Yohana Kilimba
JF-Expert Member
- Dec 25, 2012
- 8,105
- 5,642
Taratiiibu mkaanza kukubali muziki wa Magufuli
Magufuli ana good intentions
kaipania hii kazi
angependa kukumbukwa kama aliekuja 'kuijenga' nchi
but.......too early kumtangaza 'chaguo la Mungu'
Mobutu na Iddi Amini pia waliwahi kutangazwa 'machaguo ya Mungu huko makwao'
miaka ya mwanzo tu walipochukua madaraka
na kila walipokuwa wanapindisha au kuvunja sheria ili 'kuharakisha maendeleo'
kwa wananchi walipigiwa vigelegele nchi nzima...mpaka pale waliopiga vigelegele walipoanza
'kuisoma namba pia'
Hata kama ana nia nzuri...sheria zifuatwe
watu wasibomolewe nyumba bila taarifa au huku kuna zuio mahakamani
na sisi turukeruke na kusherehekea kisa ni 'ccm wanaisoma namba'
jamani ni siku 20 tu hizi.....kuna miaka 5 mbele......tutamlewesha sifa tutajuta
Hivi, hii slogan ya "chaguo la Mungu" mbona inashika kasi hivyo...
Tangu JMK tunaona machaguo ya Mungu tu...
Mihemko inatusumbua sana..JPM is doing well so far...
Nakuunga mkono kabisa kuwa Magufuli ni chaguo la Allah! Ni wana UKAWA wachache wanaweza kusema haya! Hongera sana.
Hapo kwenye red umeharibu kabisa labda ueleze kiundani ni kivipi alipokwa? Mlikuwa wapi? Aliposema nyie mpige kura swala la kuzilinda mmwachie yeye ulimuelewa?
Hakika Magufuli ni chaguo la Allah tumpe ushirikiano..