnaona kampuni zangu hasa ni hizi? Na hazina dosari yoyote?" Kutokuwa na kampuni yake yoyote kwa jina lake kuanazua swali kwamba anafanya nini hasa hapa nchini?
 
Nami pia naamini haya majina ni feki lakini jamani kwanini tusikate mizizi ya fitina? huyu RA hakujisajilia makapuni lazima wapo waliomsajilia yani ofsi ya kusajili makapuni Na kama sijakosea kabla ya kusajili kampuni lazima uache huko fotokopi ya passport ama vitaburisho ama kuapa mahakamani upate affidavit.

Sasa badala yake mimi naonelea tungeanza na hizi organ kuzibana kama kuna sehemu alidaganya tutamtia tu jamaa nguvuni.Maana kabla ya usajili huo lazima kuna vyombo vya dola ambavyo amevidaganya .

Na pia naonelea huko ndiko kuna matatizo tukidhibiti huko RA hatatokea tena lakini kujaribu kumdhibiti RA bila kuvidhibiti vyombo hivi ni kuiahadaa jamii kwa madhumuni tofauti kabisa na ya kuwatetea watanzania wanyonge.
 
Sijui kwa habari hiyo hapo juu kuna ubaya gani kisheria. Labda kama directors/shareholders hawa-exist, au less than 18 years old. To register a company you need an address and the names of shareholders and directors (living). Kwa shughuli alizonazo Rostam sitashangaa kama ana kampuni hata mia. THis is a guy who have been also playing offshore, especially Cyprus, Isles Man etc he must be having more companies there.

IO,
Ukitumia akili yako tu ya kawaida kufanya analysis ya mambo utagundua kuwa hapa kuna undanganyifu wa wazi. Siju kama inaingia akili kweli haya majina (Rostom A. Sakarri, Rostam Sakarri, Rustom Aziz Sakarri, Rustam Sakarri na Rustam Sakaari) yakafanana kwa kubadili au kuhamisha herufi kutoka jina moja kwenda jina lingine kwa kiasi hicho. Kwa hakika RA ni balaa. Atalifilisi hili taifa kama hatashughulikiwa. Anapojitetea kuwa yeye ni mzalendo lakini kwa matendo yake haya anakana na kusema yeye yupo hapa TZ kuchuma na kudhoofisha uchumi wa Tanzania na kama inavyojulikana yeye ana uraia wa nchi tatu (TZ, Iran na Canada) kwahiyo yuko mguu pande. Ooooooh GOD forbid.
 
huyu hajakoma sio, tindikali haikumtosha, safari hii watakuua.

Omr,
Je wewe ni mojawapo wa akina Rostom A. Sakarri, Rostam Sakarri, Rustom Aziz Sakarri, Rustam Sakarri na Rustam Sakaari. Sawa muueni kama mnaamua hivyo lakini jueni ya kuwa yuko MUNGU. Kama hamtajirekebisha na kuyaacha hayo maovu yenu, MUNGU ni hakimu wa haki, nanyi iko siku mtasimama mbele yake kutoa hesabu ya hayo maovu yenu mliyofanya. Miaka yenu hapa duniani hata kama mtaishi miaka 120 ni kidogo sana mkilinganisha na maisha ya milele katika taabu na dhiki katika moto wa milele. Nawapa ushauri mgeuke mziache njia zenu mbaya na MUNGU wa rehema atawarehemu vinginevyo mtaangamia milele.
 
mi sina hata la kusema jamaa ni kifaru hata huko atown ana mabiashara yamawe maduka na .kadhalika mi namuomba asaidie mashule yale watoto wanakaa chini na vilema wanahangaika hawana ajira wala mlo wasiku maana nae atajibu huko mbele ya mungu kujilimbikizia mijimali hadi wapi mh mh mh
 
Back
Top Bottom