Madela Wa- Madilu
JF-Expert Member
- Mar 24, 2007
- 3,063
- 743
Hili la shule za Nzega (+Igunga) wakati huo liko wazi kwani walikuwa wanasoma darasa la kwanza mpaka la nne na wakifaulu mtihani kwenda darasa la tano basi ilikuwa wanaenda boarding ambazo zilikuwa Busongo,Bukene,Izinga na Ndalla girls wakati shule za Day maarufu zilikuwa Uchama, Mwanh'ala, na Upungu, na mara nyingi kila mwaka kulikuwa na michezo ya mashule ambapo zaidi wanafunzi wote wanamichezo walikuwa wanakutana Uchama,sasa basi ataje shule ipi kati ya hizo yeye RA alisomea kama primary school? watu wa Nzega wa enzi hizo tunajuana mpaka leo....wapi Bernald M?....
Cha msingi jamaa AMECHEMSHA! na hiyo kutamka kuwa Kazaliwa Ndalla it doesn't justify kuwa alisomea Tanzania unless true birth certificate is produced
Utaratibu wa kusoma mpaka Darasa la 4 na kufanya mtihani ulifutwa zamanoi Rostam akiwa na miaka 3. Mimi umri wangu ni mkubwa miaka 4 kwa umri wa Rostam kama kweli ana 40 bado sikusoma katika utaratibu huo wa mpaka std 4.Kama ni kweli Rostam alisoma enzi hizo za kufanya mtihani std 4, basi Rostam alianza shule kabla hata mimba yake haijatungwa tumboni mwa mama yake.Naona tunapata taabu sana kupata historia ya Rostam Aziz, wakati ni rahisi sana kupata historia za watu wengine kama Bakharesa, Marehemu Gulamali, Abood nk.Naamini kabisa kwamba kuna kitu kikubwa kinaendelea katika maisha ya MH huyu, kitu hicho kikiwekwa wazi Break ya kwanza ya Rostam ni Jangwani kule Dubai, kwani hawezi kurudi Iran kwa sababu kwa uzembe na mazoea ya tabia kanuni za Mamulla wa kule hatoziweza.