Leokweli,
Nimekuapata mkuu ila naongezea kitu kidogo tu..Mkuu usinielewe vibatya najaribu kuelewa kilichotokea kabla sijaweka lawama zangu ktk issue nisiyoifahamu..nitapenda sana kumhukumu Mengi au Idd Simba kwa maelezo yanayoniingia kichwani...
1. Hivi vyombo vilianzishwa vipi maanake naona vyombo viwili vyenye malengo sawa. Je, zilikuwa taasisi za serikali au vyombo binafsi..
2. Na kwa nini wafanyabiashara wengi wenye credit nzuri walikuwa TCCIA badala ya CTI wakati wakifahamu watawezeshwa huko CTI.
3.Kisha Idd Simba kama waziri akakisaidia zaidi chombo hiki cha CTI.. sidhani kama sababu ni Mengi na uhusiano wake na Idd Simba..
4. Ningependa sana kuelewa Mengi alitakiwa kufanya nini kama kiongozi wa CTI kama sii kuhakikisha wanachama wake wanapewa mikopo hiyo..Je, Mengi angekuwa kiongozi wa TCCI angefanya tofauti? kwa nini tusiwalaumu viongozi wa TCCIA kwa kushindwa kuhakikisha wafanyabiashara wake wanapata mikopo hiyo iwe kwa nguvu zote za kimashindao..na kama zipo sababu ni zipi zilizowakwamisha..
Mwisho wa yote haya mkuu wangu mimi nachofahamu na kulia nacho ni kwamba fedha hizi za mikopo ya CIS haijaridishwa na kwa taarifa za sasa hivi ni zaidi ya 180/b hazijarudishwa..Hasara kwangu mwananchi ni hasara tu iwe imetokana na CTI au TCCI kwa sababu fedha hii leo hii imeonekana kuwa ni hujuma kubwa ilifanyika..Ikiwa sehemu kubwa ya fedha hii imekopeshwa CTI chombo ambacho Mengi alikuwa kiongozi wake itabidi atufahamishe vizuri kilichoendelea huko na kina nani ni wadaiwa wa fedha hizo..
Mkandara
TCCIA ilianzaishwa mwaka kwa support ya serikali ya Tanzania ili kuipa nguvu private sector wakati tanzania inaingia kwenye open economy or mixed economy.
Kilichotekea ni kwamba Iddy Simba,Mengi na baadhi ya waasia wachache waliona kuwa the flow of information process ilkuwa haiwanufaishi because it was so open, na zaidi hwakuweza kuchaguliwa kwenye nafasi za uongozi,Kilichofanyika wakajitoa TCCIA wakaanzisha CTI. Iddy Simba alikuwa na conflict of intrest kupitia Viwanda vyake kuisupport CTI
CTI ilipoanzishwa wakaweka masharti magumu ya membership,hivyo wakachukuana members wachache sana, kutokana na requirements zao biashara nyingi za kawaida zilikuwa haziqulify. Hivyo unakuta biashar inaweza kuwa credit worth but haiqulity membership requirement yao
Tatizo la kimsingi ni kwamba Mengi na simba hawakujali Uzalendo wanaoongelea leo , kwasababu waliungana na wasia kuiua nguvu TCCIA na ndio maana walikimbia TCCIA ambayo ilikuwa inawanufaisha wafanyabiashara katika mikoa 21, Kukimbia kwao hakuwa na lengo lingine zaidi ya kutumia access ya Iddi Simba Kunyonya opportunity zote peke yao na wasia wachache. Kwahiyo kwa kitendo cha mengi kusema waasia wanatunyonya wakati yeye na Iddi Simba ndio walikuwa mafacilitator haiingii akilini.
Ninakuunga mkono na hitimisho lako, Kutorudishwa kwa pesa hizo kumesababisha kufa kwa private sector kwasababu pesa hizo kama zingerudishwa in time zingeweza kusaidia kuendeleza private sector Tanzania , lakini hili halikutokea.
Ndio maana ninasema tunahitaji tufute uchafu kila kona bila kuangaliana usoni, na tusiruhusu walewale mafisadi Warudi na ngozi ya kondoo.